Ukimya wa Katiba ya JMT Kuhusu Kifo cha Mgombea Urais

Hamna mada fikirishi hapa ni uvivu tu wenu wa kutafuta maarifa....mgombea urais akifariki kwenye kampeni zoezi zima linaitishwa upya Chama kitatakiwa kuteua mtu ambaye atakuja na mwenza wake.
Watu hawasomi, na hawafuatilii matukio ya nchi, 2005 lilitokea hili analoongelea mtoa mada na uchaguzi ulisimama.

Uchaguzi hausimamiwi na katiba bali ni sheria ya uchaguzi

Mleta mada anazungumzia uchaguzi wakati hajui hata sheria na taratibu za uchaguzi.

Watanzania tumejaa ujuaji sana
 
Hii ni mada fikirishi ila katiba imetoa mwongozo mzuri, na tunaweza kuchukua two cases kama rejea.

Kama 2015 mgombea wa urais wa CCM angefariki maana yake JK angeendelea kuwa seating president na CCM walikuwa na nafasi ya kuamua SSH agombee kama Rais dhidi ya EL wa CDM au CCM wangekuwa na mikutano maalumu ya CC, NEC na Mkutano mkuu kuona nani angeweza kusimama na EL na wengine waliokuwa kwenye game.

2005 aliekuwa mgombea wa makamu wa Rais kwa CDM alifariki katikati ya race, uchaguzi ulisogezwa mbele na Rais Mkapa aliendelea ku-govern majuma kadhaa mpaka uchaguzi ulipofanyika na JK kuapishwa Nov badala ya late October kama ilivyokuwa huko nyuma.

Kama ingetokea JPM aliekuwa seating president akafariki katikati ya race 2020, maana yake SSH alitakiwa kuapishwa ili kumalizia muda wa JPM mpaka the next president atakapopatikana kwenye uchaguzi wa 2020. Pengine CCM wangepima maji kama SSH ambae ni angekuwa seating President kama angeweza kuchuana na TL, BKM na wengine au wangelazimika kuitisha mkutano mikutano maalum ya CC, NEC na Mkutano mkuu ili wateue mgombea ambae wanaona anaweza kuwavusha kwa wapiga kura.

Nadhani hoja hii inafikirisha na tuombeaneni uzima na afya njema kati yetu; ikitokea kuna kudra za mwenyezi Mungu, basi vingunge kwenye vyama husika wangeamua nini kifanyike.
Mkuu Matuja uko vizuri, ila hapo kwenye para ya 4, vipi kama chama kina uhakika kuwa aliyeapa kuchukuwa nafasi ya marehemu aliyefariki kwenye kampeni hauziki kwa wapiga kura alafu wakaitisha vikao hivyo kumtokosa ugombea wa urais wakati ameishaonja tamu ya urais alafu akawaza kuwa si mimi ndiyo ninaamuru majeshi? Si mimi ndiyo nina mamlaka ya kuahirisha/kufuta uchaguzi? Kwanini nikubali kuachia urais na kurudi kugombea kama running mate alafu nije nirudi Ikulu ambayo tayari nimeishakuwa rais lakini nirudi humo kama Makamu wa Rais? What is chama after all? Si ni wawahi viongozi wa chama kwa kufuta uchaguzi wote alafu naunda chama changu nakisajili na ndipo niitishe uchaguzi mkuu baada ya muda hukooo?

Mkuu Matuja, tupe maarifa.
 
Kama ni wa upinzani, moja kwa moja anakuwa amejitoa kwenye kampeni na kama ni wa CCM kampeni zinasitishwa na mgombea mwenza anakuwa mshindi ili kumfariji kwa kufiwa.
Hapana mkuu sheria iko wazi juu ya hili uchaguzi utasimama.
 
Mwaka 2005 mgombea mwenza wa Freeman Mbowe alifariki dunia zikiwa zimebaki siku 15 uchaguzi kufanyika.

Uchaguzi ulisimama kwa siku 28 kwa chama kuteua mgombea mwenza mwingine kisha tukaendelea na kampeni kama ilivyoada.

Kama unakumbuka uchaguzi wa 2005 haukufanyika October kama ilivyozoeleka.
Kumradhi mkuu, alikuwa Mgombea Mwenza wa Mbowe au wa Dr. Slaa?
 
Mkuu, naomba nikusaidie maana unachanganya mambo mawili. Mambo unayochanganya moja linahusu kumpata Rais endapo Rais amefariki, pili ni kumpata mgombea wa kiti cha Rais endapo mgombea amefariki wakati wa Kampeni.

Ikiwa Rais mfano Magufuri angefariki wakati wa Kampeni ( wakati wa kugombea muhala wake wa pili) ,yafuatayo yangefanyika. Kwa kuwa kiti cha Rais kingebaki wazi utaratibu wa kujaza nafasi ya Rais ungefanyika yahani makamu wa Rais angeapishwa kuwa Rais wa nchi.

Pili,kwa kuwa chama cha mapinduzi (CCM) kingekuwa kimepoteza mgombea sharia ya uchaguzi inataka chama kilichopoteza mgombea kujaza ( kuteua) mgombea ndani ya wiki mbili,alafu mchakato wa uchaguzi ungeendelea.

Kutokana na utaratibu huo, ingebaki utashi wa CCM kuamua kama Samia S.Hassan ateuliwe kuwa mgombea au wateue mwingine. Hivyo katiba katika hilo haijanyamaza, tatizo ni wewe na watu wa aina yako kutokutofautisha mambo ya serikali na yale ya CCM kama chama.

Baada ya ufafanuzi huu wa chumla nitakuwa najibu hoja zako mojamoja.


Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
Kwa mazingira hayo mtu si unaweza kuwa raisi mda mfupi halafu ukawa makamu wa raisi kama chama kitaamua kuteua mgombea raisi mwingine halafu wewe wakakuacha kama mgombea mwenza,kama nimeelewa sawasawa.
 
Hilo si suala katiba,itabaki utashi wa chama husika,mfano CCM wangeamua mgombea awe Mama Samia ( ambaye angekuwa ameapishwa tayari kuwa Rais) au wangeweza kuteua mwingine.Ili mradi sheria ya uchaguzi inawataka wateue mgombea mwingine baada ya kifo cha mgombea wao.



Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
Mkuu vipi kama akigundua kuwa chama kinampendekeza mwingine kuwa mgombea urais na yeye ambaye tayari ni rais arudishwe kugombea umakamu na ameishaonja utamu wa urais alafu akaamua kufuta uchaguzi, akaunda chama chake na kuruhusu uchaguzi baadaye hukoooo ili agombee kama rais? Tusaidie mkuu.
 
Watu hawasomi, na hawafuatilii matukio ya nchi, 2005 lilitokea hili analoongelea mtoa mada na uchaguzi ulisimama.

Uchaguzi hausimamiwi na katiba bali ni sheria ya uchaguzi

Mleta mada anazungumzia uchaguzi wakati hajui hata sheria na taratibu za uchaguzi.

Watanzania tumejaa ujuaji sana
Hao ndo wanahitaji katiba yaani akilala katiba akienda haja ndogo katiba ili hali hata hii iliyopo hawaifaham lakin ni wajuaji balaa
 
Mkuu vipi kama akigundua kuwa chama kinampendekeza mwingine kuwa mgombea urais na yeye ambaye tayari ni rais arudishwe kugombea umakamu na ameishaonja utamu wa urais alafu akaamua kufuta uchaguzi, akaunda chama chake na kuruhusu uchaguzi baadaye hukoooo ili agombee kama rais? Tusaidie mkuu.
Haya ni mambo ya vyama kama hajavinj sheria kun shida gani
 
Hao ndo wanahitaji katiba yaani akilala katiba akienda haja ndogo katiba ili hali hata hii iliyopo hawaifaham lakin ni wajuaji balaa
Msomi tufundishe unawezaje kutenganisha Katiba na Sheria? Kipi kinamuelekeza mwenzie cha kufanya? Aidha, ninajuwa kuna maelekezo ya Katiba kutaka sheria zifuatwe lakini matumizi hayo ya sheria km entity yanapoleta mtafaruku je, Katiba inakaa kimya?
 
Mada Fikirishi

Katiba yetu inaongelea kifo cha Rais akiwa madarakani lakini haiongelei Mgombea Urais ambaye tayari ni Rais akifa akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mkuu. Natoa mfano ili uelewe kwa urahisi kwamba JPM angekufa akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mkuu Katiba haisemi kitu gani kifanyike zaidi tu ya kusema nafasi ya Rais itachukuliwa na Makamu wa Rais. Sasa yafuatayo hayana majibu ya Katiba:-

1. Je, kama Mgeombea Urais akifa kwenye kampeni za uchaguzi nafasi yake itajazwaje?

2. Je, Makamu wa Rais anayerithi kiti cha Rais ndiye atakuwa Mgombea nafasi ya Urais?

3. Je, atateuliwa mwingine na chama kujaza nafasi ya Mgombea Urais? Au atajaza nafasi ya Makamu wa Rais kwa kuwa Makamu wa Rais aliyekuwepo tayari amerithi kiti cha Rais na kuwa Rais?

4. Kama Makamu anayerithi kiti cha Rais siyo strong kushinda uchaguzi yaani siyo kipenzi cha wapiga kura wengi na kwamba akipewa kurithi pia nafasi ya Mgombea Urais aliyekufa kwenye kampeni huenda chama kikapoteza ushindi je, hapa chama au serikali iliyoko madarakani itamshusha Rais huyu (ambaye alikuwa Makamu zamani) toka kwenye kiti cha Rais ili arudi aendelee kugombea nafasi yake ile ile ya awali ya Makamu wa Rais aliyokuwa akigombea kabla Mgombea Urais (ambaye alikuwa Rais) kufa wakati wa kampeni za uchaguzi?

5. Je, hiyo siyo demotion/kushushwa cheo kwa Rais?

6. Je, Katiba inatoa maelekezo yoyote kuhusu demotion ya Rais toka kuwa Rais na kurudi kuwa Makamu wa Rais?

7. Japokuwa iko wenye Katiba kuhusu kifo cha Rais akiwa madarakani lakini kama taifa hatukujiandaa na kifo cha Rais akiwa madarakani, ni vivyo hivyo kumbe kwamba hata sasa kama taifa hatujajiandaa na kifo cha Rais ambaye ni Mgombea nafasi ya Urais; kwenye kampeni za uchaguzi mkuu. Kipi kifanyike? Au tuige Katiba ya Urusi ambayo Rais anaweza kuondoka Ikulu na akawa Waziri Mkuu na kurudi kuwa tena Rais Ikulu?
Kwani kuna wakati taifa linakosa Rais wa nchi ikiwa kwenye uchaguzi? Rais wa nchi anafahamika wakati wote wa uchaguzi labda Rais wa nchi akifa wakati wa uchaguzi - chama kinapewa muda gani wa kuchagua mgombea mwingine.
 
Issue sio majimbo issue ni population ya wakazi wake hiyo kanda ina theluthi ya wakazi wote na wanasiasa hawezi kupuuza hilo.
Zanzibar ina majimbo mengi lakin population yake kama wiilaya moja ya dar ambayo ni jimbo moja.
Siasa za majimbo zipo Marekani kila jimbo linapewa nguvu ya kupiga kura baada ya kura za wananchi ndio maana Trump alishinda.
Kanda yote ya ziwa ina wapiga kura kama 25% tu. Hiyo asilimia inamwongezea tu kura mgombea lakini haina uwezo wa kuamua mshindi.

Sijui kwa nini wakati wa Magufuli watu walidanganywa na kuaminishwa kuwa kanda ya Ziwa pekee inaweza kuamua juu ya kura za Rais. Ujinga ni mzigo.
 
Kwa upande wangu hili suala nililifikiria baada ya kuona nguvu kubwa Rais alikuwa nayo wakati na yeye pia ni mgombea. Mizani haikuwa sawa, nakumbuka kuna watu wakaibua hoja humu ya ulinzi na hata magari ya serikali yalipokuwa yanatumika kwenye kampeni. Hoja za wengine zilikuwa kwamba bado ni Rais!

Kwenye uhalisia wa mambo na yote tuliyoshuhudia, hivi Lissu angeshindwa kuendelea na kampeni wiki moja kabla ya uchaguzi, unadhani kweli uchaguzi ule ungesimamishwa hata kama sheria inatamka hivyo?

Mleta mada ana hoja ya msingi sana.
Mbona mwaka 2005 ulisimamishwa?
 
Mada Fikirishi

Katiba yetu inaongelea kifo cha Rais akiwa madarakani lakini haiongelei Mgombea Urais ambaye tayari ni Rais akifa akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mkuu. Natoa mfano ili uelewe kwa urahisi kwamba JPM angekufa akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mkuu Katiba haisemi kitu gani kifanyike zaidi tu ya kusema nafasi ya Rais itachukuliwa na Makamu wa Rais. Sasa yafuatayo hayana majibu ya Katiba:-

1. Je, kama Mgeombea Urais akifa kwenye kampeni za uchaguzi nafasi yake itajazwaje?

2. Je, Makamu wa Rais anayerithi kiti cha Rais ndiye atakuwa Mgombea nafasi ya Urais?

3. Je, atateuliwa mwingine na chama kujaza nafasi ya Mgombea Urais? Au atajaza nafasi ya Makamu wa Rais kwa kuwa Makamu wa Rais aliyekuwepo tayari amerithi kiti cha Rais na kuwa Rais?

4. Kama Makamu anayerithi kiti cha Rais siyo strong kushinda uchaguzi yaani siyo kipenzi cha wapiga kura wengi na kwamba akipewa kurithi pia nafasi ya Mgombea Urais aliyekufa kwenye kampeni huenda chama kikapoteza ushindi je, hapa chama au serikali iliyoko madarakani itamshusha Rais huyu (ambaye alikuwa Makamu zamani) toka kwenye kiti cha Rais ili arudi aendelee kugombea nafasi yake ile ile ya awali ya Makamu wa Rais aliyokuwa akigombea kabla Mgombea Urais (ambaye alikuwa Rais) kufa wakati wa kampeni za uchaguzi?

5. Je, hiyo siyo demotion/kushushwa cheo kwa Rais?

6. Je, Katiba inatoa maelekezo yoyote kuhusu demotion ya Rais toka kuwa Rais na kurudi kuwa Makamu wa Rais?

7. Japokuwa iko wenye Katiba kuhusu kifo cha Rais akiwa madarakani lakini kama taifa hatukujiandaa na kifo cha Rais akiwa madarakani, ni vivyo hivyo kumbe kwamba hata sasa kama taifa hatujajiandaa na kifo cha Rais ambaye ni Mgombea nafasi ya Urais; kwenye kampeni za uchaguzi mkuu. Kipi kifanyike? Au tuige Katiba ya Urusi ambayo Rais anaweza kuondoka Ikulu na akawa Waziri Mkuu na kurudi kuwa tena Rais Ikulu?
MIMI NINAVYOELEWA INAPOTOKEA RAIS ALIYEPO MADARAKANI AKIFA AKIWA KWENYE KAMPENI NI KWAMBA KWANZA TUELEWE KUWA RAIS KUWA KWENYE KAMPENI MAANA YAKE MUDA WAKE WA KUKAA MADARAKANI UMEISHA HIVYO IKITOKEA KIFO NI KWAMBA TUME YA UCHAGUZI ITASITISHA KAMPENI KWA WAGOMBEA URAIS TU (MAANA YAKE KAMPENI ZINGINE YA UBUNGE NA UDIWANI ZITAENDELEA) NA CHAMA HUSIKA ITAPEWA NAFASI YA KUTAFUTA MGOMBEA MWINGINE NA ASKISHAPATIKANA KAMPENI ZITAENDELEA KAMA KAWAIDA. kama kuna mwenye uelewa zaidi wa hayo mambo anaweza kutusaidia
 
Back
Top Bottom