Ukimya wa Katiba ya JMT Kuhusu Kifo cha Mgombea Urais

Mkuu kweli mada fikirishi!japo naona kama mpango wa kukatisha ndoto za hangaya 2025 ukawepo kwa wenye kinyongo cha kuondokewa na mpendwa wao!!kuna uzi humu uliletwa eti kanda ile italipa kisasi japo hatujui watalipa kwa nani!!!!!Labda ndio maana ulinzi wa hangaya umeimarishwa????!!!na hangaya kesha anza rasmi kampeni kule Arusha!!!!
Yani jamaa.hawaamini kuwa kuna kifo na kuna Mungu
Wanataka kumdhuru hangaya ili wawe na amani
Kwa Tabia zao za mauaji tunavishauri vyombo vya Usalama hususani TISS kuhakikisha wanazidisha ulinzi na intelligensia ya Rais
 
1. Je, kama Mgeombea Urais akifa kwenye kampeni za uchaguzi nafasi yake itajazwaje?

2. Je, Makamu wa Rais anayerithi kiti cha Rais ndiye atakuwa Mgombea nafasi ya Urais?
Mbona haya ni rahisi Sana.
Katiba yetu inasema "mtu atakoma kuwa rais siku ambayo rais mwingine atakpokula kiapo.

Sasa endapo JPM angekufa wakati wa kampeni 2020, Samia angechukua nafasi yake. Chama chake kingemtafuta VP kama walichofanya JPM alipokufa kweli.

Kuhusu nani angekuwa mgombea. Kampeni husitishwa kwa miezi mitatu. Halafu chama chake kingefanya mchakato wa kumpata mgombea kwa mujibu wa utaratibu wa chama chake
 
Hamna mada fikirishi hapa ni uvivu tu wenu wa kutafuta maarifa....mgombea urais akifariki kwenye kampeni zoezi zima linaitishwa upya Chama kitatakiwa kuteua mtu ambaye atakuja na mwenza wake.
Nakumbuka ilishatokea, nadhani uchaguzi wa 2010 mgombea urais wa chama fulani alifariki uchaguzi ukasimama.

Sijui kwann mleta mada hakutaka kupekuwa mitandaoni!
 
Mada Fikirishi

Katiba yetu inaongelea kifo cha Rais akiwa madarakani lakini haiongelei Mgombea Urais ambaye tayari ni Rais akifa akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mkuu. Natoa mfano ili uelewe kwa urahisi kwamba JPM angekufa akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mkuu Katiba haisemi kitu gani kifanyike zaidi tu ya kusema nafasi ya Rais itachukuliwa na Makamu wa Rais. Sasa yafuatayo hayana majibu ya Katiba:-

1. Je, kama Mgeombea Urais akifa kwenye kampeni za uchaguzi nafasi yake itajazwaje?

2. Je, Makamu wa Rais anayerithi kiti cha Rais ndiye atakuwa Mgombea nafasi ya Urais?

3. Je, atateuliwa mwingine na chama kujaza nafasi ya Mgombea Urais? Au atajaza nafasi ya Makamu wa Rais kwa kuwa Makamu wa Rais aliyekuwepo tayari amerithi kiti cha Rais na kuwa Rais?

4. Kama Makamu anayerithi kiti cha Rais siyo strong kushinda uchaguzi yaani siyo kipenzi cha wapiga kura wengi na kwamba akipewa kurithi pia nafasi ya Mgombea Urais aliyekufa kwenye kampeni huenda chama kikapoteza ushindi je, hapa chama au serikali iliyoko madarakani itamshusha Rais huyu (ambaye alikuwa Makamu zamani) toka kwenye kiti cha Rais ili arudi aendelee kugombea nafasi yake ile ile ya awali ya Makamu wa Rais aliyokuwa akigombea kabla Mgombea Urais (ambaye alikuwa Rais) kufa wakati wa kampeni za uchaguzi?

5. Je, hiyo siyo demotion/kushushwa cheo kwa Rais?

6. Je, Katiba inatoa maelekezo yoyote kuhusu demotion ya Rais toka kuwa Rais na kurudi kuwa Makamu wa Rais?

7. Japokuwa iko wenye Katiba kuhusu kifo cha Rais akiwa madarakani lakini kama taifa hatukujiandaa na kifo cha Rais akiwa madarakani, ni vivyo hivyo kumbe kwamba hata sasa kama taifa hatujajiandaa na kifo cha Rais ambaye ni Mgombea nafasi ya Urais; kwenye kampeni za uchaguzi mkuu. Kipi kifanyike? Au tuige Katiba ya Urusi ambayo Rais anaweza kuondoka Ikulu na akawa Waziri Mkuu na kurudi kuwa tena Rais Ikulu?
Akifa nafasi ya Rais itajazwa na Makamu na swala la ugombea wake litasimamiwa na sheria ya tume ya Uchaguzi ambapo chama kitateua mwingine na siku za kampeni kuongezwa

2010 Mgombea Mwenza wa Dr Slaa Mzee Jumbe alifariki tarehe ya Uchaguzi ikasogezwa mbele kwa siku kadhaa

Sent from my TECNO P704a using JamiiForums mobile app
 
Mkuu, naomba nikusaidie maana unachanganya mambo mawili. Mambo unayochanganya moja linahusu kumpata Rais endapo Rais amefariki, pili ni kumpata mgombea wa kiti cha Rais endapo mgombea amefariki wakati wa Kampeni.

Ikiwa Rais mfano Magufuri angefariki wakati wa Kampeni ( wakati wa kugombea muhala wake wa pili) ,yafuatayo yangefanyika. Kwa kuwa kiti cha Rais kingebaki wazi utaratibu wa kujaza nafasi ya Rais ungefanyika yahani makamu wa Rais angeapishwa kuwa Rais wa nchi.

Pili,kwa kuwa chama cha mapinduzi (CCM) kingekuwa kimepoteza mgombea sharia ya uchaguzi inataka chama kilichopoteza mgombea kujaza ( kuteua) mgombea ndani ya wiki mbili,alafu mchakato wa uchaguzi ungeendelea.

Kutokana na utaratibu huo, ingebaki utashi wa CCM kuamua kama Samia S.Hassan ateuliwe kuwa mgombea au wateue mwingine. Hivyo katiba katika hilo haijanyamaza, tatizo ni wewe na watu wa aina yako kutokutofautisha mambo ya serikali na yale ya CCM kama chama.

Baada ya ufafanuzi huu wa chumla nitakuwa najibu hoja zako mojamoja.


Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
Kwa upande wangu hili suala nililifikiria baada ya kuona nguvu kubwa Rais alikuwa nayo wakati na yeye pia ni mgombea. Mizani haikuwa sawa, nakumbuka kuna watu wakaibua hoja humu ya ulinzi na hata magari ya serikali yalipokuwa yanatumika kwenye kampeni. Hoja za wengine zilikuwa kwamba bado ni Rais!

Kwenye uhalisia wa mambo na yote tuliyoshuhudia, hivi Lissu angeshindwa kuendelea na kampeni wiki moja kabla ya uchaguzi, unadhani kweli uchaguzi ule ungesimamishwa hata kama sheria inatamka hivyo?

Mleta mada ana hoja ya msingi sana.
 
Mkuu, naomba nikusaidie maana unachanganya mambo mawili. Mambo unayochanganya moja linahusu kumpata Rais endapo Rais amefariki, pili ni kumpata mgombea wa kiti cha Rais endapo mgombea amefariki wakati wa Kampeni.

Ikiwa Rais mfano Magufuri angefariki wakati wa Kampeni ( wakati wa kugombea muhala wake wa pili) ,yafuatayo yangefanyika. Kwa kuwa kiti cha Rais kingebaki wazi utaratibu wa kujaza nafasi ya Rais ungefanyika yahani makamu wa Rais angeapishwa kuwa Rais wa nchi.

Pili,kwa kuwa chama cha mapinduzi (CCM) kingekuwa kimepoteza mgombea sharia ya uchaguzi inataka chama kilichopoteza mgombea kujaza ( kuteua) mgombea ndani ya wiki mbili,alafu mchakato wa uchaguzi ungeendelea.

Kutokana na utaratibu huo, ingebaki utashi wa CCM kuamua kama Samia S.Hassan ateuliwe kuwa mgombea au wateue mwingine. Hivyo katiba katika hilo haijanyamaza, tatizo ni wewe na watu wa aina yako kutokutofautisha mambo ya serikali na yale ya CCM kama chama.

Baada ya ufafanuzi huu wa chumla nitakuwa najibu hoja zako mojamoja.


Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
Kww msingi huu hata wanaodai katiba wanafuata tu mkumbo maana hata hii iliyoo hawaifahamu kabisa
 
Kigoma na Tabora ziko Kanda ya Magharibi.
Kanda ya Ziwa na idadi ya Majimbo yake:-
1. Mara - 7
2. Mwanza - 7
3. Geita - 6
4. Kagera - 9
5. Shinyanga - 6
6. Simiyu - 7
Point of correction
Mkoa wa Mwanza majimbo yake ya uchaguzi ni 9 na sio 7. Wilaya ndio 7.
Hapa chini nimeainisha majimbo ya uchaguzi mkoani Mwanza.
1. Nyamagana
2. Ilemela
3. Magu
4. Sengerema
5. Buchosa (Wilayani Sengerema)
6. Ukerewe
7. Kwimba
8. Sumve (Wilayani Kwimba)
9. Misungwi
Ikumbukwe, Mwanza ina Wilaya 7 kati ya hizo Sengerema na Kwimba zina majimbo mawili kila mmoja..

Kama Zanzibar wanaingiza wabunge 50; kwa size ya eneo na idadi ya wakazi wa Z'bar, hao jamaa wanapiga bao kweli kweli
 
Mada Fikirishi

Katiba yetu inaongelea kifo cha Rais akiwa madarakani lakini haiongelei Mgombea Urais ambaye tayari ni Rais akifa akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mkuu. Natoa mfano ili uelewe kwa urahisi kwamba JPM angekufa akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mkuu Katiba haisemi kitu gani kifanyike zaidi tu ya kusema nafasi ya Rais itachukuliwa na Makamu wa Rais. Sasa yafuatayo hayana majibu ya Katiba:-

1. Je, kama Mgeombea Urais akifa kwenye kampeni za uchaguzi nafasi yake itajazwaje?

2. Je, Makamu wa Rais anayerithi kiti cha Rais ndiye atakuwa Mgombea nafasi ya Urais?

3. Je, atateuliwa mwingine na chama kujaza nafasi ya Mgombea Urais? Au atajaza nafasi ya Makamu wa Rais kwa kuwa Makamu wa Rais aliyekuwepo tayari amerithi kiti cha Rais na kuwa Rais?

4. Kama Makamu anayerithi kiti cha Rais siyo strong kushinda uchaguzi yaani siyo kipenzi cha wapiga kura wengi na kwamba akipewa kurithi pia nafasi ya Mgombea Urais aliyekufa kwenye kampeni huenda chama kikapoteza ushindi je, hapa chama au serikali iliyoko madarakani itamshusha Rais huyu (ambaye alikuwa Makamu zamani) toka kwenye kiti cha Rais ili arudi aendelee kugombea nafasi yake ile ile ya awali ya Makamu wa Rais aliyokuwa akigombea kabla Mgombea Urais (ambaye alikuwa Rais) kufa wakati wa kampeni za uchaguzi?

5. Je, hiyo siyo demotion/kushushwa cheo kwa Rais?

6. Je, Katiba inatoa maelekezo yoyote kuhusu demotion ya Rais toka kuwa Rais na kurudi kuwa Makamu wa Rais?

7. Japokuwa iko wenye Katiba kuhusu kifo cha Rais akiwa madarakani lakini kama taifa hatukujiandaa na kifo cha Rais akiwa madarakani, ni vivyo hivyo kumbe kwamba hata sasa kama taifa hatujajiandaa na kifo cha Rais ambaye ni Mgombea nafasi ya Urais; kwenye kampeni za uchaguzi mkuu. Kipi kifanyike? Au tuige Katiba ya Urusi ambayo Rais anaweza kuondoka Ikulu na akawa Waziri Mkuu na kurudi kuwa tena Rais Ikulu?
Hii ni mada fikirishi ila katiba imetoa mwongozo mzuri, na tunaweza kuchukua two cases kama rejea.

Kama 2015 mgombea wa urais wa CCM angefariki maana yake JK angeendelea kuwa seating president na CCM walikuwa na nafasi ya kuamua SSH agombee kama Rais dhidi ya EL wa CDM au CCM wangekuwa na mikutano maalumu ya CC, NEC na Mkutano mkuu kuona nani angeweza kusimama na EL na wengine waliokuwa kwenye game.

2005 aliekuwa mgombea wa makamu wa Rais kwa CDM alifariki katikati ya race, uchaguzi ulisogezwa mbele na Rais Mkapa aliendelea ku-govern majuma kadhaa mpaka uchaguzi ulipofanyika na JK kuapishwa Nov badala ya late October kama ilivyokuwa huko nyuma.

Kama ingetokea JPM aliekuwa seating president akafariki katikati ya race 2020, maana yake SSH alitakiwa kuapishwa ili kumalizia muda wa JPM mpaka the next president atakapopatikana kwenye uchaguzi wa 2020. Pengine CCM wangepima maji kama SSH ambae ni angekuwa seating President kama angeweza kuchuana na TL, BKM na wengine au wangelazimika kuitisha mkutano mikutano maalum ya CC, NEC na Mkutano mkuu ili wateue mgombea ambae wanaona anaweza kuwavusha kwa wapiga kura.

Nadhani hoja hii inafikirisha na tuombeaneni uzima na afya njema kati yetu; ikitokea kuna kudra za mwenyezi Mungu, basi vingunge kwenye vyama husika wangeamua nini kifanyike.
 
Point of correction
Mkoa wa Mwanza majimbo yake ya uchaguzi ni 9 na sio 7. Wilaya ndio 7.
Hapa chini nimeainisha majimbo ya uchaguzi mkoani Mwanza.
1. Nyamagana
2. Ilemela
3. Magu
4. Sengerema
5. Buchosa (Wilayani Sengerema)
6. Ukerewe
7. Kwimba
8. Sumve (Wilayani Kwimba)
9. Misungwi
Ikumbukwe, Mwanza ina Wilaya 7 kati ya hizo Sengerema na Kwimba zina majimbo mawili kila mmoja..

Kama Zanzibar wanaingiza wabunge 50; kwa size ya eneo na idadi ya wakazi wa Z'bar, hao jamaa wanapiga bao kweli kweli
Your point of correction taken. Kwahiyo ni Majimbo 43 kwa 222.
 
Makamu wa Rais angekula kiapo kuwa Rais, baada ya hapo kwa kushauriana na chama chake angemteua makamu wa Rais.

Chama cha mgombea aliyefariki ambaye pia alikuwa Rais,kingependekeza mgombea mwingine wa kiti cha Urais. Kwa utashi wa chama husika wangeweza kumpendekeza Rais aliyekula kiapo ( yahani aliyekuwa makamu wa Rais) ama wangependekeza jina la mwanachama mwingine kuwa mgombea wao.

Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
Good solution kichama, ila Katiba ya nchi iko silent.
 
Hili litabaki utashi wa chama na mgombea wanayemtaka wao. Wanaweza kuamua kumpendekeza Rais aliyerithi kiti cha Urais kilichoachwa wazi au kumpendekeza mwanachama Mwingine.Katiba yetu haijamzuia Mtu yeyote aliyewahi kuwa rais, kushikilia Wadhifa au nyadhifa zingine. Imeweka ukomo tu wa kuwa Rais Kwa muda husiozidi mihula miwili ya miaka mitano Kitano.Ndiyo maana tuna marais wastaafu anbao ni wakuu wa vyuo.




Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
Mkuu, majibu yako yana mashiko. Rais mstaafu anaweza kushika nyadhifa zingine lakini siyo za ndani ya Ikulu au Cabinet siyo?.
 
Mbona haya ni rahisi Sana.
Katiba yetu inasema "mtu atakoma kuwa rais siku ambayo rais mwingine atakpokula kiapo.

Sasa endapo JPM angekufa wakati wa kampeni 2020, Samia angechukua nafasi yake. Chama chake kingemtafuta VP kama walichofanya JPM alipokufa kweli.

Kuhusu nani angekuwa mgombea. Kampeni husitishwa kwa miezi mitatu. Halafu chama chake kingefanya mchakato wa kumpata mgombea kwa mujibu wa utaratibu wa chama chake
Mkuu, akishaonja utamu wa asali atakubali kuachia kirahisi bila shinikizo la Katiba? Ukumbuke amepewa mamlaka ya kuamuru majeshi.
 
Akifa nafasi ya Rais itajazwa na Makamu na swala la ugombea wake litasimamiwa na sheria ya tume ya Uchaguzi ambapo chama kitateua mwingine na siku za kampeni kuongezwa

2010 Mgombea Mwenza wa Dr Slaa Mzee Jumbe alifariki tarehe ya Uchaguzi ikasogezwa mbele kwa siku kadhaa

Sent from my TECNO P704a using JamiiForums mobile app
Mkuu umekurupuka kujibu kitu ambacho hakijaulizwa na mfano wako hauna mzani mlinganyo

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Akifa nafasi ya Rais itajazwa na Makamu na swala la ugombea wake litasimamiwa na sheria ya tume ya Uchaguzi ambapo chama kitateua mwingine na siku za kampeni kuongezwa

2010 Mgombea Mwenza wa Dr Slaa Mzee Jumbe alifariki tarehe ya Uchaguzi ikasogezwa mbele kwa siku kadhaa

Sent from my TECNO P704a using JamiiForums mobile app
Mkuu, atakubali kuwa rais kwa siku hizo chache tu? Wakati anaamuru majeshi? Na pia anayo mamlaka ya kufuta/kuahirisha uchaguzi? Hapa ndiyo maana tunatafuta kujuwa Katiba inasema nini ili haya yasije kutokea.
 
Umeleta mada muhimu saaana. Nakumbuka kuwaza hili jambo kipindi cha Uchaguzi wa 2020.

Sheria kama hii haitakiwi kubagua akifariki 'fulani' itakuwaje. Inatakiwa iseme tu ikitokea amefariki mgombea urais wa chama chochote, awe ndiye anashikilia Urais wakati huo au wa chama kidogo sana asiye hata na jina, utaratibu unakuwaje.

Kwa utaratibu uliopo sasa, mfano angefariki mgombea Urais wa chama kidogo uchaguzi wa 2020, maana tulikuwa na wagombea zaidi ya 20, kuna uwezekano mkubwa kuwa uchaguzi ungeendelea. Ila kama ingekuwa inamuhusu mgombea wa CCM tena akiwa na upinzani mkali kama tuliokuwa nao wakati ule, uchaguzi ungeahirishwa. Hili linakuwa siyo sawa kisheria. Sheria haitakiwi kubagua nani amedhurika ifanyeje kazi. Ni moja ya sababu nyingine ya kuifumua upya Katiba yetu badala ya kuziba viraka.
Mwaka 2005 mgombea mwenza wa Freeman Mbowe alifariki dunia zikiwa zimebaki siku 15 uchaguzi kufanyika.

Uchaguzi ulisimama kwa siku 28 kwa chama kuteua mgombea mwenza mwingine kisha tukaendelea na kampeni kama ilivyoada.

Kama unakumbuka uchaguzi wa 2005 haukufanyika October kama ilivyozoeleka.
 
Umeleta mada muhimu saaana. Nakumbuka kuwaza hili jambo kipindi cha Uchaguzi wa 2020.

Sheria kama hii haitakiwi kubagua akifariki 'fulani' itakuwaje. Inatakiwa iseme tu ikitokea amefariki mgombea urais wa chama chochote, awe ndiye anashikilia Urais wakati huo au wa chama kidogo sana asiye hata na jina, utaratibu unakuwaje.

Kwa utaratibu uliopo sasa, mfano angefariki mgombea Urais wa chama kidogo uchaguzi wa 2020, maana tulikuwa na wagombea zaidi ya 20, kuna uwezekano mkubwa kuwa uchaguzi ungeendelea. Ila kama ingekuwa inamuhusu mgombea wa CCM tena akiwa na upinzani mkali kama tuliokuwa nao wakati ule, uchaguzi ungeahirishwa. Hili linakuwa siyo sawa kisheria. Sheria haitakiwi kubagua nani amedhurika ifanyeje kazi. Ni moja ya sababu nyingine ya kuifumua upya Katiba yetu badala ya kuziba viraka.
Mwaka 2005 mgombea mwenza wa Freeman Mbowe alifariki dunia zikiwa zimebaki siku 15 uchaguzi kufanyika.

Uchaguzi ulisimama kwa siku 28 kwa chama kuteua mgombea mwenza mwingine kisha tukaendelea na kampeni kama ilivyoada.

Kama unakumbuka uchaguzi wa 2005 haukufanyika October kama ilivyozoeleka.

Ila ccm walitumia mwanya huo kutoa rushwa hatari kwenye zile kampeni za nyumba kwa nyumba zilizaliwa hapa, ccm walikuwa walipita majumbani mwa watu usiku wakigawa chupi, kanga, viberiti, chumvi, mafuta ya kula na 5000
 
Back
Top Bottom