Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,577
Hebu someni hapa na hii inatia wazimu kuwa kwa kuwa jeshi lina nguvu hivyo linaamua kuwafanyia watanzania wenzetu majaribio bila hata ya kupata vibali huu ni ufisadi wa hali ya juu.
Mbunge wa upinzani aibua kashfa nyingine nzito bungeni kuhusu ukimwi
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MBUNGE wa Karatu (Chadema), Dk Willibroad Slaa, ameibua kashfa nyingine inayomhusisha Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) mstaafu, kwamba hospitali yake ilihusika kufanya utafiti wa dawa za ugonjwa wa Ukimwi iliyotengenezwa Afrika Kusini, licha ya serikali kuzuia utafiti huo.
Bila kutaja jina la IGP huyo aliyehusika katika sakata hilo, Dk Slaa alitaka kujua kauli ya serikali kuhusu suala hilo na chombo kilichohusika kutoa kibali cha majaribio hayo kufanyika Hosptiali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo na kuhusisha Watanzania 64.
Naibu Waziri wa Afya, Dk Aisha Kigoda katika jibu lake alisema hakuna taasisi yoyote ya serikali iliyowahi kutoa kibali cha kufanya utafiti wa dawa za Ukimwi kutoka Afrika Kusini.
Dk Kigoda alisema, kumbukumbu zinaonyesha ombi la kibali cha kufanya utafiti liliwasilishwa NIMR mwaka 2000, lakini baada ya tathmini serikali ilikataa ombi hilo kutokanana maombi ya utafiti huo kuwa na upungufu mkubwa wa sayansi na maadili.
Alisema utafiti huo umefanywa kinyume cha taratibu za utafiti kwa sababu sio serikali wala Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Tume ya Sayansi na Teknolojia (CoSTECH) waliohusika na utoaji wa kibali cha utafiti huo.
Hata hivyo, Dk Kigoda alisema kwa sasa serikali imesimamisha utafiti huo, kuzuia uingizaji dawa pia kuzirejesha Afrika Kusini.
Alisema suala hilo ni kosa la jinai na kwamba, wananchi wana haki kufuata mkondo wa sheria kudai fidia kwa kuhusishwa na utafiti huo ambao hauna baraza za serikali.
Hata hivyo, Waziri Kigoda alisema baada ya serikali kufanya mazungumzo na viongozi wa JWTZ, taarifa zilionyesha kukataa kuhusika na kuwezesha kufanyika kwa utafiti huo.
Naibu Waziri huyo alisema, wizara yake inajitahidi kuongeza uwezo wa TDFA na NIMR,
kuchunguza tafiti mbalimbali zinazofanywa nchini kuhusiana na dawa na magonjwa ili
kuhakikisha zinafanywa kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo.
source;mwananchi.
Mbunge wa upinzani aibua kashfa nyingine nzito bungeni kuhusu ukimwi
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MBUNGE wa Karatu (Chadema), Dk Willibroad Slaa, ameibua kashfa nyingine inayomhusisha Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) mstaafu, kwamba hospitali yake ilihusika kufanya utafiti wa dawa za ugonjwa wa Ukimwi iliyotengenezwa Afrika Kusini, licha ya serikali kuzuia utafiti huo.
Bila kutaja jina la IGP huyo aliyehusika katika sakata hilo, Dk Slaa alitaka kujua kauli ya serikali kuhusu suala hilo na chombo kilichohusika kutoa kibali cha majaribio hayo kufanyika Hosptiali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo na kuhusisha Watanzania 64.
Naibu Waziri wa Afya, Dk Aisha Kigoda katika jibu lake alisema hakuna taasisi yoyote ya serikali iliyowahi kutoa kibali cha kufanya utafiti wa dawa za Ukimwi kutoka Afrika Kusini.
Dk Kigoda alisema, kumbukumbu zinaonyesha ombi la kibali cha kufanya utafiti liliwasilishwa NIMR mwaka 2000, lakini baada ya tathmini serikali ilikataa ombi hilo kutokanana maombi ya utafiti huo kuwa na upungufu mkubwa wa sayansi na maadili.
Alisema utafiti huo umefanywa kinyume cha taratibu za utafiti kwa sababu sio serikali wala Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Tume ya Sayansi na Teknolojia (CoSTECH) waliohusika na utoaji wa kibali cha utafiti huo.
Hata hivyo, Dk Kigoda alisema kwa sasa serikali imesimamisha utafiti huo, kuzuia uingizaji dawa pia kuzirejesha Afrika Kusini.
Alisema suala hilo ni kosa la jinai na kwamba, wananchi wana haki kufuata mkondo wa sheria kudai fidia kwa kuhusishwa na utafiti huo ambao hauna baraza za serikali.
Hata hivyo, Waziri Kigoda alisema baada ya serikali kufanya mazungumzo na viongozi wa JWTZ, taarifa zilionyesha kukataa kuhusika na kuwezesha kufanyika kwa utafiti huo.
Naibu Waziri huyo alisema, wizara yake inajitahidi kuongeza uwezo wa TDFA na NIMR,
kuchunguza tafiti mbalimbali zinazofanywa nchini kuhusiana na dawa na magonjwa ili
kuhakikisha zinafanywa kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo.
source;mwananchi.