robinson crusoe
JF-Expert Member
- Oct 22, 2020
- 740
- 1,214
Watu hawa tumewadekeza sana na wanazidi kuwa wezi na mafisadi siku hadi siku.
Mwinyi alikuwa na matatizo ya kuuza Loliondo bila aibu na maeneo ya wazi Dar yakachukuliwa. Mkapa akauza viwanda hovyo hovyo na kujiuzia yeye mwenyewe pia, akagawa Tanesco kwa Netgroup solutions ya SA, akagawa ATC kwa SA, migodi ikapewa watu, tukasikia ana hotel SA. Kikwete akaja kutia fola na IPTL, escrow aliyoonesha ushenzi eti siyo pesa za serikali, twiga wakauzwa uarabuni, TRC ikauzwa kwa wahindi, rada na chenji yake ikapotea, ukodishaji wa ndege, Bandari ya bagamoyo, n.k.
Magufuli haijaeleweka sana ni nini alichojineemesha. wengi wanasema Chato Chato lakini ujenzi wa chato kwa upendeleo, iwe airport, iwe hospitali, iwe Burigi N.P, vyote hivi ni vya serikali na wananchi na vimebaki tunaviona. Hawa wengine walijineemesha wao binafsi.
Sasa amekuja Samia ameanza kunadi Bagamoyo kwa nguvu zote, anawaachia mafisadi kama akina Singh kwa bei ya chini kuliko pesa walizo pora. Mwaka haujaisha lakini ni ishara kwamba yajayo yanafurahisha. Sidhani kama muda wa siku 100 ulimtosha kufahamu undani wa mradi na niya njema au mbaya juu ya mradi huu.
Naweza kuhisi kwa 70% kwamba ameambiwa na wanaofahamu mradi ili aendelee, wafaidi. Wananchi anawapoza kwa kuwaambia analeta uhuru na demokrasia. Huu ni mtindo wa Mobutu alivyowaachia wakongo kucheza ndombolo yeye akipora.
Mwinyi alikuwa na matatizo ya kuuza Loliondo bila aibu na maeneo ya wazi Dar yakachukuliwa. Mkapa akauza viwanda hovyo hovyo na kujiuzia yeye mwenyewe pia, akagawa Tanesco kwa Netgroup solutions ya SA, akagawa ATC kwa SA, migodi ikapewa watu, tukasikia ana hotel SA. Kikwete akaja kutia fola na IPTL, escrow aliyoonesha ushenzi eti siyo pesa za serikali, twiga wakauzwa uarabuni, TRC ikauzwa kwa wahindi, rada na chenji yake ikapotea, ukodishaji wa ndege, Bandari ya bagamoyo, n.k.
Magufuli haijaeleweka sana ni nini alichojineemesha. wengi wanasema Chato Chato lakini ujenzi wa chato kwa upendeleo, iwe airport, iwe hospitali, iwe Burigi N.P, vyote hivi ni vya serikali na wananchi na vimebaki tunaviona. Hawa wengine walijineemesha wao binafsi.
Sasa amekuja Samia ameanza kunadi Bagamoyo kwa nguvu zote, anawaachia mafisadi kama akina Singh kwa bei ya chini kuliko pesa walizo pora. Mwaka haujaisha lakini ni ishara kwamba yajayo yanafurahisha. Sidhani kama muda wa siku 100 ulimtosha kufahamu undani wa mradi na niya njema au mbaya juu ya mradi huu.
Naweza kuhisi kwa 70% kwamba ameambiwa na wanaofahamu mradi ili aendelee, wafaidi. Wananchi anawapoza kwa kuwaambia analeta uhuru na demokrasia. Huu ni mtindo wa Mobutu alivyowaachia wakongo kucheza ndombolo yeye akipora.