Ukimshitaki Mzigua mkapelekana hadi Mahakamani, uwezekano wa Kushinda kesi ni zero percent

Kwa hio yasipokukuta wewe means wengine hayawakuti au hayapo kabisa?

we jamaa una masikhara! mi nimeishi Tanga mzee naandika vitu najua!

Ishu za zongo nazijua sana
ishu za vibwengo nazijua sana na vibwengo nishakutana navyo sana huko milima ya usambara korogwe huko

waulize wanaotokea mashewa huko kwa shambalai watakwambia!

waulize watanga watakwambia Maji Marefu ni nani...

kaka hujafa hujaumbika! kua uyaone
Ishi maisha yako acha kukariri mambo,
 
Wachawi na waganga walikuwa wa zamani..sahivi miyeyusho tu

Waganga wa sahavi nikama madalali wa kariakoo. Wanawaza pesa na kuibia watu.

Kuwa makini uchawi upo
Dawa za asili zipo
Waganga wa kweli wapo

Yotekwa yote MUNGU ndio nguvu kuu kuliko zote. Na ndiko amani na utulivu wa nafsi na moyo unapatikana
 
Huyu kaja kwa nia ya kusoma upepo ili baadae washikaji zake wasapoti alafu ageuke kwa kujifanya anaweza kuwasaidia wenye matatizo. Sasa tunamkata upepo mapema
Wanasimuliana kijiweni uwongo huku wakipata kahawa
 
Kuamini story za kusadikika za uchawi ni upungufu wa akili.
 
Vitu vingine ni uwongo kabisa mimi niliwahi fanya kazi Handeni kipindi hicho niliishi nao vizuri mno maana hakuna sehemu tutakwazana...na walikuwa wananipa dili za kupata mbao kwa bei nzuri nikitaka kwenda daslm kusalimia familia kuku wa kumwaga mpaka mbuzi kwa bei ya chini kabisa ishi na jamii vizuri upate matunda...
 
Endeleeni kulishana matango pori na imani zenu za giza, mwaka 2013 nilienda kununua shamba huko, nilibahatika kupata ekari 50, baada ya kununua nilianza kusikia tetesi kwamba hautokaa ulime, na hata ukilima hautovuna, kwamba utaona mahindi yamebeba lakini ukivuna hupati kitu, au yataliwa na mchwa yote.
Sikuwasikiliza nikajaribu kulima kwanza ekari 10, nikafanikiwa kuvuna nimeendelea hivo na kwa sasa nalima mpka ekari 60, ikitokea mwaka umekuwa mbaya ni kwa sababu ya hali ya hewa na si uchawi.
Ikitokea mchwa umeibuka unadeal nao kwa madawa.
Kujidanganya eti mziguwa hashindwi kesi ni uwezo mdogo wa kufikiri ukichangiwa na makuzi uliokulia yanayoamini ktk waganga wa kienyeji.

Ulibahatika kununua shamba heka 50 ila kwa sasa umefanikiwa unalima “mpaka heka 60”....

Sawa.
 
Back
Top Bottom