Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,337
- 51,852
Kwema Wakuu!
Nisikilize mke wangu, nisikilize vizuri Kabisa, sipo hapa kumwakilisha yeyote Yule isipokuwa Nafsi yangu na Yule aliyenipa Nafsi hii. Usiniangalie Kwa macho yako mabaya Kama ya Kondoo, Kama ukijua ukilazimisha kuniacha na kuwachukua watoto kimabavu kaa ukijua kabisa Kwanza hatutarudiana. Sitaki uwe na shida wala Mimi sitaki niwe na shida ya kurudiana na wewe!
Sitakuhudumia wewe na hao watoto wako Kwa sababu ulinikimbia mwenyewe kwa kiburi chako.
Usiseme ni watoto wangu, nimewakataa pamoja na wewe mama Yao.
Kama mama Yao ulikuwa mjinga hivi na kiburi hata hao watoto sitaki watambulike Kwa jina langu. Nimewakataa tangu Leo hii.
Wala hautahesabika ulikuwa mke wangu, na hao watoto watakuwa wako. Nao watakuwa watoto wasio na Baba, Kwa sababu mama Yao ulikuwa Shetani wa mapangoni uliyejificha katika nyumba yangu.
Nawe ulipojipandisha ukaona utaweza kuwalea mwenyewe, ukaleta mambo ya wanawake makahaba katika nyumba yangu. Mimi Taikon mumeo nitakufukuza wala sitakuonea huruma.
Nami upendo wangu nitauhifadhi uwe akiba Kwa malkia wa Tibeli, hiyo ndiye ataumiliki, naye atatawala Enzi yangu. Nani nitampa yote niliyokuwa nimekupa wewe, tena nitampa nyongeza ya Yale niliyokupunja na kukunyima.
Kwa maana nafasi ya mwanamke Mpumbavu itachukuliwa na Mwanamke mwenye busara.
Nao hao watoto watageuka kumbikumbi watokao kwenye kichuguu, watakuacha mwenyewe ukitanga tanga mpaka utakapoangamia.
Enyi wanangu, iweni na roho za kiume ili mpate kuheshimika na watu wenye heshima, wala msitafute kuheshimiwa na watu wapuuzi! Msitake utukufu Kwa kila mtu isipokuwa watu wa maana ambao wanajua thamani ya Baba.
Ila msisahau kutenda Kama wababa waaminifu mkitenda haki Kwa wenye haki. Na ubaya Kwa waliowabaya.
Nipumzike sasa!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Nisikilize mke wangu, nisikilize vizuri Kabisa, sipo hapa kumwakilisha yeyote Yule isipokuwa Nafsi yangu na Yule aliyenipa Nafsi hii. Usiniangalie Kwa macho yako mabaya Kama ya Kondoo, Kama ukijua ukilazimisha kuniacha na kuwachukua watoto kimabavu kaa ukijua kabisa Kwanza hatutarudiana. Sitaki uwe na shida wala Mimi sitaki niwe na shida ya kurudiana na wewe!
Sitakuhudumia wewe na hao watoto wako Kwa sababu ulinikimbia mwenyewe kwa kiburi chako.
Usiseme ni watoto wangu, nimewakataa pamoja na wewe mama Yao.
Kama mama Yao ulikuwa mjinga hivi na kiburi hata hao watoto sitaki watambulike Kwa jina langu. Nimewakataa tangu Leo hii.
Wala hautahesabika ulikuwa mke wangu, na hao watoto watakuwa wako. Nao watakuwa watoto wasio na Baba, Kwa sababu mama Yao ulikuwa Shetani wa mapangoni uliyejificha katika nyumba yangu.
Nawe ulipojipandisha ukaona utaweza kuwalea mwenyewe, ukaleta mambo ya wanawake makahaba katika nyumba yangu. Mimi Taikon mumeo nitakufukuza wala sitakuonea huruma.
Nami upendo wangu nitauhifadhi uwe akiba Kwa malkia wa Tibeli, hiyo ndiye ataumiliki, naye atatawala Enzi yangu. Nani nitampa yote niliyokuwa nimekupa wewe, tena nitampa nyongeza ya Yale niliyokupunja na kukunyima.
Kwa maana nafasi ya mwanamke Mpumbavu itachukuliwa na Mwanamke mwenye busara.
Nao hao watoto watageuka kumbikumbi watokao kwenye kichuguu, watakuacha mwenyewe ukitanga tanga mpaka utakapoangamia.
Enyi wanangu, iweni na roho za kiume ili mpate kuheshimika na watu wenye heshima, wala msitafute kuheshimiwa na watu wapuuzi! Msitake utukufu Kwa kila mtu isipokuwa watu wa maana ambao wanajua thamani ya Baba.
Ila msisahau kutenda Kama wababa waaminifu mkitenda haki Kwa wenye haki. Na ubaya Kwa waliowabaya.
Nipumzike sasa!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam