Ukikuta minyoo kwenye haja kubwa, tatizo ni nini?

baghozed

JF-Expert Member
May 26, 2011
532
96
Habari zenu wana JF,ningependa kujua kama ukikuta mnyoo katika haja kubwa ni tatizo gani?na linasabababishwa na nini?na tiba yake ni nini?
 
Imeandikwa na: Dr.Henry Mayala Jr Mnamo: Mar 29
Mojawapo ya tatizo linaloathiri jamii katika nchi nyingi zinazoendelea ikiwemo Tanzania ni magonjwa yanayohusiana na minyoo. Duniani kwa ujumla, takribani watu billion moja wameripotiwa kuwa na uvamizi wa minyoo aina ya helminthes kwenye miili yao.​
Minyoo huenezwa kwa njia zipi?​
Minyoo huenezwa pale maji au chakula vinapokuwa vimeathiriwa na mayai au mabuu ya minyoo. Hali kadhalika, uwezekano wa kupata minyoo huchangiwa pia na kutonawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka kujisaidia haja kubwa. Aidha watoto wadogo chini ya miaka mitano ambao hupenda kuchezea mchanga au uchafu kwa ujumla na ambao hupendelea pia kunyonya vidole nao pia huambukizwa kwa urahisi. Mambo mengine yanayochangia katika kupata uvamizi wa minyoo ni pamoja na kuishi katika mazingira machafu, kutembea bila viatu (pekupeku) na kula vyakula ambavyo havijaiva au visivyopikwa vizuri (undercooked foods).​
Aina za minyoo na madhara yake kwa binadamu​
Kuna aina kadhaa za minyoo ambazo, ukiachilia mbali kuwashambulia wanyama wengine kama ngombe, nguruwe, mbuzi na kondoo, humshambulia pia binadamu. Aina hizi ni pamoja na​
  • Minyoo jamii ya round worms kwa mfano Ascaris lumbricoides ambao husababisha utumbo kuziba (intestinal obstruction) au uambukizi katika kidole tumbo (appendicitis)
  • Minyoo jamii ya hook worms kwa mfano Ancylostoma duodenale ambao huishi kwa kunyonya damu kwenye utumbo mdogo na hivyo kusababisha upungufu wa damu mwilini.
  • Minyoo jamii ya pin worms au thread worm kwa mfano Enterobius vermicularishusababisha kuwashwa hasa sehemu za haja kubwa kwa sababu ya mcharuko mwili unaotokana na minyoo hii kutoa mayai yao eneo hilo hasa kipindi cha usiku.
  • Minyoo jamii ya whip worms kwa mfano Trichuris trichiura husababisha kinyesi kuchanganyika na damu, kupungua uzito, upungufu wa damu na kutoka nje kwa puru (rectal prolapse).
  • Minyoo jamii ya tegu (tape worms) kama vile Taenia solium husababisha kifafa pindi wanapovamia ubongo hasa katika hatua ya ukuaji iitwayo cystercosis
Dalili za minyoo ni zipi?​
Minyoo-dalili-150x150.jpg
Dalili za kuwepo kwa uvamizi wa minyoo mwilini hutegemea sana aina ya minyoo inayomuathiri mgonjwa. Lakini kwa ujumla, dalili ni pamoja na​
  • Maumivu ya tumbo
  • Kupata choo kigumu sana
  • Kuharisha
  • Kujisikia mchovu na mlegevu kutokana na kupungukiwa damu
  • Kupoteza hamu ya kula
  • Tumbo kuwa na gesi na kuhisi limejaa
  • Kukohoa na kupiga chafya
  • Kwa watoto kusugua meno, kujipinduapindua pamoja na kujikojolea kitandani
  • Kichwa kuuma au kupata kifafa kama minyoo (jamii ya taenia solium) ikitaga mayai yake kwenye ubongo
  • Kuwashwa, na
  • Huathiri ukuaji kwa watoto
Utatambuaje kama umeathiriwa na minyoo?​
Vipimo vinavyoweza kusaidia kugundua uvamizi wa minyoo, aina zake na hata madhara yaliyosababishwa na minyoo ni pamoja na:​
  • Kupima choo kikubwa (Stool examination) kwa ajili ya kuchunguza mayai na mabuu ya minyoo iliyo katika haja kubwa kwa kutumia darubini
  • Kupima damu (Complete blood count) huku mkazo zaidi ukiwa kwenye Eosinophil na kiwango cha damu (Hb). Iwapo kuna uvamizi wa minyoo, kiwango cha Eosinophil huwa juu zaidi kuliko kawaida.
  • X-ray yaweza kusaidia kuchunguza hatua mojawapo ya ukuaji wa minyoo ya Taenia solium iitwayo cystercosis katika ubongo au paja.
  • CT na MRI pia zaweza kurahisisha kugundua na kutambua cyst (vifuko vyenye majimaji) za minyoo aina ya hydatid ambayo huvamia ini, ubongo, figo na sehemu nyingine za mwili.
  • Kipimo cha puru (proctoscopy) husaidia kutambua uvamizi wa minyoo aina ya trichiuris trichiura kwenye puru.
Minyoo inatibika?
Minyoo-matibabu-150x150.jpg
Bila shaka kabisa, minyoo inatibika. Dawa zifuatazo hutumika katika kutibu minyoo kulingana na aina ya minyoo inayomuathiri mgonjwa​
  • Mebendazole hutumika kutibu zaidi uvamizi wa minyoo aina ya round worms
  • Albendazole yaweza kutibu minyoo aina ya tegu (tape worms) pamoja na hydatid
  • Ivermectin hutumika kutibu aina mbalimbali za minyoo
  • Ketrax (levamisole) nayo pia ina uwezo wa kutibu aina kadhaa za minyoo
  • Piperazzine pia ina uwezo wa kutibu aina nyingine nyingi za minyoo.
Hata hivyo, tunashauri sana matumizi ya dawa hizi hasa kwa watoto, yafanyike mara baada ya kupata ushauri wa daktari na si vinginevyo.​
Inawezekana kujinga dhidi ya uvamizi wa minyoo?​
Njia za kujikinga na minyoo ni pamoja na​
  • Kuishi katika mazingira safi.
  • Kunawa mikono na sabuni baada ya kutoka msalani na kabla ya kula
  • Kukata kucha (kucha ndefu huweza kutunza uchafu)
  • Kuwa muangalifu hasa unapokuwa na wanyama kama paka na mbwa
  • Kutumia dawa za kuzuia uvamizi (deworming) kila baada ya miezi mitatu au sita
chanzo Fahamu kuhusu Minyoo (Helminthesis) – TanzMED(old) - Afya Kwa Wote​
 
umekuta minyoo mingapi? Ina pingili pingili au ni ya mviringo aafu mirefu kama kijiti? Hilo tatizo linatokana kula uchafu/chakula chenye vimelea vya minyoo. Mara nyingine huingia mwilini kupitia ngozi kama hao wadudu wapo kwenye udongo. Watoto mara nyingi huathirika zaid kwa sabab ya tabia ya kula kula udongo,hii pia hata wanawake wenye tabia hiyo. Tiba yake inategemea aina ya minyoo iliyopo,maana yake kuna hook worms(and round worms) ambazo hutumika albendazole 400mg single dose na taeniasis(yenye pingili) ambayo ni sensitive kwa niclosamide 2g as single dose kwa mtu mzima.
 
nilikuta mmoja mweupe na mrefu kama urefu wa kidole kidogo,
 
Imeandikwa na: Dr.Henry Mayala Jr Mnamo: Mar 29


Mojawapo ya tatizo linaloathiri jamii katika nchi nyingi zinazoendelea ikiwemo Tanzania ni magonjwa yanayohusiana na minyoo. Duniani kwa ujumla, takribani watu billion moja wameripotiwa kuwa na uvamizi wa minyoo aina ya helminthes kwenye miili yao.
Minyoo huenezwa kwa njia zipi?
Minyoo huenezwa pale maji au chakula vinapokuwa vimeathiriwa na mayai au mabuu ya minyoo. Hali kadhalika, uwezekano wa kupata minyoo huchangiwa pia na kutonawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka kujisaidia haja kubwa. Aidha watoto wadogo chini ya miaka mitano ambao hupenda kuchezea mchanga au uchafu kwa ujumla na ambao hupendelea pia kunyonya vidole nao pia huambukizwa kwa urahisi. Mambo mengine yanayochangia katika kupata uvamizi wa minyoo ni pamoja na kuishi katika mazingira machafu, kutembea bila viatu (pekupeku) na kula vyakula ambavyo havijaiva au visivyopikwa vizuri (undercooked foods).
Aina za minyoo na madhara yake kwa binadamu

Kuna aina kadhaa za minyoo ambazo, ukiachilia mbali kuwashambulia wanyama wengine kama ng'ombe, nguruwe, mbuzi na kondoo, humshambulia pia binadamu. Aina hizi ni pamoja na
  • Minyoo jamii ya round worms kwa mfano Ascaris lumbricoides ambao husababisha utumbo kuziba (intestinal obstruction) au uambukizi katika kidole tumbo (appendicitis)
  • Minyoo jamii ya hook worms kwa mfano Ancylostoma duodenale ambao huishi kwa kunyonya damu kwenye utumbo mdogo na hivyo kusababisha upungufu wa damu mwilini.
  • Minyoo jamii ya pin worms au thread worm kwa mfano Enterobius vermicularishusababisha kuwashwa hasa sehemu za haja kubwa kwa sababu ya mcharuko mwili unaotokana na minyoo hii kutoa mayai yao eneo hilo hasa kipindi cha usiku.
  • Minyoo jamii ya whip worms kwa mfano Trichuris trichiura husababisha kinyesi kuchanganyika na damu, kupungua uzito, upungufu wa damu na kutoka nje kwa puru (rectal prolapse).
  • Minyoo jamii ya tegu (tape worms) kama vile Taenia solium husababisha kifafa pindi wanapovamia ubongo hasa katika hatua ya ukuaji iitwayo cystercosis
Dalili za minyoo ni zipi?
Dalili za kuwepo kwa uvamizi wa minyoo mwilini hutegemea sana aina ya minyoo inayomuathiri mgonjwa. Lakini kwa ujumla, dalili ni pamoja na
  • Maumivu ya tumbo
  • Kupata choo kigumu sana
  • Kuharisha
  • Kujisikia mchovu na mlegevu kutokana na kupungukiwa damu
  • Kupoteza hamu ya kula
  • Tumbo kuwa na gesi na kuhisi limejaa
  • Kukohoa na kupiga chafya
  • Kwa watoto kusugua meno, kujipinduapindua pamoja na kujikojolea kitandani
  • Kichwa kuuma au kupata kifafa kama minyoo (jamii ya taenia solium) ikitaga mayai yake kwenye ubongo
  • Kuwashwa, na
  • Huathiri ukuaji kwa watoto
Utatambuaje kama umeathiriwa na minyoo?
Vipimo vinavyoweza kusaidia kugundua uvamizi wa minyoo, aina zake na hata madhara yaliyosababishwa na minyoo ni pamoja na:
  • Kupima choo kikubwa (Stool examination) kwa ajili ya kuchunguza mayai na mabuu ya minyoo iliyo katika haja kubwa kwa kutumia darubini
  • Kupima damu (Complete blood count) huku mkazo zaidi ukiwa kwenye Eosinophil na kiwango cha damu (Hb). Iwapo kuna uvamizi wa minyoo, kiwango cha Eosinophil huwa juu zaidi kuliko kawaida.
  • X-ray yaweza kusaidia kuchunguza hatua mojawapo ya ukuaji wa minyoo ya Taenia solium iitwayo cystercosis katika ubongo au paja.
  • CT na MRI pia zaweza kurahisisha kugundua na kutambua cyst (vifuko vyenye majimaji) za minyoo aina ya hydatid ambayo huvamia ini, ubongo, figo na sehemu nyingine za mwili.
  • Kipimo cha puru (proctoscopy) husaidia kutambua uvamizi wa minyoo aina ya trichiuris trichiura kwenye puru.
Minyoo inatibika?
Bila shaka kabisa, minyoo inatibika. Dawa zifuatazo hutumika katika kutibu minyoo kulingana na aina ya minyoo inayomuathiri mgonjwa
  • Mebendazole hutumika kutibu zaidi uvamizi wa minyoo aina ya round worms
  • Albendazole yaweza kutibu minyoo aina ya tegu (tape worms) pamoja na hydatid
  • Ivermectin hutumika kutibu aina mbalimbali za minyoo
  • Ketrax (levamisole) nayo pia ina uwezo wa kutibu aina kadhaa za minyoo
  • Piperazzine pia ina uwezo wa kutibu aina nyingine nyingi za minyoo.
Hata hivyo, tunashauri sana matumizi ya dawa hizi hasa kwa watoto, yafanyike mara baada ya kupata ushauri wa daktari na si vinginevyo.

Inawezekana kujinga dhidi ya uvamizi wa minyoo?
Njia za kujikinga na minyoo ni pamoja na
  • Kuishi katika mazingira safi.
  • Kunawa mikono na sabuni baada ya kutoka msalani na kabla ya kula
  • Kukata kucha (kucha ndefu huweza kutunza uchafu)
  • Kuwa muangalifu hasa unapokuwa na wanyama kama paka na mbwa
  • Kutumia dawa za kuzuia uvamizi (deworming) kila baada ya miezi mitatu au sita
chanzo Fahamu kuhusu Minyoo (Helminthesis) – TanzMED(old) - Afya Kwa Wote

mzizi naomba unisaidie dawa ya hook worm mkuu
 
Zipo Dawa za kizungu za kutibu minyoo ikiwa hazijakusaidia jaribu kutumia Dawa zangu za Asilia kisha unipe Feedback.

1) Dawa ya minyoo: Ponda tembe 3 za kitunguu thoum, tia ndani ya maziwa na kunywa (bila kutia sukari) usiku kabla ya kulala na asubuhi kunywa mafuta ya mbono. Inshallah dawa hio inaweza kukusaidia.

2) Dawa za kizungu ni Mebendazole capsules (Vermox--Generic only by prescription in the USA)
zinapatikana hapo mnapoishi. (kama zikipatikana, Insha Allah; Matumizi: Kwa watoto, chukua kibonge (capsule) moja mara tatu kwa siku) kwa wiki miwili. Kwa watu wazima, chukua kibonge miwili mara tatu kwa siku. Tumia dawa mpaka minyoo hazionikani tena..... Tumia mpaka baada ya wiki 2 ama mwezi moja.

Alafu kuna Vitaklenz: Ni vidonge (capsules---herbal dietary supplement) zinatumika kuondoa minyoo za aina mbali mbali: (tapeworms, pinworms, hookworms, threadworms, bacteria). Matumizi: Kwa watoto, chukua kibonge (capsule) moja maratatu kwa siku) kwa wiki miwili. Kwa watu wazima, chukua vibonde viwili mara tatu kwa siku. Tumia dawa mpaka minyoo hazionikani tena..... mpaka baada ya wiki 2 ama mwezi moja.


3) Minyoo:
Kunywa Habbat-Sawdaa pamoja na siki kuondoa minyoo itwange hiyo habbat sawdaa kisha uchekeche upate unga chemsha maji ya uvuguvugu tiya kijiko kimoja hiyo habbat

Sawdaa kwenye glasi ya maji ya uvuguvugu na utie kijiko kimoja kidogo cha siki ya zabibu au siki ya apple kunywa kabla ya kula kitu kila asubuhi unapoamka kwa muda wa mwezi mmoja Minyoo yako itakwisha kabisa inshallah tumia dawa kisha unipe Feed back.

Nb. Habbat Sawdaa kwa lugha ya kiingereza inaitwa Nigella Sativa. Na Siki ni Vinegar. kama upo Dar ,au mji wowote Tanzania kaulize kwenye maduka makubwa ya Super Market au kaulizie Sokoni kariakoo kwenye maduka wanayouza maduka ya kiaarabu ya Wapemba.
 
MziziMkavu unawasaidia sana watu aisee kila kona upo hata sijui professional yako ni ipi aisee, hongerA sana mkuu
 
Last edited by a moderator:
MziziMkavu unawasaidia sana watu aisee kila kona upo hata sijui professional yako ni ipi aisee, hongerA sana mkuu
Mkuu UKI Proffessional yangu ni hii hapa (Investigator and Research Professionals Herbs) Kwa Lugha ya Kiswahili unaweza kusema hivi ( Mchunguzi na Matafiti Mtalaam wa Dawa za mitishamba) Au kwa kifupi unaweza kusema Mtu Mwenye Kipaji cha kuzaliwa na Mungu.
 
mkuu uki proffessional yangu ni hii hapa (investigator and research professionals herbs) kwa lugha ya kiswahili unaweza kusema hivi ( mchunguzi na matafiti mtalaam wa dawa za mitishamba) au kwa kifupi unaweza kusema mtu mwenye kipaji cha kuzaliwa na mungu.

glory to God
 
Katika dawa izi za albendazol na mebendazol ipi ni nzuri sana kutumia. Na ushauri unakula dawa ya minyoo kwa muda gani?
 
Back
Top Bottom