Ukikopesha tarajia kukosa undugu, urafiki na hizo pesa

Mzee wa kusawazisha

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
1,587
1,136
Habari za mwamko wakuu humu ndani, nabandika uzi huu ili tulijadili kwa pamoja swala hili.

Binafsi Nina roho ya huruma pale mtu unakuja na shida serious unataka kuzima pesa. Nitolee mfano mzuri ndio ulionifanya niandike uzi huu..

Mwaka 2016 dada yangu mmoja baba na mama mmoja walikua wanacheza vikoba kwa kawaida siku ya kuvunja kama una deni hupati kitu. Sasa yeye alikwama Sana. Nilikua chuoni mwaka wa Kwanza aliniomba nimwazime pesa jumla Laki mbili na 80 ili akivuja tu vikoba atanirudishia.. Walivunja na hakunipigia hata simu nikasamehe,.

Mwaka 2017 alitetereka kidogo kibiashara kiasi hata kodi ya fremu anadaiwa Mwenye fremu alitaka atoe vyombo vyake ndani akanipigia simu nikiwa chuoni tena wiki ya UE Nika risk nikaweka bond simu ili nimuokoe nikamtumia laki 1 japo nilipata baada mwezi m1 na tulipatana baada ya wiki 1.

Mwaka Jana mwezi wa 12 Mwanzoni alinijia tena kuniazima pesa alikwama tena Kuna akaahidi baada ya wiki atanirejeshea Kuna pesa anaisubiri nikampa laki 1 na nusu. Wiki imepita akaomba nimwongezee tena nikampa 20000.
Wiki hii juma 3 anarudisha laki 1 badala ya laki na 70..nikatulia bila kuuliza nikajua Kesho yake angeniambia lolote.

Nami pia kwa Kua niliamini angenirudishia hiyo pesa nikakopa kwa mtu laki na nusu ili niendeleshe biashara yangu kwa bahati biashara hajaenda Sawa jamaa ananidai pesa yake Maana mda umeisha laki nimempa ila bado anataka yote. Na Dada yangu mpaka kufikia Jana nilibidi nifoke kwa Mara ya Kwanza kabisa maana na mimi nadaiwa..

Familia imekaa kikao kwa ajili yangu kisa nadai ela naambiwa Sina utu na sisaidii wenzangu na sisi ni ndugu wa kuzaana Nguvu zote zimeisha hapa sina la kufanya nikikumbuka niliyoyafanya kwa Dada yangu Toka mwaka juzi. Karibuni kwa upembuzi wa kina juu ya jambo hili nadai ili nirudishe deni najibiwa hivyo hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nikikopesha hela huwa naangalia ziada inayobaki,, naangalia pia Kama nitaweza survive incase isiporudi.

Na usiponirudishia Deni la awali ukaja kukopa Tena sikupi

Shida ya watu wakopaji hawawi wazi,Ni Bora uombe kuliko unakopa Hali ukijua hutalipa

Asilimia ya mtu kulipa Deni Ni ndogo Sana..Kama una roho ya huruma Basi kopesha lakini akilini ujue tu kuwa umetoka sadaka .kama sio mtu was huruma Sana Ni vema tu usikopeshe maana utaishia kupoteza vyote hela yako na urafiki(undugu)


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nikikopesha hela huwa naangalia ziada inayobaki,, naangalia pia Kama nitaweza survive incase isiporudi.

Na usiponirudishia Deni la awali ukaja kukopa Tena sikupi

Shida ya watu wakopaji hawawi wazi,Ni Bora uombe kuliko unakopa Hali ukijua hutalipa

Asilimia ya mtu kulipa Deni Ni ndogo Sana..Kama una roho ya huruma Basi kopesha lakini akilini ujue tu kuwa umetoka sadaka .kama sio mtu was huruma Sana Ni vema tu usikopeshe maana utaishia kupoteza vyote hela yako na urafiki(undugu)


Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu upo sahihi kabisa cha Ajabu MI natoaga yooote Maana Hua natengeneza mazingira ya kukuamini ili kujenga urafiki

Cha Ajabu mtu akishachukua anafurahia Sana Ile siku.. Sasa ukorofi unakuja wakati wa kulipa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu upo sahihi kabisa cha Ajabu MI natoaga yooote Maana Hua natengeneza mazingira ya kukuamini ili kujenga urafiki

Cha Ajabu mtu akishachukua anafurahia Sana Ile siku.. Sasa ukorofi unakuja wakati wa kulipa

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi ilishawahi kunicost hiyo..hela yangu yote nikamuazima mtu halafu hajanilipa,,
Hapo nilijifunza Kama kila kitu kina kiasi...nikajifunza kuwa na kiasi..

Nikawa na kiasi,napokukopesha naangalia kabisa na Mimi sitabaki katika mazingira magumu

Na nisivyojua kudai,Nina huruma kupita kiasi
Ko hata mtu asipolipa Basi natoa tu sadaka..ila ndo asije Tena kukopa kwangu

Wengi huwa wanaogopa kuja kukopa tena




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ilishawahi kunicost hiyo..hela yangu yote nikamuazima mtu halafu hajanilipa,,
Hapo nilijifunza Kama kila kitu kina kiasi...nikajifunza kuwa na kiasi..

Nikawa na kiasi,napokukopesha naangalia kabisa na Mimi sitabaki katika mazingira magumu

Na nisivyojua kudai,Nina huruma kupita kiasi
Ko hata mtu asipolipa Basi natoa tu sadaka..ila ndo asije Tena kukopa kwangu

Wengi huwa wanaogopa kuja kukopa tena




Sent using Jamii Forums mobile app
Kokopesha no kipaji mku haiwezekani mtu unakopwa hakulipi baada ya miezi 7 ama 8 anajisahaulisha Kua alikuzima pesa siku za nyuma anakuja omba tena umkopeshe.. Dah ubinadamu kazi kweli kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kokopesha no kipaji mku haiwezekani mtu unakopwa hakulipi baada ya miezi 7 ama 8 anajisahaulisha Kua alikuzima pesa siku za nyuma anakuja omba tena umkopeshe.. Dah ubinadamu kazi kweli kweli

Sent using Jamii Forums mobile app

Mimi Hadi Sasa nimepoteza hela nyingi Sana..nikianza kuhesabu

Sema Ni vile siwez kumuacha mtu halafu na shida Hali ninao uwezo wa kumsaidia,nafsi yangu huwa inanisuta.

Kama Ana uhitaji kweli nitamsaidia tu,nitalipwa na Mungu



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waliosema udugu si kufanana bali kufaana,hawakukosea...watu tumepoteza hadi marafiki kwasababu ya kudai mali yako..piga moyo konde ndugu songa mbele,uzuri wa shida haina siku moja we mtazame tuu siku akikwama tena mwambie akulipe madeni yako ndio umpe hiyo anayotaka...full stop.
 
Waliosema udugu si kufanana bali kufaana,hawakukosea...watu tumepoteza hadi marafiki kwasababu ya kudai mali yako..piga moyo konde ndugu songa mbele,uzuri wa shida haina siku moja we mtazame tuu siku akikwama tena mwambie akulipe madeni yako ndio umpe hiyo anayotaka...full stop.
Halafu atakapokuja kukopa Mara nyingine,,anakuja as if Hana Deni,Mimi huo ujasiri Sina kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi pia wakuu, nimepoteza hela nyingi sana kwenye kukopesha ndugu na marafiki! Wakati wa kukopa wanakupigia simu tele, na utakapo wapigia kuwakumbusha warejeshe mkopo hawatapokea simu, yaani wanaingia mitini kabisa! Marafiki wengi ambao nilikuwa nawapenda, nimewapoteza kwa sababu ya kuwakopesha!

Dah! kama nikipiga mahesabu hela zote nilizopoteza kwa kukopesha, inafika mamillioni kadha! Halafu, sasa hivi nina wakati mgumu, na hakuna hata mmoja wa kuniulizia hali?? Shukrani ya punda kweli ni mateke!
 
Kwasasa nilichokifanya ni kutobakiwa na ela ya ziada, zaidi ninaziweka fixed account.

Nabakisha fedha ya mahitaji yangu ya mwezi mzima, hivyo nashindwa kuwa na pesa ya kukopesha au kusaidiaa....

Kama ni kutuma nyumbani, naweka akiba ya hiyo pesa mapema, na wenyewe nimesha wambia wakihitaji pesa kwangu wanitaarifu mapema na sio kushtukiza.

Kukaa na pesa nyingi pasipokuwa na matumizi nayo, kunasababisha matumizi mabaya ya pesa au kukopesha watu kwa huruma tu.

Mwaka huu, kwa jinsi nilivyobahili, kunitoa pesa kizembe unahitaji kunishawishi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwasasa nilichokifanya ni kutobakiwa na ela ya ziada, zaidi ninaziweka fixed account.

Nabakisha fedha ya mahitaji yangu ya mwezi mzima, hivyo nashindwa kuwa na pesa ya kukopesha au kusaidiaa....

Kama ni kutuma nyumbani, naweka akiba ya hiyo pesa mapema, na wenyewe nimesha wambia wakihitaji pesa kwangu wanitaarifu mapema na sio kushtukiza.

Kukaa na pesa nyingi pasipokuwa na matumizi nayo, kunasababisha matumizi mabaya ya pesa au kukopesha watu kwa huruma tu.

Mwaka huu, kwa jinsi nilivyobahili, kunitoa pesa kizembe unahitaji kunishawishi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app

Huyu kweli mangi
Ila hii njia nzuri,inazuia vishawishi vya kukopesha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kopesha tu mkuu ni baraka izo mm nilimkopesha Dada tangu tumbo moja million 1 hakunilipa nikamkopesha rafiki yangu moja million 1 akanilipa laki 8 wote nikawapotezea leo hii siwazi tena kuwadai na miaka ishapita Mungu kanibariki kivingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom