shalet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2013
- 3,428
- 3,510
Imagine umekaa miaka miwili ndani ya ndoa lakini mkeo hajashika ujauzito, siku upo na simu ya mkeo inaingia meseji kutoka kwa mtoto wa dada yake mkeo " Bibi (mama mkubwa wa mkeo) amesema huwezi shika mimba sababu ukiwa shule uliwahi kutoa mimba hii mara ya pili ananiambia lakini nambishai mara ya kwanza nilijua ananitania".
Unamwambia mkeo akufafanulie meseji anasema huyo ma mkubwa hajawahi ishi naye alijuaje kuwa yeye amewahi toa mimba kwanza yeye hajawahi kushika mimba. nikamuuliza kwaiyo anajuaje kuwa wewe saizi hauna mimba manake bado hamjaonana, akasema hajui yule mama mkubwa ni kama mwanga ndio maana ndugu huwa wanamtenga hata kwetu hajawahi kuja toka tuko shule ya msingi walikosana na mama.
Pia, nakumbukua kuna picha fulani ya wife niliona facebook ilikuwa birthday yake akiwa chuo ni kama alikuwa mjamzito nilipomuuliza mbona hapa kama ulikuwa mjamzito akasema alinenenepa tu boom tamu tukacheka yakaisha, jana baada ya hiyo meseji nimesearch ile picha nimegundua alifuta ila kuna post fulani aliandika facebook anatamani kuwa na mtoto na yeye aitwe mama cha ajabu hiyo post ni ya mwaka huo huo wa ile picha hii hakufuta.
Sina mpango wa kuachana naye wala kukuza ugomvi kwa miaka miwili amekuwa akionana na mdokta mbalimbali lakini wanampa dawa anatumia bado hashiki ujauzito, hapa nishaurini nifanyaje manake kama naona hili jambo lina ukweli japo yeye anakataa huyo ex wake wa chuo namjua nafikiria kumuuliza pengine yeye ndio atasema ukweli, endapo atakuwa kweli alitoa ujauzito na hawezi kushika mimba nina option moja tu ya kuzaa nje ila kwa sasa nataka jua ukweli wa hili suala.
Unamwambia mkeo akufafanulie meseji anasema huyo ma mkubwa hajawahi ishi naye alijuaje kuwa yeye amewahi toa mimba kwanza yeye hajawahi kushika mimba. nikamuuliza kwaiyo anajuaje kuwa wewe saizi hauna mimba manake bado hamjaonana, akasema hajui yule mama mkubwa ni kama mwanga ndio maana ndugu huwa wanamtenga hata kwetu hajawahi kuja toka tuko shule ya msingi walikosana na mama.
Pia, nakumbukua kuna picha fulani ya wife niliona facebook ilikuwa birthday yake akiwa chuo ni kama alikuwa mjamzito nilipomuuliza mbona hapa kama ulikuwa mjamzito akasema alinenenepa tu boom tamu tukacheka yakaisha, jana baada ya hiyo meseji nimesearch ile picha nimegundua alifuta ila kuna post fulani aliandika facebook anatamani kuwa na mtoto na yeye aitwe mama cha ajabu hiyo post ni ya mwaka huo huo wa ile picha hii hakufuta.
Sina mpango wa kuachana naye wala kukuza ugomvi kwa miaka miwili amekuwa akionana na mdokta mbalimbali lakini wanampa dawa anatumia bado hashiki ujauzito, hapa nishaurini nifanyaje manake kama naona hili jambo lina ukweli japo yeye anakataa huyo ex wake wa chuo namjua nafikiria kumuuliza pengine yeye ndio atasema ukweli, endapo atakuwa kweli alitoa ujauzito na hawezi kushika mimba nina option moja tu ya kuzaa nje ila kwa sasa nataka jua ukweli wa hili suala.