ksny
JF-Expert Member
- Mar 30, 2016
- 1,693
- 1,657
Nafikiri hapa tunachanganya. Unyonge na kukata tamaa ni vitu viwili tofauti. Wakati kukata tamaa ni kosa au dhambi kubwa lakini unyonge siku zote upo. Nadhani hao wanadai kuwa unyonge haupo na mtu asijiite mnyonge ni wale ambao hawajakumbana na changa moto. Nitatoa mfano mmoja tena wa kweli. Kuna binti mmoja alimaliza kidato cha sita na kushinda vizuri na maksi nzuri tu. Yeye alichukuwa PCB. Hakuna somo aliloshinda chini C, nafikiri alipata A moja, B moja na C moja. Yeye ni mtoto yatima. Kuna wakati aliwahi kupata matatizo shule ya serkali akaenda private school ya kanisa kumalizia kidato cha nne. Kidato cha tano na sita alisoma shule ya serkali. Alichaguliwa kwenda SAUT St Augustine University), lakini alinyimwa mkopo. Huyu alinyimwa mkopo kwa sababu ni mnyonge, na hana wa kumtetea. Mtu kama huyu ana haki ya kujiita mnyonge.👏👏👏Hata kama una uwezo mdogo jione unaweza,ww kidume...uniite mnyonge kwani mi kilema siwez kujitetea?