Ukiegesha gari vibaya, faini kwa gari ndogo ni Tsh 200,000 na Tsh 10,000 ni gharama ya gari kulala yard kwa siku moja

RaiaMimi

Member
Jun 3, 2021
11
51
Habari Wadau!

Wiki hii katika harakati zangu nimekumbana na kadhia ambayo ikanisikitisha sana. Ilikuwa majira ya mchana niliposimamisha harakati zangu na kuelekea sehemu ya kupata chakula cha mchana.

Nilipofika pale kama ilivyo siku nyingine zote ambazo huwa naenda kula mahali hapo, nikaegesha gari pembezoni mwa barabara kwani kijiwe hicho kama ilivyo vijiwe vingine vingi tu vya hapa DSM hakina maegesho maalumu ya magari ya wateja.

Baada ya kuegesha gari nikaingia ndani na kuagiza chakula na maji ya kukata kiu nikisubiri chakula. Ghafla nikashtuliwa na mtu akiniambia kuwa angalia gari yako inafungwa kule. Kuangalia kweli nawaona vijana na suti zao nyeusi wanaendelea kufunga nyororo na chuma kwenye gurudumu la mbele.

Nikahamaki nikaenda kwa haraka na kuwasha gari ili niliweke pembeni kuepuka usumbufu na hasara zisizo za lazima ambazo niliona zinafata wakati bado jamaa anaendelea na zoezi lake la kufunga. Lakini nikashtuka kuwa nitaharibu gari kwani alishazungusha chuma kwenye gurudumu.

Majibizano yalifata kila pande ikionesha iko sahihi bila mafanikio yoyote kwani niliona ni dhahili kuwa hawa jamaa wanachokifanya ni kuvidhia na kufunga magari ya watu ili wajipatie pesa tu. Baada ya kuona wameanza niletea habari za faini ya hili kosa ni Tsh 210,000.00 na ukiendelea kuleta ubishi tunaita break down tunavuta gari na gharama itakuwa yangu. Na mimi wakati huo hiyo pesa sina nikaona ni bora niendeshe hadi huko ofisini kwao (wenyewe wanaita yard) zilizopo Ubungo Mawasiliano Stendi labda kama ni faini nitapewa muda nitalipa au pengine nitakutana na mtu ambaye tunaweza ongea kwa kusikilizana na kuheshimiana bila kutishana tishana.

Kufika ofisini kwao wakajaza fomu zao pale wakanikabidhi kwa mwenzao. Nikaanza kwa kumuuliza kwanini mnakamata gari imeegeshwa pembezoni mwa barabara bila ata kuathili watumiaji wengine na ni sehemu ya biashara inayoonekana kabisa? Pia kwa muda mrefu tu nimekuwa nikipaki pale pale walipoikuta gari na kula chakula hadi namaliza naondoka bila shida yoyote?

Majibu yake ndio yalinifanya nimkumbuke Hayati Rais Magufuli.

Alisema enzi za Magufuli haya mambo ya mawakala wa halmashauri hayakuwepo. Aliyakataa. Ila kwa sasa yamerudi. So jitahidi kuwa makini unapoegesha gari lako kama yule mtoza ushuru wa maegesho ya magari hatakuwepo.

Akanieleza kuwa ni kweli faini kwa gari ndogo ni Tsh 200,000 na Tsh 10,000 ni gharama ya gari kupaki yard kwa siku moja.
Nikamuuliza tena hamuoni kuwa mnaua Biashara London Lounge?

Akajibu ni kweli mwenyewe inatakiwa aende kuomba kibali cha maegesho na ataletwa mtu wa Ushuru pale. Hili likifanyika, ata gari zipaki hadi zifunge njia hazitakamatwa.

Nikashangaa sana. Kwahiyo mimi nalipishwa Tsh 210,000 kwa sababu mtu wa kutoza Tsh 500 kwa saa hayupo ila nyie wa kutoza Tsh 210,000 mpo????

Nikamuuliza kwa hiyo hiyo faini nikiandikiwa nitailipa kwa muda gani?

Akajibu akasema siku yoyote ila gari utachukua utakapo kamilisha malipo ila hii Tsh 10,000 kwa siku itaendelea kukua.

Wacha niishie hapo na maelezo yangu.

Swali langu. Je, serikali ya sasa imeona hii ni njia sahihi kweli?? Baada ya malalamiko yote iliyojinasibu kuyafanyia kazi kuhusu watu kufunga biashara zao.

Sababu mimi binafsi sitakanyaga tena London Lounge kwa hichi kilichonipata leo na rafiki yangu yoyote atakayependekeza twende mahali hapo nitamueleza haya na tutaelekea sehemu nyingine. Serikali ya sasa katika hili nanyi pia mtaaua biashara za watu.
 
Mkuu.
Pale london ni kwel hamna parking mi huwa napark mbele ya gate ya kampuni sjui lile garage bovu pale....tje other side ya london...na wale jamaa wanakuaga pale wanavizia magar .wanakula na watu wakarib wa pale. Ukipark wanawaita sometime.wanapark pale kituo cha polis oposite na mkapa export zone..so kuwa makin. ..ukipark kuanzia mida ya sa kumi na mbili kwenda mbele sawa .ila sa kumi kurud nyuma usithubutu .na yule london anakosa wateja sabab hana parking..pamepoa..mi nakaaga juu kule sometime
 
Mbona hao jamaa wapo toka enzi za Mwendazake?
Mimi naona kwenye hicho kisa chako hakiwezi mtakatisha mwendazake na kuulaumu utawala wa sasa kuwa ni onevu.
Hapana. Utawala wa sasa si onevu ila unawaacha watendaji kujitengenezea dili za kuumiza watu kama hizi.

Sababu katika mazungumzo nao nilifahamishwa kuwa hiyo faini ya 200,000 inagawanyika kama ifuatavyo:
Tsh 100,000 inaenda kwa halmashauri
Tsh 50,000 inaenda kwa mzabuni/kampuni ya kukamata kamata na Tsh 50,000 inayobaki inaenda kwa mkamataji (mtu). Enzi za mwendazake hawa watu mikataba yao haikuhuishwa na tulitulia kwa raha tu ila baada ya kifo chake mambo ndio yamekuwa hivyo.

Hii maana yake wananchi tumegeuzwa dili katika ishu ambazo zina ufumbuzi rahisi na usioumiza upande wowote. Na ufumbuzi wenyewe ni aletwe mtoza ushuru wa maegesho ya magari atoze Tsh 500 kwa kila saa.
 
Hili suala lilinitokea pia. Nilikuwa kimara. Ile nimeshuka nimeenda dukani wakafika kwenye gari wakamkuta wife afu gari sijazima. Wakataka kunitoza fine finally hawakuambulia chochote zaidi ya kupoteza muda kwa sound nilizowapiga
 
Habari Wadau!

Wiki hii katika harakati zangu nimekumbana na kadhia ambayo ikanisikitisha sana. Ilikuwa majira ya mchana niliposimamisha harakati zangu na kuelekea sehemu ya kupata chakula cha mchana.

Nilipofika pale kama ilivyo siku nyingine zote ambazo huwa naenda kula mahali hapo, nikaegesha gari pembezoni mwa barabara kwani kijiwe hicho kama ilivyo vijiwe vingine vingi tu vya hapa DSM hakina maegesho maalumu ya magari ya wateja.

Baada ya kuegesha gari nikaingia ndani na kuagiza chakula na maji ya kukata kiu nikisubiri chakula. Ghafla nikashtuliwa na mtu akiniambia kuwa angalia gari yako inafungwa kule. Kuangalia kweli nawaona vijana na suti zao nyeusi wanaendelea kufunga nyororo na chuma kwenye gurudumu la mbele.

Nikahamaki nikaenda kwa haraka na kuwasha gari ili niliweke pembeni kuepuka usumbufu na hasara zisizo za lazima ambazo niliona zinafata wakati bado jamaa anaendelea na zoezi lake la kufunga. Lakini nikashtuka kuwa nitaharibu gari kwani alishazungusha chuma kwenye gurudumu.

Majibizano yalifata kila pande ikionesha iko sahihi bila mafanikio yoyote kwani niliona ni dhahili kuwa hawa jamaa wanachokifanya ni kuvidhia na kufunga magari ya watu ili wajipatie pesa tu. Baada ya kuona wameanza niletea habari za faini ya hili kosa ni Tsh 210,000.00 na ukiendelea kuleta ubishi tunaita break down tunavuta gari na gharama itakuwa yangu. Na mimi wakati huo hiyo pesa sina nikaona ni bora niendeshe hadi huko ofisini kwao (wenyewe wanaita yard) zilizopo Ubungo Mawasiliano Stendi labda kama ni faini nitapewa muda nitalipa au pengine nitakutana na mtu ambaye tunaweza ongea kwa kusikilizana na kuheshimiana bila kutishana tishana.

Kufika ofisini kwao wakajaza fomu zao pale wakanikabidhi kwa mwenzao. Nikaanza kwa kumuuliza kwanini mnakamata gari imeegeshwa pembezoni mwa barabara bila ata kuathili watumiaji wengine na ni sehemu ya biashara inayoonekana kabisa? Pia kwa muda mrefu tu nimekuwa nikipaki pale pale walipoikuta gari na kula chakula hadi namaliza naondoka bila shida yoyote?

Majibu yake ndio yalinifanya nimkumbuke Hayati Rais Magufuli.

Alisema enzi za Magufuli haya mambo ya mawakala wa halmashauri hayakuwepo. Aliyakataa. Ila kwa sasa yamerudi. So jitahidi kuwa makini unapoegesha gari lako kama yule mtoza ushuru wa maegesho ya magari hatakuwepo.

Akanieleza kuwa ni kweli faini kwa gari ndogo ni Tsh 200,000 na Tsh 10,000 ni gharama ya gari kupaki yard kwa siku moja.
Nikamuuliza tena hamuoni kuwa mnaua Biashara London Lounge?

Akajibu ni kweli mwenyewe inatakiwa aende kuomba kibali cha maegesho na ataletwa mtu wa Ushuru pale. Hili likifanyika, ata gari zipaki hadi zifunge njia hazitakamatwa.

Nikashangaa sana. Kwahiyo mimi nalipishwa Tsh 210,000 kwa sababu mtu wa kutoza Tsh 500 kwa saa hayupo ila nyie wa kutoza Tsh 210,000 mpo????

Nikamuuliza kwa hiyo hiyo faini nikiandikiwa nitailipa kwa muda gani?

Akajibu akasema siku yoyote ila gari utachukua utakapo kamilisha malipo ila hii Tsh 10,000 kwa siku itaendelea kukua.

Wacha niishie hapo na maelezo yangu.

Swali langu. Je, serikali ya sasa imeona hii ni njia sahihi kweli?? Baada ya malalamiko yote iliyojinasibu kuyafanyia kazi kuhusu watu kufunga biashara zao.

Sababu mimi binafsi sitakanyaga tena London Lounge kwa hichi kilichonipata leo na rafiki yangu yoyote atakayependekeza twende mahali hapo nitamueleza haya na tutaelekea sehemu nyingine. Serikali ya sasa katika hili nanyi pia mtaaua biashara za watu.
Aisee, ila ile sehemu gari huwa zinapaki sehemu sio, kwa kweli
 
Habari Wadau!

Wiki hii katika harakati zangu nimekumbana na kadhia ambayo ikanisikitisha sana. Ilikuwa majira ya mchana niliposimamisha harakati zangu na kuelekea sehemu ya kupata chakula cha mchana.

Nilipofika pale kama ilivyo siku nyingine zote ambazo huwa naenda kula mahali hapo, nikaegesha gari pembezoni mwa barabara kwani kijiwe hicho kama ilivyo vijiwe vingine vingi tu vya hapa DSM hakina maegesho maalumu ya magari ya wateja.

Baada ya kuegesha gari nikaingia ndani na kuagiza chakula na maji ya kukata kiu nikisubiri chakula. Ghafla nikashtuliwa na mtu akiniambia kuwa angalia gari yako inafungwa kule. Kuangalia kweli nawaona vijana na suti zao nyeusi wanaendelea kufunga nyororo na chuma kwenye gurudumu la mbele.

Nikahamaki nikaenda kwa haraka na kuwasha gari ili niliweke pembeni kuepuka usumbufu na hasara zisizo za lazima ambazo niliona zinafata wakati bado jamaa anaendelea na zoezi lake la kufunga. Lakini nikashtuka kuwa nitaharibu gari kwani alishazungusha chuma kwenye gurudumu.

Majibizano yalifata kila pande ikionesha iko sahihi bila mafanikio yoyote kwani niliona ni dhahili kuwa hawa jamaa wanachokifanya ni kuvidhia na kufunga magari ya watu ili wajipatie pesa tu. Baada ya kuona wameanza niletea habari za faini ya hili kosa ni Tsh 210,000.00 na ukiendelea kuleta ubishi tunaita break down tunavuta gari na gharama itakuwa yangu. Na mimi wakati huo hiyo pesa sina nikaona ni bora niendeshe hadi huko ofisini kwao (wenyewe wanaita yard) zilizopo Ubungo Mawasiliano Stendi labda kama ni faini nitapewa muda nitalipa au pengine nitakutana na mtu ambaye tunaweza ongea kwa kusikilizana na kuheshimiana bila kutishana tishana.

Kufika ofisini kwao wakajaza fomu zao pale wakanikabidhi kwa mwenzao. Nikaanza kwa kumuuliza kwanini mnakamata gari imeegeshwa pembezoni mwa barabara bila ata kuathili watumiaji wengine na ni sehemu ya biashara inayoonekana kabisa? Pia kwa muda mrefu tu nimekuwa nikipaki pale pale walipoikuta gari na kula chakula hadi namaliza naondoka bila shida yoyote?

Majibu yake ndio yalinifanya nimkumbuke Hayati Rais Magufuli.

Alisema enzi za Magufuli haya mambo ya mawakala wa halmashauri hayakuwepo. Aliyakataa. Ila kwa sasa yamerudi. So jitahidi kuwa makini unapoegesha gari lako kama yule mtoza ushuru wa maegesho ya magari hatakuwepo.

Akanieleza kuwa ni kweli faini kwa gari ndogo ni Tsh 200,000 na Tsh 10,000 ni gharama ya gari kupaki yard kwa siku moja.
Nikamuuliza tena hamuoni kuwa mnaua Biashara London Lounge?

Akajibu ni kweli mwenyewe inatakiwa aende kuomba kibali cha maegesho na ataletwa mtu wa Ushuru pale. Hili likifanyika, ata gari zipaki hadi zifunge njia hazitakamatwa.

Nikashangaa sana. Kwahiyo mimi nalipishwa Tsh 210,000 kwa sababu mtu wa kutoza Tsh 500 kwa saa hayupo ila nyie wa kutoza Tsh 210,000 mpo????

Nikamuuliza kwa hiyo hiyo faini nikiandikiwa nitailipa kwa muda gani?

Akajibu akasema siku yoyote ila gari utachukua utakapo kamilisha malipo ila hii Tsh 10,000 kwa siku itaendelea kukua.

Wacha niishie hapo na maelezo yangu.

Swali langu. Je, serikali ya sasa imeona hii ni njia sahihi kweli?? Baada ya malalamiko yote iliyojinasibu kuyafanyia kazi kuhusu watu kufunga biashara zao.

Sababu mimi binafsi sitakanyaga tena London Lounge kwa hichi kilichonipata leo na rafiki yangu yoyote atakayependekeza twende mahali hapo nitamueleza haya na tutaelekea sehemu nyingine. Serikali ya sasa katika hili nanyi pia mtaaua biashara za watu.
Umeandika vizuri Ila ulipoanza kutaja mambo ya Magufuli ndio nimeshindwa kuelewa sasa unatakaje?

Hatuwezi kupaki magari bila utaratibu, na hata enzi ya Magufuli watu wa kukamata magari kwa wrong parking walikuwepo sana. Mfano mie Mara nyingi sana kazi zangu nafanya Baraza la Kazi la Kinondoni pale Akiba mbona wapo miaka yote au wewe mwenzetu wakati wa Magufuli ulikuwa haujaja mjini bado?

Msipende kutaka kulaumu kwa kulinganisha wakati uliopita na wa sasa halafu Marais hawakuwa wawili tu nchi hii.

Nachofahamu watu wanaokamata magari kwa wrong parking wapo sana tu hata lumumba, nkrumah street, Arusha town wanakamata tu miaka yote.

Kama tunafukuza machinga pembezoni mwa barabara basi na wenye magari tujitahidi kupaki kwenye maeneo rasmi ya maegesho ya magari.
 
Sina hamu yashanitokea
Habari Wadau!

Wiki hii katika harakati zangu nimekumbana na kadhia ambayo ikanisikitisha sana. Ilikuwa majira ya mchana niliposimamisha harakati zangu na kuelekea sehemu ya kupata chakula cha mchana.

Nilipofika pale kama ilivyo siku nyingine zote ambazo huwa naenda kula mahali hapo, nikaegesha gari pembezoni mwa barabara kwani kijiwe hicho kama ilivyo vijiwe vingine vingi tu vya hapa DSM hakina maegesho maalumu ya magari ya wateja.

Baada ya kuegesha gari nikaingia ndani na kuagiza chakula na maji ya kukata kiu nikisubiri chakula. Ghafla nikashtuliwa na mtu akiniambia kuwa angalia gari yako inafungwa kule. Kuangalia kweli nawaona vijana na suti zao nyeusi wanaendelea kufunga nyororo na chuma kwenye gurudumu la mbele.

Nikahamaki nikaenda kwa haraka na kuwasha gari ili niliweke pembeni kuepuka usumbufu na hasara zisizo za lazima ambazo niliona zinafata wakati bado jamaa anaendelea na zoezi lake la kufunga. Lakini nikashtuka kuwa nitaharibu gari kwani alishazungusha chuma kwenye gurudumu.

Majibizano yalifata kila pande ikionesha iko sahihi bila mafanikio yoyote kwani niliona ni dhahili kuwa hawa jamaa wanachokifanya ni kuvidhia na kufunga magari ya watu ili wajipatie pesa tu. Baada ya kuona wameanza niletea habari za faini ya hili kosa ni Tsh 210,000.00 na ukiendelea kuleta ubishi tunaita break down tunavuta gari na gharama itakuwa yangu. Na mimi wakati huo hiyo pesa sina nikaona ni bora niendeshe hadi huko ofisini kwao (wenyewe wanaita yard) zilizopo Ubungo Mawasiliano Stendi labda kama ni faini nitapewa muda nitalipa au pengine nitakutana na mtu ambaye tunaweza ongea kwa kusikilizana na kuheshimiana bila kutishana tishana.

Kufika ofisini kwao wakajaza fomu zao pale wakanikabidhi kwa mwenzao. Nikaanza kwa kumuuliza kwanini mnakamata gari imeegeshwa pembezoni mwa barabara bila ata kuathili watumiaji wengine na ni sehemu ya biashara inayoonekana kabisa? Pia kwa muda mrefu tu nimekuwa nikipaki pale pale walipoikuta gari na kula chakula hadi namaliza naondoka bila shida yoyote?

Majibu yake ndio yalinifanya nimkumbuke Hayati Rais Magufuli.

Alisema enzi za Magufuli haya mambo ya mawakala wa halmashauri hayakuwepo. Aliyakataa. Ila kwa sasa yamerudi. So jitahidi kuwa makini unapoegesha gari lako kama yule mtoza ushuru wa maegesho ya magari hatakuwepo.

Akanieleza kuwa ni kweli faini kwa gari ndogo ni Tsh 200,000 na Tsh 10,000 ni gharama ya gari kupaki yard kwa siku moja.
Nikamuuliza tena hamuoni kuwa mnaua Biashara London Lounge?

Akajibu ni kweli mwenyewe inatakiwa aende kuomba kibali cha maegesho na ataletwa mtu wa Ushuru pale. Hili likifanyika, ata gari zipaki hadi zifunge njia hazitakamatwa.

Nikashangaa sana. Kwahiyo mimi nalipishwa Tsh 210,000 kwa sababu mtu wa kutoza Tsh 500 kwa saa hayupo ila nyie wa kutoza Tsh 210,000 mpo????

Nikamuuliza kwa hiyo hiyo faini nikiandikiwa nitailipa kwa muda gani?

Akajibu akasema siku yoyote ila gari utachukua utakapo kamilisha malipo ila hii Tsh 10,000 kwa siku itaendelea kukua.

Wacha niishie hapo na maelezo yangu.

Swali langu. Je, serikali ya sasa imeona hii ni njia sahihi kweli?? Baada ya malalamiko yote iliyojinasibu kuyafanyia kazi kuhusu watu kufunga biashara zao.

Sababu mimi binafsi sitakanyaga tena London Lounge kwa hichi kilichonipata leo na rafiki yangu yoyote atakayependekeza twende mahali hapo nitamueleza haya na tutaelekea sehemu nyingine. Serikali ya sasa katika hili nanyi pia mtaaua biashara za watu.
 
Habari Wadau!

Wiki hii katika harakati zangu nimekumbana na kadhia ambayo ikanisikitisha sana. Ilikuwa majira ya mchana niliposimamisha harakati zangu na kuelekea sehemu ya kupata chakula cha mchana.

Nilipofika pale kama ilivyo siku nyingine zote ambazo huwa naenda kula mahali hapo, nikaegesha gari pembezoni mwa barabara kwani kijiwe hicho kama ilivyo vijiwe vingine vingi tu vya hapa DSM hakina maegesho maalumu ya magari ya wateja.

Baada ya kuegesha gari nikaingia ndani na kuagiza chakula na maji ya kukata kiu nikisubiri chakula. Ghafla nikashtuliwa na mtu akiniambia kuwa angalia gari yako inafungwa kule. Kuangalia kweli nawaona vijana na suti zao nyeusi wanaendelea kufunga nyororo na chuma kwenye gurudumu la mbele.

Nikahamaki nikaenda kwa haraka na kuwasha gari ili niliweke pembeni kuepuka usumbufu na hasara zisizo za lazima ambazo niliona zinafata wakati bado jamaa anaendelea na zoezi lake la kufunga. Lakini nikashtuka kuwa nitaharibu gari kwani alishazungusha chuma kwenye gurudumu.

Majibizano yalifata kila pande ikionesha iko sahihi bila mafanikio yoyote kwani niliona ni dhahili kuwa hawa jamaa wanachokifanya ni kuvidhia na kufunga magari ya watu ili wajipatie pesa tu. Baada ya kuona wameanza niletea habari za faini ya hili kosa ni Tsh 210,000.00 na ukiendelea kuleta ubishi tunaita break down tunavuta gari na gharama itakuwa yangu. Na mimi wakati huo hiyo pesa sina nikaona ni bora niendeshe hadi huko ofisini kwao (wenyewe wanaita yard) zilizopo Ubungo Mawasiliano Stendi labda kama ni faini nitapewa muda nitalipa au pengine nitakutana na mtu ambaye tunaweza ongea kwa kusikilizana na kuheshimiana bila kutishana tishana.

Kufika ofisini kwao wakajaza fomu zao pale wakanikabidhi kwa mwenzao. Nikaanza kwa kumuuliza kwanini mnakamata gari imeegeshwa pembezoni mwa barabara bila ata kuathili watumiaji wengine na ni sehemu ya biashara inayoonekana kabisa? Pia kwa muda mrefu tu nimekuwa nikipaki pale pale walipoikuta gari na kula chakula hadi namaliza naondoka bila shida yoyote?

Majibu yake ndio yalinifanya nimkumbuke Hayati Rais Magufuli.

Alisema enzi za Magufuli haya mambo ya mawakala wa halmashauri hayakuwepo. Aliyakataa. Ila kwa sasa yamerudi. So jitahidi kuwa makini unapoegesha gari lako kama yule mtoza ushuru wa maegesho ya magari hatakuwepo.

Akanieleza kuwa ni kweli faini kwa gari ndogo ni Tsh 200,000 na Tsh 10,000 ni gharama ya gari kupaki yard kwa siku moja.
Nikamuuliza tena hamuoni kuwa mnaua Biashara London Lounge?

Akajibu ni kweli mwenyewe inatakiwa aende kuomba kibali cha maegesho na ataletwa mtu wa Ushuru pale. Hili likifanyika, ata gari zipaki hadi zifunge njia hazitakamatwa.

Nikashangaa sana. Kwahiyo mimi nalipishwa Tsh 210,000 kwa sababu mtu wa kutoza Tsh 500 kwa saa hayupo ila nyie wa kutoza Tsh 210,000 mpo????

Nikamuuliza kwa hiyo hiyo faini nikiandikiwa nitailipa kwa muda gani?

Akajibu akasema siku yoyote ila gari utachukua utakapo kamilisha malipo ila hii Tsh 10,000 kwa siku itaendelea kukua.

Wacha niishie hapo na maelezo yangu.

Swali langu. Je, serikali ya sasa imeona hii ni njia sahihi kweli?? Baada ya malalamiko yote iliyojinasibu kuyafanyia kazi kuhusu watu kufunga biashara zao.

Sababu mimi binafsi sitakanyaga tena London Lounge kwa hichi kilichonipata leo na rafiki yangu yoyote atakayependekeza twende mahali hapo nitamueleza haya na tutaelekea sehemu nyingine. Serikali ya sasa katika hili nanyi pia mtaaua biashara za watu.
Dar es salaam ndiyo mkoa pekee wamachinga wanaruhusiwa kufanya biashara popote hata katikati ya barabara,ila ukipaki gari pembezoni mwa barabara ufanye manunuzi dukani gari inakamatwa.

Walishawahi nikamata miaka flani pale kariakoo kwa wrong parking kwa kunivizia.Halafu kitu kingine cha ajabu kabisa hata wale wanaofanya biashara sehemu hiyo hawakupi kabisa tahadhari,sijui wanapewaga tips
 
Ukweli kupaki magari sehem ambayo sio sahihi inaleta kero sana, Ila kwa faini ya tshs 200,000 ni nyingi sana , naona hapo kuna maslahi binafsi yamejificha , hili jambo liangaliwe vizuri na serekali kuu
 
Back
Top Bottom