Ukicheza Simba SC hakuna lisilowezekana - Pape O. Sakho athibitisha kwa vitendo

denooJ

JF-Expert Member
Mar 31, 2020
18,511
68,141
Wazungu wanasema; The Sky is the Limit.

Hii kauli itatimia kwa mchezaji wa mpira wa miguu yeyote atakayejitahidi aichezee klabu ya Simba ya Tanzania.

Alianza Samatta, kutoka Simba SC akaenda Mazembe, baada ya hapo akawa mfungaji bora na kuitangaza nchi kimataifa mwishowe akaenda zake Ulaya.

Jana usiku mchezaji kutoka Senegal, Pape O. Sakho, ametambulishwa kwenye ulimwengu wa soka duniani kupitia Simba SC, nina hakika huyu Sakho kuna raia wa Senegal waliokuwa hawamfahamu kabisa.

Lakini nguvu ya mashabiki wa Simba SC mitandaoni, hawa wapenzi, wanachama na mashabiki wa Simba kwa umoja wao wakiungana kusimamia jambo lao, hakuna yeyote wa kuwazuia, sio tu hapa Tanzania, au Afrika Mashariki na kati, bali ni kwa bara zima la Afrika.

Naandika haya sio kwa kusifia bila sababu, hapana, yeyote anayeona sina sababu aende akaangalie idadi ya followers ya mashabiki wa Simba SC kwenye mitandao, aanzie FB, aende twitter, kisha akamalizie na Instagram halafu alete majibu hapa.

Hata huyu jamaa yao aliyepigwa "rungu la utosini" jana na Kamati ya Maadili TFF, sehemu kubwa ya followers wake anaotamba nao leo, aliwapata akiwa Simba SC, this is the truth, usirushe ngumi mtani!
 
Hivi leo kama ikitokea klabu inataka kumnunua Sakho, naamini thamani yake imepanda mara mia mbili kutokana na ile tuzo aliyopokea jana.

Hii ni sawa na kusema Simba SC ina jiwe la "ruby" kwenye kikosi chake!.
 
Jaribuni kutohusisha Simba kwenye hili swala la Sakho kubeba tunzo,mkihusisha Simba kuna watu wanaumia wanateseka maumivu wanayopata ni makubwa mno.
Sasa tufanyeje? hatuwezi kusema Simba SC ni timu iliyopo Afghanistan wakati inajulikana ipo Tanzania, nawashauri wavumilie tu kwa kweli, haya maumivu hayamalizwi na Panadol.
 
Kule BBC sports nako ni habari kubwa .... "...Long-standing Senegalese boss Aliou Cisse won coach of the year, with his side named men's team of the year, while Pape Sarr was named young player of the year and another Senegalese, Pape Ousmane Sakho, won best goal for his overhead kick for Tanzanian side Simba..."
 
Kule BBC sports pia ni habari kubwa .... "...Long-standing Senegalese boss Aliou Cisse won coach of the year, with his side named men's team of the year, while Pape Sarr was named young player of the year and another Senegalese, Pape Ousmane Sakho, won best goal for his overhead kick for Tanzanian side Simba..."
"Tanzanian Side Simba" this is from BBC.

Sasa hebu zunguka huko ulimwenguni uwaulize kama wanaijua utopolo?!

Wakikuuliza ndio nini hicho, waambie ni aina ya vyura wa kipekee wanaopatikana Tanzania.
 
Wazungu wanasema; The Sky is the Limit.

Hii kauli itatimia kwa mchezaji wa mpira wa miguu yeyote atakayejitahidi aichezee klabu ya Simba ya Tanzania.

Alianza Samatta, kutoka Simba SC akaenda Mazembe, baada ya hapo akawa mfungaji bora na kuitangaza nchi kimataifa mwishowe akaenda zake Ulaya.

Jana usiku mchezaji kutoka Senegal, Pape O. Sakho, ametambulishwa kwenye ulimwengu wa soka duniani kupitia Simba SC, nina hakika huyu Sakho kuna raia wa Senegal waliokuwa hawamfahamu kabisa.

Lakini nguvu ya mashabiki wa Simba SC mitandaoni, hawa wapenzi, wanachama na mashabiki wa Simba kwa umoja wao wakiungana kusimamia jambo lao, hakuna yeyote wa kuwazuia, sio tu hapa Tanzania, au Afrika Mashariki na kati, bali ni kwa bara zima la Afrika.

Naandika haya sio kwa kusifia bila sababu, hapana, yeyote anayeona sina sababu aende akaangalie idadi ya followers ya mashabiki wa Simba SC kwenye mitandao, aanzie FB, aende twitter, kisha akamalizie na Instagram halafu alete majibu hapa.

Hata huyu jamaa yao aliyepigwa "rungu la utosini" jana na Kamati ya Maadili TFF, sehemu kubwa ya followers wake anaotamba nao leo, aliwapata akiwa Simba SC, this is the truth, usirushe ngumi mtani!
Hii ni habari mbaya kwa wale washabiki oya oya wa Yanga kama kina Demigod,Anduru na vilaza wenziwe
 
"Tanzanian Side Simba" this is from BBC.

Sasa hebu zunguka huko ulimwenguni uwaulize kama wanaijua utopolo?!

Wakikuuliza ndio nini hicho, waambie ni aina ya vyura wa kipekee wanaopatikana Tanzania.
20220712_155125.jpg

Mavyura maarufu aina ya utopolo
 
Nikweli Ukichezea Simba hakuna linalo shindikana, kitendo Cha kufanya mambo ya kishirikina uwanjani Kwa kuwasha moto Tena ugenini nimeamini Kwa Simba hakuna linalo shindikana.
 
Back
Top Bottom