G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,874
Hivi hawa wasanii wanaojitokeza eti wanataka kuwania ubunge wanajipima kweli? Kwakuwa wameona wanaweza kupata dezo kutokana na upuuzi unaoendelea ndani ya CCM kwa sasa basi wameona sehemu ya wao kupata mpunga wa laini laini ni kwenye ubunge! Hovyo kabisa kabisa
Sasa wamegeuka watu wa kusifia mpaka akili zimewaruka kabisa, wamewehuka kuliko kuwehuka kwenyewe. Yani wanaona sehemu sahihi ya wao kukimbia kutafuta kwa jasho ni kwenye ubunge. Ushenzi huu kiuhalisia umesababishwa na hii CCM ya leo ambayo imepoteza kabisa hata ule uhalisia waliokuwa nao
Eti Steve Nyerere anataka Ubunge, sijui kina Shilole eti wanataka na wao kuitwa waheshimiwa! Kweli! Kwanza ili uwe mbunge ni lazima kwanza ujitambue, hawa hakuna anayejitambua
Warudi nyuma wamuangalie Sugu alivyokuja na uthubutu mwaka 2010 akiwa katikati ya fitina za CCM akapenya tena kutokea upinzani. Huyu ukimuangalia tu na mazingira aliyokuwepo ni mtu anayejua maana ya Ubunge! Alithubutu kwa kutumia akili na utashi.
Mwenzake Prof. Jay ambaye walianza wote mziki akajiandaa kwa miaka mitano ya ziada kutengeneza mazingira naye akapenya tena ndani ya mkoa wenye kila aina ya figisu dhidi ya upinzani. Huyu anajielewa na alijipima kwa kina ikiwemo kujijenga kwa muda si chini ya miaka 10.
Yupo mwanadada Jay Dee ama Jide ambaye naye ni mkongwe, ameiva na hata ukimtazama unasema yes. Huyu akijitambua akaenda kwao ukuryani akachukua jimbo basi mapema tu anashinda. Amejijenga kwa miaka 15 sasa. Hawa ni watu pekee ambao hawajawahi kutegemea mbeleko ya dola. Walipambana kama walivyoanza kwenye mziki.
Hawa wa sasa eti utasikia anakwambia Rais kasema nigombee jimbo fulani, eti natekeleza maagizo ya Rais. Upuuzi mtupu! Ujinga wa kiwango chake! Unagombea ubunge eti unatekeleza maagizo ya Rais! What a shame! Eti ndiyo wasanii wetu hao.
Karibu sana kamanda mwingine uliyeiva Jide. Nakukubali na unajielewa nakuomba uianze safari uliyoiandaa kwa miaka 10 sasa! Unaweza kusimama pekee na unanikosha zaidi kuwa ni mwanamke unawazidi uwezo kwa mbali sana hawa wasanii uchwara wanapenda eti kugombea kwa kutimiza matakwa ya fulani.
Ukumbi wa bunge siyo sokoni useme eti umetumwa bidhaa fulani!
Sasa wamegeuka watu wa kusifia mpaka akili zimewaruka kabisa, wamewehuka kuliko kuwehuka kwenyewe. Yani wanaona sehemu sahihi ya wao kukimbia kutafuta kwa jasho ni kwenye ubunge. Ushenzi huu kiuhalisia umesababishwa na hii CCM ya leo ambayo imepoteza kabisa hata ule uhalisia waliokuwa nao
Eti Steve Nyerere anataka Ubunge, sijui kina Shilole eti wanataka na wao kuitwa waheshimiwa! Kweli! Kwanza ili uwe mbunge ni lazima kwanza ujitambue, hawa hakuna anayejitambua
Warudi nyuma wamuangalie Sugu alivyokuja na uthubutu mwaka 2010 akiwa katikati ya fitina za CCM akapenya tena kutokea upinzani. Huyu ukimuangalia tu na mazingira aliyokuwepo ni mtu anayejua maana ya Ubunge! Alithubutu kwa kutumia akili na utashi.
Mwenzake Prof. Jay ambaye walianza wote mziki akajiandaa kwa miaka mitano ya ziada kutengeneza mazingira naye akapenya tena ndani ya mkoa wenye kila aina ya figisu dhidi ya upinzani. Huyu anajielewa na alijipima kwa kina ikiwemo kujijenga kwa muda si chini ya miaka 10.
Yupo mwanadada Jay Dee ama Jide ambaye naye ni mkongwe, ameiva na hata ukimtazama unasema yes. Huyu akijitambua akaenda kwao ukuryani akachukua jimbo basi mapema tu anashinda. Amejijenga kwa miaka 15 sasa. Hawa ni watu pekee ambao hawajawahi kutegemea mbeleko ya dola. Walipambana kama walivyoanza kwenye mziki.
Hawa wa sasa eti utasikia anakwambia Rais kasema nigombee jimbo fulani, eti natekeleza maagizo ya Rais. Upuuzi mtupu! Ujinga wa kiwango chake! Unagombea ubunge eti unatekeleza maagizo ya Rais! What a shame! Eti ndiyo wasanii wetu hao.
Karibu sana kamanda mwingine uliyeiva Jide. Nakukubali na unajielewa nakuomba uianze safari uliyoiandaa kwa miaka 10 sasa! Unaweza kusimama pekee na unanikosha zaidi kuwa ni mwanamke unawazidi uwezo kwa mbali sana hawa wasanii uchwara wanapenda eti kugombea kwa kutimiza matakwa ya fulani.
Ukumbi wa bunge siyo sokoni useme eti umetumwa bidhaa fulani!