Mdudu halisi
JF-Expert Member
- May 7, 2014
- 2,730
- 4,768
Ni rahisi sana kumng'oa huyu mzee pale Newala. Tatizo litakalopelekea ashindwe kung'oka ni mpasuko ndani ya CUF ambacho ndicho chama pinzani chenye nguvu pale Newala Mjini. Kuna jamaa aliyepambana na Mkuchika katika uchaguzi uliopita, anaitwa Manguya.
Jamaa anakubalika hadi leo licha ya kwamba alishindwa uchaguzi uliopita baada ya polisi kuwapiga mabomu wananchi na kisha kumtangaza Mkuchika kuwa mshindi huku moshi wa mabomu ukifuka. Kama suluhisho likipatikana kwa makundi yanayokinzana ndani ya CUF ni dhahiri ya kwamba CCM hawatakuwa na chao pale Newala Mjini ifikapo 2020.
Jamaa anakubalika hadi leo licha ya kwamba alishindwa uchaguzi uliopita baada ya polisi kuwapiga mabomu wananchi na kisha kumtangaza Mkuchika kuwa mshindi huku moshi wa mabomu ukifuka. Kama suluhisho likipatikana kwa makundi yanayokinzana ndani ya CUF ni dhahiri ya kwamba CCM hawatakuwa na chao pale Newala Mjini ifikapo 2020.