Tutafika
JF-Expert Member
- Nov 4, 2009
- 1,443
- 631
Mwanzoni ilianzia kwa wapinzani (kina Zitto) kwamba serikali imefilisika, imeishiwa, haikopesheki..n.k, kama kawaida CCM wakaona hii hoja ni kweli lakini ikibebwa na wapinzani, itakua balaa!, haraka haraka Mkulo alikanusha vikali sana. Tukaendelea kuchechemea katika ukweli ule (Ukata), mara migomo ikaanza kuibuka ya watoto wa vyuo na walimu nao wakaanza vitisho (kama kawaida yao), baadae ikabidi Mkulo awahi haraka sana kupanua mkopo kutoka benki za ndani, basi tukapumua kidogo.
Sasa ndani tumekopa tumemaliza, Nje ndio tulishamaliza zamani, hatuna pa kukimbilia kukopa ili kuendelea kuficha ule ukweli (Ukata), tunalazimika kusema ukweli, liwalo na liwe!
Ghafla Mkuchika akapiga mbiu, jamani ukataaaaa!, JK nae akadakia, UKATAAAAA! (Ila tuko makini hatuwezi kumtuma Mkulo yule yule kusema hili japo mambo ya ukata na ukwasi ndie anaehusika zaidi), Haya!
SASA NDUGU YANGU MPENDWA JK, Kwanini ulilainika ukasitisha utekelezaji wa mipango hii ambayo ulijaribu ''kuthubutu''?
1. Mpango wa kutenganisha biashara na siasa
2. Mpango wa kuondoa msamaha wa kodi katika taasisi za dini
Inawezekana hukuzibuni wewe na aliezibuni hakukushawishi vya kutosha kwamba utekelezaji wake ingekua mkombozi mkubwa kutoka katika janga la ukata!, au inawezekana kelele za Wafanyabiashara, Maaskofu na Masheikh zilikutisha sana!, au inawezekana yote hayo sio sababu hata kidogo iliyokufanya ukachelea kutekeleza hiyo mipango. NAKUSHAURI USIKOMAZE SHINGO, GEUKA MZEE!
Sasa ndani tumekopa tumemaliza, Nje ndio tulishamaliza zamani, hatuna pa kukimbilia kukopa ili kuendelea kuficha ule ukweli (Ukata), tunalazimika kusema ukweli, liwalo na liwe!
Ghafla Mkuchika akapiga mbiu, jamani ukataaaaa!, JK nae akadakia, UKATAAAAA! (Ila tuko makini hatuwezi kumtuma Mkulo yule yule kusema hili japo mambo ya ukata na ukwasi ndie anaehusika zaidi), Haya!
SASA NDUGU YANGU MPENDWA JK, Kwanini ulilainika ukasitisha utekelezaji wa mipango hii ambayo ulijaribu ''kuthubutu''?
1. Mpango wa kutenganisha biashara na siasa
2. Mpango wa kuondoa msamaha wa kodi katika taasisi za dini
Inawezekana hukuzibuni wewe na aliezibuni hakukushawishi vya kutosha kwamba utekelezaji wake ingekua mkombozi mkubwa kutoka katika janga la ukata!, au inawezekana kelele za Wafanyabiashara, Maaskofu na Masheikh zilikutisha sana!, au inawezekana yote hayo sio sababu hata kidogo iliyokufanya ukachelea kutekeleza hiyo mipango. NAKUSHAURI USIKOMAZE SHINGO, GEUKA MZEE!