Amavulandlela
New Member
- Jul 6, 2009
- 2
- 0
Ndugu zangu, naomba kutoa angalizo kuhusu haya mashindano ya Miss Tanzania. Ikumbukwe kuwa hayo mashindano yameendeshwa wakati wenzetu Wazanzibari wamekumbwa na msiba uliotamkwa kuwa wa kitaifa na viongozi wa nchi hii kutangaza siku tatu za maombolezo. Kwa kuwa waandaji wakiongozwa na Hashim Lundenga na timu yake ya Mafia na wadhamini wakiongozwa na Vodacom wamepuuzia haya yaliyojiri, naomba kutoa hoja kuwa Watanzania wayalaani haya mashindano na kuyasusia mpaka atakapopatikana mtu mwingine wa kuyaandaa. Aidha BASATA waone busara kumsimamisha Lundenga kuanzia sasa. Vilevile huyo mrembo aliyepatikana jana asitishwe kuhudhuria hayo mashindano ya Miss World kama mfano kwa wakaidi wanaopuuzia maswala nyeti ya kitaifa!! Naomba kuwasilisha!!