Ukaguzi Wa Magari Ya South Africa

Domo Kaya

JF-Expert Member
May 29, 2007
531
59
Jamani watanzania wenzangu naombeni kuuliza kuhusu huu ukaguzi unaoendelea kuhusu magari yalioyoibiwa south Africa ni halali?????? mtu umedungiliza umenunua gari lako zuri ili likusaidie ktk kuwahi makazini unafika barabarani unasimamishwa eti makaburu walikague kama ni la wizi huku wewe unachelewa kazini. Swali je kama Mtanzania kaibiwa gari na ameenda South Africa kuomba ukaguzi kama huu ufanyike nchini kwao watakubali.?? Nchi yetu imezidi kuendekeza ngozi nyeupe au kwa sababu Rais wetu anaenda nchi na ulaya kuomba misaada kila kukikucha. Wenzetu Wakenya wamekataa zoezi hili lisifanyike chini kwao vipi sisi tukubari kila kitu wazungu wanachoamua?????
 
eti makaburu walikague

Kaka inabidi uangalie kwanza lugha yako, si vizuri kuwaaita binadamu wenzako lugha za Kejeli. Lakini ni kweli kuwa magari mengi yanaibiwa Afrika kusini yanauzwa Tanzania. Mengine hayaibiwa isipokuwa yanauzwa na wenyewe tena wanakusaidia kulivusha mpaka Botswana halafu wanatanganza kwao kuwa wameibiwa ili waweze kupewa jipya na bima. Kwa hiyo kazi wanayofanya ni halali kwa sababu Dar ni sehemu ambayo kuna magari mengi ya wizi. Again watch your language.
 
Kaka inabidi uangalie kwanza lugha yako, si vizuri kuwaaita binadamu wenzako lugha za Kejeli. Lakini ni kweli kuwa magari mengi yanaibiwa Afrika kusini yanauzwa Tanzania. Mengine hayaibiwa isipokuwa yanauzwa na wenyewe tena wanakusaidia kulivusha mpaka Botswana halafu wanatanganza kwao kuwa wameibiwa ili waweze kupewa jipya na bima. Kwa hiyo kazi wanayofanya ni halali kwa sababu Dar ni sehemu ambayo kuna magari mengi ya wizi. Again watch your language.

Naomba nikuulize ndugu yangu hivi wa-sauth africa wanaitwaje kama sio makaburu???????? naomba nipe jina lao tafadhari.
 
Naomba nikuulize ndugu yangu hivi wa-sauth africa wanaitwaje kama sio makaburu???????? naomba nipe jina lao tafadhari.

Teh,teh,te..... labda alitaka uwaite wazungu! Maana hata mimi simuelewi. Labda atusaidie jina la kiuungwana.
 
Jamani kumwita mtu mkaburu si tusi si ndio tafsiri ya Boers kwa kimombo au?
Alafu hao watu sio wastaarabu kabisa wana kiburi mno jana walikuja ofisin wakavunja baadhi ya sheria za kiusalama nikawareport.
Serikali inawaendekeza tuu hatuwakatazi kuja ila nasi ngozi nyeupe twaishadadia uku tukijishusha kwa kishindo ndo maana nao wanafanya mambo kama wako kwao.
Mbaya zaidi wakishakukagua na kijlaptop chao hawakupi clearance certificate so unaweza kutana nao tena next week wakakukagua.
Something must be done here comrade hatuwezi buruzwa eti kisa Mzungu.
Sisi ndo tumpe mwongozo sio wao ndo watuburuze.
 
Mwakasege go back to the books. Kaburu ina maana zaidi ya mzungu aliyezaliwa na kukulia Afrika Kusini ambaye asili yake ni Uholanzi, ina maana pia ni mzungu na mbaguzi, hili neno hasa lilikuja wakati wa ubaguzi wa rangi kule Afrika Kusini. Hata hivyo magari hayo sio kama "wanaibiwa" wao tu, hata weusi wanaibiwa pia. Unajua ni vizuri kumuta biaadamu mwenzio kwa jina zuri, sio vizuri kumtambulisha mwenzio kwa rangi yake....kama unakumbuka hata JKN aliwahi kuwaita baadhi ya watu Tanzania ndani ya CCM ni makaburu, what did he mean?
 
Mwakasege umeongea hawa wazungu wamezidi kutupelekesha sana. Kwa siku unaweza kukaguliwa hata mara tatu kwa wakati tofauti maana wapo kila barabara. Sasa sisi hatuna kazi ya kufanya zaidi ya kukaguliwa magari tu, kisa magari yameibiwa nchini kwao. Tumechoka kufanywa watumwa na hizi ngozi nyeupe.
 
Haya mambo yalikuwa yakijinga sana wanashindwa kuzuia wizi kwao wanavuka mpaka Bongo Land kufanya ukaguzi aisee kweli lilikuwa shamba la bibi
 
Wale walikua ni matapeli mbona hawaendi hapo mozambique kukagua wanajifanya eti gari la wizi Tanzania na yaliyoibiwa Tanzania na huku yapo inakuaje hapo..walikua wanatafuta scraper that time kulikua na uhaba sana wa scraper ikabidi warudishe vyuma chakavu bure wao waendelee kupiga hela Mkuu wa police wakati huo ndio huyu anasota jela kwa kura rushwa kubwa kubwa tuu..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom