Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 13,832
- 15,836
Nimesoma kwa masikitiko sana pale Dr. Lwaitama alipoelezea msimamo wa UDASA kuhusu mgogoro wa kisiasa uliopo Kenya hivi sasa na kugusia wasiwasi wake kuhusu kuanza kwa vyama vyenye mlengo wa ukabila pale UDSM.
Kwa maoni yangu, nadhani kuwa tabia hii ya ukabila ilianza wakati wa utawala wa awamu ya pili ambapo mikutano ilikuwa inaitishwa na watu wa kutoka eneo fulani la nchi ili kuchangia maendeleo ya eneo lao. Juzi juzi kulikuwa na mkutano wa aina hiyo uliofanywa na watu wa Kagera. Inawezekana tatizo la Ukabila likatukumba na sisi baada ya muda si mrefu endapo hatutakuwa makini. Mwanzo wa Ngoma ni lele
"Katika hili, sisi pia tunasikitishwa na tabia za ukabila hasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia vyama vya wanafunzi vya kikabila, tunawashauri wanafunzi kuanzisha vyama vyenye sura ya kitaifa na kizalendo, vyuo vikuu vinatakiwa kuwa vituo mkakati vya mapambano dhidi ya ukabila, ubeberu na ufisadi, visiwe makambi ya maovu hayo," alisisitiza Dk Lwaitama
Kwa maoni yangu, nadhani kuwa tabia hii ya ukabila ilianza wakati wa utawala wa awamu ya pili ambapo mikutano ilikuwa inaitishwa na watu wa kutoka eneo fulani la nchi ili kuchangia maendeleo ya eneo lao. Juzi juzi kulikuwa na mkutano wa aina hiyo uliofanywa na watu wa Kagera. Inawezekana tatizo la Ukabila likatukumba na sisi baada ya muda si mrefu endapo hatutakuwa makini. Mwanzo wa Ngoma ni lele