UK-Africa Investment Summit 2020: Where is top level Tanzania representative?

Biashara fursa na mipango ndio waingereza wanachofanya.

Hawa wenzetu awachezi kamali na maswala uchumi haya ni maandalizi ya life after BREXIT.

Ukiwa ndani ya jumuiya trade negotiations zilikuwa chini ya block control kwa lugha nyingine wana negotiate kwa pamoja hakuna kufanya mambo individually ndio maana wakaja na EPA.

UK wanatoka EU by next year watakuwa full independent and responsible na uchumi wao ivyo inabidi wawe na trade zao kote duniani sio Africa tu hata EU itabidi wanegotiate nao upya jinsi yakufanya nao biashara. Ndio maandalizi yenyewe.

Kuna faida gani kwa Africa, picture this kwa EU member state hakuna ushuru wa kuagiza bidhaa nchi moja kwenda nyingine. Maana yake nini mfano muuzaji mkubwa wa maua EU ni Kenya na kwa sasa yanaingia kupitia Holland; retailers wa EU wana nunua ndio yanasambazwa nchi nyingine freely gharama ni usafiri tu.

UK wakitoka EU either inabidi wawe na deal nzuri na block kwenye hizi movement za bidhaa hili kusiwe na madhara ya bei au sasa waagize wenyewe maua kutoka Kenya.

Sasa imagine kuna bidhaa ngapi zinatoka nchi za Africa ambazo main supplier yupo nje ya UK na kutakuwa na impact gani wasipota trade nzuri na EU?

Kuondoa hayo madhara baada ya BREXIT ndio sasa wanatafuta trade zao wenyewe; UK kuna waafrica wengi pia na asilimia kubwa ya vyakula vyao main supplier wapo Holland (wao ndio wananunua Africa au nchi zingine) na kuuzia UK retailers.

Sie tuendelee kujifungia tu, fursa zitatufuata because we are very special breed in planet earth.
'Sie tuendelee kujifungia tu, fursa zitatufuata because we are very special breed in planet earth.'

Hahah no wonder Kigwangala alipoulizwa mna mpango wowote ule wa kuidhamini timu huko EPL ili itangaze utalii wetu akasema hapana lkn mpk timu kubwa za ulaya(Man u,Chelsea,Arsenal) hua zina tubembeleza tuzidhini,hahah akili zetu bana.

dodge
 
UK ni moja wa nchi yenye FDIs nyingi na inayotoa misaada mingi Tanzania. Kuikwepa ni sawa na kuingiza kichwa chini ya mchanga huku kiwiliwili chote kipo nje.

Kwahiyo ule mkutano ni wakujihakikishia uwekezaji zaidi?
 
Acha mawazo finyu mkuu achana na wengine wa jumuia ya madola. Tunaongelea sisi kama watanzania nchi hii ina watu zaidi ya milion 50, wasomi na wasio wasomi, wakulima, wajasiliamali n.k wote wanatafuta fursa. Si rais wetu kila siku anaongea kuhusu swala la fursa sasa hiyo ni nini? Kila akiapisha balozi anasisitiza waende wakalete wawekezaji si ndiyo? Halafu yeye mwenyewe kwenye fursa kama hizo anakaa kando:(. Ndiyo maana tunashindwa hata na Rwanda na hili ni tatizo la watu wenye mawazo kama yako mkuu. Hawatolipeleka hili taifa mbali shauri ya muono hafifu wa uchumi na maendeleo.
Mnangagwa alikuwa DAVOS last year na aliona msaada.Je alipewa?
 
Wewe unaamini kweli kuwa UK inataka kufanya biashara na Afrika?

Kama kweli mbona wao wanafanya biashara na wachina wakati sisi wanatuzuia?

Umeamka sasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Nisiamini vipi kwani kilichofanyika ni siri? Kongamano hilo lilikuwa la kuipa fursa Africa kufanya biashara na UK sababu UK ikishatoka EU itakuwa na uwezo wa kufanya biashara moja kwa moja na nchi yeyote. Sio kama sasa biashara nyingi lazima zifate masharti ya EU. Kuhusu swala la kwa nini UK wanatuzuia kufanya biashara na China wakati wao wanafanya nao?? Wewe aliyekwambia UK wanatuzuia sisi kufanya biashara na wachina nani??? Hebu acha maneno ya uzushi yasiyo na ushahidi.
 
Haya ni mapambano ya kisiasa na kiuchumi kati ya Umoja wa nchi za Ulaya na Uingereza baada ya kujitoa kwenye Jumuiya ya nchi za Ulaya.

Hoja ya msingi sio kuhudhuria summit bali kuchagua upande wa vita ya kiuchumi kati ya Umoja wa Nchi za Ulaya na Uingereza!
Kwa hiyo nyie mmechagua Ulaya?
 
Komenti za ajabu sana hizi.

Kwani ni lazima kuchagua upande?

Matokeo ya haya yanayofanywa na serikali ya awamu hii bila shaka tutayajutia hapo baadae tukishayaona matokeo yake ambayo hayapo sasa hivi, na watu wala hawajishughulishi kuzitambua athari zitakazotukabili, na hata bila kujishughulisha hata kuzichambua tu tuzijue.

Sisi tumekomalia kuwa ni matajiri, na wengine wote wanatafuta tu kuja kutuibia utajiri wetu. Na bado watu na akili zao wanaamini mambo kama haya.

Nchi haikatazwi kulinda mali zake, lakini nyakati hizi sio za kujitenga na dunia.

Hapo namwona Rwanda, Uganda, Kenya..., wote washirika wetu kwenye jumuia yetu ya Afrika Mashariki. Sisi tutakuwa soko la hawa wenzetu bila ya ubishi.

Hata tukiamua kuwa na TanzaExit yetu hatutafua dafu, tutakwenda wapi! SADC nako hapatatosha na huko AfCFTA tutauziwa tu na hawa wenzetu wanaojenga misingi ya uwekezaji imara katika wakati 'critical' kama huu.

BTW: Hivi 2019 tumepata FDI kiasi gani? Hata kutaja tu siku hizi inakuwa ni aibu?
Kama mna akili finyu wakati mwingine mkae kimya tu badala ya kubwata mambo ambayo hamyajui.

Rwanda baada ya vita wasamalia wema wamewapa pesa kibao. Wako wangapi? Wana soko gani ukilinganisha na sisi?

Kenya imeweka rehani bandari yake ya Mombasa kwa SGR ambayo imekost hela nyingi kuliko SGR yetu ya umeme kwa wachina. Uhuru alienda tena kukopa kwa ajili ya kuendeleza Reli amenyimwa. Sasa unata kutuambia nini? Kenya ni vibaraka wa Europe. Bila Europe Kenya haiwezi ku exist. Wakenya ni wanafiki sana. Kila kitu mzungu anacho taka nao wanakubali bila kujiuliza. Wakenya sio watu wa kuwaamini hata mara moja.

Wazungu lazima watupige vita sisi, kwani wanajua kuwa tukifanikiwa sisi tutakuwa mfano kwa nchi nyingi za Afrika. Wanaliogooa hilo. Hawata kuwa na watu wa kuwaheshimu na kuwasujudu tena. Wa Asia wanajiamini na kufanya mambo yao.
 
Saa zingine mi vizuri kuwa na kiburi cha uzima, if we can do things on our own, kuna ulazima gani wa kwenda kutembeza bakuri kwa mabeberu?
Sisi tuendelee na juhudi zetu za kujifamyia mambo yetu na kujiletea maendeleo kwa kutumia nguvu zetu, wakituona 'we are not giving a f*ck' watakuja wao wenyewe kujikomba kwetu.
Ni msimamo mzuri sana. Asante.
 
You can say that, again and again..., huo ndio ukweli.
Nchi yetu Tanzania haijawahi, hata siku moja kuwa katika hali iliyomo kidiplomasia hivi sasa.

Tumebaki tu na wimbo "Economic Diplomaticy" bila hata ya kujishughulisha nayo. Mabalozi wanateuliwa na kupewa maagizo wafanye kivyao ambavyo hata 'support' kutoka nyumbani hakuna!

Wanabaki wanatishwa tu siku wanapolishwa viapo vyao, na hakuna lolote linalofuata baada ya hapo.
Ni tatizo la nani sasa? La Magu? Acha kelele. Kosa la Magufuli ni kuwa anawapeleka wasomi wa vitabu na sio wasomi ambao wanajua thamani ya vitu.
 
Kama mna akili finyu wakati mwingine mkae kimya tu badala ya kubwata mambo ambayo hamyajui.

Rwanda baada ya vita wasamalia wema wamewapa pesa kibao. Wako wangapi? Wana soko gani ukilinganisha na sisi?

Kenya imeweka rehani bandari yake ya Mombasa kwa SGR ambayo imekost hela nyingi kuliko SGR yetu ya umeme kwa wachina. Uhuru alienda tena kukopa kwa ajili ya kuendeleza Reli amenyimwa. Sasa unata kutuambia nini? Kenya ni vibaraka wa Europe. Bila Europe Kenya haiwezi ku exist. Wakenya ni wanafiki sana. Kila kitu mzungu anacho taka nao wanakubali bila kujiuliza. Wakenya sio watu wa kuwaamini hata mara moja.

Wazungu lazima watupige vita sisi, kwani wanajua kuwa tukifanikiwa sisi tutakuwa mfano kwa nchi nyingi za Afrika. Wanaliogooa hilo. Hawata kuwa na watu wa kuwaheshimu na kuwasujudu tena. Wa Asia wanajiamini na kufanya mambo yao.
Kwenye "akili finyu" hainipi shida kwa sababu nakufahamu vyema sana wewe kwa michango yako humu JF.

Kuhusu Kenya kuwa kibaraka na mnafiki, hapo nakupongeza sana kwa kulijua hilo, lakini sio jambo jipya ulilogundua wewe na kulifanya likuonyeshe wewe kutokuwa na akili finyu.

Kuhusu "wazungu kutupiga vita", hata mkijipiga vita nyinyi wenyewe mnalia "wazungu wanawapiga vita".

Sasa niambie, hii yako sio "akili finyu" kwa sababu gani?
 
Ni tatizo la nani sasa? La Magu? Acha kelele. Kosa la Magufuli ni kuwa anawapeleka wasomi wa vitabu na sio wasomi ambao wanajua thamani ya vitu.
Hapo tu, bado huoni unavyojipinga?
Kama sio kosa la Magufuli, kwa nini "awapeleke wasomi wa vitabu..."

Hivi unaelewa unachoandika, au unajiandikia tu!
 
Acha mawazo finyu mkuu achana na wengine wa jumuia ya madola. Tunaongelea sisi kama watanzania nchi hii ina watu zaidi ya milion 50, wasomi na wasio wasomi, wakulima, wajasiliamali n.k wote wanatafuta fursa. Si rais wetu kila siku anaongea kuhusu swala la fursa sasa hiyo ni nini? Kila akiapisha balozi anasisitiza waende wakalete wawekezaji si ndiyo? Halafu yeye mwenyewe kwenye fursa kama hizo anakaa kando:(. Ndiyo maana tunashindwa hata na Rwanda na hili ni tatizo la watu wenye mawazo kama yako mkuu. Hawatolipeleka hili taifa mbali shauri ya muono hafifu wa uchumi na maendeleo.
Rwanda ametushinda maeneo yapi na kwa kiwango gani be specific, kwa propaganda sawa
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom