UK-Africa Investment Summit 2020: Where is top level Tanzania representative?

Sasa mbona hiyo lugha ya kitaa uijue wewe tu, yaani hata Watanzania wenzio hawaifahamu, lugha za mtaani zipo kote hata huku.
Wamekwambia hilo neno ni kama 'Dogo' hadi wabongo wote walifahamu.... Angalia mwenzako hapo juu kalitumia kiufasaha zaidi.
 
Mcheza kwao hutuzwa. Au siyo?

Mara ya mwisho mkutano wa Heads of States wa EAC ulitakiwa ufanyike November 2019. Kina PK na wenzie wakapiga chenga. Pale makao makuu ya Jumuiya napafananisha na kijiwe kwa hali iliyopo.

Haya ya kwetu wanayashindwa, sembuse hayo ya kipumbavu kupitiliza? Economic diplomacy kama neno lilivyo halimaanishi umalaya unaofanywa na wapuuzi walovalia ngozi za uongozi.
 
Komenti za ajabu sana hizi.

Kwani ni lazima kuchagua upande?

Matokeo ya haya yanayofanywa na serikali ya awamu hii bila shaka tutayajutia hapo baadae tukishayaona matokeo yake ambayo hayapo sasa hivi, na watu wala hawajishughulishi kuzitambua athari zitakazotukabili, na hata bila kujishughulisha hata kuzichambua tu tuzijue.

Sisi tumekomalia kuwa ni matajiri, na wengine wote wanatafuta tu kuja kutuibia utajiri wetu. Na bado watu na akili zao wanaamini mambo kama haya.

Nchi haikatazwi kulinda mali zake, lakini nyakati hizi sio za kujitenga na dunia.

Hapo namwona Rwanda, Uganda, Kenya..., wote washirika wetu kwenye jumuia yetu ya Afrika Mashariki. Sisi tutakuwa soko la hawa wenzetu bila ya ubishi.

Hata tukiamua kuwa na TanzaExit yetu hatutafua dafu, tutakwenda wapi! SADC nako hapatatosha na huko AfCFTA tutauziwa tu na hawa wenzetu wanaojenga misingi ya uwekezaji imara katika wakati 'critical' kama huu.

BTW: Hivi 2019 tumepata FDI kiasi gani? Hata kutaja tu siku hizi inakuwa ni aibu?
Polepole mkuu.
Screenshot_2019-12-21-09-59-03-1.jpeg


dodge
 
Saa zingine mi vizuri kuwa na kiburi cha uzima, if we can do things on our own, kuna ulazima gani wa kwenda kutembeza bakuri kwa mabeberu?
Sisi tuendelee na juhudi zetu za kujifamyia mambo yetu na kujiletea maendeleo kwa kutumia nguvu zetu, wakituona 'we are not giving a f*ck' watakuja wao wenyewe kujikomba kwetu.
Unawavimbia mabeberu sio?
tapatalk_1574965554979.jpeg


dodge
 
Hao wa nchi nyingine ambao hawajahudhuria sisi wanatuhusu nini?
Ni Marais 14 wa nchi za Africa ndo wamehudhulia wengine hawakuhudhulia,Kwahiyo sio Tanzania peke yake


Sent from my iPhone using JamiiForums

dodge
 
Haya ni mapambano ya kisiasa na kiuchumi kati ya Umoja wa nchi za Ulaya na Uingereza baada ya kujitoa kwenye Jumuiya ya nchi za Ulaya.

Hoja ya msingi sio kuhudhuria summit bali kuchagua upande wa vita ya kiuchumi kati ya Umoja wa Nchi za Ulaya na Uingereza!
Naunagana na wewe.
 
Acha mawazo finyu mkuu achana na wengine wa jumuia ya madola. Tunaongelea sisi kama watanzania nchi hii ina watu zaidi ya milion 50, wasomi na wasio wasomi, wakulima, wajasiliamali n.k wote wanatafuta fursa. Si rais wetu kila siku anaongea kuhusu swala la fursa sasa hiyo ni nini? Kila akiapisha balozi anasisitiza waende wakalete wawekezaji si ndiyo? Halafu yeye mwenyewe kwenye fursa kama hizo anakaa kando:(. Ndiyo maana tunashindwa hata na Rwanda na hili ni tatizo la watu wenye mawazo kama yako mkuu. Hawatolipeleka hili taifa mbali shauri ya muono hafifu wa uchumi na maendeleo.
Rwanda inaishinda URT maeneo yapi haswa au ndiyo kazi zenu za kutumika kama toilet paper
 
Komenti za ajabu sana hizi.

Kwani ni lazima kuchagua upande?

Matokeo ya haya yanayofanywa na serikali ya awamu hii bila shaka tutayajutia hapo baadae tukishayaona matokeo yake ambayo hayapo sasa hivi, na watu wala hawajishughulishi kuzitambua athari zitakazotukabili, na hata bila kujishughulisha hata kuzichambua tu tuzijue.

Sisi tumekomalia kuwa ni matajiri, na wengine wote wanatafuta tu kuja kutuibia utajiri wetu. Na bado watu na akili zao wanaamini mambo kama haya.

Nchi haikatazwi kulinda mali zake, lakini nyakati hizi sio za kujitenga na dunia.

Hapo namwona Rwanda, Uganda, Kenya..., wote washirika wetu kwenye jumuia yetu ya Afrika Mashariki. Sisi tutakuwa soko la hawa wenzetu bila ya ubishi.

Hata tukiamua kuwa na TanzaExit yetu hatutafua dafu, tutakwenda wapi! SADC nako hapatatosha na huko AfCFTA tutauziwa tu na hawa wenzetu wanaojenga misingi ya uwekezaji imara katika wakati 'critical' kama huu.

BTW: Hivi 2019 tumepata FDI kiasi gani? Hata kutaja tu siku hizi inakuwa ni aibu?
Sisi hatutajuta kwa kuwa tunajua serikali inafanya nini.UK wanatuhitaji kuliko tunavyowahitaji. Kaa kimya
 
Uchumi wetu unakua kwa kasi ya zaidi ya 7% , wananchi wetu kipato kiko juu sasa na wanafurahia maisha, watoto wetu wanasoma buree, huduma za afya bora kabisa na zakisasa..

Tumeshaanza kujitegemea nakutoa misaada kwa nchi za kiafrica, hatuhitaji kwenda kwenye hizo summit acha waende mataifa masikini....
Hats kama hatukwenda Jiwe atapata misaada juu kwa juu. Jiwe hana muda was kupoteza kwenye talk shops!
 
Berlin Conference 1884.Sasa naona wameamua kuja mmoja mmoja. France-Africa. Uk-Africa,Russia-Africa,China-Africa,Japan-Africa. Hapa naweka conclusion Africa is potentiel. Thomas Sankara,Patrice Lumumba i wish mngekuwa hai.
Kuna waliotoa comments hawajaona hili wanashadadia jiwe aende ovyo ovyo. Jana tu ilikuwepo Berlin conference kwa ajili ya kuigawanya Libya dhidi ya mabeberu. Halafu baadhi ya viongozi wana biashara zao binafsi badala ya biashara za nchi.
 
Tunakuja kwa 'lesi' moja ya ajab. Kando na dili za KES 170Billion kwenye summit ya UK-Africa Invest. kuna hii biashara nyingine ya kando. Rais Uhuru alifungua rasmi shughuli za LSE.
images
Akazindua rasmi pia float ya green bond ya kwanza kutoka Kenya, yenye thamani ya $40Million! Corporate green bond kutoka kwa kampuni ya kikenya ambayo itakuwa 'denominated' kwa KES. Tegemea kuona kampuni zingine za Kenya zikichangamkia fursa kama hiyo ya kutanua misuli hadi UK na kuvutia wawekezaji. Tena chini ya muongozo wa serikali ya Kenya.
Dah! Huyu jamaa anajua kucheza na akili za wananchi. Ananikumbusha alivyoruka na dili la parachichi.
 
Nchi 21 za Afrika zimehudhuria

Wawakilishi zaid ya 1500

Miradi ya jumla ya Pauni Bil 6.5 imetangazwa.

Je hatutaki fursa hii na sisi wanachama wa jumuia ya madola? Baada ya Brexit mwezi huu kuna fursa kubwa za biashara na waingereza. Au ni bora inatosha kufanya biashara na wachina tu? Deal kama hizi rais wa nchi anatakiwa awepo kwenye meza ili na Tanzania ipate mgao wa keki yake.


21 African nations

🔹

1500+ attendees

🔹

£6.5bn of commercial deals announced

View attachment 1328928
Rais Magufuli 2015~2020 Ni kunyoosha nchi tu marufuku ziara nchi za Ulaya. Marekani na Asia…!
 
Afadhali hakwenda mtu yeyote Yule , Kabudi alienda Kuhutubia UN hotuba nzima ilikuwa na mambo ya Tanzania vile Kama vile reli ya SGR na bwawa la umeme la Stiegler
 
Na yeye kaita Mabalozi wote uone kama... MABALOZI SUMMIT
Uliza ni nchi ngapi na Organization ngapi zimewakilishwa.
 
Back
Top Bottom