Ujumbe wangu kwa wabunge wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Gosbertgoodluck

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,856
401
Siyo siri kwamba Mhe. Sita ameleta mapinduzi makubwa kwenye utendaji wa mojawapo ya mihimili ya uongozi hapa nchini. Chini ya uongozi wake wa bunge watanzania wengi wamepata mwamko wa kisiasa na wameanza kufuatilia utendaji wa wawakilishi wao ndani ya vikao vya bunge. Kutokana na utendaji wake huo, wa Mhe. Sita alitengeneza maadui zake wengi kutoka ndani na nje ya chama chake cha ccm. Maadui waliokuwa hatari ni wale wanaotoka ndani ya chama chake ambao wengi wao ni mafisadi wakubwa. Kwa nguvu yao ya kifedha hatimaye wamemwangusha na kumwondoa kwenye kiti kikuu cha enzi.

Ndugu zangu wabunge hususan wazalendo mnaoipenda kwa dhati nchi yenu, msifanye kosa kuwachagua akina mama waliopitishwa na ccm. majina hayo yamepitishwa kwa nguvu ya kifisadi ili kukiponya chama chao na vidonda vilivyotokana na uongozi wa Mhe. Sita. Wanataka bunge letu lililoanza kupata umaarufu ndani na nje ya bara letu la afrika, lianze kusinzia tena.

Watanzania tunawaomba tena tupo chini ya miguu yenu, tafadhali mchagueni Mhe. Marando ili kuendeleza kazi iliyoanza kufanywa na Mhe. Sita. Hiyo itakuwa ni zawadi yenu ya kwanza kwa wapiga kura wenu tangu mpate huo uheshimiwa.

Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.
 
Siyo siri kwamba Mhe. Sita ameleta mapinduzi makubwa kwenye utendaji wa mojawapo ya mihimili ya uongozi hapa nchini. Chini ya uongozi wake wa bunge watanzania wengi wamepata mwamko wa kisiasa na wameanza kufuatilia utendaji wa wawakilishi wao ndani ya vikao vya bunge. Kutokana na utendaji wake huo, wa Mhe. Sita alitengeneza maadui zake wengi kutoka ndani na nje ya chama chake cha ccm. Maadui waliokuwa hatari ni wale wanaotoka ndani ya chama chake ambao wengi wao ni mafisadi wakubwa. Kwa nguvu yao ya kifedha hatimaye wamemwangusha na kumwondoa kwenye kiti kikuu cha enzi.

Ndugu zangu wabunge hususan wazalendo mnaoipenda kwa dhati nchi yenu, msifanye kosa kuwachagua akina mama waliopitishwa na ccm. majina hayo yamepitishwa kwa nguvu ya kifisadi ili kukiponya chama chao na vidonda vilivyotokana na uongozi wa Mhe. Sita. Wanataka bunge letu lililoanza kupata umaarufu ndani na nje ya bara letu la afrika, lianze kusinzia tena.

Watanzania tunawaomba tena tupo chini ya miguu yenu, tafadhali mchagueni Mhe. Marando ili kuendeleza kazi iliyoanza kufanywa na Mhe. Sita. Hiyo itakuwa ni zawadi yenu ya kwanza kwa wapiga kura wenu tangu mpate huo uheshimiwa.

Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.
Mwenye masikio ya kusikia.....
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom