The iron batterfly
JF-Expert Member
- Jul 31, 2018
- 1,952
- 2,520
Habari za jumapili wanajukwaa.Mungu ni mwema kila wakati.
Niende moja kwa moja kwenye lengo la mada hii.
Kwako waziri Wa ardhi,mhe. Sana William Vangamembe Lukuvi,salamu kwako,aidha baada ya salamu Nina kaujumbe kadogo kwako.
Umekabidhiwa wizara hii toka kwa mhe.profesa Anna Tibaijuka.Kongole kwani kuna mengi aliyaacha njiani uliyakamilisha,kama punguzo la rate za tozo za ardhi na malipo ya premium.
Ila Nina mambo mawili nataka zungumza nawe mhe waziri.
Jambo la kwanza ni utendaji wa wataalamu Wa ardhi waliopo wizarani,wakiwemo maafisa ardhi,maafisa mipangomiji,wapimaji,warasimu ramani,wathamini,wanasheria,watu wa masjala nk.
Utendaji wa wataalamu hawa hauridhishi.Wanafanya kazi kwa mazoea.Wanajiona miunguwatu.Wamekubuhu kwa urasimu na rushwa.
Ushahidi wa haya yote upo. Mfano mdogo kanda ya Mashariki na pwani toka imevunjwa umepita mwaka sasa,Ila Mteja akienda wizarani anaambiwa afatilie kazi yake morogoro,kweli?
Mteja mwingine zaidi ya miaka miwili jalada halisomi kwenye system. Swali dogo tu ni jukumu la nani kuliingiza hilo jalada katika system kama siyo afisa husika?jalada linaweza ingiza taarifa zake zenyewe kwenye system? Jibu ni uzembe wa maafisa wanaoshungulikia system kutokufanya kazi zao kwa weledi na wakati.
Tukija kwenye upimaji na ramani,huko ndio majanga hadi aibu.Ramani zaidi ya moja zinapewa namba za usajili ,namba za Viwanja na hata block moja,kwa kifupi double numbering. Swali dogo tu,ina maana mkurugenzi wa upimaji na ramani hana database? Anafanyaje kazi?wanaguess?miaka mi4 waliotumia ardhi university ama UCLA's ilikuwa ya nini?hili ni jipu lililoiva,litumbue kabla halijaleta madhara.
Sijamsahau mkurugenzi wa Mipangomiji;anafanyaje kazi?ana database? Ramani zinaandaliwa ila ukienda wizarani hakuna kumbukumbu,kweli?walisomea wapi hawa?wanajua majukumu yao?Halafu inakuwaje mtu awe na mamlaka ya kuja kuchomoa ramani wizarani, inayosubiri kusainiwa nakusajiliwa?is it professional? Kama kuna tatizo kwanini wasiirudishe halmashauri husika tena kwa barua kama ilivyoletwa?Maafisa Mipangomiji ni jipu lililokwiva,litazame mhe.
Suala la pili ni ukabila;bila kupepesa macho wizara imegeuka ya wasukuma na wachaga.kwanini?is it a coincidence? Mhe nakuomba rekebisha hilo.Fanya panguapangua hapo wizarani,hakuna alioandikiwa kukaa wizarani zaidi ya miaka 20?kwalipi?kwa ufanisi gani?wanayepi ya kujisifia kwa kukaa wizarani zaidi ya miaka 10,20?kuna tija gani?Je taratibu za kiutumishi zinaruhusu?Tanzania ni yetu sote.Nakuomba kabla hujasafisha halmashauri za miji na majiji,safisha hapo wizarani, kuna tatizo.
Kwa leo niishie hapa,nikipata wasaa nitaleta mengine ila kwa leo ,nakuomba fanyia uchunguzi hayo na uyafanyie kazi,kama kweli una dhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko katika wizara hii.
Sent using Jamii Forums mobile app
Niende moja kwa moja kwenye lengo la mada hii.
Kwako waziri Wa ardhi,mhe. Sana William Vangamembe Lukuvi,salamu kwako,aidha baada ya salamu Nina kaujumbe kadogo kwako.
Umekabidhiwa wizara hii toka kwa mhe.profesa Anna Tibaijuka.Kongole kwani kuna mengi aliyaacha njiani uliyakamilisha,kama punguzo la rate za tozo za ardhi na malipo ya premium.
Ila Nina mambo mawili nataka zungumza nawe mhe waziri.
Jambo la kwanza ni utendaji wa wataalamu Wa ardhi waliopo wizarani,wakiwemo maafisa ardhi,maafisa mipangomiji,wapimaji,warasimu ramani,wathamini,wanasheria,watu wa masjala nk.
Utendaji wa wataalamu hawa hauridhishi.Wanafanya kazi kwa mazoea.Wanajiona miunguwatu.Wamekubuhu kwa urasimu na rushwa.
Ushahidi wa haya yote upo. Mfano mdogo kanda ya Mashariki na pwani toka imevunjwa umepita mwaka sasa,Ila Mteja akienda wizarani anaambiwa afatilie kazi yake morogoro,kweli?
Mteja mwingine zaidi ya miaka miwili jalada halisomi kwenye system. Swali dogo tu ni jukumu la nani kuliingiza hilo jalada katika system kama siyo afisa husika?jalada linaweza ingiza taarifa zake zenyewe kwenye system? Jibu ni uzembe wa maafisa wanaoshungulikia system kutokufanya kazi zao kwa weledi na wakati.
Tukija kwenye upimaji na ramani,huko ndio majanga hadi aibu.Ramani zaidi ya moja zinapewa namba za usajili ,namba za Viwanja na hata block moja,kwa kifupi double numbering. Swali dogo tu,ina maana mkurugenzi wa upimaji na ramani hana database? Anafanyaje kazi?wanaguess?miaka mi4 waliotumia ardhi university ama UCLA's ilikuwa ya nini?hili ni jipu lililoiva,litumbue kabla halijaleta madhara.
Sijamsahau mkurugenzi wa Mipangomiji;anafanyaje kazi?ana database? Ramani zinaandaliwa ila ukienda wizarani hakuna kumbukumbu,kweli?walisomea wapi hawa?wanajua majukumu yao?Halafu inakuwaje mtu awe na mamlaka ya kuja kuchomoa ramani wizarani, inayosubiri kusainiwa nakusajiliwa?is it professional? Kama kuna tatizo kwanini wasiirudishe halmashauri husika tena kwa barua kama ilivyoletwa?Maafisa Mipangomiji ni jipu lililokwiva,litazame mhe.
Suala la pili ni ukabila;bila kupepesa macho wizara imegeuka ya wasukuma na wachaga.kwanini?is it a coincidence? Mhe nakuomba rekebisha hilo.Fanya panguapangua hapo wizarani,hakuna alioandikiwa kukaa wizarani zaidi ya miaka 20?kwalipi?kwa ufanisi gani?wanayepi ya kujisifia kwa kukaa wizarani zaidi ya miaka 10,20?kuna tija gani?Je taratibu za kiutumishi zinaruhusu?Tanzania ni yetu sote.Nakuomba kabla hujasafisha halmashauri za miji na majiji,safisha hapo wizarani, kuna tatizo.
Kwa leo niishie hapa,nikipata wasaa nitaleta mengine ila kwa leo ,nakuomba fanyia uchunguzi hayo na uyafanyie kazi,kama kweli una dhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko katika wizara hii.
Sent using Jamii Forums mobile app