Ujumbe Wa wazi kwa waziri Wa Ardhi, mhe Lukuvi

The iron batterfly

JF-Expert Member
Jul 31, 2018
1,952
2,520
Habari za jumapili wanajukwaa.Mungu ni mwema kila wakati.

Niende moja kwa moja kwenye lengo la mada hii.

Kwako waziri Wa ardhi,mhe. Sana William Vangamembe Lukuvi,salamu kwako,aidha baada ya salamu Nina kaujumbe kadogo kwako.
Umekabidhiwa wizara hii toka kwa mhe.profesa Anna Tibaijuka.Kongole kwani kuna mengi aliyaacha njiani uliyakamilisha,kama punguzo la rate za tozo za ardhi na malipo ya premium.

Ila Nina mambo mawili nataka zungumza nawe mhe waziri.

Jambo la kwanza ni utendaji wa wataalamu Wa ardhi waliopo wizarani,wakiwemo maafisa ardhi,maafisa mipangomiji,wapimaji,warasimu ramani,wathamini,wanasheria,watu wa masjala nk.

Utendaji wa wataalamu hawa hauridhishi.Wanafanya kazi kwa mazoea.Wanajiona miunguwatu.Wamekubuhu kwa urasimu na rushwa.

Ushahidi wa haya yote upo. Mfano mdogo kanda ya Mashariki na pwani toka imevunjwa umepita mwaka sasa,Ila Mteja akienda wizarani anaambiwa afatilie kazi yake morogoro,kweli?

Mteja mwingine zaidi ya miaka miwili jalada halisomi kwenye system. Swali dogo tu ni jukumu la nani kuliingiza hilo jalada katika system kama siyo afisa husika?jalada linaweza ingiza taarifa zake zenyewe kwenye system? Jibu ni uzembe wa maafisa wanaoshungulikia system kutokufanya kazi zao kwa weledi na wakati.

Tukija kwenye upimaji na ramani,huko ndio majanga hadi aibu.Ramani zaidi ya moja zinapewa namba za usajili ,namba za Viwanja na hata block moja,kwa kifupi double numbering. Swali dogo tu,ina maana mkurugenzi wa upimaji na ramani hana database? Anafanyaje kazi?wanaguess?miaka mi4 waliotumia ardhi university ama UCLA's ilikuwa ya nini?hili ni jipu lililoiva,litumbue kabla halijaleta madhara.

Sijamsahau mkurugenzi wa Mipangomiji;anafanyaje kazi?ana database? Ramani zinaandaliwa ila ukienda wizarani hakuna kumbukumbu,kweli?walisomea wapi hawa?wanajua majukumu yao?Halafu inakuwaje mtu awe na mamlaka ya kuja kuchomoa ramani wizarani, inayosubiri kusainiwa nakusajiliwa?is it professional? Kama kuna tatizo kwanini wasiirudishe halmashauri husika tena kwa barua kama ilivyoletwa?Maafisa Mipangomiji ni jipu lililokwiva,litazame mhe.

Suala la pili ni ukabila;bila kupepesa macho wizara imegeuka ya wasukuma na wachaga.kwanini?is it a coincidence? Mhe nakuomba rekebisha hilo.Fanya panguapangua hapo wizarani,hakuna alioandikiwa kukaa wizarani zaidi ya miaka 20?kwalipi?kwa ufanisi gani?wanayepi ya kujisifia kwa kukaa wizarani zaidi ya miaka 10,20?kuna tija gani?Je taratibu za kiutumishi zinaruhusu?Tanzania ni yetu sote.Nakuomba kabla hujasafisha halmashauri za miji na majiji,safisha hapo wizarani, kuna tatizo.

Kwa leo niishie hapa,nikipata wasaa nitaleta mengine ila kwa leo ,nakuomba fanyia uchunguzi hayo na uyafanyie kazi,kama kweli una dhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko katika wizara hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za jumapili wanajukwaa.Mungu ni mwema kila wakati.

Niende moja kwa moja kwenye lengo la mada hii.

Kwako waziri Wa ardhi,mhe. Sana William Vangamembe Lukuvi,salamu kwako,aidha baada ya salamu Nina kaujumbe kadogo kwako.
Umekabidhiwa wizara hii toka kwa mhe.profesa Anna Tibaijuka.Kongole kwani kuna mengi aliyaacha njiani uliyakamilisha,kama punguzo la rate za tozo za ardhi na malipo ya premium.

Ila Nina mambo mawili nataka zungumza nawe mhe waziri.

Jambo la kwanza ni utendaji wa wataalamu Wa ardhi waliopo wizarani,wakiwemo maafisa ardhi,maafisa mipangomiji,wapimaji,warasimu ramani,wathamini,wanasheria,watu wa masjala nk.

Utendaji wa wataalamu hawa hauridhishi.Wanafanya kazi kwa mazoea.Wanajiona miunguwatu.Wamekubuhu kwa urasimu na rushwa.

Ushahidi wa haya yote upo. Mfano mdogo kanda ya Mashariki na pwani toka imevunjwa umepita mwaka sasa,Ila Mteja akienda wizarani anaambiwa afatilie kazi yake morogoro,kweli?

Mteja mwingine zaidi ya miaka miwili jalada halisomi kwenye system. Swali dogo tu ni jukumu la nani kuliingiza hilo jalada katika system kama siyo afisa husika?jalada linaweza ingiza taarifa zake zenyewe kwenye system? Jibu ni uzembe wa maafisa wanaoshungulikia system kutokufanya kazi zao kwa weledi na wakati.

Tukija kwenye upimaji na ramani,huko ndio majanga hadi aibu.Ramani zaidi ya moja zinapewa namba za usajili ,namba za Viwanja na hata block moja,kwa kifupi double numbering. Swali dogo tu,ina maana mkurugenzi wa upimaji na ramani hana database? Anafanyaje kazi?wanaguess?miaka mi4 waliotumia ardhi university ama UCLA's ilikuwa ya nini?hili ni jipu lililoiva,litumbue kabla halijaleta madhara.

Sijamsahau mkurugenzi wa Mipangomiji;anafanyaje kazi?ana database? Ramani zinaandaliwa ila ukienda wizarani hakuna kumbukumbu,kweli?walisomea wapi hawa?wanajua majukumu yao?Halafu inakuwaje mtu awe na mamlaka ya kuja kuchomoa ramani wizarani, inayosubiri kusainiwa nakusajiliwa?is it professional? Kama kuna tatizo kwanini wasiirudishe halmashauri husika tena kwa barua kama ilivyoletwa?Maafisa Mipangomiji ni jipu lililokwiva,litazame mhe.

Suala la pili ni ukabila;bila kupepesa macho wizara imegeuka ya wasukuma na wachaga.kwanini?is it a coincidence? Mhe nakuomba rekebisha hilo.Fanya panguapangua hapo wizarani,hakuna alioandikiwa kukaa wizarani zaidi ya miaka 20?kwalipi?kwa ufanisi gani?wanayepi ya kujisifia kwa kukaa wizarani zaidi ya miaka 10,20?kuna tija gani?Je taratibu za kiutumishi zinaruhusu?Tanzania ni yetu sote.Nakuomba kabla hujasafisha halmashauri za miji na majiji,safisha hapo wizarani, kuna tatizo.

Kwa leo niishie hapa,nikipata wasaa nitaleta mengine ila kwa leo ,nakuomba fanyia uchunguzi hayo na uyafanyie kazi,kama kweli una dhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko katika wizara hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu umenena Mh.Waziri watendaji wa sekta ya ardhi Manispaa zote za Dar es salaam waliokaa zaidi ya miaka 5 wahamishwe wamekuwa chanzo kikubwa cha Migogoro isiyoisha.Pia wana mahusiano Makubwa na Matapeli wa Ardhi .Watawanye leta wengine kutoka mikoani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana Mkuu
Waziri Lukuvi huko Ardhi kuna watu wanakuharibia kazi
Mlisema watu wajiandikishe kwenye maeneo yao viwanja vipimwe
Ok viwanja vimepimwa mkasema watu watapewa hati za viwanja mkaja na gharama za kutoa roho za watu mkasema mahesabu yalikosewa mtafanya mahesabu upya yatakayojumuisha na property tax.
Zoezi hili mlianza na Kigamboni mkaenda Makongo Goba Madale etc imekuwa kero kwa wananchi kila wakati ni vikaooo tuuuuu kwa serikali za mitaaa.

Waziri ni mwaka wa pili huu unaanza kama sio watatu ni storiii tu huko serikali za mitaa

Sasa nani wa kuchongewa hapa ili kazi ifanyike
Tupe mwongozo Waziri

*Tz kupata hati ya viwanja ni mtihani mkubwa shida iko wapi Waziri
 
Hilo suala la Rushwa ndio usiseme. Maafisa ardhi wamejisahau, wameshajigeuzia utaratibu wa kazi ni kuwa mpaka umpe hela ndiyo afanye shughuli yako.
Pia kuna tatizo la migogoro ya ardhi. Migogoro ya ardhi 98% inaletwa na maafisa ardhi. Utakuta kiwanjakilicho eneo zuri kinapewa watu hata watatu, kwa imani kuwa mgogoro ukizuka hao wengine watatafutiwa maeneo mengine (ambayo sio mazuri kama la awali, na kwa kuwa mtu hutataka mgogoro tena utachukua, wao watakuwa wameshapiga hela)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa naona ana allerge na Wachaga. Kazunguka koote ila lengo lake awataje
 
Mkuu umenena Mh.Waziri watendaji wa sekta ya ardhi Manispaa zote za Dar es salaam waliokaa zaidi ya miaka 5 wahamishwe wamekuwa chanzo kikubwa cha Migogoro isiyoisha.Pia wana mahusiano Makubwa na Matapeli wa Ardhi .Watawanye leta wengine kutoka mikoani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio wana mtandao na matapeli Wa Viwanja DSM
Watawanywe wapelekwe mikoani,Tanzania hii ni kubwa sana
Sioni mantiki Mtumishi anakaa kituo kimoja zaidi ya miaka 10,ni kutengeneza urasimu,umungumtu,mtandao Wa rushwa na kufanya kazi kwa mazoea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hilo suala la Rushwa ndio usiseme. Maafisa ardhi wamejisahau, wameshajigeuzia utaratibu wa kazi ni kuwa mpaka umpe hela ndiyo afanye shughuli yako.
Pia kuna tatizo la migogoro ya ardhi. Migogoro ya ardhi 98% inaletwa na maafisa ardhi. Utakuta kiwanjakilicho eneo zuri kinapewa watu hata watatu, kwa imani kuwa mgogoro ukizuka hao wengine watatafutiwa maeneo mengine (ambayo sio mazuri kama la awali, na kwa kuwa mtu hutataka mgogoro tena utachukua, wao watakuwa wameshapiga hela)

Sent using Jamii Forums mobile app
Migogoro ya ardhi asilimia 99 inasababishwa na wataalamu Wa ardhi
Kama mhe. Yuko serious afanyie kazi maoni ya wananchi,otherwise itabaki business as usual

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana Mkuu
Waziri Lukuvi huko Ardhi kuna watu wanakuharibia kazi
Mlisema watu wajiandikishe kwenye maeneo yao viwanja vipimwe
Ok viwanja vimepimwa mkasema watu watapewa hati za viwanja mkaja na gharama za kutoa roho za watu mkasema mahesabu yalikosewa mtafanya mahesabu upya yatakayojumuisha na property tax.
Zoezi hili mlianza na Kigamboni mkaenda Makongo Goba Madale etc imekuwa kero kwa wananchi kila wakati ni vikaooo tuuuuu kwa serikali za mitaaa.

Waziri ni mwaka wa pili huu unaanza kama sio watatu ni storiii tu huko serikali za mitaa

Sasa nani wa kuchongewa hapa ili kazi ifanyike
Tupe mwongozo Waziri

*Tz kupata hati ya viwanja ni mtihani mkubwa shida iko wapi Waziri
Maafisa mipangomiji na wapima ardhi ni jipu lililoiva,wanachukua hela za wananchi halafu hawatekelezi kazi
Mhe. Waziri najua walijua hili,na kama una dhamira ya dhati na sekta ya ardhi nakuomba lifanyie kazi.Vinginevyo itabaki story zisizokuwa na utekelezaji,ili tufike tunapotaka kuchukua maamuzi magumu,is not an option.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom