Lowassa ni kipenzi cha mke wake na familia yake, at least hilo tuna uhakika nalo.
Watanzania wengine tungefarijika kuelewa kiini cha utajiri wake na umahiri wake wa kutengeneza fwedha(akiwa serikalini) ulikotoka ili na sisi tumpende.
Mkuu nakugongea senksi. Watu wanajaribu kuleta mlolongo wa orodha ya mafanikio ambayo hayana kichwa wala miguu kwa sababu suala la shule za kata ulikuwa ni mpango wa serikali yote na yeye kama waziri mkuu alikuwa na wajibu wa kulisimamia (kama ilivyo Kilimo Kwanza na Pinda). Hili suala la Halmashauri kumuogopa ni la kweli kwamba kwa vile yeye alikuwa na hulka ya kufokea watu na kuwajengea hofu walikuwa na haki ya kumuogopa lakini ufanisi haukuwepo na wala hakuwahi kudhibiti ubadhirifu uliokuwa umekithiri na ndiyo maana halmashauri zilizokuwa na hati chafu zilikuwa nyingi sana tofauti na sasa hivi ambapo halmshauri nyingi zina hati safi na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa inafanya kazi vizuri kuliko wakati wake. Kwa ujumla hatuna lolote la kukumbuka wakati wa Lowassa zaidi ya kutajirika kwake na wizi aliowafanyia watanzania kwa phantom projects zake. Wanaosema alikuwa muungwana kwa kuachia uwaziri mkuu, wamuangalie usoni ndipo wataona hasira alizo nazo baada ya kuwa nje ya serikali kwa muda huu. Alichofanya yeye ni kama mlinzi anayelazimishwa kujifunga goli na forward machachari (ambaye kwa kesi hii ni Kamati ya Mwakyembe). Ndo maana alilia lia sana kwenye hotuba yake.