Uchaguzi 2020 Ujumbe wa Mungu kwa Lissu na Magufuli ni katika Yeremia

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,883
UJUMBE WA MUNGU KWA LISU NA MAGUFULI

Na, Robert Heriel

ZINGATIA; Maneno yaliyowekolezwa (Bolded word)

Ama kwa hakika hakuna kazi ngumu kwa binadamu kama kusema ukweli na kutenda kwa haki. Haya nimeyaona kwa macho yangu, na kuyashuhudia mimi mwenyewe wala sio kwa kuhadithiwa.

Je ni nani awezaye kusimama mbele ya wakuu na kusema ukweli, Ni nani asiyeogopa kumuonya mwenye mamlaka. Ama ni nani awezaye kuutazama uso wa Mtawala na kumkaripia pale atelezapo na kufanya kwa uovu.

Basi mimi Taikon hali nikijua hatari inayoweza kunikabili, nikajitia ujasiri, nami nikaapa kwa jina la Mungu wangu kutetea haki, tena nikasema; nitasema ukweli pasipokuogopa uso wa mtu. Hata hivyo sikusahau kuomba hekima kwa Mungu, kwa maana kumuonya Mfalme yahitaji hekima, tena kumkaripia Mtawala yahitaji busara na kujitoa kwa dhati.

Basi ikiwa nilikengeuka kwa tamaa zangu, tena ubinafsi uliniendesha, hata nikampendelea mtawala muovu, nikashindwa kusema iliyo kweli na kumkemea, basi Mungu atanihukumu.

Tupo katika uchaguzi, ni baina ya Mzee wangu Mhe. Rais, Dkt John Pombe Magufuli na Kaka yangu Mhe. Tundu Antipas Lisu. Wote ninawaheshimu katika haki, wema na uadilifu. Wote ni ndugu zangu katika nchi hii. Jambo moja la muhimu kwa yeyote atakayechaguliwa bila kujali mimi nimemchagua nani, kwanza nitamuunga mkono kwa yaliyomema, haki na uadilifu. Lakini kwa mabaya nitamkosoa, kumkemea, na kumkaripia. Nafahamu ugumu wa kumuonya Mtawala, lakini kwa vile sio kwa nia mbaya basi nitafanya.

Leo nitawapa ujumbe wa Mungu kutoka katika Kitabu cha Yeremia; Naomba kunukuu

YEREMIA 22;

1Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Nenda katika ikulu ya mfalme wa Yuda, uwape watu ujumbe huu: 2Wewe mfalme wa Yuda unayekikalia kiti cha enzi cha mfalme Daudi, pamoja na watumishi wako na watu wako wanaopita katika malango haya, sikilizeni neno langu mimi Mwenyezi-Mungu.

3. Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Tendeni mambo ya haki na uadilifu. Mwokoeni mikononi mwa mdhalimu mtu yeyote aliyenyanganywa mali zake. Msiwatendee vibaya au ukatili wageni, yatima na wajane wala msimwage damu ya mtu asiye na hatia mahali hapa.

4. Kama mkishika neno hili nililowaambia basi, wafalme wanaokikalia kiti cha enzi cha Daudi wataendelea kuingia kwa kupitia malango ya ikulu hii. Watapita pamoja na watumishi wao na watu wao, wakiwa wamepanda farasi na magari ya farasi. 5Lakini kama hamtatii maneno haya, mimi Mwenyezi-Mungu naapa kwa nafsi yangu kwamba mahali hapa patakuwa magofu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

6. Mwenyezi-Mungu asema hivi kuhusu ikulu ya mfalme wa Yuda:
“Ingawa waonekana kuwa mzuri kama nchi ya Gileadi
kama kilele cha Lebanoni,
Lakini naapa kuwa nitakufanya uwe jangwa,
uwe mji usiokaliwa na watu.

7Nitawatayarisha waangamizi dhidi yako,
kila mmoja na silaha yake mkononi.
Wataikata mierezi yako mizuri,
na kuitumbukiza motoni.

8“Kisha watu wengi wa mataifa watapita karibu na mji huu, na kila mmoja atamwuliza mwenzake: ‘Kwa nini Mwenyezi-Mungu ameutenda hivi mji huu mkubwa?’ 9Wenzao watawajibu, ‘Ni kwa sababu waliliacha agano la Mwenyezi-Mungu, Mungu wao, wakaiabudu miungu mingine na kuitumikia.’”

10. Msimlilie mtu aliyekufa,
wala msiombolezee kifo chake.
Bali mlilieni kwa uchungu yule aendaye mbali,
kwa kuwa hatarudi tena kuiona nchi yake.

11. Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya Shalumu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyetawala baada ya Yosia baba yake, na ambaye aliondoka mahali hapa: “Shalumu hatarudi tena mahali hapa, 12bali atafia hukohuko walikomchukua utumwani. Kamwe hataiona tena nchi hii.
Ujumbe juu ya Yehoyakimu

13“Ole wako Yehoyakimu
wewe unayejenga nyumba kwa dhuluma
na kuiwekea ghorofa bila kutumia haki.
Unawaajiri watu wakutumikie bure
wala huwalipi mishahara yao.


14Wewe wasema:
‘Nitalijenga jumba kubwa,
lenye vyumba vikubwa ghorofani.’
Kisha huifanyia madirisha,
ukafunika kuta zake kwa mbao za mierezi,
na kuipaka rangi nyekundu!

15Unadhani umekuwa mfalme
kwa kushindana kujenga kwa mierezi?
Baba yako alikula na kunywa,
akatenda mambo ya haki na mema
ndipo mambo yake yakamwendea vema.

16Aliwapatia haki maskini na wahitaji,
na mambo yake yakamwendea vema.
Hii ndiyo maana ya kunijua mimi Mwenyezi-Mungu.

17. Lakini macho yako wewe na moyo wako,
hungangania tu mapato yasiyo halali.
Unamwaga damu ya wasio na hatia,


Mungu awasaidie mnapolitafakari neno hili.

Nakala zifike kwa:

1. Mhe. Rais, Dkt John Pombe Magufuli
2. Mhe Tundu Antipas Lisu

Pia Ziwafikie;
1. Wenyeviti na Makatibu wote wa Vyama vya siasa
2. Viongozi wa Nyanja zote za kitaifa na kijamii

Ipende nchi yako, penda watu wako. Kuwa Mzalendo.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dar es Salaam
 
1602756982334.png
 

Mtu hawezi fanya mambo yote, walakini ya muhimu na yalazima ni wajibu ayafanye. Nafikiri jana niliandika makala isemayo kilichomponza Magufuli,

Kama atarekebisha hapo, anaweza kuwa Rais bora kuwahi kutokea Hapa Tanzania, kumbuka huwezi fanya mambo yote, na hata ukifanya mambo yote lakini ukasahahu ya lazima na muhimu basi jua huna ulichofanya
 
Mkuu Heriel, hizo sentensi ambazo zipo "bolded" kwa hakika zimebeba ujumbe mzito sana na wa hekima nyingi mno, iwe kwa watawala wa sasa ama wale wanaokuja. Ila dah! Ni kama zinahakisi kwa 100% mtawala fulani ambaye yupo midomoni sana kwa watu wengi hivi sasa.
 
Kati yao hao wawili anayewanyima haki wengine anafahamika, na anayewaahidi watu haki anafahamika.

Kwahiyo aliyepata kibali machoni pa Mungu anafahamika.

Huyo mwingine aendelee kusema "nileteeni fulaniiiiii", atapelekewa gwajima kijijini kwake baada ya kustaafishwa kwa manufaa ya umma oct 28.
 
Kati yao hao wawili anayewanyima haki wengine anafahamika, na anayewaahidi watu haki anafahamika.

Kwahiyo aliyepata kibali machoni pa Mungu anafahamika.

Huyo mwingine aendelee kusema "nileteeni fulaniiiiii", atapelekewa gwajima kijijini kwake baada ya kustaafishwa kwa manufaa ya umma oct 28.


😲😲😲😲
 
Mkuu Heriel, hizo sentensi ambazo zipo "bolded" kwa hakika zimebeba ujumbe mzito sana na wa hekima nyingi mno, iwe kwa watawala wa sasa ama wale wanaokuja. Ila dah! Ni kama zinahakisi kwa 100% mtawala fulani ambaye yupo midomoni sana kwa watu wengi hivi sasa.


Naam Mkuu
 
UJUMBE WA MUNGU KWA LISU NA MAGUFULI

Na, Robert Heriel

ZINGATIA; Maneno yaliyowekolezwa (Bolded word)

Ama kwa hakika hakuna kazi ngumu kwa binadamu kama kusema ukweli na kutenda kwa haki. Haya nimeyaona kwa macho yangu, na kuyashuhudia mimi mwenyewe wala sio kwa kuhadithiwa.

Je ni nani awezaye kusimama mbele ya wakuu na kusema ukweli, Ni nani asiyeogopa kumuonya mwenye mamlaka. Ama ni nani awezaye kuutazama uso wa Mtawala na kumkaripia pale atelezapo na kufanya kwa uovu.

Basi mimi Taikon hali nikijua hatari inayoweza kunikabili, nikajitia ujasiri, nami nikaapa kwa jina la Mungu wangu kutetea haki, tena nikasema; nitasema ukweli pasipokuogopa uso wa mtu. Hata hivyo sikusahau kuomba hekima kwa Mungu, kwa maana kumuonya Mfalme yahitaji hekima, tena kumkaripia Mtawala yahitaji busara na kujitoa kwa dhati.

Basi ikiwa nilikengeuka kwa tamaa zangu, tena ubinafsi uliniendesha, hata nikampendelea mtawala muovu, nikashindwa kusema iliyo kweli na kumkemea, basi Mungu atanihukumu.

Tupo katika uchaguzi, ni baina ya Mzee wangu Mhe. Rais, Dkt John Pombe Magufuli na Kaka yangu Mhe. Tundu Antipas Lisu. Wote ninawaheshimu katika haki, wema na uadilifu. Wote ni ndugu zangu katika nchi hii. Jambo moja la muhimu kwa yeyote atakayechaguliwa bila kujali mimi nimemchagua nani, kwanza nitamuunga mkono kwa yaliyomema, haki na uadilifu. Lakini kwa mabaya nitamkosoa, kumkemea, na kumkaripia. Nafahamu ugumu wa kumuonya Mtawala, lakini kwa vile sio kwa nia mbaya basi nitafanya.

Leo nitawapa ujumbe wa Mungu kutoka katika Kitabu cha Yeremia; Naomba kunukuu

YEREMIA 22;

1Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Nenda katika ikulu ya mfalme wa Yuda, uwape watu ujumbe huu: 2Wewe mfalme wa Yuda unayekikalia kiti cha enzi cha mfalme Daudi, pamoja na watumishi wako na watu wako wanaopita katika malango haya, sikilizeni neno langu mimi Mwenyezi-Mungu.

3. Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Tendeni mambo ya haki na uadilifu. Mwokoeni mikononi mwa mdhalimu mtu yeyote aliyenyanganywa mali zake. Msiwatendee vibaya au ukatili wageni, yatima na wajane wala msimwage damu ya mtu asiye na hatia mahali hapa.

4. Kama mkishika neno hili nililowaambia basi, wafalme wanaokikalia kiti cha enzi cha Daudi wataendelea kuingia kwa kupitia malango ya ikulu hii. Watapita pamoja na watumishi wao na watu wao, wakiwa wamepanda farasi na magari ya farasi. 5Lakini kama hamtatii maneno haya, mimi Mwenyezi-Mungu naapa kwa nafsi yangu kwamba mahali hapa patakuwa magofu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

6. Mwenyezi-Mungu asema hivi kuhusu ikulu ya mfalme wa Yuda:
“Ingawa waonekana kuwa mzuri kama nchi ya Gileadi
kama kilele cha Lebanoni,
Lakini naapa kuwa nitakufanya uwe jangwa,
uwe mji usiokaliwa na watu.

7Nitawatayarisha waangamizi dhidi yako,
kila mmoja na silaha yake mkononi.
Wataikata mierezi yako mizuri,
na kuitumbukiza motoni.

8“Kisha watu wengi wa mataifa watapita karibu na mji huu, na kila mmoja atamwuliza mwenzake: ‘Kwa nini Mwenyezi-Mungu ameutenda hivi mji huu mkubwa?’ 9Wenzao watawajibu, ‘Ni kwa sababu waliliacha agano la Mwenyezi-Mungu, Mungu wao, wakaiabudu miungu mingine na kuitumikia.’”

10. Msimlilie mtu aliyekufa,
wala msiombolezee kifo chake.
Bali mlilieni kwa uchungu yule aendaye mbali,
kwa kuwa hatarudi tena kuiona nchi yake.

11. Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya Shalumu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyetawala baada ya Yosia baba yake, na ambaye aliondoka mahali hapa: “Shalumu hatarudi tena mahali hapa, 12bali atafia hukohuko walikomchukua utumwani. Kamwe hataiona tena nchi hii.
Ujumbe juu ya Yehoyakimu

13“Ole wako Yehoyakimu
wewe unayejenga nyumba kwa dhuluma
na kuiwekea ghorofa bila kutumia haki.
Unawaajiri watu wakutumikie bure
wala huwalipi mishahara yao.


14Wewe wasema:
‘Nitalijenga jumba kubwa,
lenye vyumba vikubwa ghorofani.’
Kisha huifanyia madirisha,
ukafunika kuta zake kwa mbao za mierezi,
na kuipaka rangi nyekundu!

15Unadhani umekuwa mfalme
kwa kushindana kujenga kwa mierezi?
Baba yako alikula na kunywa,
akatenda mambo ya haki na mema
ndipo mambo yake yakamwendea vema.

16Aliwapatia haki maskini na wahitaji,
na mambo yake yakamwendea vema.
Hii ndiyo maana ya kunijua mimi Mwenyezi-Mungu.

17. Lakini macho yako wewe na moyo wako,
hungangania tu mapato yasiyo halali.
Unamwaga damu ya wasio na hatia,


Mungu awasaidie mnapolitafakari neno hili.

Nakala zifike kwa:

1. Mhe. Rais, Dkt John Pombe Magufuli
2. Mhe Tundu Antipas Lisu

Pia Ziwafikie;
1. Wenyeviti na Makatibu wote wa Vyama vya siasa
2. Viongozi wa Nyanja zote za kitaifa na kijamii

Ipende nchi yako, penda watu wako. Kuwa Mzalendo.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Dar es Salaam
 
Back
Top Bottom