Ujumbe wa leo; Wapungie mkono

Matanga

JF-Expert Member
Nov 13, 2019
2,281
3,973
Siku moja nilichukua taxi nikiwa naelekea uwanja wa ndege. Dereva huku akiendesha kwa ustaarabu sana mara ghafla pasipo kutegemea gari ya taka ikajitokeza mbele yetu kutokea nje ya barabara.

Dereva wa taxi kwa umakini na neema ya Mungu akalikwepa gari hilo na ilikuwa kidogo agonge gari zingine mbele yetu. Pasipo kutegemea dereva wa gari la taka akaanza kufoka na kutoa matusi kwa kelele kubwa!

Katika hali ya kushangaza dereva wa taxi alitabasamu na kuwapungia mkono waliokuwa kwenye gari la taka na ndipo kwa mshangao nilimuuliza; "Inakuwaje ufanye hivyo wakati walitaka kutuua na hata kuharibu mali yako?"

Akajibu kwa upole akinitazama kwa tabasamu akasema. “Katika maisha yetu, kuna watu wako kama gari la taka. Wamejaa misongo, hasira, maumivu, wamechoka kifikra, kiuchumi na kimaisha, na wamejaa masikitiko mengi. Watu hao takataka zao zinazopowazidi hutafuta mahali pa kuzitupa na haijalishi mazingira wanakozitupia.

Hivyo jIfunze kutogombana nao. Wapungie mkono, wape tabasamu, songa mbele. Haikupunguzii kitu. Wala usiruhusu takataka zao zikupate."

Uliumbwa kuyafurahia maisha. Usiyafupishe kwa kuamka asubuhi na kinyongo, na hasira, na ghadhabu kwa sababu ya mtu fulani.

Neno linasema ; “Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi, wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi.”

Watafiti wanasema 10% ya maisha ni vile ulivyoyatengeneza lakini 90% ya maisha ni vile unavyoyachukulia .
USIACHE KUMTEGEMEA MWENYEZI MUNGU

Mchana mwema
 
hakika dereva tax alikuwa sahihi 100%.

wakati mwingine tafakari jambo kwa kutokea mbele,usilifate kama lilivyokuja ugongane nalo.

kujishusha kwa mpumbavu hakukupunguzii heshima yako,bali kumfanya ajitafakari wakati mwingine.
 
hakika dereva tax alikuwa sahihi 100%.

wakati mwingine tafakari jambo kwa kutokea mbele,usilifate kama lilivyokuja ugongane nalo.

kujishusha kwa mpumbavu hakukupunguzii heshima yako,bali kumfanya ajitafakari wakati mwingine.
Huo ndy ukweli mtupu
 
Siku moja nilichukua taxi nikiwa naelekea uwanja wa ndege. Dereva huku akiendesha kwa ustaarabu sana mara ghafla pasipo kutegemea gari ya taka ikajitokeza mbele yetu kutokea nje ya barabara.

Dereva wa taxi kwa umakini na neema ya Mungu akalikwepa gari hilo na ilikuwa kidogo agonge gari zingine mbele yetu. Pasipo kutegemea dereva wa gari la taka akaanza kufoka na kutoa matusi kwa kelele kubwa!

Katika hali ya kushangaza dereva wa taxi alitabasamu na kuwapungia mkono waliokuwa kwenye gari la taka na ndipo kwa mshangao nilimuuliza; "Inakuwaje ufanye hivyo wakati walitaka kutuua na hata kuharibu mali yako?"

Akajibu kwa upole akinitazama kwa tabasamu akasema. “Katika maisha yetu, kuna watu wako kama gari la taka. Wamejaa misongo, hasira, maumivu, wamechoka kifikra, kiuchumi na kimaisha, na wamejaa masikitiko mengi. Watu hao takataka zao zinazopowazidi hutafuta mahali pa kuzitupa na haijalishi mazingira wanakozitupia.

Hivyo jIfunze kutogombana nao. Wapungie mkono, wape tabasamu, songa mbele. Haikupunguzii kitu. Wala usiruhusu takataka zao zikupate."

Uliumbwa kuyafurahia maisha. Usiyafupishe kwa kuamka asubuhi na kinyongo, na hasira, na ghadhabu kwa sababu ya mtu fulani.

Neno linasema ; “Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi, wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi.”

Watafiti wanasema 10% ya maisha ni vile ulivyoyatengeneza lakini 90% ya maisha ni vile unavyoyachukulia .
USIACHE KUMTEGEMEA MWENYEZI MUNGU

Mchana mwema

waooh i love this
 
Back
Top Bottom