EINSTEIN112
JF-Expert Member
- Oct 26, 2018
- 21,713
- 35,525
Ayubu 7:17-18
[17]Je! Mtu ni kitu gani, hata ukamtukuza,
Na kumtia moyoni mwako,
[18]Na kumwangalia kila asubuhi,
Na kumjaribu kila dakika?
Mithali 3:1-8
[1]Mwanangu, usiisahau sheria yangu,
Bali moyo wako uzishike amri zangu.
[2]Maana zitakuongezea wingi wa siku.
Na miaka ya uzima, na amani.
[3]Rehema na kweli zisifarakane nawe;
Zifunge shingoni mwako;
Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
[4]Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri,
Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.
[5]Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote,
Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
[6]Katika njia zako zote mkiri yeye,
Naye atayanyosha mapito yako.
[7]Usiwe mwenye hekima machoni pako;
Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.
[8]Itakuwa afya mwilini pako,
Na mafuta mifupani mwako.
1 NYAKATI. 28:9
Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA hutafuta-tafuta mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, ataonekana nawe; ukimwacha, atakutupa milele
Muwe na siku njema
[17]Je! Mtu ni kitu gani, hata ukamtukuza,
Na kumtia moyoni mwako,
[18]Na kumwangalia kila asubuhi,
Na kumjaribu kila dakika?
Mithali 3:1-8
[1]Mwanangu, usiisahau sheria yangu,
Bali moyo wako uzishike amri zangu.
[2]Maana zitakuongezea wingi wa siku.
Na miaka ya uzima, na amani.
[3]Rehema na kweli zisifarakane nawe;
Zifunge shingoni mwako;
Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
[4]Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri,
Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.
[5]Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote,
Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
[6]Katika njia zako zote mkiri yeye,
Naye atayanyosha mapito yako.
[7]Usiwe mwenye hekima machoni pako;
Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.
[8]Itakuwa afya mwilini pako,
Na mafuta mifupani mwako.
1 NYAKATI. 28:9
Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA hutafuta-tafuta mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, ataonekana nawe; ukimwacha, atakutupa milele
Muwe na siku njema