Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,597
- 215,272
MEMBE, KINANA, MAKAMBA EPUKENI UPUMBAVU WA JANUARY, NGELEJA NA NAPE, MTAMALIZWA!
Na Bollen Ngetti
SIASA za kutukanana na kuombana misamaha hadharani ni siasa mpya ndani ya CCM na nchini kwa ujumla. Ni siasa za majitaka tusizotakiwa kuendekeza hata kidogo.
Kwanza ieleweke kwamba katika siasa hakuna matusi. Hivi tunajua matusi? Kwenye siasa kuna vijembe, kejeli, mizaha, hoja, ukiita matusi sawa lakini hawaombani misamaha mbele ya kamera.
Mfano; Mwenyekiti wangu Rais Magufuli inadaiwa kina Nape walimwita "mshamba na limbukeni wa madaraka" hili ni tusi kweli. Kama mwanasiasa nilitegemea Magufuli naye kutafuta jukwaa na kuwapa za usoni mfano; "sawa mimi mshamba na limbukeni wa madaraka lakini si mimi ndiye Mwenyekiti wenu wa chama na Rais wenu? Nani mshamba sasa". Kwa kauli hii vijana hawa wangekaa kimya na maisha yangeendelea nao wangeendelea kufanya siasa.
Huku kuomba msamaha kunajenga picha mbili kwanza unayeomba msamaha hujiamini na huamini kauli yako na kuusimamia. Pili inatujengea Picha hasi kwa Mwenyekiti kwamba si mpambanaji wa kisiasa. Kwamba ni mtu wa visasi. Hili si sahihi.
Kama mlimuona Rais mshamba na limbukeni wa madaraka kwa nini msisimamie hilo na kutoa sababu za kushawishi wengine tuamini huo ushamba na ulimbukeni wa Mwenyekiti? Kumbe mlijua mnatenda kosa ndio maana sasa mnajidhalilisha kutubu? Ni lini tutapata mwanasiasa makini na jasiri wanaoamini maneno yao?
Kwani hamkuwa na ushahidi wa maneno mliyosema dhidi ya Rais ? Mmempa Magufuli karata nzuri sana ya kuwamaliza. Lakini pia kumbukeni January, Nape na Mwigulu 2016 niliwaandikia kuwa, " enyi vijana watatu Nape, January na Mwigulu ondokeni peke yenu mtaaibishwa hamtakiwi" mkapuuza. Sasa mmekatwa si mikia tu bali hadi macho ya kisiasa mmetobolewa. Kwani mnaogopa nini kufukuzwa CCM? Kwani siasa ni mpaka uwe CCM? Jinga kabisa.
Nape ni miongoni mwa mwanasiasa vijana aliyejijengea umaarufu kutokana na misimamo. Kwenye hili unakosea wapi? Ngeleja sitaki kumsemea maana ni msaka tonge wa kawaida aliyeingizwa kwenye siasa na Rostam Aziz kwa kazi maalum ya kufanikisha dili la Dowans. Tumweke pembeni lakini Nape ni zao la siasa. Kwa nini Leo ajidhalilishe namna hii?
Tujenge utamaduni wa kushindana kwa hoja na kusimamia unachoamini mwanzo mwisho hata kama kwa kufanya hivyo kutakugharimu jasho na damu.
Nitasikitika na kuumia siku nikiona Bernard Membe naye akibisha hodi Ikulu kwenda kutubu kwa "makosa" yake. Atambue huo utakuwa ni tamati ya maisha yake kisiasa kitakachofuata ni kwenda kuwinda ngiri kijijini Rondo huko Lindi. Haki kadhalika Mzee Kijana na Makamba japo siwaamini sana maana hawana ambition ya madaraka ya kisiasa kama Membe. Lakini all in all hawapaswi kupitia njia walimopitia vijana wao waoga wa vivuli vyao. Kosa la mauti kisiasa.
Mwisho nitoe wito kwa upinzani kuacha kubweteka na yanayoendelea huku kwetu na kuyashadadia. Katika political science the more you talk about us ndivyo tunavyojijenga kisiasa maana vichwani kumejaa Nape, January, Membe, Kinana nakadhalika. Mnasahau kuwa tunaelekea uchaguzi Mkuu. Ni wakati wa kutafakari na kuunganisha vyama vyote vya upinzani na kumpata strong candidate atakayepambana na mgombea wa CCM ambaye hajatangazwa.
Ni wakati wa kutafuta pesa za kampeni kwa njia za uwazi bila kutegemea ruzuku. Kampeni za Urais ni fedha nyingi anzeni sasa. Nunueni vyombo vya habari hasa local radios stations. Sijui kama mnanielewa maana natamani tuzifundishe nchini JIRANI demokrasia.
2020 sitopenda kuona utitiri wa wagombea Urais. Badala yake wawe wawili tu? Vivyo hivyo nafasi za Ubunge. Ili hatimaye Bunge na Serikali visimamie maendeleo kwa hofu kuogopa kung'olewa next time.
#AchaWoga2020
#MguseniAnuke
Na Bollen Ngetti
SIASA za kutukanana na kuombana misamaha hadharani ni siasa mpya ndani ya CCM na nchini kwa ujumla. Ni siasa za majitaka tusizotakiwa kuendekeza hata kidogo.
Kwanza ieleweke kwamba katika siasa hakuna matusi. Hivi tunajua matusi? Kwenye siasa kuna vijembe, kejeli, mizaha, hoja, ukiita matusi sawa lakini hawaombani misamaha mbele ya kamera.
Mfano; Mwenyekiti wangu Rais Magufuli inadaiwa kina Nape walimwita "mshamba na limbukeni wa madaraka" hili ni tusi kweli. Kama mwanasiasa nilitegemea Magufuli naye kutafuta jukwaa na kuwapa za usoni mfano; "sawa mimi mshamba na limbukeni wa madaraka lakini si mimi ndiye Mwenyekiti wenu wa chama na Rais wenu? Nani mshamba sasa". Kwa kauli hii vijana hawa wangekaa kimya na maisha yangeendelea nao wangeendelea kufanya siasa.
Huku kuomba msamaha kunajenga picha mbili kwanza unayeomba msamaha hujiamini na huamini kauli yako na kuusimamia. Pili inatujengea Picha hasi kwa Mwenyekiti kwamba si mpambanaji wa kisiasa. Kwamba ni mtu wa visasi. Hili si sahihi.
Kama mlimuona Rais mshamba na limbukeni wa madaraka kwa nini msisimamie hilo na kutoa sababu za kushawishi wengine tuamini huo ushamba na ulimbukeni wa Mwenyekiti? Kumbe mlijua mnatenda kosa ndio maana sasa mnajidhalilisha kutubu? Ni lini tutapata mwanasiasa makini na jasiri wanaoamini maneno yao?
Kwani hamkuwa na ushahidi wa maneno mliyosema dhidi ya Rais ? Mmempa Magufuli karata nzuri sana ya kuwamaliza. Lakini pia kumbukeni January, Nape na Mwigulu 2016 niliwaandikia kuwa, " enyi vijana watatu Nape, January na Mwigulu ondokeni peke yenu mtaaibishwa hamtakiwi" mkapuuza. Sasa mmekatwa si mikia tu bali hadi macho ya kisiasa mmetobolewa. Kwani mnaogopa nini kufukuzwa CCM? Kwani siasa ni mpaka uwe CCM? Jinga kabisa.
Nape ni miongoni mwa mwanasiasa vijana aliyejijengea umaarufu kutokana na misimamo. Kwenye hili unakosea wapi? Ngeleja sitaki kumsemea maana ni msaka tonge wa kawaida aliyeingizwa kwenye siasa na Rostam Aziz kwa kazi maalum ya kufanikisha dili la Dowans. Tumweke pembeni lakini Nape ni zao la siasa. Kwa nini Leo ajidhalilishe namna hii?
Tujenge utamaduni wa kushindana kwa hoja na kusimamia unachoamini mwanzo mwisho hata kama kwa kufanya hivyo kutakugharimu jasho na damu.
Nitasikitika na kuumia siku nikiona Bernard Membe naye akibisha hodi Ikulu kwenda kutubu kwa "makosa" yake. Atambue huo utakuwa ni tamati ya maisha yake kisiasa kitakachofuata ni kwenda kuwinda ngiri kijijini Rondo huko Lindi. Haki kadhalika Mzee Kijana na Makamba japo siwaamini sana maana hawana ambition ya madaraka ya kisiasa kama Membe. Lakini all in all hawapaswi kupitia njia walimopitia vijana wao waoga wa vivuli vyao. Kosa la mauti kisiasa.
Mwisho nitoe wito kwa upinzani kuacha kubweteka na yanayoendelea huku kwetu na kuyashadadia. Katika political science the more you talk about us ndivyo tunavyojijenga kisiasa maana vichwani kumejaa Nape, January, Membe, Kinana nakadhalika. Mnasahau kuwa tunaelekea uchaguzi Mkuu. Ni wakati wa kutafakari na kuunganisha vyama vyote vya upinzani na kumpata strong candidate atakayepambana na mgombea wa CCM ambaye hajatangazwa.
Ni wakati wa kutafuta pesa za kampeni kwa njia za uwazi bila kutegemea ruzuku. Kampeni za Urais ni fedha nyingi anzeni sasa. Nunueni vyombo vya habari hasa local radios stations. Sijui kama mnanielewa maana natamani tuzifundishe nchini JIRANI demokrasia.
2020 sitopenda kuona utitiri wa wagombea Urais. Badala yake wawe wawili tu? Vivyo hivyo nafasi za Ubunge. Ili hatimaye Bunge na Serikali visimamie maendeleo kwa hofu kuogopa kung'olewa next time.
#AchaWoga2020
#MguseniAnuke