Sonara
JF-Expert Member
- Oct 2, 2008
- 726
- 68
Haikunishanga kumuona huyu mama Ann Makinda amefika hapa Zanzibar kuendeleza mchezo wao wa kuwacheza (shere )viongozi wa serekali na wananchi wa Zanzibar (siku zote kikulacho kinguoni mwako) huyu ndie mama aliyekataa kata kata kuwapa wabunge wakati wa kufuatilkia ajali iliyotokea, wakiwa ndani ya Bunge lililochaguliwa na wananchi hao au jamaa zao waliofikwa na maafa nakuwafanya wao kujiita wabunge wa Jamhuri ya Tanzania,nilitegemea hilo kutokea kwa yeye kufika zanzibar lakini simlaumu mama Anna makinda kwani akifanyacho ni sawa na muwamba ngoma huvutia kwake,Nimekuwa najiuliza Viongozi wa serekali ya Zanzibar wataendelea kuridhia kupakwa mafuta kwa nyuma ya chupa mpaka lini ? au ndio kusema wametiwa shemere?