Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndugu zangu wazalendo wa nchi hii,
Nimekuwa nikifuatilia kwa umakini mkubwa mwenendo wa matokeo ya uchaguzi kutoka maeneo mbalimbali hususan kwa nafasi ya urais. Kwa wale wenzangu walioanza kufuatilia mapema kabisa, lazima watakuwa wameshtuka sana na namna "trend" ya matokeo ya urais ilivyobadilika ghafla. Matokeo ya awali kutoka mikoani yalianza kuonyesha tofauti ndogo ya kura kati ya Dr. Slaa na Jakaya Kikwete. Hali hiyo iliendelea kwa kipindi kirefu na kwenye baadhi ya majimbo kama Iringa, Mbeya, Moshi na Arusha Dr. Slaa alikuwa anaongoza kwa mbali kabisa. Baadaye nilishtuka nilipoambiwa kwamba matokeo ya urais yatakuwa yanatangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) na siyo wasimamizi wa uchaguzi kutoka kwenye majimbo. Kama suala la uchaguzi ni la wazi na huru, kwa nini wasimamizi wa uchaguzi wasitangaze tu matokeo ya urais sambamba na matokeo ya ubunge na udiwani. Ni nini kinachozuia?????
Ndugu zangu ninachokiona hapa, ni kama kuna ujanja unaotaka kufanywa na watanzania wazalendo hatutakiwa hata mara moja kukaa kimya na kuridhika na matokeo ya urais yaliyoanza kutangazwa na NEC. Ninawaomba sana tena sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati wote nchini wafuatilie mlingano wa matokeo (yaliyoidhinishwa na mawakala wa vyama husika) kutoka kwenye majimbo na matokeo yanayotangazwa na NEC. Sina hakika kama jambo hili linaweza kuruhusiwa lakini ninaona kuwa ni jambo la msingi sana. Lazima wananchi tujiridhishe kwamba kinachotangazwa na NEC kwamba ndiyo jumla ya kura za urais kwa mgombea fulani kutoka jimbo fulani lazima iwe kweli ndiyo jumla ya matokeo ya vituo vyote vya jimbo husika. Ninawaomba sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati mlifuatilie jambo hili kwa ukaribu sana kwani inawezekana hapa ndipo ujanja mkubwa unaofanyika ili kuwezesha chama tawala kuendelea kuongoza nchi hii.
Nsdugu zangu, ninaandika haya kwa uchungu mkubwa sana baada ya kusoma maoni ya wananchi ninaokutana nao mitaani na hata ninaposoma kwenye mitandao. Ukweli ni kwamba watanzania wengi hivi sasa wameichoka ccm na wanataka mabadiliko. Hali hii imeonekana dhahiri wakati wa mikutano ya chadema kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini. Mwaka huu wananchi walidhamiria kuiangusha ccm tena kwa kishindo kikubwa. Tafadhali viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati tusiwakatishe tamaa wananchi lazima tuthamini na kuenzi harakati za wananchi kutaka mabadiliko. Fuatilieni kwa ukaribu zaidi hasa matokeo ya urais yanayotangazwa na NEC ili wananchi wazalendo wajiridhishe.
Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.
Nimekuwa nikifuatilia kwa umakini mkubwa mwenendo wa matokeo ya uchaguzi kutoka maeneo mbalimbali hususan kwa nafasi ya urais. Kwa wale wenzangu walioanza kufuatilia mapema kabisa, lazima watakuwa wameshtuka sana na namna "trend" ya matokeo ya urais ilivyobadilika ghafla. Matokeo ya awali kutoka mikoani yalianza kuonyesha tofauti ndogo ya kura kati ya Dr. Slaa na Jakaya Kikwete. Hali hiyo iliendelea kwa kipindi kirefu na kwenye baadhi ya majimbo kama Iringa, Mbeya, Moshi na Arusha Dr. Slaa alikuwa anaongoza kwa mbali kabisa. Baadaye nilishtuka nilipoambiwa kwamba matokeo ya urais yatakuwa yanatangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) na siyo wasimamizi wa uchaguzi kutoka kwenye majimbo. Kama suala la uchaguzi ni la wazi na huru, kwa nini wasimamizi wa uchaguzi wasitangaze tu matokeo ya urais sambamba na matokeo ya ubunge na udiwani. Ni nini kinachozuia?????
Ndugu zangu ninachokiona hapa, ni kama kuna ujanja unaotaka kufanywa na watanzania wazalendo hatutakiwa hata mara moja kukaa kimya na kuridhika na matokeo ya urais yaliyoanza kutangazwa na NEC. Ninawaomba sana tena sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati wote nchini wafuatilie mlingano wa matokeo (yaliyoidhinishwa na mawakala wa vyama husika) kutoka kwenye majimbo na matokeo yanayotangazwa na NEC. Sina hakika kama jambo hili linaweza kuruhusiwa lakini ninaona kuwa ni jambo la msingi sana. Lazima wananchi tujiridhishe kwamba kinachotangazwa na NEC kwamba ndiyo jumla ya kura za urais kwa mgombea fulani kutoka jimbo fulani lazima iwe kweli ndiyo jumla ya matokeo ya vituo vyote vya jimbo husika. Ninawaomba sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati mlifuatilie jambo hili kwa ukaribu sana kwani inawezekana hapa ndipo ujanja mkubwa unaofanyika ili kuwezesha chama tawala kuendelea kuongoza nchi hii.
Nsdugu zangu, ninaandika haya kwa uchungu mkubwa sana baada ya kusoma maoni ya wananchi ninaokutana nao mitaani na hata ninaposoma kwenye mitandao. Ukweli ni kwamba watanzania wengi hivi sasa wameichoka ccm na wanataka mabadiliko. Hali hii imeonekana dhahiri wakati wa mikutano ya chadema kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini. Mwaka huu wananchi walidhamiria kuiangusha ccm tena kwa kishindo kikubwa. Tafadhali viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati tusiwakatishe tamaa wananchi lazima tuthamini na kuenzi harakati za wananchi kutaka mabadiliko. Fuatilieni kwa ukaribu zaidi hasa matokeo ya urais yanayotangazwa na NEC ili wananchi wazalendo wajiridhishe.
Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.