Elections 2010 Ujumbe Muhimu kwa Viongozi Wote wa Chadema na Wanaharakati Wote Nchini

Gosbertgoodluck

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,855
401
Ndugu zangu wazalendo wa nchi hii,

Nimekuwa nikifuatilia kwa umakini mkubwa mwenendo wa matokeo ya uchaguzi kutoka maeneo mbalimbali hususan kwa nafasi ya urais. Kwa wale wenzangu walioanza kufuatilia mapema kabisa, lazima watakuwa wameshtuka sana na namna "trend" ya matokeo ya urais ilivyobadilika ghafla. Matokeo ya awali kutoka mikoani yalianza kuonyesha tofauti ndogo ya kura kati ya Dr. Slaa na Jakaya Kikwete. Hali hiyo iliendelea kwa kipindi kirefu na kwenye baadhi ya majimbo kama Iringa, Mbeya, Moshi na Arusha Dr. Slaa alikuwa anaongoza kwa mbali kabisa. Baadaye nilishtuka nilipoambiwa kwamba matokeo ya urais yatakuwa yanatangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) na siyo wasimamizi wa uchaguzi kutoka kwenye majimbo. Kama suala la uchaguzi ni la wazi na huru, kwa nini wasimamizi wa uchaguzi wasitangaze tu matokeo ya urais sambamba na matokeo ya ubunge na udiwani. Ni nini kinachozuia?????

Ndugu zangu ninachokiona hapa, ni kama kuna ujanja unaotaka kufanywa na watanzania wazalendo hatutakiwa hata mara moja kukaa kimya na kuridhika na matokeo ya urais yaliyoanza kutangazwa na NEC. Ninawaomba sana tena sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati wote nchini wafuatilie mlingano wa matokeo (yaliyoidhinishwa na mawakala wa vyama husika) kutoka kwenye majimbo na matokeo yanayotangazwa na NEC. Sina hakika kama jambo hili linaweza kuruhusiwa lakini ninaona kuwa ni jambo la msingi sana. Lazima wananchi tujiridhishe kwamba kinachotangazwa na NEC kwamba ndiyo jumla ya kura za urais kwa mgombea fulani kutoka jimbo fulani lazima iwe kweli ndiyo jumla ya matokeo ya vituo vyote vya jimbo husika. Ninawaomba sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati mlifuatilie jambo hili kwa ukaribu sana kwani inawezekana hapa ndipo ujanja mkubwa unaofanyika ili kuwezesha chama tawala kuendelea kuongoza nchi hii.

Nsdugu zangu, ninaandika haya kwa uchungu mkubwa sana baada ya kusoma maoni ya wananchi ninaokutana nao mitaani na hata ninaposoma kwenye mitandao. Ukweli ni kwamba watanzania wengi hivi sasa wameichoka ccm na wanataka mabadiliko. Hali hii imeonekana dhahiri wakati wa mikutano ya chadema kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini. Mwaka huu wananchi walidhamiria kuiangusha ccm tena kwa kishindo kikubwa. Tafadhali viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati tusiwakatishe tamaa wananchi lazima tuthamini na kuenzi harakati za wananchi kutaka mabadiliko. Fuatilieni kwa ukaribu zaidi hasa matokeo ya urais yanayotangazwa na NEC ili wananchi wazalendo wajiridhishe.

Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.
 
I concur with you, mimi nashauri vyama husika kwa kuwa wana mawakala sehemu zote, wahakikishe matokeo ya vituoni yaliyosainiwa na mawakala na haya ya NEC. Kuna haja ya kuwa makini na hii NEC ya ajabu ambayo siku zote walisema wako tayari wamejiandaa, wana vifaa na teknonolojia ghafla sasa wamebadirika.
 
pole ndg zangu uchungu ni mkubwa unafikiri ni urais tu watu wamelala viwanjani kupata watokeo bila mafanikio kuna nini ?
 
Mawazo mazuri.

Naomba nipigwe shule kidogo.
Sheria ya uchaguzi inasema nini kuhusu kutangazwa kwa matokeo ya Urais, Ubunge na Udiwani??
Je tunaweza kupata nakala ya sheria ya uchaguzi hapa mtandaooni JF ili nasi mafundi mchundo tujinoe na sheria za uchaguzi.

Asandi sana wajameni
 
Wewe kwani hujuwi kuwa hao hao Viongozi wa hiyo ( Tume ya Uchaguzi (NEC) ni watu wa CCM? malalimiko yako hayatasaidia kitu bwana Mambo ya ngoswe muachie ngoswe

Maisha bora kwa kila Mtanzania. Hio ni nyumba ya mmoja wa mwanachama wetu. Mara baada ya Uchaguzi tutamjengea
 
Ndugu zangu wazalendo wa nchi hii,

Nimekuwa nikifuatilia kwa umakini mkubwa mwenendo wa matokeo ya uchaguzi kutoka maeneo mbalimbali hususan kwa nafasi ya urais. Kwa wale wenzangu walioanza kufuatilia mapema kabisa, lazima watakuwa wameshtuka sana na namna "trend" ya matokeo ya urais ilivyobadilika ghafla. Matokeo ya awali kutoka mikoani yalianza kuonyesha tofauti ndogo ya kura kati ya Dr. Slaa na Jakaya Kikwete. Hali hiyo iliendelea kwa kipindi kirefu na kwenye baadhi ya majimbo kama Iringa, Mbeya, Moshi na Arusha Dr. Slaa alikuwa anaongoza kwa mbali kabisa. Baadaye nilishtuka nilipoambiwa kwamba matokeo ya urais yatakuwa yanatangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) na siyo wasimamizi wa uchaguzi kutoka kwenye majimbo. Kama suala la uchaguzi ni la wazi na huru, kwa nini wasimamizi wa uchaguzi wasitangaze tu matokeo ya urais sambamba na matokeo ya ubunge na udiwani. Ni nini kinachozuia?????

Ndugu zangu ninachokiona hapa, ni kama kuna ujanja unaotaka kufanywa na watanzania wazalendo hatutakiwa hata mara moja kukaa kimya na kuridhika na matokeo ya urais yaliyoanza kutangazwa na NEC. Ninawaomba sana tena sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati wote nchini wafuatilie mlingano wa matokeo (yaliyoidhinishwa na mawakala wa vyama husika) kutoka kwenye majimbo na matokeo yanayotangazwa na NEC. Sina hakika kama jambo hili linaweza kuruhusiwa lakini ninaona kuwa ni jambo la msingi sana. Lazima wananchi tujiridhishe kwamba kinachotangazwa na NEC kwamba ndiyo jumla ya kura za urais kwa mgombea fulani kutoka jimbo fulani lazima iwe kweli ndiyo jumla ya matokeo ya vituo vyote vya jimbo husika. Ninawaomba sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati mlifuatilie jambo hili kwa ukaribu sana kwani inawezekana hapa ndipo ujanja mkubwa unaofanyika ili kuwezesha chama tawala kuendelea kuongoza nchi hii.

Nsdugu zangu, ninaandika haya kwa uchungu mkubwa sana baada ya kusoma maoni ya wananchi ninaokutana nao mitaani na hata ninaposoma kwenye mitandao. Ukweli ni kwamba watanzania wengi hivi sasa wameichoka ccm na wanataka mabadiliko. Hali hii imeonekana dhahiri wakati wa mikutano ya chadema kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini. Mwaka huu wananchi walidhamiria kuiangusha ccm tena kwa kishindo kikubwa. Tafadhali viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati tusiwakatishe tamaa wananchi lazima tuthamini na kuenzi harakati za wananchi kutaka mabadiliko. Fuatilieni kwa ukaribu zaidi hasa matokeo ya urais yanayotangazwa na NEC ili wananchi wazalendo wajiridhishe.

Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.
habari zingine zimekaa kichochezi sana
 
Mawazo mazuri.

Naomba nipigwe shule kidogo.
Sheria ya uchaguzi inasema nini kuhusu kutangazwa kwa matokeo ya Urais, Ubunge na Udiwani??
Je tunaweza kupata nakala ya sheria ya uchaguzi hapa mtandaooni JF ili nasi mafundi mchundo tujinoe na sheria za uchaguzi.

Asandi sana wajameni


Hata kama sheria inaipa nguvu NEC kutangaza matokeo lakini lazima kuwe na a room ya mgombea ambaye hajaridhika kupitia upya process yote na hii itaongezewa nguvu zaidi na wananchi wenyewe ikiwezekana hata kwa kufanya maandamano ya amani kuonesha kutoridhishwa na matokeo ya urais. Lazima tuoneshe mbele ya jamii za kimataifa kwamba wananchi hawajaridhika na matokeo ili NEC ikubali ikiwezekana kuunda independent team ya kufanya mapitio. Tukikubali kirahisi hatutafanikiwa kuiondoa ccm kwenye kiti cha urais milele. Huo ndiyo ujumbe wangu kwa Dr. Slaa, Prof. Lipumba na wanaharakati wote nchini.
 
Ndugu zangu wazalendo wa nchi hii,

Nimekuwa nikifuatilia kwa umakini mkubwa mwenendo wa matokeo ya uchaguzi kutoka maeneo mbalimbali hususan kwa nafasi ya urais. Kwa wale wenzangu walioanza kufuatilia mapema kabisa, lazima watakuwa wameshtuka sana na namna "trend" ya matokeo ya urais ilivyobadilika ghafla. Matokeo ya awali kutoka mikoani yalianza kuonyesha tofauti ndogo ya kura kati ya Dr. Slaa na Jakaya Kikwete. Hali hiyo iliendelea kwa kipindi kirefu na kwenye baadhi ya majimbo kama Iringa, Mbeya, Moshi na Arusha Dr. Slaa alikuwa anaongoza kwa mbali kabisa. Baadaye nilishtuka nilipoambiwa kwamba matokeo ya urais yatakuwa yanatangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) na siyo wasimamizi wa uchaguzi kutoka kwenye majimbo. Kama suala la uchaguzi ni la wazi na huru, kwa nini wasimamizi wa uchaguzi wasitangaze tu matokeo ya urais sambamba na matokeo ya ubunge na udiwani. Ni nini kinachozuia?????

Ndugu zangu ninachokiona hapa, ni kama kuna ujanja unaotaka kufanywa na watanzania wazalendo hatutakiwa hata mara moja kukaa kimya na kuridhika na matokeo ya urais yaliyoanza kutangazwa na NEC. Ninawaomba sana tena sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati wote nchini wafuatilie mlingano wa matokeo (yaliyoidhinishwa na mawakala wa vyama husika) kutoka kwenye majimbo na matokeo yanayotangazwa na NEC. Sina hakika kama jambo hili linaweza kuruhusiwa lakini ninaona kuwa ni jambo la msingi sana. Lazima wananchi tujiridhishe kwamba kinachotangazwa na NEC kwamba ndiyo jumla ya kura za urais kwa mgombea fulani kutoka jimbo fulani lazima iwe kweli ndiyo jumla ya matokeo ya vituo vyote vya jimbo husika. Ninawaomba sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati mlifuatilie jambo hili kwa ukaribu sana kwani inawezekana hapa ndipo ujanja mkubwa unaofanyika ili kuwezesha chama tawala kuendelea kuongoza nchi hii.

Nsdugu zangu, ninaandika haya kwa uchungu mkubwa sana baada ya kusoma maoni ya wananchi ninaokutana nao mitaani na hata ninaposoma kwenye mitandao. Ukweli ni kwamba watanzania wengi hivi sasa wameichoka ccm na wanataka mabadiliko. Hali hii imeonekana dhahiri wakati wa mikutano ya chadema kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini. Mwaka huu wananchi walidhamiria kuiangusha ccm tena kwa kishindo kikubwa. Tafadhali viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati tusiwakatishe tamaa wananchi lazima tuthamini na kuenzi harakati za wananchi kutaka mabadiliko. Fuatilieni kwa ukaribu zaidi hasa matokeo ya urais yanayotangazwa na NEC ili wananchi wazalendo wajiridhishe.

Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.

NEC wanatakiwa kutangaza mshindi tu. Hivi yale matokeo ya Urais yanayobandikwa kila kituo sio kutangaza matokeo huko? Hivi kutangaza ni mpaka utoe sauti? Je, matangazo ya kwenye magazeti yanatoa sauti? Narudia tena NEC wanatanganza mshindi tu.

Naamini mafunzo yangu ya JKT yatanisaidia mara itakapokuwa vinginevyo!!
 
Gosbert, Acha kutushawishi visivyowezekana. Tangu mwanzo niliwaambia kuwa ni vigumu kumshinada kiongozi aliye na majimbo 16 ya wabunge waliopita bila kupingwa. Tusidangayane hapa. Maeneo mengi ya nchi CCM wameachiwa watambe bila kusimamisha wapinzani wenye nguvu na hivyo kuipa CCM ushindi wa asilimia mia moja. Ukweli ni kwamba Dk. Slaa atapata kura nyingi ambazo hazitatosha kumpiku Dk. JK. Haiwezekani hata ukiomba kwa kuelekeza ****** ya juu mbinguni. Sipendi mtu aanze ku-instigate fujo kwa kutumia madai yasiyo na msingi na ukweli. Usituaminishe kuwa kuna uchakachuaji wa matokeo huku CCM ikiendelea kupata majimbo mengi kila kona ya nchi. Hizo hesabu zako za chekechea hazina msingi kwenye forum hii. Umeniudhi sana kwa kutaka kutupofusha kana kwamba unawaandikia ujumbe mazezeta. Sisi sio mazezeta. Chama cha Chadema kimefanikiwa katika uchaguzi huu na nilazima kijipongeze lakini kwa nafasi ya Urais, No, no no no noooooooooooo! haiwezekani kushinda Urais. CCM itashinda kwa margin kubwa tu.
Chadema ijipange kwa ajili ya uchaguzi wa 2015. Hongera kwa sasa imefanikiwa kuongeza idadi kubwa ya wabunge lakini kwa Urais, haiwezekani.
Angalizo. Kwa mawazo yako, Hapa bara kungekuwa na ushindani kama ule wa Zanzibar sijui ungetuambiaje wana JF.
 
ndugu zangu wazalendo wa nchi hii,

nimekuwa nikifuatilia kwa umakini mkubwa mwenendo wa matokeo ya uchaguzi kutoka maeneo mbalimbali hususan kwa nafasi ya urais. Kwa wale wenzangu walioanza kufuatilia mapema kabisa, lazima watakuwa wameshtuka sana na namna "trend" ya matokeo ya urais ilivyobadilika ghafla. Matokeo ya awali kutoka mikoani yalianza kuonyesha tofauti ndogo ya kura kati ya dr. Slaa na jakaya kikwete. Hali hiyo iliendelea kwa kipindi kirefu na kwenye baadhi ya majimbo kama iringa, mbeya, moshi na arusha dr. Slaa alikuwa anaongoza kwa mbali kabisa. Baadaye nilishtuka nilipoambiwa kwamba matokeo ya urais yatakuwa yanatangazwa na tume ya uchaguzi (nec) na siyo wasimamizi wa uchaguzi kutoka kwenye majimbo. Kama suala la uchaguzi ni la wazi na huru, kwa nini wasimamizi wa uchaguzi wasitangaze tu matokeo ya urais sambamba na matokeo ya ubunge na udiwani. Ni nini kinachozuia?????

Ndugu zangu ninachokiona hapa, ni kama kuna ujanja unaotaka kufanywa na watanzania wazalendo hatutakiwa hata mara moja kukaa kimya na kuridhika na matokeo ya urais yaliyoanza kutangazwa na nec. Ninawaomba sana tena sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati wote nchini wafuatilie mlingano wa matokeo (yaliyoidhinishwa na mawakala wa vyama husika) kutoka kwenye majimbo na matokeo yanayotangazwa na nec. Sina hakika kama jambo hili linaweza kuruhusiwa lakini ninaona kuwa ni jambo la msingi sana. Lazima wananchi tujiridhishe kwamba kinachotangazwa na nec kwamba ndiyo jumla ya kura za urais kwa mgombea fulani kutoka jimbo fulani lazima iwe kweli ndiyo jumla ya matokeo ya vituo vyote vya jimbo husika. Ninawaomba sana viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati mlifuatilie jambo hili kwa ukaribu sana kwani inawezekana hapa ndipo ujanja mkubwa unaofanyika ili kuwezesha chama tawala kuendelea kuongoza nchi hii.

Nsdugu zangu, ninaandika haya kwa uchungu mkubwa sana baada ya kusoma maoni ya wananchi ninaokutana nao mitaani na hata ninaposoma kwenye mitandao. Ukweli ni kwamba watanzania wengi hivi sasa wameichoka ccm na wanataka mabadiliko. Hali hii imeonekana dhahiri wakati wa mikutano ya chadema kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini. Mwaka huu wananchi walidhamiria kuiangusha ccm tena kwa kishindo kikubwa. Tafadhali viongozi wa chadema, cuf na wanaharakati tusiwakatishe tamaa wananchi lazima tuthamini na kuenzi harakati za wananchi kutaka mabadiliko. Fuatilieni kwa ukaribu zaidi hasa matokeo ya urais yanayotangazwa na nec ili wananchi wazalendo wajiridhishe.

Mungu ibariki tanzania,
mungu ibariki afrika.

kwa kweli huo ndio wajibu wa msingi wa chama, wagombea ubunge na udiwani, ni lazima wahakiki matokeo ya urais. Kwa kuwa wanafahamu kuwa vyama vya upinzani vinaweza kuridhika kwa kupata madiwani na wabunge na kuanza kushangilia ndio maana wapo akina miraji kiwete na wana it wa ccm kuchakachua matokeo ya urais
 
Ndugu watanzania wenzangu hii inakatisha tamaa wapiga kura/watanzania ndiyo maana Wengi huwa hawapigi kura wakidai ni kupoteza muda sasa ninaanza kuamini hata mimi sijui km 2015 nitapiga, siyo urais tu mpaka udiwani, ubunge pia. kila wapinzani waliposhinda tume imekuwa na kigugumizi kutangaza matokeo mpaka wananchi wamepigwa mabomu na polisi, mfano Mwanza wananchi walijua ukweli lakini tume haikutaka kutoa matokeo mpaka jana usiku, unafikiri mwananchi ataendelea kuwa na imani na kupiga kura tena, kwaani kupigia upinzania unaambulia mabomu km si kukamatwa na kuwekwa rumande, hii siyo demokrasia. Kuna majimbo mengine pia ambayo ni fujo tu, km Tandika, temeke, kote polisi wanatumia nguvu kuzuia wananchi kudai haki yao. Kigoma tume imechelewa kutoa matokeo, mpaka jana jioni tume ilikuwa na kigugumizi kuwatangaza washindi wa jimbo Kasulu mjini na vijijini na madiwani wao. kwa nini sehemu ambayo CCM imeshinda tume imekuwa rahisi kutangaza? ukweli km demokrasia inasiginwa na tume tusubiri kumwaga damu tu tusiwacheke wenzetu. :nono:
 
I concur with you, mimi nashauri vyama husika kwa kuwa wana mawakala sehemu zote, wahakikishe matokeo ya vituoni yaliyosainiwa na mawakala na haya ya NEC. Kuna haja ya kuwa makini na hii NEC ya ajabu ambayo siku zote walisema wako tayari wamejiandaa, wana vifaa na teknonolojia ghafla sasa wamebadirika.

vyama vyetu haviko makini, kama vyama vilikuwa na mawakala ktk majimbo yote kwanini havitoi matokeo yake. Nashauri ktk chaguzi zijazo vyama vyote vya upinzani viwe na tume yake itakayo ratibu na kutoa matokeo yake yenyewe
 
Gosbert, Acha kutushawishi visivyowezekana. Tangu mwanzo niliwaambia kuwa ni vigumu kumshinada kiongozi aliye na majimbo 16 ya wabunge waliopita bila kupingwa. Tusidangayane hapa. Maeneo mengi ya nchi CCM wameachiwa watambe bila kusimamisha wapinzani wenye nguvu na hivyo kuipa CCM ushindi wa asilimia mia moja. Ukweli ni kwamba Dk. Slaa atapata kura nyingi ambazo hazitatosha kumpiku Dk. JK. Haiwezekani hata ukiomba kwa kuelekeza ****** ya juu mbinguni. Sipendi mtu aanze ku-instigate fujo kwa kutumia madai yasiyo na msingi na ukweli. Usituaminishe kuwa kuna uchakachuaji wa matokeo huku CCM ikiendelea kupata majimbo mengi kila kona ya nchi. Hizo hesabu zako za chekechea hazina msingi kwenye forum hii. Umeniudhi sana kwa kutaka kutupofusha kana kwamba unawaandikia ujumbe mazezeta. Sisi sio mazezeta. Chama cha Chadema kimefanikiwa katika uchaguzi huu na nilazima kijipongeze lakini kwa nafasi ya Urais, No, no no no noooooooooooo! haiwezekani kushinda Urais. CCM itashinda kwa margin kubwa tu.
Chadema ijipange kwa ajili ya uchaguzi wa 2015. Hongera kwa sasa imefanikiwa kuongeza idadi kubwa ya wabunge lakini kwa Urais, haiwezekani.
Angalizo. Kwa mawazo yako, Hapa bara kungekuwa na ushindani kama ule wa Zanzibar sijui ungetuambiaje wana JF.

Brother, hatuna maana kuchochea fujo!! Ambacho tunaweza kufanya ni kuhakiki hizo kura kuona kama zina-tally na zile ambazo mawakala wa CHADEMA wanazo na kama kuna tofauti basi kuna kila sababu ya kuyakataa matokeo hayo ya NEC na kuchukua hatua zinazofaa.
TUSIWE WAOGA NDUGU ZANGU, LIBERATION HAS A PRICE!!!! IT WILL NEVER BE SERVED ON A SILVER PLATTER!!!!!
 
Rugumye, kwa kauli hii --Nakunukuu--'ukweli km demokrasia inasiginwa na tume tusubiri kumwaga damu tu tusiwacheke wenzetu. :nono:'. Mm nashauri ianze damu yako kwanza halafu utuachie nchi yetu. Ukikasirika sana si uchukue sumu ya panya uikoroge kwenye glass na uinywe.
Ila utuambie wana JF ili tuje kushiriki mazishi yako. Huo ndio uamuzi wa busara. Mkwawa alikuwa jasiri, unaweza kfuata nyayo zake pia, just hang up yourself, boy. JF na familia yako itakukumbuka kwa ujasiri huo
 
Mikael, Usiwe na jazba, Nyerere alisema, mtu akikuambia jambo la kijinga, huku akijua kabisa kuwa anakuambia ujinga nawe ukakubali ujinga huo. Atakudharau.
Huwezi kuandika ujinga halafu ukategemea ukakubaliwa tu. When You post none sense we hit your assy immediately. Jf Hoyee!
 
Habari nilizozipata hivi punde, Mpendazoe ameshinda na ametangazwa rasmi
 
Gosbert, Acha kutushawishi visivyowezekana. Tangu mwanzo niliwaambia kuwa ni vigumu kumshinada kiongozi aliye na majimbo 16 ya wabunge waliopita bila kupingwa. Tusidangayane hapa. Maeneo mengi ya nchi CCM wameachiwa watambe bila kusimamisha wapinzani wenye nguvu na hivyo kuipa CCM ushindi wa asilimia mia moja. Ukweli ni kwamba Dk. Slaa atapata kura nyingi ambazo hazitatosha kumpiku Dk. JK. Haiwezekani hata ukiomba kwa kuelekeza ****** ya juu mbinguni. Sipendi mtu aanze ku-instigate fujo kwa kutumia madai yasiyo na msingi na ukweli. Usituaminishe kuwa kuna uchakachuaji wa matokeo huku CCM ikiendelea kupata majimbo mengi kila kona ya nchi. Hizo hesabu zako za chekechea hazina msingi kwenye forum hii. Umeniudhi sana kwa kutaka kutupofusha kana kwamba unawaandikia ujumbe mazezeta. Sisi sio mazezeta. Chama cha Chadema kimefanikiwa katika uchaguzi huu na nilazima kijipongeze lakini kwa nafasi ya Urais, No, no no no noooooooooooo! haiwezekani kushinda Urais. CCM itashinda kwa margin kubwa tu.
Chadema ijipange kwa ajili ya uchaguzi wa 2015. Hongera kwa sasa imefanikiwa kuongeza idadi kubwa ya wabunge lakini kwa Urais, haiwezekani.
moz-screenshot-2.png

Angalizo. Kwa mawazo yako, Hapa bara kungekuwa na ushindani kama ule wa Zanzibar sijui ungetuambiaje wana JF.
[https://www.jamiiforums.com/members/jackob.html
Join DateFri Oct 2010
Posts44
Thanks0
 
i concur with you, mimi nashauri vyama husika kwa kuwa wana mawakala sehemu zote, wahakikishe matokeo ya vituoni yaliyosainiwa na mawakala na haya ya nec. Kuna haja ya kuwa makini na hii nec ya ajabu ambayo siku zote walisema wako tayari wamejiandaa, wana vifaa na teknonolojia ghafla sasa wamebadirika.

kiraka kweli kweli, nec ya ajabu ila mawakala wamesaini matokeo na nakala mnazo, mkijumlisha chadema leo yawa ya harakati. Ushauri hesabuni kura zilizosainiwa na mawakala, kama ni sawa na za nec nyiwe uharakati weni ni viraka, kidumu chama cha mapinduzi
 
Back
Top Bottom