Amani Msumari
JF-Expert Member
- Aug 21, 2016
- 1,830
- 976
Ndugu Rais, nakusalimu.
Awali ya yote ninakupongeza kwa dhati kabisa kwa kuchaguliwa kwako kwa kishindo kuingoza tena Tanzania kwa miaka mingine mitano. Ushindi huo sio bahati mbaya. Watanzania wameridhishwa na uongozi wako unaoacha alama.
Ndugu Rais, ninaomba niende moja kwa moja kwenye hoja yangu. Serikali hii utakayoiongoza kwa kipindi hiki cha miaka mitano itakuwa ni serikali yenye deni kubwa sana kwa watanzania. Kipindi cha kampeni uliomba watanzania wakuletee madiwani na wabunge wa CCM, nao wamekusikia
Ninaamini spika wa bunge atatoka CCM hivyo ninaomba akapatikane mtu ambaye atashirikiana vizuri na serikali katika kuendesha bunge ili kuhakikisha watanzania wanapata neema zaidi. Ikiwapendeza, Job Yustino Ndugai bado anafaa
Naomba pia uelekeze (Kama mwenyekiti wa CCM taifa) pati kokasi kuhakikisha inalishawishi bunge kupitia sheria mbalimbali zinazolalamikiwa ili zilete tija zaidi kwa watanzania. Mfano mmoja wapo ni sheria ya mafao ya wastaafu pamoja na fao la kujitoa kwa watumishi wa kazi za muda mfupi
Kasi yako kwenye maendeleo imeonekana kuanzia usambazaji wa umeme vijijini, maji, huduma za afya na elimu, kilimo, barabara na nidhanu serikalini. Umekuwa sauti ya wale wasio na sauti na kuwawezesha kuwa na sauti.
Pamoja na hayo, wapo baadhi ya viongozi ambao hawawajibiki ipasavyo, unakuta ni mpaka ufike wewe mwenyewe ndio unakuta viongozi wanawajibika.
Mheshimiwa Rais naomba sana hili ukaliangalie ili wateule wako wachape kazi zaidi na kutatua kero za wananchi na wewe ukifika usikutane na shida ndogondogo.
Naomba ikikupendeza, waelekeze wateule wako wahangaike usiku na mchana kubuni miradi, kupanua wigo wa vipato vya halmashauri, kudhibiti rushwa na kuhakikisha wanasimamia sera za serikali ili vijana waweze kujiajiri.
Kilimo, ufugaji na ujasiriamali vikipewa msukumo mkubwa zaidi katika ngazi za wilaya na halmashauri, Mheshimiwa Rais tutatoa ajira nyingi na Kukuza uchumi wa taifa letu.
Ninakutakia afya njema na kila lililo jema.
Amani Msumari
Tanga
Cc: Dkt. Bashiru Ally Kakurwa
Katibu Mkuu - CCM
Awali ya yote ninakupongeza kwa dhati kabisa kwa kuchaguliwa kwako kwa kishindo kuingoza tena Tanzania kwa miaka mingine mitano. Ushindi huo sio bahati mbaya. Watanzania wameridhishwa na uongozi wako unaoacha alama.
Ndugu Rais, ninaomba niende moja kwa moja kwenye hoja yangu. Serikali hii utakayoiongoza kwa kipindi hiki cha miaka mitano itakuwa ni serikali yenye deni kubwa sana kwa watanzania. Kipindi cha kampeni uliomba watanzania wakuletee madiwani na wabunge wa CCM, nao wamekusikia
Ninaamini spika wa bunge atatoka CCM hivyo ninaomba akapatikane mtu ambaye atashirikiana vizuri na serikali katika kuendesha bunge ili kuhakikisha watanzania wanapata neema zaidi. Ikiwapendeza, Job Yustino Ndugai bado anafaa
Naomba pia uelekeze (Kama mwenyekiti wa CCM taifa) pati kokasi kuhakikisha inalishawishi bunge kupitia sheria mbalimbali zinazolalamikiwa ili zilete tija zaidi kwa watanzania. Mfano mmoja wapo ni sheria ya mafao ya wastaafu pamoja na fao la kujitoa kwa watumishi wa kazi za muda mfupi
Kasi yako kwenye maendeleo imeonekana kuanzia usambazaji wa umeme vijijini, maji, huduma za afya na elimu, kilimo, barabara na nidhanu serikalini. Umekuwa sauti ya wale wasio na sauti na kuwawezesha kuwa na sauti.
Pamoja na hayo, wapo baadhi ya viongozi ambao hawawajibiki ipasavyo, unakuta ni mpaka ufike wewe mwenyewe ndio unakuta viongozi wanawajibika.
Mheshimiwa Rais naomba sana hili ukaliangalie ili wateule wako wachape kazi zaidi na kutatua kero za wananchi na wewe ukifika usikutane na shida ndogondogo.
Naomba ikikupendeza, waelekeze wateule wako wahangaike usiku na mchana kubuni miradi, kupanua wigo wa vipato vya halmashauri, kudhibiti rushwa na kuhakikisha wanasimamia sera za serikali ili vijana waweze kujiajiri.
Kilimo, ufugaji na ujasiriamali vikipewa msukumo mkubwa zaidi katika ngazi za wilaya na halmashauri, Mheshimiwa Rais tutatoa ajira nyingi na Kukuza uchumi wa taifa letu.
Ninakutakia afya njema na kila lililo jema.
Amani Msumari
Tanga
Cc: Dkt. Bashiru Ally Kakurwa
Katibu Mkuu - CCM