Ujumbe kwa viongozi wa chadema na sakata la shibuda

CHUAKACHARA

JF-Expert Member
Jun 3, 2011
12,358
6,422
Tafadhali nawaomba viongozi wa Chadema hekima ya hali ya juu itumike kulimaliza tatizo la Shibuda. Nawaomba msikurupuke. Najua alifanya makosa kwenda na msimamo wa chama, lakini kwa vile Chadema ni kioo cha jamii kwa sasa kisiasa, tafadhali mpe muda ajirekebishe. Ajue kuwa yupo mahali ambapo ni tofauti na CCM. Itawajengea heshima kubwa sana kuliko kumfukuza.
Mimi si mwnachama wa Chadema, lakini nina matumaini makubwa sana na Chadema kuhusu mustakabali wa taifa hili.
 
Tafadhali nawaomba viongozi wa Chadema hekima ya hali ya juu itumike kulimaliza tatizo la Shibuda. Nawaomba msikurupuke. Najua alifanya makosa kwenda na msimamo wa chama, lakini kwa vile Chadema ni kioo cha jamii kwa sasa kisiasa, tafadhali mpe muda ajirekebishe. Ajue kuwa yupo mahali ambapo ni tofauti na CCM. Itawajengea heshima kubwa sana kuliko kumfukuza.
Mimi si mwnachama wa Chadema, lakini nina matumaini makubwa sana na Chadema kuhusu mustakabali wa taifa hili.
hayo mambo ya 'luvumiliana' watuw anapokiuka taratibu na sheria ndio yameifanya nchi hii leo kukumbatia wezi wa mali ya umma na wengine bado wapo kwenye nafasi za uongozi. Naamini kwua kama Chadema wanataka waaminike, wasijali cheo wala rangi ya mtu, kila anayefanya makosa aadhibiwe kwa mujibu wa kanuni, taratibu na sheria zilizopo. kama wakianza kuchekeana, huo utakuwa ni mwanzo mbaya sana
 
hayo mambo ya 'luvumiliana' watuw anapokiuka taratibu na sheria ndio yameifanya nchi hii leo kukumbatia wezi wa mali ya umma na wengine bado wapo kwenye nafasi za uongozi. Naamini kwua kama Chadema wanataka waaminike, wasijali cheo wala rangi ya mtu, kila anayefanya makosa aadhibiwe kwa mujibu wa kanuni, taratibu na sheria zilizopo. kama wakianza kuchekeana, huo utakuwa ni mwanzo mbaya sana

I believe, in some circumstances, one has to sacrifice some interests to achieve certain goals-CHADEMA, play altruism!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! particularly to this guy Shibuda. I am trying to imagine of the repercussion from your opponents particularly CCM and the society in general. Give him time to repent.
 
Mimi si mfuasi wa chama chochote kile kama wewe ulivyosema si mwanaCDM lakini Shibuda ni mamluki aliyepandikizwa purposely kwa mlaengo ya kuleta chuki, fitna, migogoro na masengenyo ndani ya chama ili hali isiwe shwari ndani ya CDM. Kiukweli CCM hiahofii chama chchote kile kuliko CDM hivyo Shibuda ni bora atoswe hiyo itakuwa onyo na karipio kwa watu wengine wowote ambao ni mamluki! Hivi mimi najiuliza kwenye Simba na Yanga mchezaji akionekana ni alikula mlungura ili ahujumu mechi hufukuzwa kwa fedheha na hata kutishiwa kuuwawa na mwanachama, sembuse kwenye siasa!
Shibuda afukuzwe kwa dhihaka na kejeli aliyoionyesha kwa chama chake.
 
Mie naunga mkono mtoa hoja kuwa Shibuda asifukuzwe ila apewe adhabu kulingana na taratibu ambazo cdm imejiwekea. Hiyo itakuwa fundisho kwake na wengine.
 
Kama ulivosema kuwa cdm ni kioo kwa sasa,basi huyu shibuda anawaharibia image ya chama.Hii sio mara ya kwanza,usisahau mchango wake wa kwanza ndani ya bunge jipya!Alivumiliwa.Ndani ya michango yake miwili ndani ya bunge amekisasambua chama mara zote mbili mfululizo!Pia nje ya bunge matendo yake yamekuwa ni ya kupingana na msimamo wa chama.kumbuka ile ishu ya mnuso na jk.Avumiliwe tu?Hafai huyu.
 
Shibuda afukuzwe, anazingua kwani kuwepo ndani ya chama ni mzigo. Anadamu ya kijani!
 
Wamtose tu hana issue. Bora wabaki wabunge wawili lakini wanaoamini katika chama. si mia wasiokiamini!
 
Mie naunga mkono mtoa hoja kuwa Shibuda asifukuzwe ila apewe adhabu kulingana na taratibu ambazo cdm imejiwekea. Hiyo itakuwa fundisho kwake na wengine.

Kufukuzwa au kutofukuzwa kwwake kutategemeana kwa kiasi kikubwa na taratibu zilizopo CDM. Hata akisamehewa ni lazima akabiliane na matokeo ya kosa lake. alifanya kosa na hivyo lazima akabiliane na matokeo ya makosa yake. Kumwachia hivi hivi ni kuongeza rejea zitakazotumiwa na mamluki wengine kama yeye waliotumwa kukimaliza CDM. Ikumbukwe kuwa siyo mara ya kwanza na kama kumuondoa ni maamuzi magumu, ni vema yakafanywa. wananchi wajifunze kuwa CDM si cha mchezo!
 
Mie naunga mkono mtoa hoja kuwa Shibuda asifukuzwe ila apewe adhabu kulingana na taratibu ambazo cdm imejiwekea. Hiyo itakuwa fundisho kwake na wengine.

Adhabu pekee inayomfaa Shibuda ni kufukuzwa kwa kuwa amewasaliti wenzake.
 
Poleni sana kwa wale wanaoumizwa kama mimi kuhusu suala la Shibuda. Nami pamoja na haya naona apewe tahadhari ya mwisho maana kama sikosei hili ni kosa lake kubwa la tatu. Kizuri ni kwamba asije akapewa dhamana yoyote kwani anaonekana hana nia kubwa nzuri na watanzania pamoja na hiki chama chetu. Lets give hm another chance.
 
Mimi namwomba amalizane na Viongozi huko kwenye ngazi ya kamati kuu. Akiletwa baraza kuu ambayo ni hatua inayofuata kazi anayo. Katika Baraza kuu wengi ni vijana tusio na msamaha na watu wa aina Shibuda.
 
Dawa ni maamuzi magumu tu...Kesha fanya upumbavu zaidi ya mara 3 why wanaendelea kumlea? Timua tu weka heshima hata kama jimbo wakilikosa poa tu. Asije tunga usaa bure.
 
Nakuunga mkono Antonov 225 lakini ktk mazingira tu iwapo katiba na kanuni za CDM zinataka hivyo, makosa ya Shibuda kiufundi yanakidhalilisha CDM anatakiwa ajifunze kuwa tunaposema CDM ajue tofauti iliyopo baina yake na CCM, CDM imeonyesha umakini ktk mambo mengi na ya msingi kwa Mtz sasa yeye alizoea kule ambako anatangaza atagombea urais sababu rais ameshindwa kazi halafu muda wa uchaguzi anasema hatagombea bali atamuunga mkono JK sababu amefanya vizuri!!!!!!!!
 
Poleni sana kwa wale wanaoumizwa kama mimi kuhusu suala la Shibuda. Nami pamoja na haya naona apewe tahadhari ya mwisho maana kama sikosei hili ni kosa lake kubwa la tatu. Kizuri ni kwamba asije akapewa dhamana yoyote kwani anaonekana hana nia kubwa nzuri na watanzania pamoja na hiki chama chetu. Lets give hm another chance.

Thats true. Kimsingi kosa alilofanya Shibuda ni kubwa mno kuliacha hivi hivi. Kwa maoni yangu, adhabu ya chini kabisa anayoweza kupewa ni kupewa karipio kali na kutakiwa mbele ya vikao vitatu vya Mkutano wa Bunge unaoendelea na kwa uzito ule ule alioongea awali kukana suala la posho na kuomba wananchi msamaha kwa kauli yake ambayo imekwaza wengi na pia kutorudia kosa lolote la kwenda kinyume na sera au maadili ya Chama. Vinginevyo, kama atashindwa kutimiza masharti haya, hana budi kufukuzwa.
 
Hata JK aliwashauri wale mafisadi waache ufisadi "tusijekulamiana" baadaye ilikuwa 2005 hadi leo hakuna kilichotendeka wameendelea na wizi mpaka tumekuwa mufilisi.
Alisema anawajua wauza unga na kwamba "waache" lakini hadi sasa wanapeta.
Tabia ya kulindana ni UCCM. Aende haraka sana.!!!! avuliwe uanachama. Tumekijenga chama chetu kwa damu yetu hadi leo, hakujakuwepo mtelemko popote!!!!!!!!!!!
 
Kwanza aende jimboni kwake aitishe mkutano wa hadhara awaombe msamaha wapiga kura wake,Pia aitishe Press Conference auelezee umma wa Watanzania wapenda maendeleo kuwa alikwenda kinyume na Katiba ya chama aombe msamaha and then kamati kuu wamsamehe kwa kumpa onyo kali.
 
hayo mambo ya 'luvumiliana' watuw anapokiuka taratibu na sheria ndio yameifanya nchi hii leo kukumbatia wezi wa mali ya umma na wengine bado wapo kwenye nafasi za uongozi. Naamini kwua kama Chadema wanataka waaminike, wasijali cheo wala rangi ya mtu, kila anayefanya makosa aadhibiwe kwa mujibu wa kanuni, taratibu na sheria zilizopo. kama wakianza kuchekeana, huo utakuwa ni mwanzo mbaya sana

Kwa ukomavu wake katika uwanja wa Siasa angeyafanya haya chipukizi kama Sugu au kama ambavyo mara kadhaa amekuwa akiteleza ndugu yangu Lema hili lingekuwa na Tija. Lakini si kwa mwansiasa Mkongwe kama Shibuda. Kanuni na taratibu za Chama zichukue mkondo wake.
 
Back
Top Bottom