Ujumbe kwa Tanesco: Mpango wa usambazaji umeme vijijini (REA) umekumbwa na ubadhirifu na rushwa

Freesoule

JF-Expert Member
Jun 18, 2013
269
272
TANESCO, kuna malalamiko sehemu mbalimbali za nchi kuhusiana na mpango wa usambazaji umeme vijijini (REA) ila sauti za wananchi zimekosa uwakilishi. Nitazungumzia yale niliyoyaona huko Rungwe, katika vijiji vya kata ya Kalalo.
Sehemu nyingi umeme waliunganishiwa watu wachache tu, tena wale wa barabarani, ili viongozi wakipita wafikiri wananchi wa eneo husika wamepata huduma ya umeme. Sijui kama kuna ukaguzi wa aina yoyote hufanyika, na kama upo basi wahusika huwa hawafanyi kazi inayoridhisha hata kwa nusu asilimia. Zaidi ya asilimia 99 ya kaya bado zilikuwa gizani pale mpango wa REA kwa eneo hilo ulipotangazwa 'kumalizika'. Wengi wa waliopata umeme baadaye wametumia gharama zao wenyewe, tena mara nyingi kwa kutoa rushwa kwa wafanyakazi wa TANESCO.
Pia, kuna sehemu wananchi walichangishwa fedha ili kuunganishiwa umeme (wakati umeme wa REA ni bure), na wengine walichangishwa fedha hadi Tsh 150 000 ili kusukiwa umeme kwenye nyumba zao, kinyume kabisa na utaratibu. Wajibu wa TANESCO/REA ni kuwafikishia umeme wateja, usukaji wa umeme ndani ya nyumba si jukumu lao, ni jukumu la mteja husika. Lakini wafanyakazi wasio waadilifu wa TANESCO/REA walitumia mwanya wa uelewa mdogo wa wananchi kuwachangisha fedha za kuwasukia umeme, kinyume na utaratibu. Wakipokea pesa wanakufungia 'distribution box' (almaarufu 'main switch' kama ijulikanavyo kwa wengi wetu), soketi moja ya taa sebuleni na pengine soketi ya ukutani. Wale waliosuka umeme kwa gharama zao walitozwa faini na watu wa TANESCO/REA wakishirikiana na wenyeviti wa vijiji na mitaa. Fedha zote hizi hazikutolewa risiti, kwa hiyo hazikuingia kwenye mfuko wowote wa umma. Fedha za watu masikini, ambapo kwa umasikini wao wafadhili waliamua kuwafadhili kwa umeme wa bure kupitia mradi wa REA, zilitafunwa na wajanja bila huruma. Hata hivyo waliishia kutokupata umeme.
Haya yote yametokea katika vijiji vya kata ya Kalalo wilayani Rungwe. Wananchi wamepitia madhila yote hayo na bado hawajapata umeme huu mwaka wa pili. Wakidai kuwekewa umeme huambiwa 'phase ya REA' ilishapita. Kwa maana hiyo, wakitaka kupata umeme itabidi watumie gharama zao wenyewe.
Ni muhimu sana kwa TANESCO kufuatilia ufanisi wa mpango wa REA kwa nchi nzima, kufanya ukaguzi makini na siyo kuwatuma watu wanaochoma petroli kwenye 'malendi kruza ya mkonga' na kusema kila kitu kiko sawa. Wafanyakazi wengi wa TANESO na mawakala wa REA wasio waadilifu wamehusika kwa kiasi kikubwa kuuvuruga mradi wa REA kwa ubadhirifu na rushwa.
 
TANESCO, kuna malalamiko sehemu mbalimbali za nchi kuhusiana na mpango wa usambazaji umeme vijijini (REA) ila sauti za wananchi zimekosa uwakilishi. Nitazungumzia yale niliyoyaona huko Rungwe, katika vijiji vya kata ya Kalalo.
Sehemu nyingi umeme waliunganishiwa watu wachache tu, tena wale wa barabarani, ili viongozi wakipita wafikiri wananchi wa eneo husika wamepata huduma ya umeme. Sijui kama kuna ukaguzi wa aina yoyote hufanyika, na kama upo basi wahusika huwa hawafanyi kazi inayoridhisha hata kwa nusu asilimia. Zaidi ya asilimia 99 ya kaya bado zilikuwa gizani pale mpango wa REA kwa eneo hilo ulipotangazwa 'kumalizika'. Wengi wa waliopata umeme baadaye wametumia gharama zao wenyewe, tena mara nyingi kwa kutoa rushwa kwa wafanyakazi wa TANESCO.
Pia, kuna sehemu wananchi walichangishwa fedha ili kuunganishiwa umeme, na wengine walichangishwa fedha hadi Tsh 150 000 ili kusukiwa umeme kwenye nyumba zao, kinyume kabisa na utaratibu. Wale waliosuka umeme kwa gharama zao walitozwa faini na watu wa TANESCO waliohusika na REA wakishirikiana na wenyeviti wa vijiji na mitaa. Hata hivyo waliishia kutokupata umeme.
Haya yote yametokea katika vijiji vya kata ya Kalalo wilayani Rungwe. Wananchi wamepitia madhila yote hayo na bado hawajapata umeme huu mwaka wa pili. Wakidai kuwekewa umeme huambiwa 'phase ya REA' ilishapita. Kwa maana hiyo, wakitaka kupata umeme itabidi watumie gharama zao wenyewe.
Ni muhimu sana kwa TANESCO kufuatilia ufanisi wa mpango wa REA kwa nchi nzima, kufanya ukaguzi makini na siyo kuwatuma watu wanaochoma petroli kwenye 'malendi kruza ya mkonga' na kusema kila kitu kiko sawa. Wafanyakazi wengi wa TANESO na mawakala wa REA wasio waadilifu wamehusika kwa kiasi kikubwa kuuvuruga mradi wa REA kwa ubadhirifu na rushwa.
Duuh
 
Hiyo kusuka ndio wiring?.Hizo gharama ni za mteja sio tanesco kama umefanya wiring mwenyewe lazima mhandisi binafsi aje akague nyumba yako na no lazima umlipe.
 
Hiyo kusuka ndio wiring?.Hizo gharama ni za mteja sio tanesco kama umefanya wiring mwenyewe lazima mhandisi binafsi aje akague nyumba yako na no lazima umlipe.
Ndio Kiswahili chake hicho. Najua utaratibu ila wahusika waliamua kuupindua ili wajikusanyie pesa
 
TANESCO, kuna malalamiko sehemu mbalimbali za nchi kuhusiana na mpango wa usambazaji umeme vijijini (REA) ila sauti za wananchi zimekosa uwakilishi. Nitazungumzia yale niliyoyaona huko Rungwe, katika vijiji vya kata ya Kalalo.
Sehemu nyingi umeme waliunganishiwa watu wachache tu, tena wale wa barabarani, ili viongozi wakipita wafikiri wananchi wa eneo husika wamepata huduma ya umeme. Sijui kama kuna ukaguzi wa aina yoyote hufanyika, na kama upo basi wahusika huwa hawafanyi kazi inayoridhisha hata kwa nusu asilimia. Zaidi ya asilimia 99 ya kaya bado zilikuwa gizani pale mpango wa REA kwa eneo hilo ulipotangazwa 'kumalizika'. Wengi wa waliopata umeme baadaye wametumia gharama zao wenyewe, tena mara nyingi kwa kutoa rushwa kwa wafanyakazi wa TANESCO.
Pia, kuna sehemu wananchi walichangishwa fedha ili kuunganishiwa umeme, na wengine walichangishwa fedha hadi Tsh 150 000 ili kusukiwa umeme kwenye nyumba zao, kinyume kabisa na utaratibu. Wale waliosuka umeme kwa gharama zao walitozwa faini na watu wa TANESCO waliohusika na REA wakishirikiana na wenyeviti wa vijiji na mitaa. Hata hivyo waliishia kutokupata umeme.
Haya yote yametokea katika vijiji vya kata ya Kalalo wilayani Rungwe. Wananchi wamepitia madhila yote hayo na bado hawajapata umeme huu mwaka wa pili. Wakidai kuwekewa umeme huambiwa 'phase ya REA' ilishapita. Kwa maana hiyo, wakitaka kupata umeme itabidi watumie gharama zao wenyewe.
Ni muhimu sana kwa TANESCO kufuatilia ufanisi wa mpango wa REA kwa nchi nzima, kufanya ukaguzi makini na siyo kuwatuma watu wanaochoma petroli kwenye 'malendi kruza ya mkonga' na kusema kila kitu kiko sawa. Wafanyakazi wengi wa TANESO na mawakala wa REA wasio waadilifu wamehusika kwa kiasi kikubwa kuuvuruga mradi wa REA kwa ubadhirifu na rushwa.
Ni mara chache kusikia hili shirika likisifiwa, kwenye ajira ndiyo kabisaaaa wanaajiri kiundungu matokeo yake wanakwamisha utendaji wa shirika. Mfano Tabora Mjini kitengo cha stoo panalalamikiwa mno kuwa wameajiri watu ambao hawajasomea mambo ya stoo na kuacha wale wenye sifa na vigezo vya kazi hiyo. Jicho la nne litupiwe hapo Tabora.
 
Hii rushwa jamani itaisha lini mbona watu wanakuwa wagumu hivi, dini zinapiga vita rushwa, raisi anapiga vita rushwa ila wenye dhamana wachache wanaichafua serikali. Sidhani kama mleta uzi ametunga hili tuhuma naimani yanatokea sehemu nyingi tu hapa nchini ila inatakiwa wapatikane wachache watiwe nguvuni ili iwe fundisho kwa wengine.
 
TANESCO, kuna malalamiko sehemu mbalimbali za nchi kuhusiana na mpango wa usambazaji umeme vijijini (REA) ila sauti za wananchi zimekosa uwakilishi. Nitazungumzia yale niliyoyaona huko Rungwe, katika vijiji vya kata ya Kalalo.
Sehemu nyingi umeme waliunganishiwa watu wachache tu, tena wale wa barabarani, ili viongozi wakipita wafikiri wananchi wa eneo husika wamepata huduma ya umeme. Sijui kama kuna ukaguzi wa aina yoyote hufanyika, na kama upo basi wahusika huwa hawafanyi kazi inayoridhisha hata kwa nusu asilimia. Zaidi ya asilimia 99 ya kaya bado zilikuwa gizani pale mpango wa REA kwa eneo hilo ulipotangazwa 'kumalizika'. Wengi wa waliopata umeme baadaye wametumia gharama zao wenyewe, tena mara nyingi kwa kutoa rushwa kwa wafanyakazi wa TANESCO.
Pia, kuna sehemu wananchi walichangishwa fedha ili kuunganishiwa umeme, na wengine walichangishwa fedha hadi Tsh 150 000 ili kusukiwa umeme kwenye nyumba zao, kinyume kabisa na utaratibu. Wale waliosuka umeme kwa gharama zao walitozwa faini na watu wa TANESCO waliohusika na REA wakishirikiana na wenyeviti wa vijiji na mitaa. Hata hivyo waliishia kutokupata umeme.
Haya yote yametokea katika vijiji vya kata ya Kalalo wilayani Rungwe. Wananchi wamepitia madhila yote hayo na bado hawajapata umeme huu mwaka wa pili. Wakidai kuwekewa umeme huambiwa 'phase ya REA' ilishapita. Kwa maana hiyo, wakitaka kupata umeme itabidi watumie gharama zao wenyewe.
Ni muhimu sana kwa TANESCO kufuatilia ufanisi wa mpango wa REA kwa nchi nzima, kufanya ukaguzi makini na siyo kuwatuma watu wanaochoma petroli kwenye 'malendi kruza ya mkonga' na kusema kila kitu kiko sawa. Wafanyakazi wengi wa TANESO na mawakala wa REA wasio waadilifu wamehusika kwa kiasi kikubwa kuuvuruga mradi wa REA kwa ubadhirifu na rushwa.
Huo mradi hapo rungwe ulikuwa unatekelezwa na kampuni gani? Maana kila mkoa umekasimia mamlaka na REA kutekeleza miradi,taja hiyo kampuni tafadhali
 
REA Kuna Rushwa ya kutisha ukienda Kibaha vijijini kuna vijijini kupita Boko mnemera kuna kijiji kinaitwa Kibaoni mpaka leo umeme hakuna na wamechangishwa hela ni zaidi ya miaka 3
 
TANESCO, kuna malalamiko sehemu mbalimbali za nchi kuhusiana na mpango wa usambazaji umeme vijijini (REA) ila sauti za wananchi zimekosa uwakilishi. Nitazungumzia yale niliyoyaona huko Rungwe, katika vijiji vya kata ya Kalalo.
Sehemu nyingi umeme waliunganishiwa watu wachache tu, tena wale wa barabarani, ili viongozi wakipita wafikiri wananchi wa eneo husika wamepata huduma ya umeme. Sijui kama kuna ukaguzi wa aina yoyote hufanyika, na kama upo basi wahusika huwa hawafanyi kazi inayoridhisha hata kwa nusu asilimia. Zaidi ya asilimia 99 ya kaya bado zilikuwa gizani pale mpango wa REA kwa eneo hilo ulipotangazwa 'kumalizika'. Wengi wa waliopata umeme baadaye wametumia gharama zao wenyewe, tena mara nyingi kwa kutoa rushwa kwa wafanyakazi wa TANESCO.
Pia, kuna sehemu wananchi walichangishwa fedha ili kuunganishiwa umeme, na wengine walichangishwa fedha hadi Tsh 150 000 ili kusukiwa umeme kwenye nyumba zao, kinyume kabisa na utaratibu. Wale waliosuka umeme kwa gharama zao walitozwa faini na watu wa TANESCO waliohusika na REA wakishirikiana na wenyeviti wa vijiji na mitaa. Hata hivyo waliishia kutokupata umeme.
Haya yote yametokea katika vijiji vya kata ya Kalalo wilayani Rungwe. Wananchi wamepitia madhila yote hayo na bado hawajapata umeme huu mwaka wa pili. Wakidai kuwekewa umeme huambiwa 'phase ya REA' ilishapita. Kwa maana hiyo, wakitaka kupata umeme itabidi watumie gharama zao wenyewe.
Ni muhimu sana kwa TANESCO kufuatilia ufanisi wa mpango wa REA kwa nchi nzima, kufanya ukaguzi makini na siyo kuwatuma watu wanaochoma petroli kwenye 'malendi kruza ya mkonga' na kusema kila kitu kiko sawa. Wafanyakazi wengi wa TANESO na mawakala wa REA wasio waadilifu wamehusika kwa kiasi kikubwa kuuvuruga mradi wa REA kwa ubadhirifu na rushwa.
Naunga hoja mkono 100%, huku losokonoi, karibu na landanai, wilaya ya Simanjiro, nkoa was manyara, umeme was REA, umepekekwa zaidi ya km 10, kufuata shule ya msingi moja,dispensary moja na nyumba mbili za walimu, Kwa mantiki hiyo zaidi ya kaya 300 hazikupelekewa huko umeme. Cha kushangaza zaidi shule na dispensary iliyopelekewa umeme inatoa huduma Kwa hizo kaya 300. Shule inayopelekewa umeme had I Kwa wanakijiji wanakoishi ni kms 7, ila watoto wanatoka kms 7 kuja kusoma shule ya msingi losokonoi.Kwa maana hiyo wnafunzi watalala gizani asubuhi wanakuja shule kufundishwa watakuta umeme shuleni ila utakuwa umezimwa Kwa sababuni mchana.
Umeme umepitishwa barabara kuu ya landanai kuelekea orkesmet ili viongozi wauone ila sio Kwa faida ya wananchi.
Pili eneo hili tanesco haikupata rushwa hats sent tank wakaamua kuchora ramani ya hovyo ya kupeleka umeme eneo lisilo na wanachi Kwa gharama kubwa na mradi huu,hautawanufaisha wananchi hats mmoja.
REA ni shida kubwa.
 
Binafsi nimekuwa mhanga wa kufuatilia huu umeme wa REA lakini mwisho nimeamini hii REA si ya Watanzania wote haswa waishio vijijini km sera inavyosema, ukweli na hili Mh Rais inabidi aingilie kati, vijiji vingi sana na vitongoji vyake havina umeme wala havina dalili za kupata umeme na uenda visipate umeme km watanzania wanavyo aminishwa. Mfn unakuta kijiji umeme unawekwa tu kwenye maeneo km shule, zahanati, au sehemu wanakotoka watu wenye majina makubwa tu, raia walio wengi wanabaki bila kupata umeme, Mh Waziri, hebu wafuatilieni kwa umakini wakandarasi au km ndivyo makubaliano yalivyo serikali na wakandarasi, waelezeni Watanzania ukweli kuwa REA si kwa ajili ya vijiji na vitongoji vyote. Naomba yeyote atakaye kuwa na namba ya sim ya mkononi ya Mh Waziri au Mh naibu Waziri wa Nishati anisaidie ili nijaribu kuwaeleza ukweli wa baadhi ya mambo labda sisi wanyonge twaweza kusaidika.
 
Binafsi nimekuwa mhanga wa kufuatilia huu umeme wa REA lakini mwisho nimeamini hii REA si ya Watanzania wote haswa waishio vijijini km sera inavyosema, ukweli na hili Mh Rais inabidi aingilie kati, vijiji vingi sana na vitongoji vyake havina umeme wala havina dalili za kupata umeme na uenda visipate umeme km watanzania wanavyo aminishwa. Mfn unakuta kijiji umeme unawekwa tu kwenye maeneo km shule, zahanati, au sehemu wanakotoka watu wenye majina makubwa tu, raia walio wengi wanabaki bila kupata umeme, Mh Waziri, hebu wafuatilieni kwa umakini wakandarasi au km ndivyo makubaliano yalivyo serikali na wakandarasi, waelezeni Watanzania ukweli kuwa REA si kwa ajili ya vijiji na vitongoji vyote. Naomba yeyote atakaye kuwa na namba ya sim ya mkononi ya Mh Waziri au Mh naibu Waziri wa Nishati anisaidie ili nijaribu kuwaeleza ukweli wa baadhi ya mambo labda sisi wanyonge twaweza kusaidika.
Ndugu mpendwa mteja wetu tunaomba utusaidie taarifa za kijiji husika na namba yako ya rmtaarifa tuangalie kipo kwenye awamu ipi ya utekelezaji wa miradi yetu
 
REA Kuna Rushwa ya kutisha ukienda Kibaha vijijini kuna vijijini kupita Boko mnemera kuna kijiji kinaitwa Kibaoni mpaka leo umeme hakuna na wamechangishwa hela ni zaidi ya miaka 3
Kinachoshangaza unakuta watendaji wa wizara fulani wanafanya vitendo vya rushwa halafu wizara husika wanakuwa kama hawaoni wanataka mpaka raisi aseme au akemee. Mimi huwa najiuliza ni kweli hawa viongozi huwa hawafahamu hivi vitendo au kuviona au hata kuambiwa mpaka kufikia wananchi kulalamika?

Ni vyema wasipuunze malalamiko ya wananchi kuhusiana na rushwa ya aina yeyote ile sababu itawakatisha tamaa wale wachache wasiopenda rushwa nao wataingia kwenye mkumbo huo kisha watakuwa hatari zaidi punde wakishaonja.
 
Kinachoshangaza unakuta watendaji wa wizara fulani wanafanya vitendo vya rushwa halafu wizara husika wanakuwa kama hawaoni wanataka mpaka raisi aseme au akemee. Mimi huwa najiuliza ni kweli hawa viongozi huwa hawafahamu hivi vitendo au kuviona au hata kuambiwa mpaka kufikia wananchi kulalamika?

Ni vyema wasipuunze malalamiko ya wananchi kuhusiana na rushwa ya aina yeyote ile sababu itawakatisha tamaa wale wachache wasiopenda rushwa nao wataingia kwenye mkumbo huo kisha watakuwa hatari zaidi punde wakishaonja.
Wanafahamu Sana Tatizo hata ajira na miradi wanapeana wao ndio maana ni ngumu kuwajibashana kunapotokea matatizo
Rushwa bado ni mbichi sana
 
Ndugu mpendwa mteja wetu tunaomba utusaidie taarifa za kijiji husika na namba yako ya rmtaarifa tuangalie kipo kwenye awamu ipi ya utekelezaji wa miradi yetu
Tangia mwaka juzi nimekuwa nikiwaomba msaada juu ya hili, mmekuwa mkinipa majibu mbalimbali lakini zaidi nimekata tamaa japo sijachoka, sasa naeleza tena. Mkoa wa Kagera, Wilaya ya Missenyi, Kata ya Kassambya, Kijiji Mabuye na Kitongoji cha KIJUKA. Kitongoji cha KIJUKA ni miongoni mwa vitongoji vinne vya kijiji Mabuye, tulijitahidi sana kufuatilia juu ya Kitongoji cha KIJUKA kupatiwa umeme wa REA lakini majibu tuliyoyapata yanakatisha tamaa, hatimaye ikaonekana kuwa vitongoji vitakavyopata umeme KIJUKA (haijulikani kama itapata au la!) japo kina sifa zote za kupatiwa umeme. Mwaka jana Mh Waziri Mkuu alikuwa na ziara huko Missenyi, kabla ya ziara hiyo REA waliweza kusambaza nguzo kwa baadhi ya maeneo machache vitongoji vya RUHAMA na MABUYE ndani ya Kijiji cha MABUYE lakini hadi leo hakuna kinacho endelea baada ya Mh Waziri Mkuu kuondoka maeneo hayo. Kwa vitongoji ambavyo nguzo ziliwekwa walau hao wana matumaini, lakini kwenye Kitongoji cha KIJUKA hamna matumaini wala taarifa juu ya ni lini umeme utawekwa au la! Kinacho sikitisha wananchi wa eneo hili la KIJUKA wana utayari mkubwa wa kuupokea umeme wa REA japo nuru inazidi kufifia kila uchao.Mbaya zaidi hata viongozi hawatoi ushirikiano kwa wananchi. Aidha katika vitongoji vya ITALA, RUHAMA na MABUYE hamna shida sana maana tayari kuna jitihada za kupatiwa umeme japo bado( nawapongeza kwa hili) lakini kwenye kitongoji cha KIJUKA ndipo hatuelewi kama tunapata umeme au hatupati na kama tunapata ni lini? Namba ya sim nimeshawapa mara kibao lakini nawapatia tena sitachoka maana umeme tunauhitaji sana. 0684542853
 
Tangia mwaka juzi nimekuwa nikiwaomba msaada juu ya hili, mmekuwa mkinipa majibu mbalimbali lakini zaidi nimekata tamaa japo sijachoka, sasa naeleza tena. Mkoa wa Kagera, Wilaya ya Missenyi, Kata ya Kassambya, Kijiji Mabuye na Kitongoji cha KIJUKA. Kitongoji cha KIJUKA ni miongoni mwa vitongoji vinne vya kijiji Mabuye, tulijitahidi sana kufuatilia juu ya Kitongoji cha KIJUKA kupatiwa umeme wa REA lakini majibu tuliyoyapata yanakatisha tamaa, hatimaye ikaonekana kuwa vitongoji vitakavyopata umeme KIJUKA (haijulikani kama itapata au la!) japo kina sifa zote za kupatiwa umeme. Mwaka jana Mh Waziri Mkuu alikuwa na ziara huko Missenyi, kabla ya ziara hiyo REA waliweza kusambaza nguzo kwa baadhi ya maeneo machache vitongoji vya RUHAMA na MABUYE ndani ya Kijiji cha MABUYE lakini hadi leo hakuna kinacho endelea baada ya Mh Waziri Mkuu kuondoka maeneo hayo. Kwa vitongoji ambavyo nguzo ziliwekwa walau hao wana matumaini, lakini kwenye Kitongoji cha KIJUKA hamna matumaini wala taarifa juu ya ni lini umeme utawekwa au la! Kinacho sikitisha wananchi wa eneo hili la KIJUKA wana utayari mkubwa wa kuupokea umeme wa REA japo nuru inazidi kufifia kila uchao.Mbaya zaidi hata viongozi hawatoi ushirikiano kwa wananchi. Namba ya sim nimeshawapa mara kibao lakini nawapatia tena sitachoka maana umeme tunauhitaji sana. 0684542853
Tunafatilia swala hili na kukupa ufafanuzi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom