Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,894
Muheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa inayoitwa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania.
Muheshimiwa, wakati unafungua bunge kule Dodoma ,tarehe 30/12/2005,ulisema kwamba Zanzibar kuna mpasuko wa kisiasa katia ya Pemba na Unguja,na ukaahidi kuushughulikia. Japo kauli yako hii haikukidhi ukweli halisi wako waliokupa imani na kuwa na subra.Wakisubiri kile ulichokianzisha na kukiiita mazungumzo ya kutafuta suluhu la kudumu la huo ufa. Lakini kama kawaida ya CCM ilikua ni ule ule usanii wenu wa kupoteza muda kusubiri uchaguzi mwengine.
Katika kikao cha Halimashauri kuu ya CCM huko Butiama, wajumbe kutoka ZNZ walisamama na kutoa maneno ya kashafa dhidi ya Wapemba na kila alie CUF na kusema wazi hawako tayari kushirikiana nao, na wakafika hata kudai ASP yao ili wakawacharange mapanga, Wapemba, Waarabu na maCUF.
Muheshimiwa baada ya kikao hicho tulikusikia pale Diamond Jublee ukisema walichokifanya CCM wenzako hao ni kutumia haki yao ya KIDEMOKRASIA KUJIELEZA.
Wewe mwenyewe ,ulikua miongoni ya wabunge 55 (G55) kutoka Tanganyika mliopeleka hoja bungeni kudai serikali ya Tanganyika. Wachaga walishawahi kudai Ndani ya UN, kupitia aliekua chifu wao Marehemu chifu Mareale, kwamba wapewe serikali yao. Hata hivi karibuni, Kigoma wameshawahi kudai kujitenga kama hawatapewa haki zao za kiraia.
Hakuna hata mmoja katika hao hapo juu alidaswa au kuulizwa na kuambiwa kwamba ni haini. Tunavyojua vyama vilivyokuwepo Tanganyika na ZNZ kabla ya 1964 au mpaka 1977 vimepigwa marufuku katika sheria ya vyama vingi ya mwaka 1992. Sasa hawa wanaodai ASP mbona wao hawaitwi mahaini?
Wapemba wananyimwa haki zao za msingi kama Wazanzibari, hayo yanafanywa na serikali zote mbili za CCM, chama ambacho wewe ni mwenyekiti, na wewe ndie rais waserikali kuu yaani hiyo ya Muungano. Kwa lugha fupi maovu wanayofanyiwa Wapemba wewe unayasimamia.
Sasa , katika hali kama hiyo, Wapemba kwa sababu kama destri ya wazanzibari ni watu waungwana na wastaarabu, wametumia njia ya kistaarabu kupeleka malalamiko na mawazo yao katika UN, ambayo Tanzania ni mwanachama na imesaini maazimio yote muhimu, au matangazo yote muhimu ya UN. Tena wamekwenda wazi wazi bila kujificha.
Muheshimiwa , hao wazee 12 ni wawakilishi tuu ya Wananchi wa Pemba, na katika waraka wao kuna sahihi za Wapemba 10,000, hawa pia ni kama wawakilishi ya wananchi wote wa Pemba.
Cha ajabu, kwa sababu tuu wao ni Wapemba , na kwasababu wameikataa CCM, ulikua kama walivyomumiani wa KiCCM kila anaekaaa lazima anyonye damu ya Wapemba, umeamua kuonyesha makucha yako, umetuma makomandoo, majeshi ya kitanganyika , usiku wa manane na masilaha makubwa, kwenda kuwakamata na kuwadhalilisha wazee wetu, wazee wasio kuwa na hata na kisu cha ukindu, iweje watekwe nyara usiku wa manane na makomandoo 40.
Sasa mmewachukua, mmewapeleka kusikojulikana, hakuna anaejua wapi wapo, lengo ni kuwadhalilisha kwa sababu tuu ni Wapemba.
Kama ni mahaini kama mnavyosema, kwanini wasiwe mikononi mwa polisi, kwa nini sasa ni wiki, hamjawafikisha mahakamani ,na kuwapa haki zao zote za msingi kama binaadam mwengine. Kwanini wawe katika mikono ya majeshi katika makambi yao, kwa sheria gani mnayoitumia?
Muheshimiwa jaaliwa ingekua ni wazee wako wewe wanaofanyiwa haya ungejisikia vipi, au kwasababu wao ni Wapemba walioikataa CCM? Juzijuzi tuliona mama Kikwete na baadae Serikali ilivyoingilia kati harakaharaka sakata la mahujaji, baada ya ndege yao kuchelewa kuondoka Dar. Kwa nini? Kwa sababu ya uchungu wa wazee.
Tunachokueleza muheshimiwa Kikwete ni kwamba mnachokifanya ni kuwadhalilisha na kuwatesa wazee wetu pasi na kosa lolote, mnawatesa kiakili wao na familia zao na Wapemba wenzao na wapenda haki na amani wote, kwa sababu wao hawajui wako wapi na familia zao ziko vipi, na familia zao hazijui wako wapi na wako vipi.
Kwa sababu sasa matunda ya uovu mlioupanda kwa miaka 40 unaaza kutoa matunda, mnajaribu kupoteza malengo kwa kuwakama na kuwadhalilisha wazee wetu.
Nadhani huzijui hasira na ghadhabu zetu, muheshimiwa hii sio 1964 kama mliwakama wazee na ndugu za watu na jamaa zao wakakaa kimya na watu hao kupotea. Hii ni 2008. Ujue kwamba dhamana ya wazee wetu hao iko mikononi mwako, na wewe ndie tunaekujua, madhara yoyote yatakayo wapata kwa kitendo mnachokifanya sisi tunakujua wewe. Maradhi yoyote yatakayowapata sasa au baadae kwasabau ya udhalilisho mnaowafanyia jukumu liko juu yako wewe.
Tafadhali waachie wazee wetu warudi wakakae na familia zao,na kujishughulikia na maradhi tofauti yanayowasumbua.
Msimamo ni ule ule kama mmeshindwa kuwatendea haki Wapemba katika nchi yao, basi muwe ni wenye kukubali mawazo yao kama nyinyi mlivyo na haki ya kutoa mawazo yenu.
Madai hayo ni ya Wapemba wote, wala kuwakamata na kuwadhalilisha wazee wetu hao haitobadilisha msimamo wetu, tunachodai ni haki yetu. Mapambano yanaendela. Kama nyinyi hamko tayari kutupa haki zetu iweje kukerwe na sisi kutaka chetu.
Tafadhali warudisheni wazee wetu katika familia zao, msikitie kidonda msumari wa moto, chumvi iliyotiwa inatosha. Tafadhalini Tafadhalini.
Muheshimiwa, wakati unafungua bunge kule Dodoma ,tarehe 30/12/2005,ulisema kwamba Zanzibar kuna mpasuko wa kisiasa katia ya Pemba na Unguja,na ukaahidi kuushughulikia. Japo kauli yako hii haikukidhi ukweli halisi wako waliokupa imani na kuwa na subra.Wakisubiri kile ulichokianzisha na kukiiita mazungumzo ya kutafuta suluhu la kudumu la huo ufa. Lakini kama kawaida ya CCM ilikua ni ule ule usanii wenu wa kupoteza muda kusubiri uchaguzi mwengine.
Katika kikao cha Halimashauri kuu ya CCM huko Butiama, wajumbe kutoka ZNZ walisamama na kutoa maneno ya kashafa dhidi ya Wapemba na kila alie CUF na kusema wazi hawako tayari kushirikiana nao, na wakafika hata kudai ASP yao ili wakawacharange mapanga, Wapemba, Waarabu na maCUF.
Muheshimiwa baada ya kikao hicho tulikusikia pale Diamond Jublee ukisema walichokifanya CCM wenzako hao ni kutumia haki yao ya KIDEMOKRASIA KUJIELEZA.
Wewe mwenyewe ,ulikua miongoni ya wabunge 55 (G55) kutoka Tanganyika mliopeleka hoja bungeni kudai serikali ya Tanganyika. Wachaga walishawahi kudai Ndani ya UN, kupitia aliekua chifu wao Marehemu chifu Mareale, kwamba wapewe serikali yao. Hata hivi karibuni, Kigoma wameshawahi kudai kujitenga kama hawatapewa haki zao za kiraia.
Hakuna hata mmoja katika hao hapo juu alidaswa au kuulizwa na kuambiwa kwamba ni haini. Tunavyojua vyama vilivyokuwepo Tanganyika na ZNZ kabla ya 1964 au mpaka 1977 vimepigwa marufuku katika sheria ya vyama vingi ya mwaka 1992. Sasa hawa wanaodai ASP mbona wao hawaitwi mahaini?
Wapemba wananyimwa haki zao za msingi kama Wazanzibari, hayo yanafanywa na serikali zote mbili za CCM, chama ambacho wewe ni mwenyekiti, na wewe ndie rais waserikali kuu yaani hiyo ya Muungano. Kwa lugha fupi maovu wanayofanyiwa Wapemba wewe unayasimamia.
Sasa , katika hali kama hiyo, Wapemba kwa sababu kama destri ya wazanzibari ni watu waungwana na wastaarabu, wametumia njia ya kistaarabu kupeleka malalamiko na mawazo yao katika UN, ambayo Tanzania ni mwanachama na imesaini maazimio yote muhimu, au matangazo yote muhimu ya UN. Tena wamekwenda wazi wazi bila kujificha.
Muheshimiwa , hao wazee 12 ni wawakilishi tuu ya Wananchi wa Pemba, na katika waraka wao kuna sahihi za Wapemba 10,000, hawa pia ni kama wawakilishi ya wananchi wote wa Pemba.
Cha ajabu, kwa sababu tuu wao ni Wapemba , na kwasababu wameikataa CCM, ulikua kama walivyomumiani wa KiCCM kila anaekaaa lazima anyonye damu ya Wapemba, umeamua kuonyesha makucha yako, umetuma makomandoo, majeshi ya kitanganyika , usiku wa manane na masilaha makubwa, kwenda kuwakamata na kuwadhalilisha wazee wetu, wazee wasio kuwa na hata na kisu cha ukindu, iweje watekwe nyara usiku wa manane na makomandoo 40.
Sasa mmewachukua, mmewapeleka kusikojulikana, hakuna anaejua wapi wapo, lengo ni kuwadhalilisha kwa sababu tuu ni Wapemba.
Kama ni mahaini kama mnavyosema, kwanini wasiwe mikononi mwa polisi, kwa nini sasa ni wiki, hamjawafikisha mahakamani ,na kuwapa haki zao zote za msingi kama binaadam mwengine. Kwanini wawe katika mikono ya majeshi katika makambi yao, kwa sheria gani mnayoitumia?
Muheshimiwa jaaliwa ingekua ni wazee wako wewe wanaofanyiwa haya ungejisikia vipi, au kwasababu wao ni Wapemba walioikataa CCM? Juzijuzi tuliona mama Kikwete na baadae Serikali ilivyoingilia kati harakaharaka sakata la mahujaji, baada ya ndege yao kuchelewa kuondoka Dar. Kwa nini? Kwa sababu ya uchungu wa wazee.
Tunachokueleza muheshimiwa Kikwete ni kwamba mnachokifanya ni kuwadhalilisha na kuwatesa wazee wetu pasi na kosa lolote, mnawatesa kiakili wao na familia zao na Wapemba wenzao na wapenda haki na amani wote, kwa sababu wao hawajui wako wapi na familia zao ziko vipi, na familia zao hazijui wako wapi na wako vipi.
Kwa sababu sasa matunda ya uovu mlioupanda kwa miaka 40 unaaza kutoa matunda, mnajaribu kupoteza malengo kwa kuwakama na kuwadhalilisha wazee wetu.
Nadhani huzijui hasira na ghadhabu zetu, muheshimiwa hii sio 1964 kama mliwakama wazee na ndugu za watu na jamaa zao wakakaa kimya na watu hao kupotea. Hii ni 2008. Ujue kwamba dhamana ya wazee wetu hao iko mikononi mwako, na wewe ndie tunaekujua, madhara yoyote yatakayo wapata kwa kitendo mnachokifanya sisi tunakujua wewe. Maradhi yoyote yatakayowapata sasa au baadae kwasabau ya udhalilisho mnaowafanyia jukumu liko juu yako wewe.
Tafadhali waachie wazee wetu warudi wakakae na familia zao,na kujishughulikia na maradhi tofauti yanayowasumbua.
Msimamo ni ule ule kama mmeshindwa kuwatendea haki Wapemba katika nchi yao, basi muwe ni wenye kukubali mawazo yao kama nyinyi mlivyo na haki ya kutoa mawazo yenu.
Madai hayo ni ya Wapemba wote, wala kuwakamata na kuwadhalilisha wazee wetu hao haitobadilisha msimamo wetu, tunachodai ni haki yetu. Mapambano yanaendela. Kama nyinyi hamko tayari kutupa haki zetu iweje kukerwe na sisi kutaka chetu.
Tafadhali warudisheni wazee wetu katika familia zao, msikitie kidonda msumari wa moto, chumvi iliyotiwa inatosha. Tafadhalini Tafadhalini.
Last edited by a moderator: