Ujumbe kwa mkuu wa chuo DIT na waziri wa Elimu Prof. Ndalichako

maroon7

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
11,144
15,144
Kwanza nichukue fursa hii kuipongeza serikali yetu chini ya Rais wetu Dr. John Pombe Magufuli ambae anapambana usiku na mchana kuhakikisha nchi inasonga kwa kasi usiku na mchana. Pili niwapongeze baadhi ya watendaji wake akiwemo waziri wa Elimu Prof Ndalichako kwa kuendana na kasi ya Rais wetu.

Ila pamoja na juhudi zao hizi bado kuna baadhi ya watendaji hawafanyi inavyotakikana kitu kinachoweza kutafsiriwa kama hujuma kwa juhudi za Rais wetu.

Mfano mdogo ni hiki kinachoendelea sasahivi cha walimu wa part time kusumbuliwa malipo yao kwa miezi 6 na hata mwaka mzima kuhangaikia malipo huku wakitakiwa kuwa wanaendelea kufundisha kishingo upande wakiwa na njaa na hata kukosa nauli wakati mwingine.

Hivi usawa huu nani anaweza kukaa miezi 6 au mwaka bila kulipwa na aka-survive? Maana hata hapa ninapoandika leo mwezi June walimu wa part time wanadai malipo yao ya January na kila siku hawatulii ni kufuatilia tu badala ya kufundisha.

Naamini hata Prof Ndomba mwenyewe hana ubavu huo wa kufanya kazi bila kulipwa huku akitakiwa aingie darasani kufundisha kwa miez 6.

Na hata akiingia kufundisha hatofundisha kwa moyo wala kwa kujituma..na hiki ndicho kinachotokea kwa walimu wa part time badala ya kufundisha muda mwingi wanalazimika kufuatilia malipo na hata wakati mwingine kukosa nauli ya kufika chuo kufundisha.

Wanaoathirika ni wanafunzi na huku ni kurudisha nyuma juhudi za serikali ya awamu ya 5 na mbaya zaidi hiki ni chuo cha serikali ambako uzembe huu hautakiwa kuwa unajirudiarudia.

Kwa ujumbe huu naomba mkuu wa chuo kwa usikivu wake afanye hima kuhakikisha tatizo hili linalozorotesha elimu yetu halifumbiwi macho maana wanafunzi wanalipa ada na wanastahili elimu bora sio bora elimu kama kinachotokea sasahivi walimu kukosa hata nauli za kwenda chuo.

Na mwisho nimuombe waziri wetu mchapakazi kuangalia kwa ukaribu na kusaidia utendaji wa taasisi hii muhimu ya elimu kwakuwa inajikita kutoa zaidi elimu ya sayansi na teknolojia hakutakiwi kuwe na ubabaishaji wa aina yoyote ambao utazorotesha utoaji wa elimu bora, maana inaonesha watendaji wake hawatambui umuhimu wa kuweka mbele maslahi ya wadau hivyo kufanya matatizo kuwa yanajirudiarudia.

Nawasilisha
 
Ni aibu sana authorities zipo,watu wanadai basic stahiki zao namna hii

Kwanza kama unaendesha taasisi yoyote au kampuni au serikali au chochote,halafu hulipi misharahara,ina maana huna akili ya kuendesha hiyo taasisi!
 
Hapo wa kubeba lawama ni serikali kupitia wizara ya Elimu ambayo inapaswa kupeleka fungu DIT
Ni aibu sana authorities zipo,watu wanadai basic stahiki zao namna hii

Kwanza kama unaendesha taasisi yoyote au kampuni au serikali au chochote,halafu hulipi misharahara,ina maana huna akili ya kuendesha hiyo taasisi!
 
Ni aibu sana authorities zipo,watu wanadai basic stahiki zao namna hii

Kwanza kama unaendesha taasisi yoyote au kampuni au serikali au chochote,halafu hulipi misharahara,ina maana huna akili ya kuendesha hiyo taasisi!
Halafu wanaoendesha hizi taasisi ni maprofesa kabisa lakini hata kuwaza namna gani inaathiri wanafunzi ,walimu na familia zao..hawajali mradi wao wanakula na kusaza
 
Hapo wa kubeba lawama ni serikali kupitia wizara ya Elimu ambayo inapaswa kupeleka fungu DIT
Mkuu

Basi ni serikali nzima ipo dysfunctional

Jamaa ka centralize the whole revenue streams kila kitu lazima kitoke kwake...

Kuna jamaa yangu anadai bilions MSD pale anavyoona watamrusha...

Na as we speak commercial banks zote TZ hazina dollar currency za kutosha!

Dysfucntional government..basi hizi zitakua ni trickle down effects ya cummulative bad decisions done by these "people"!
 
Halafu wanaoendesha hizi taasisi ni maprofesa kabisa lakini hata kuwaza namna gani inaathiri wanafunzi ,walimu na familia zao..hawajali mradi wao wanakula na kusaza
Ni kweli mkuu,ila awamu hii nayo inachangia

Hili tatizo la mishahara limezidi sana awamu hii....kuna bad decisions in the central govt....somewhere,somehow kuna watu hawatumii akili zao sawasawa
 
Hivi NACTE wanakazi gani, andikeni Magazetini, mitandaoni ili ujumbe ufike kwa wahusika
 
Hapo wa kubeba lawama ni serikali kupitia wizara ya Elimu ambayo inapaswa kupeleka fungu DIT
Mkuu ni uzembe wa mkuu wa chuo mbona vyuo vingine wanalipa vizuri tena kwa wakati na hata rate yao ni elfu 25 kwa saa sio kama DIT wanaolipa elfu 10 na bado hawalipi kwa wakati
 
Ni kweli mkuu,ila awamu hii nayo inachangia

Hili tatizo la mishahara limezidi sana awamu hii....kuna bad decisions in the central govt....somewhere,somehow kuna watu hawatumii akili zao sawasawa
Ni kweli ila kwanini vyuo vingine vilipe kwa wakati n DIT washindwe huoni kuna tatizo hapo?
 
Inakuwaje ufanye kazi mwaka mzima usilipwe na uendelee kufanya? Ndiyo maana hamlipwi kwasababu mkuu wenu anajua lazima mtafanya tu. Part time 10000 si ukafuge kuku? Gharama za usafiri kufika hapo hiyo 10000 si itakuwa imeisha?
 
Mkuu

Basi ni serikali nzima ipo dysfunctional

Jamaa ka centralize the whole revenue streams kila kitu lazima kitoke kwake...

Kuna jamaa yangu anadai bilions MSD pale anavyoona watamrusha...

Na as we speak commercial banks zote TZ hazina dollar currency za kutosha!

Dysfucntional government..basi hizi zitakua ni trickle down effects ya cummulative bad decisions done by these "people"!
Ni kweli vitu vingi viko centralized na hii ndo kisingizio watendaji wazembe wengi husingizia na hawawajibiki kama huyu mkuu wa chuo hii kitu iko ndani ya uwezo wake ni uzembe tu
 
Halafu wanaoendesha hizi taasisi ni maprofesa kabisa lakini hata kuwaza namna gani inaathiri wanafunzi ,walimu na familia zao..hawajali mradi wao wanakula na kusaza

Hizo taasisi akipewa aliyekuwa mbunge wa geita vijijini ndg kasheku msukuma au L. Lusinde aka kibajaji hiyo taasisi itasimama.

Kwa utafiti wangu ndani ya taasisi zote za serikali zinazoongozwa na prophesor ni taasisi chache sana zenye mafanikio , ma-pr. Wengi wa tanzania ni makaratasi tu.

Ukikuta wizara au taasisi inaongozwa na ma pr. Au ma Dr nichache nazingine zinasaidiwa na wasaidizi wao ambao hawana kiwango cha pr.
Mfano.. makame mbarawa waziri wa maji, huyu bila naibu wake aweso mzee wa ukizingua tunazinguana nahapo angekuwa kishatumbuliwa, make mzee baba mpaka alimwambia avute bangi chooni baada ya kila alipokuwa akihamishwa hamna kitu.huyo ni prophesor.
Nenda kwenye majimbo ya ma- Doctor nawanaojifanya wasomi kama.
Dr chegeni (Busega)
Pr. Jumanne maghembe
Dr......... mbunge wa Buchoza

Nasehem zingine, kwahiyo nawashauli hapo DIT andamaneni
 
Inakuwaje ufanye kazi mwaka mzima usilipwe na uendelee kufanya? Ndiyo maana hamlipwi kwasababu mkuu wenu anajua lazima mtafanya tu. Part time 10000 si ukafuge kuku? Gharama za usafiri kufika hapo hiyo 10000 si itakuwa imeisha?
Mkuu ukosefu wa ajira unawalazimu watu kunyanyasika kama hivi, sema wanafunzi nao lazima wananyimwa haki yao hamna mtu duniani atafanyiwa huo unyanyasaji na akafundisha kwa moyo.

Ni sawa na unamnyanyasa housegirl wako halafu yeye ndo unamtegemea kubaki na watoto lazma utegemee shida kwa watoto. Sasa huyu mkuu wa chuo hajali hilo.
 
Hizo taasisi akipewa aliyekuwa mbunge wa geita vijijini ndg kasheku msukuma au L. Lusinde aka kibajaji hiyo taasisi itasimama.

Kwa utafiti wangu ndani ya taasisi zote za serikali zinazoongozwa na prophesor ni taasisi chache sana zenye mafanikio , ma-pr. Wengi wa tanzania ni makaratasi tu.

Ukikuta wizara au taasisi inaongozwa na ma pr. Au ma Dr nichache nazingine zinasaidiwa na wasaidizi wao ambao hawana kiwango cha pr.
Mfano.. makame mbarawa waziri wa maji, huyu bila naibu wake aweso mzee wa ukizingua tunazinguana nahapo angekuwa kishatumbuliwa, make mzee baba mpaka alimwambia avute bangi chooni baada ya kila alipokuwa akihamishwa hamna kitu.huyo ni prophesor.
Nenda kwenye majimbo ya ma- Doctor nawanaojifanya wasomi kama.
Dr chegeni (Busega)
Pr. Jumanne maghembe
Dr......... mbunge wa Buchoza

Nasehem zingine, kwahiyo nawashauli hapo DIT andamaneni
Mkuu uko right wengi wa hawa maprof hamna kitu ni ile kujitutumua tu hasa wakipewa madaraka. Ni wachache sana wanaoweza, sijui ni lack of leadership ama nini mtu usidelegate hata ishu ndogondogo mwisho wa siku vitu haviendi. Uongozi kweli karama
 
Back
Top Bottom