Ujue utapeli uliojificha wa kutafuta sarafu za kizamani kwa dau nono | kaa chonjo

2019

JF-Expert Member
Dec 31, 2018
2,982
4,457
Bila kupoteza muda kwenye mada.

Najua wengi mshasikia sana mambo ya kutafuta sarafu flani ya zamani na kuahidiwa kupewa donge nono la pesa.
Mf. kisa cha @LwandaMagere aliambiwa atafute tsh 100 ya mwaka 1993 atapewa milioni 100
Kwanini pesa hiyo inunuliwe kwa pesa nyingi hivyo? Utaambiwa ni dawa, madini au ina kazi maalumu.

Kwa sasa kuna page hapo Insta inajitangaza kutafuta hazina za Kijermani za kale ni vitu vingi wanasema zikiwemo hizo coins.

IMG_20210222_092437.jpg
Jambo la kujiuliza bank zote duniani hazina hii sarafu kwa dau hilo kweli? Na ina kazi gani? Labda wataiweka kwenye majumba ya makumbusho kwa ajili ya utalii, je ni kweli? Si kweli kwani kuna watu wanazo na wamecoment lakini hakuna Mrejesho au jinsi ya kukabidhiana.

UTAPELI UKO HIVI
Wanajipanga watu kadha atokezaa mtu mwenye sarafu na mwingine anatangaza kuitafuta hii kwa dau kumbwa labda mil 10, akitangaza vijana wataingia mtaani kuisaka, mwingine anajifanya anajua mwenye nayo akitaka ahadi ya pesa pindi akionyesha. Wanakubaliana kwenda kwa mwenye nayo inaonyeshwa wanapatana labda mimi nakupa mil 2

Anapigiwa bosi simu kuhakiki je unaitaka kweli? Anajibu ndio naitaka. Hapo vijana washapata uhakika hata kama hawana pesa lazima wakakope sababu wana uhakika na pesa tena ndefu. Unaingia mkopo unakwenda kulipia ile sarafu baada ya kulipa sasa uko na mtangaza tenda kwenda kwa boss kukabidhi sarafu ili upewe mil 10.

Unafika kwa boss anakwambia kashapata na haitaji tena nyingine, unapunguza dau hadi mil 2 ili kurudisha pesa yako anakataa katu kata.

Wanakwenda kwa mwenye sarafu kujaribu kurudisha anakwambia yeye mwenyewe alinunua kwa sababu ilikua inatafutwa na pesa kashatumia. Mpaka hapo hujatapeliwa? Umenunua sarafu ya sh 100 kwa mil 10 hujaishia jela?

Jambo la kutafakari huwezi kupata pesa nyingi kwa muda mfupi lazma uumie tu.

Wenye sarafu za Kijermani dili hilo hapo. Mimi ninayo tayari.
 
How the stock market works.

Once upon a time in a village, a man appeared and announced to the villagers that he would buy monkeys for $10 each.

The villagers, seeing that there were many monkeys around, went out to the forest and started catching them. The man bought thousands at $10 and as supply started to diminish, the villagers stopped their effort.

He further announced that he would now buy at $20. This renewed the efforts of the villagers and they started catching monkeys again.

Soon the supply diminished even further and people started going back to their farms.

The offer increased to $25 each and the supply of monkeys became so little that it was an effort to even see a monkey, let alone catch it!

The man now announced that he would buy monkeys at $50! However, since he had to go to the city on some business, his assistant would now buy on behalf of him.

In the absence of the man, the assistant told the villagers; “Look at all these monkeys in the big cage that the man has collected. I will sell them to you at $35 and when the man returns from the city, you can sell them to him for $50 each.”

The villagers rounded up with all their savings and bought all the monkeys. Then they never saw the man nor his assistant, only monkeys everywhere!

Now you have a better understanding of how the stock market works.
 
haya mambo yamenisotesha sana 2010-2013, hua nikikumbuka pesa na muda niloupoteza ajili ya upumbavu huu hua najutia sana.
 
Mbona nasikia kuna watu wanauza mfano sasa inatafutwa shilingi 20 ya mwaka 1993
 
Wewe ni mtoto sana.hiyo mada waachie wenyewe.kama bibi yako ni mchawi muulize rupia zina kitu gani?

Tatizo hapa ni watu wengi kutojua what is so special with rupien?ni ushirikina wa hali ya juu.
 
kuna jamaa yangu alilizwa 25m mwaka 2014, ila kila siku nikimshauri aachane na hayo makitu hakunisikia, jamaa aliokuwa nao baada ya hela kwisha kila mmoja akatoweka, yaani alikuwa anaambiwa lete nauli kias fulani tumeambiwa kuna mzigo mkoa fulani, jamaa anatoa nauli labda laki 2, jamaa wakiachana wanagawana wanaenda majumbani kwao, wanakaa kama week mbili wanampigia mzigo tunao, wakipeleka kwa bos wanaambiwa sio wenyewe watapewa 50k, kumbe 50 ni ile aliyotoa nauli, jamaa wanakuwa wametengeneza 150k, mara nyingine wanabadili mbinu, ilienda hvo mpaka jamaa akamaliza 25m aliyolipwa baada ya kampuni aliyokuwa anafanya kazi saudia kusitisha mkataba wake.
 
Back
Top Bottom