Ujue uozo wa police Wazo Hill

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
police wa Wazo Hill , ndio kituo kikuu kinachotegemewa wakazi wote wa tegeta na Boko Bunju na sehemu nyinginezo kupata huduma muhimu ya kipolice, nenda sasa pale uone kinachojiri, police hao uwaona watu kama vile hawana shughuli za kujenga taifa, wanaweza kwambia fika saa mbili bila kukosa, lakini kazi yako au shida yako itakuchukua masaa matano mpaka sita, ukienda siku kama Jmatatu utawakuta saa mbili mpaka saa nne wako kwenye mghahawa wanapiga story za juzi na jana hasa za weekend, ukitaka huduma haraka jaribu hata kununua mtori , supu ndipo unaondika nao chapu chapu, njoo sasa kama unatafuta mtuhumiwa kwenye kitabu , hapo ndio utaona makubwa, kila mtu atajifanya anatafuta kwa makini file lako lakini wapi, wananchi wengi wametelekeza watuhumiwa kwa sababu ya usumbufu wanaoupata, nilipowauliza kuwa kesi zenu za kwenda mahakama zinashughulikiwa na nani, nikajibiwa wao lakini ni mpka upangiwe mpelelezi, ambaye hufika saa nne mpaka tano, na anashughulikia mafile kama mia hivi, na wapelelezi wachache, nilipoendelea kudadisi nilitolewa baru kuwa niache majungu sio lazima kesi zote ziende mahakamani, kuna kapolisi kazee kidogo hivi nilikakuta kananuka pombe kwa wingi hako kanatukana watu na kuwashwaga kama ngombe ambao wanasubiri huduma. Imekuwa ni tabia ya police kunyanyasa watu mpaka wanafikia hatua ya kutelekeza kesi zao, baada ya kufatilia bila msaada. Sikuishia hapo, police hawa wako bega kwa bega na Vibaka wa TEGETA stand, vibaka hawa huwapola laive wao wanachekelea, ukiwapeleka pale ndipo utajua majina ya maafande wote, wakiwa sero utasikia "Afande Rafa niokoo mwenzio nipo sero nitakutoa kiaina" baada ya hapo utamkuta mitaani mana wanasema kesi imekosa ushahidi, kama kakuibia pochi na imeishalitupa ushaidi utaupata wapi na watu wote pale standi ni wapita njia. Sikuishia hapo, tukiwa tunakula supu pale, na kupiga story unakuta police anasifia mwizi/kibaka, yaani wiki hii wamemshika kibaka hatari sana ambaye ameshindikana, utumia nguo za kike na panga au bisis bisi lenye damu, au kisu, ukikutana naye anajifanya ana haraka baadaye anajifanya umemkwaa ndipo katika taharuki anatoa kisu ua panga anakuambia toa kila kitu. Samahani nimesahau jina lakini ukitaka data zake , uliza kijana anayejifanya mwanamke na kukuteka anaitwa nani , bado yupo paole sero.
naishia kwa kusema kuwa tuunaomba Kamanda KOVA afanye uchunguzi kituo hiki ambacho police hawafanyi kazi ya kuudumia wamefanya kituo kama sehemu ya kupiga soga.
 
Mimi nakaa tegeta siwaamini kabisa hao polisi maana mara kadhaa majambazi wamekuwa wanatumia udhaifu wao kwenda kuteka na kupora sehemu za starehe nakuchukua mda mrefu sehemu ya tukio wakiamini hakuna litakalo wasibu. Mimi nimeji-tune kwamba tegeta hakuna kituo cha polisi.
 
hata wezi wote wa ng'ombe wanawajua na hawa ni wachinja nyama maaharufu jijini, wanakaa karibu na Mbweni JKT kundi hili linatisha wapo kumi na nane uchinja ng'ombe kwa dakika, ukienda pale Wazo hili utakuta Gari aian ya Hiace lililotelekezwa ambalo lilitumika kuiba Ng'ombe. Mbali na haya kama kweli kuna Mapolice wanasoma hizi makala wajilekebishe Njaa uleta dharau,
 
Pole, Vijana wa kowa hawaingii humu, humu wanaingia vijana wa lipumba na mbowe tu.
 
hata wezi wote wa ng'ombe wanawajua na hawa ni wachinja nyama maaharufu jijini, wanakaa karibu na Mbweni JKT kundi hili linatisha wapo kumi na nane uchinja ng'ombe kwa dakika, ukienda pale Wazo hili utakuta Gari aian ya Hiace lililotelekezwa ambalo lilitumika kuiba Ng'ombe. Mbali na haya kama kweli kuna Mapolice wanasoma hizi makala wajilekebishe Njaa uleta dharau,

Kama rais wa nchi anasimama jukwaani na kuongopea taifa kuwa hamjui mmiliki wa Dowans
Kama rais wa nchi wanawalinda majambazi wa mali za uma kisa ni marafiki zake
Kama bunge linam-replace spika ili yule mpya alinde wezi
Kama.....
Kama...
Kama....
unategemea polisi afanya nini?????????????????????????????????????????????????
 
Back
Top Bottom