Mkuu vipo viwili vya ivyo (ila sio ivyo huo ni mfano wa muundo wa izo dawa) ambazo zinamezwa kwa ajili ya kichocho na kama nyingine muundo huo huo nusu (yaani kinavunjwa ) wanapewa watafune nazani ni za minyoo.
Yah kama ni za muundo huo ni za kichocho na hiyo ya minyoo nayo inafanana na hiyo. Kwa umri wa wanao dawa ya minyoo lazima wameze kidonge kimoja kizima kwa sababu kina 500mg kama ni mebendazole au 400mg kama walipewa albendazole. Inawezekana dawa za kichocho ndio hizo walizovunjiwa maana walipewa kidonge kimoja na nusu. Lakini all in all dawa yoyote ile inaweza kuwa na side effect kutegemeana na mtu na mtu. Mojawapo kichwa kuuma, kizunguzungu, vipele, kutapika hata kuhara, hizo ni baadhi tu lakini kuna wakati anaweza kuwa na dalili hizo kama alikuwa na vimelea vya ugonjwa na akameza dawa.