Kibanga Ampiga Mkoloni
JF-Expert Member
- Aug 9, 2007
- 18,697
- 8,843
Kwa mujibu wa GAZETI LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA la Tarehe 5 Juni, 2020 SEHEMU YA TANO Ukururasa wa 14. Angalia Kiambatisho.
5.2.2 Kamati ya Kitaifa
Itakuwa na mamlaka ya kusikiliza malalamiko ya ukiukwaji wa maadili kwenye uchaguzi wa Rais na Rufaa
kutoka Kamati ya Jimbo. Kamati hii itaundwa na-
(a) mjumbe mmoja wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambaye atakuwa Mwenyekiti wa Kamati;
(b) mwakilishi mmoja kutoka kila chama cha siasa kinachoshiriki uchaguzi wa Rais. Aidha, mwakilishi
huyo atapaswa kuwasilisha kwa Mwenyekiti wa Kamati barua ya uteuzi kutoka kwa Katibu Mkuu
wa chama husika; na
(c) mjumbe mmoja atakayewakilisha Serikali atakayeteuliwa kwa maandishi kutoka Ofisi ya Waziri
Mkuu; na
(d) Katibu na Katibu Msaidizi wa Kamati ya Maadili ya Uchaguzi kutoka miongoni mwa Maafisa
waandamizi wa Sekretarieti ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Wakati wa kikao cha kamati, Katibu au Katibu Msaidizi atachukua muhtasari wa kikao na atawajibika
kutunza kumbukumbu za vikao.
5.2.1 Kamati ya Rufaa
Itakuwa na mamlaka ya kusikiliza rufaa kutoka Kamati ya Kitaifa na itaundwa na-
(a) Mwenyekiti ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi;
(b) Makamu Mwenyekiti ambaye ni Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi;
(c) mjumbe mmoja kutoka kila chama cha siasa kinachoshiriki uchaguzi wa Rais ambaye ni Mwenyekiti
au Katibu Mkuu au mwakilishi wa chama cha siasa kinachoshiriki uchaguzi wa Rais;
(d) mjumbe mmoja atakayeiwakilisha Serikali ambaye ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu au
mwakilishi wake; na
(e) Katibu wa Kamati ambaye ni Mkurugenzi wa Uchaguzi au mwakilishi wake na Katibu Msaidizi wa
Kamati ambaye ni miongoni mwa maafisa waandamizi wa sekretarieti ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Wakati wa kikao cha kamati, Katibu au Katibu Msaidizi atachukua muhtasari wa kikao na atawajibika
kutunza kumbukumbu za vikao.
5.2.2 Kamati ya Kitaifa
Itakuwa na mamlaka ya kusikiliza malalamiko ya ukiukwaji wa maadili kwenye uchaguzi wa Rais na Rufaa
kutoka Kamati ya Jimbo. Kamati hii itaundwa na-
(a) mjumbe mmoja wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambaye atakuwa Mwenyekiti wa Kamati;
(b) mwakilishi mmoja kutoka kila chama cha siasa kinachoshiriki uchaguzi wa Rais. Aidha, mwakilishi
huyo atapaswa kuwasilisha kwa Mwenyekiti wa Kamati barua ya uteuzi kutoka kwa Katibu Mkuu
wa chama husika; na
(c) mjumbe mmoja atakayewakilisha Serikali atakayeteuliwa kwa maandishi kutoka Ofisi ya Waziri
Mkuu; na
(d) Katibu na Katibu Msaidizi wa Kamati ya Maadili ya Uchaguzi kutoka miongoni mwa Maafisa
waandamizi wa Sekretarieti ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Wakati wa kikao cha kamati, Katibu au Katibu Msaidizi atachukua muhtasari wa kikao na atawajibika
kutunza kumbukumbu za vikao.
5.2.1 Kamati ya Rufaa
Itakuwa na mamlaka ya kusikiliza rufaa kutoka Kamati ya Kitaifa na itaundwa na-
(a) Mwenyekiti ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi;
(b) Makamu Mwenyekiti ambaye ni Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi;
(c) mjumbe mmoja kutoka kila chama cha siasa kinachoshiriki uchaguzi wa Rais ambaye ni Mwenyekiti
au Katibu Mkuu au mwakilishi wa chama cha siasa kinachoshiriki uchaguzi wa Rais;
(d) mjumbe mmoja atakayeiwakilisha Serikali ambaye ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu au
mwakilishi wake; na
(e) Katibu wa Kamati ambaye ni Mkurugenzi wa Uchaguzi au mwakilishi wake na Katibu Msaidizi wa
Kamati ambaye ni miongoni mwa maafisa waandamizi wa sekretarieti ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Wakati wa kikao cha kamati, Katibu au Katibu Msaidizi atachukua muhtasari wa kikao na atawajibika
kutunza kumbukumbu za vikao.