Ujio Wangu Kigoma - shame on our leaders!

Shadow

JF-Expert Member
May 19, 2008
2,897
671
Nimefanikiwa kutembelea Kigoma mjini, Ujiji na Kigoma Kaskazini kwa lengo la kutembea kama 'mtalii wa ndani'. Niliojinea tokea pale uwanja wa ndege hadi Kigoma mjini; ujiji na kule Kigoma pande za Kaskazini yanatia simanzi. Hali ya mwananchi wa Kigoma haifanani(reflect) kama nchi hii imepata uhuru miongo kadhaa. Reli haina mabadiliko yoyote tangu Jerumani alipoitandaza, Mji umejaa vumbi, umeme wa magilini magilini,. Kweli hawa ndugu zangu wa Kigoma ni kama kisiwa pale linapokuja suala la mgawanyo wa 'keki ya taifa'. Sasa kuna jambo moja ambalo limenitatiza na kunitia simanzi na sijui nimfikishie nani kwani siwezi kulimwaga hapa kwenye 'kuku wengi' [Ashakum! Nimetumia tamathali za semi] mpaka pale wakati muhafaka utakapokuwa umetimia na kupata the 'right person' who can handle this sensitive info.

Kwa mara nyingine tena poleni ndugu zanguni wanaKigoma.

Wasalaam,

Shadow.
 
Nimefanikiwa kutembelea Kigoma mjini, Ujiji na Kigoma Kaskazini kwa lengo la kutembea kama 'mtalii wa ndani'. Niliojinea tokea pale uwanja wa ndege hadi Kigoma mjini; ujiji na kule Kigoma pande za Kaskazini yanatia simanzi. Hali ya mwananchi wa Kigoma haifanani(reflect) kama nchi hii imepata uhuru miongo kadhaa. Reli haina mabadiliko yoyote tangu Jerumani alipoitandaza, Mji umejaa vumbi, umeme wa magilini magilini,. Kweli hawa ndugu zangu wa Kigoma ni kama kisiwa pale linapokuja suala la mgawanyo wa 'keki ya taifa'. Sasa kuna jambo moja ambalo limenitatiza na kunitia simanzi na sijui nimfikishie nani kwani siwezi kulimwaga hapa kwenye 'kuku wengi' [Ashakum! Nimetumia tamathali za semi] mpaka pale wakati muhafaka utakapokuwa umetimia na kupata the 'right person' who can handle this sensitive info.

Kwa mara nyingine tena poleni ndugu zanguni wanaKigoma.

Wasalaam,

Shadow.


absolutely you are damn right,

ule mji ni kama umesahaulika,

Maisha bora kwao ni ndoto za alinacha hakuna umeme barabara ndio usiseme sijui mwokozi gani ashuke kuwanusuru lakini sio ccm
 
mie nimeuliza swali kwani huwa tunawapa hawa viongozi madaraka kwa sababu gani?????????????????????
 
au we mamluki?.....watz bwana wanasema matatizo mengi lakini hawasemi wao watafanya nini...............je,ukipata cheo hautakuwa kama waliotangilia? toa strategies watu wajue hisia zako na wajue unataka kuwafanyia nini..............sio kulalamika tuuuuuuuuu.....hatufiki
 
Kigoma ni mji wenye rasilimali nyingi sana na kijiografia pia umekaa vizuri sana kuwa 'hub' ya nchi za maziwa makuu. Reli ikiboreshwa[ Siyo na mikataba ya kina RITE] pia bandari Kigoma yaweza kufika mbali sana. Piga picha ya Mizigo ya Mashariki ya Kongo Kinshasa ikipitia Kigoma. Umeme Ukiboreshwa yamaanisha ajira zitaongezeka na kukuza rasilimali kama uvuvi.

Ukosefu wa 'patriotism' na watu kugeuza siasa mradi wa kujitajirisha ndo umeifikisha Kigoma hapa ilipo kwani sasa ni zaidi ya miongo minne ya kuimba kwamba ili tuendelee tunahitaji vitu vinne: watu, siasa safi, uongozi bora na blah blah nyingi mwisho wa siku ni kwa faida ya wachache. Lakini hili nililolisikia na kuliona ndo linanitia kichefuchefu na sijui nani wa kumwamini ambaye naweza "kumuuma sikio"
 
Sasa kuna jambo moja ambalo limenitatiza na kunitia simanzi na sijui nimfikishie nani kwani siwezi kulimwaga hapa kwenye 'kuku wengi' mpaka pale wakati muhafaka utakapokuwa umetimia na kupata the 'right person' who can handle this sensitive info

Shadow.

Unamtaka mtu gani mwenye sifa zipi ili ujue ndo 'the right person'? mwenyeji wa Kigoma au?
 
Unategemea maendeleo gani Kigoma mjini wananchi wanapodanganywa na CCm halafu wanamchagua MRUNDI Serukamba kuwa mbunge wao?? Waache wapate taabu pengine hiyo dhiki itawaamsha hao wagoma wamtose huyo BOI FISADI kwenye ubunge mwakani!!
 
Kigoma mjini na wilaya zake zote kwa kweli hali ni mbaya sana kwa mwanachi wa kawaida. I know as a fact kwamba viongozi wa serikali karibia wote wanapopelekwa kufanya kazi kule, huwa wanapiga kelele na kutaka kuhamishwa, Baada ya kukaa miezi kama miwili mitatu, zile kelele za kuhamishwa hutazisikia tena na ndo wanaanza kufight kwa udi na uvumba wabakie hapo milele.

Mkoa unaliwa vibaya mno, wananchi wamezubaa, viongozi wakubwa wanatembelea kule kwa msimu na wanadanganywa tu na watendaj. Madiwani shule hamna, wanahongwa vijipesa kidogo sana na 'wakuu wa idara' na life goes on.

Nimefanya kazi kule miaka minne na kwa kweli sitamani kurudi tena
 
Kigoma ni mji wenye rasilimali nyingi sana na kijiografia pia umekaa vizuri sana kuwa 'hub' ya nchi za maziwa makuu...
If you look at broader picture, the entire country has vast resources and is well positioned to be hub of business for more than 10 countries in the region.
Tumejaaliwa sana lakini tatizo letu lipo pengine kabisa
 
Hebu nikumbusheni jamani..... hivi Zitto anatoka wapi?

Kigoma. That said, Zito ni sawa na kuchota maji ndani ya mto na kumimina baharini. Movers and shakers wa policies za taifa na Kigoma ziko au zina baraka ya chama dola lakini that is my take and can not be taken as an excuse for failure to deliver kwa wanakigoma.
 
Last edited:
That is what you get when you have people like Peter Serukamba representing you in Bunge!!
 
Nimefanikiwa kutembelea Kigoma mjini, Ujiji na Kigoma Kaskazini kwa lengo la kutembea kama 'mtalii wa ndani'. Niliojinea tokea pale uwanja wa ndege hadi Kigoma mjini; ujiji na kule Kigoma pande za Kaskazini yanatia simanzi. Hali ya mwananchi wa Kigoma haifanani(reflect) kama nchi hii imepata uhuru miongo kadhaa. Reli haina mabadiliko yoyote tangu Jerumani alipoitandaza, Mji umejaa vumbi, umeme wa magilini magilini,. Kweli hawa ndugu zangu wa Kigoma ni kama kisiwa pale linapokuja suala la mgawanyo wa 'keki ya taifa'. Sasa kuna jambo moja ambalo limenitatiza na kunitia simanzi na sijui nimfikishie nani kwani siwezi kulimwaga hapa kwenye 'kuku wengi' [Ashakum! Nimetumia tamathali za semi] mpaka pale wakati muhafaka utakapokuwa umetimia na kupata the 'right person' who can handle this sensitive info.

Kwa mara nyingine tena poleni ndugu zanguni wanaKigoma.

Wasalaam,

Shadow.

Salaam,

Ni kweli kuwa Kigoma imekuwa nyuma muda mrefu sana toka Taifa limepata uhuru. Mkoa mzima wa Kigoma umekuwa hauna miundombinu ya uhakika tofauti na Reli aliyojenga Mjerumani. Mkoa umekuwa ukipokea wakimbizi kwa muda mrefu sana. Maji yamekuwa ni shida, Barabara na Umeme. Biashara haijachangamka sana licha ya kuwa na Bandari. Hata hivyo haina maana kuwa tumekaa kimya bila kufanya lolote


  1. Hivi sasa kuna miradi mikubwa miwili ya barabara (Mwandiga - Manyovu inayounganisha mji wa Kigoma na Mji wa Bujumbura na kisha Uvira (DRC) na ile ya Kigoma - Kidahwe kama sehemu ya barabara ya Kigoma - Tabora. Miradi hii itaunganisha Kigoma na nchi za KONGO na Burundi na hivyo kukuza biashara.
  2. Eneo lote la Kigoma Ujiji pamoja na sehemu za Kigoma Vijijini hivi sasa ni Special Economic Zone. Mwezi wa saba TRA wametoa leseni maalumu ambapo sasa Kigoma itakuwa ni destination port na hivyo kuongeza biashara na kutengeneza ajira.
  3. Bandari ndogo ya Kagunga inajengwa na soko ili kuongeza biashara katika mpaka wa Kagunga na Burundi.
  4. Miradi ya Maji mingi sasa imeanza kutekekelezwa katika maeneo ya vijijini. EU water Facility iligharamia mradi wa maji katika vijiji 5 na hivi sasa WorldBank imetoa kazi inayofanywa na Kampuni ya redeco gmbh YA Ujerumani kwa miradi ya vijiji 10 katika Wilaya ya Kigoma. Nordic fund inagharamia mradi wa maji wa Manispaa ya Kigoma.
  5. MCC inajenga mrado wa umeme Malagarasi ambao utakamilika mwaka 2012 na kuweza kumaliza tatizo la umeme katika mji wa Kigoma na mji wa Kasulu.
  6. Tumejenga shule kata zote. Baadhi ya Vijiji kama Kalinzi, Nyarubanda, Mukigo, Matizo vina shule mbili za sekondari.
Ni kweli kuwa Kigoma tupo nyuma sana. Lakini ikumbukwe kuwa hatujawahi kuomba chakula toka nchi ipate uhuru Yaani Kigoma haijawahi kuwa na njaa. Tunajilisha wenyewe na kuuza ziada nchi jirani.

Kwa vyovyote vile maendeleo ya Kigoma ambayo imekuwa marginalized kwa miaka mingi (kumbukeni Kigoma ilikuwa ni chanzo cha manamba) hayawezi kutokea kwa kulipuka tu. Inahitajika kazi kubwa sana na ya ziada. Tunajitahidi.
Ndio maana mkoa wa Kigoma haujawahi kuipa CCM zaidi ya 60% katika kura za wabunge. Mwaka 2005 national avarage ilikuwa 69% na kwa Kigoma CCM walipata 58% (10% below national avarage). Huu ni ujumbe tosha kuwa watu wa Kigoma tumechoshwa na kuwa marginalized.
Tunajiamini kuwa tutavuka viunzi hivi. Tunajiamiin kuwa tutaweza kushindana ndani ya Tanzania. Kwa kuwa tumeweza kujilisha miaka yote hii, tutaweza kushinda changamoto za maendeleo.
 
wewe sema uliloliona na linalokutatizo JF IS THE RIGHT PLACE, we will hear you n act on it.
acha utoto, unazani nani atajitambulisha kwako umuamini? ili umpe hizo info...hapa JF wapo wawakilishi wa serikali na JK mwenyewe na hata wahusika wa kigoma kama ZITO wapo....SEMA TU HAPA NDIO MUAFAKA.......
 
Nilikuwa JKT Bulombora mwaka 1988.Nilishangaa kuiona Kigoma ,jina ni kubwa kuliko utakayoyakuta.barabara ni mbovu,vumbi na ni real poor !Ungeniambia wajerumani warudi tena huko ,ningekubali.Ndio hao waliiunganisha na the rest of Tanganyika.

Lakini KIGOMA not alone,many parts of Tanzania are the same.Maana maendeleo ya nchi Viongozi wetu wanavyotafsiri ni kuwa na Magorofa Masaki,Mbezi Beach ,MSASANI,Mikocheni,4WD jijini etc.Ndio maana hawaamini ripoti za World Bank zinaposema nchi yetu ni one of the poorest in the world.

Wataalamu wanapima ubora wa elimu,afya,access ya maji safi,usafiri na barabara.
Ni wangapi wa Tanzania wana personal family doctor( no the so called Medical Assistants).Ni wangapi wa Tanzania wana tumia choo cha ndani(flush toilets).
 
Sinyolita-wamezubaa?Naomba ulibadili hilo neno, sijui kama unajua kuwa Mh.Kabwe anatoka huko?Na wako wengi wa aina yake?
Ninachouliza hivi ni kweli bidhaa hizo hapo chini hazipatikani sehemu yoyote hapa Afrika Mashariki na ya Kati?Na kama ni kweli basi si wawe kama wapemba mpaka kieleweke?Na mbona nasikia mashirika mengi ya misaada yako kule yanafanya nini?

Nasikia
1.Dagaa 2.Chumvi 3.Mawese 4.Ndumba kali kuliko zote ni kule sasa iweje?

Kigoma mjini na wilaya zake zote kwa kweli hali ni mbaya sana kwa mwanachi wa kawaida. I know as a fact kwamba viongozi wa serikali karibia wote wanapopelekwa kufanya kazi kule, huwa wanapiga kelele na kutaka kuhamishwa, Baada ya kukaa miezi kama miwili mitatu, zile kelele za kuhamishwa hutazisikia tena na ndo wanaanza kufight kwa udi na uvumba wabakie hapo milele.

Mkoa unaliwa vibaya mno, wananchi wamezubaa, viongozi wakubwa wanatembelea kule kwa msimu na wanadanganywa tu na watendaj. Madiwani shule hamna, wanahongwa vijipesa kidogo sana na 'wakuu wa idara' na life goes on.

Nimefanya kazi kule miaka minne na kwa kweli sitamani kurudi tena
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom