Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,503
- 217,764
Baada ya Mabomba ya Maji yaliyowekwa na Mabeberu wa DANIDA miaka mingi iliyopita kuziba na miundo mbinu yake kuharibika , hivyo kusababisha wananchi wa vijiji vya Kyela kuendelea kutumia visima na maji ya mito yasiyo salama , tulitegemea ziara ya Mh Rais Wilayani hapa ingechagiza ufumbuzi wa jambo hili lakini kwa bahati mbaya imekuwa kinyume chake.
Vijiji kama Isaki , Kabanga , Kasumulu , Lubele , Ngana , Mbako , Kilasilo , Ibungu , Lupembe , hadi Ikolo , ambavyo vilinufaika na mradi wa maji wa DANIDA vimekuwa na tatizo la maji salama kwa kipindi kirefu mno , tulitegemea mbunge Mwakyembe angeomba msaada kwa Rais ambaye sasa imefahamika kwamba anatembea na miradi yake mfukoni hata kama haikupitishwa na Bunge , ili asaidie vijiji hivi kupata maji kama ilivyokuwa kwenye mradi wa DANIDA
Ikumbukwe kwamba Wilaya ya Kyela ni miongoni mwa Wilaya zinazoshambuliwa mno na Kipindupindu , huku sababu zinazotajwa imo hii ya kukosa maji salama
Vijiji kama Isaki , Kabanga , Kasumulu , Lubele , Ngana , Mbako , Kilasilo , Ibungu , Lupembe , hadi Ikolo , ambavyo vilinufaika na mradi wa maji wa DANIDA vimekuwa na tatizo la maji salama kwa kipindi kirefu mno , tulitegemea mbunge Mwakyembe angeomba msaada kwa Rais ambaye sasa imefahamika kwamba anatembea na miradi yake mfukoni hata kama haikupitishwa na Bunge , ili asaidie vijiji hivi kupata maji kama ilivyokuwa kwenye mradi wa DANIDA
Ikumbukwe kwamba Wilaya ya Kyela ni miongoni mwa Wilaya zinazoshambuliwa mno na Kipindupindu , huku sababu zinazotajwa imo hii ya kukosa maji salama