LiverpoolFC
JF-Expert Member
- Apr 12, 2011
- 11,348
- 3,219
Wakati natoka kibaruani jioni hii,mara ikapita gari la matangazo inayotokea upande wa magharibi yaani toka Sakina inakuja kuelekea Mianzini ikitangaza ujio wa JK jumamosi kama tajwa hapo juu. Kulikuwepo na jam kubwa na mara nikasikia watu pembezoni mwa barabara na hata abiria walikuwa kwenye jam barabarani wakimzomea mtoa matangazo kwenye lile gari,NAWANUKUU "utakaanaye pamoja na mafisadi wenziwe na kamwe hatatuona,kwani umesikia watoto wetu wanaugua surua? Kawape watoto wa mafisadi wenzako ama peleka kwa gamba mwenziwe pale Monduli,hautatuona,Unafikiri nachotufanyia ni nzuri leo mnatutega siyo hatutegeki tena kihivyo" Mwisho wa kunukuu! Nimejiuliza maswali kivyangu lakini majibu haijanitosha na ndiyo nikasema tushirikiane ktk hili la wenyeji kumkataa rais.