Ujio wa Jenerali El-Sisi ni uchukuliwe kwa tahadhari kubwa sana

Ujio wa Jenerali El-Sisi ni uchukuliwe kwa tahadhari kubwa sana

Myb kilimo cha umwagiriaji.
South Africa na Kenya ni karibu zaidi kujifunza.
Halafu Tanzania kilimo cha umwagaji ni tofauti sana na Misri kwa sababu sisi tuna mvua nyingi wakati wao ni jangwa.
 
Makafiri bwana, utazan wanajadili mambo ya maana kumbe shida uarabu wake na dini
 
Shida ya El Sisi yeye ni military General, alikuwa mkuu wa usalama. Hajui lolote kuhusu uongozi wa nchi na hajawahi kujifunza tangu awe Rais.

Kinachonisikitisha sana kwake ni vipaumbele. Jamaa ana vipaumbele vya ajabu hata failure wa Form 4 anajua kabisa havina mantiki kwa uchumi wa nchi yake. Amekopa kupitiliza, ameuza pwani mojawapo ya nchi yake upande wa bahari ya Mediterranean, kawauzia UAE kwa mabilioni ya dola (baada ya ukata).

Pia kaua uchumi wa Misri kwa kufanya monopolization ya baadhi ya sekta na kulipa jeshi utawala wa uchumi. Badala ya kuacha raia wamiliki uchumi, mwishowe ushindani hamna na makampuni ya wawekezaji yanakimbia. Uwekezaji mpya hauji kwa sababu yeye ni kilaza na ndio kauli ya mwisho kwenye nchi, unajenga kiwanda cha simenti leo kwa $ billion kadhaa, mwakani El Sisi anatangaza kuanzia sasa uzalishaji wa simenti utafanywa na kampuni ya jeshi tu. Mwekezaji unapata hasara na ufanisi wa kampuni za kijeshi ni mdogo mno wala hakuna ushindani au ubunifu mpya.

Wakati huo pamoja na madeni yote bado katumia gharama kubwa kujenga mji mkuu mpya. Na kajenga makao makuu mapya ya kijeshi. Nilitazama wiki iliyopita anaongea na majenerali wake eti kajenga Octagon kwa sababu pale waandamanaji hawawezi fika. Administrative Complex nzima ambayo imekingwa dhidi ya waandamanaji imetumia zaidi ya dola bilioni 57.

Wakati Egypt iko kwenye mazungumzo na IMF. Huyu ni kiongozi very useless kwa Misri. Wana hasara sana na bahati mbaya kuwa naye na hawakumchagua.
 
Makafiri bwana, utazan wanajadili mambo ya maana kumbe shida uarabu wake na dini
Angekuwa Mwarabu kihivyo angekuwa anawatetea na anawaruhusu Wapalestina kuingia Misri kutibiwa, asingeshirikiana na Israel.
 
Misri ilipiga hatua kubwa sana wakati wa utawala wa kidemokrasia lakini tangu 2015 misri imekuwa kwenye hali mbaya sananya kimaendeleo na kiuchumi
Still wako juu Afrika kiuchumi, so positively kuna cha kujifunza kizuri Tu kama tukiamua.
 
Jenerali El- Sisi mtawala wa Misri aliingia Madarakani mwaka 2013 baada ya kumpindua Mohamed Morsi, rais wa kwanza Misri kuchaguliwa kidemokrasia, mwaka uliofuta aliua maelfu ya Waandamanaji waliotaka aondoke madarakani na kuirudisha nchi kwenye utawala wa demokrasia.

Ni mtawala katili aliyeuzimisha upinzani wa Misri kwa ufanisi na ukatili mkubwa ikiwemo kupoteza watu na kuigeuza misiri kuwa taifa la kipolisi kabisa lenye utawala mbaya katili na wa vitisho kuliko hata wa Hosni Mubarak.

Chini ya utawala wake Misri imegeuka kuwa ombaomba kwa Waarabu wa Gulf kufadhili uchumi na miradi ya Kifahari isiyowahusu wananchi wa chini wa kawaida. Mradi mmojawapo wa hovyo sana ni wa kujenga makao makuu ya ulinzi makubwa zaidi duniani yanayoitwa Octagon yenye eneo la ekari 22,000 ili kuweza kupambana na upinzani kwa ufanisi zaidi na kudumisha utawala wa kijeshi.

Misri chini ya utawala wake ni nchi yenye deni kubwa ukitumia hadi zaidi ya theluthi mbili ya mapato yake kwa mwaka kulipa madeni.

Huyu sio mgeni mwema, Misri haina kikubwa cha maana cha sisi kujifunza kwa sasa.
Ungelidokezea kuwa Misri ni nchi ya tatu kwa uchumi Mkubwa Afrika baada ya Afrika Kusini na Nigeria, ingelipendeza sana.
 
Ungelidokezea kuwa Misri ni nchi ya tatu kwa uchumi Mkubwa Afrika baada ya Afrika Kusini na Nigeria, ingelipendeza sana.
Tusikariri tu mambo,
GDP kubwa tu bila kutazama GDP per Capita haina maana yoyote. Misri ina GDP kubwa kuliko Oman, Qatar na Kuwait ila raia wa hizi nchi wana maisha mazuri mara elfu moja kuliko raia wa Misri na nchi zao zinaikopesha na kuipa Misri misaada
 
Jenerali El- Sisi mtawala wa Misri aliingia Madarakani mwaka 2013 baada ya kumpindua Mohamed Morsi, rais wa kwanza Misri kuchaguliwa kidemokrasia, mwaka uliofuta aliua maelfu ya Waandamanaji waliotaka aondoke madarakani na kuirudisha nchi kwenye utawala wa demokrasia.

Ni mtawala katili aliyeuzimisha upinzani wa Misri kwa ufanisi na ukatili mkubwa ikiwemo kupoteza watu na kuigeuza misiri kuwa taifa la kipolisi kabisa lenye utawala mbaya katili na wa vitisho kuliko hata wa Hosni Mubarak.

Chini ya utawala wake Misri imegeuka kuwa ombaomba kwa Waarabu wa Gulf kufadhili uchumi na miradi ya Kifahari isiyowahusu wananchi wa chini wa kawaida. Mradi mmojawapo wa hovyo sana ni wa kujenga makao makuu ya ulinzi makubwa zaidi duniani yanayoitwa Octagon yenye eneo la ekari 22,000 ili kuweza kupambana na upinzani kwa ufanisi zaidi na kudumisha utawala wa kijeshi.

Misri chini ya utawala wake ni nchi yenye deni kubwa ukitumia hadi zaidi ya theluthi mbili ya mapato yake kwa mwaka kulipa madeni.

Huyu sio mgeni mwema, Misri haina kikubwa cha maana cha sisi kujifunza kwa sasa.
Sasa biashara gani, tutafanya, na Misri? May be vijana wakasome Sharia waje wafungue misikiti kibao Dodoma, Arusha, ili kusilimisha watu!
Badala ya, kukaribisha viongozi kutoka Malaysia, India, Taiwan, unaleta jambazi, aliyeingia ikulu kwa, mapinduzi, na mauaji,
Waislam weusi huwa dhaifu(wana soft spot) mbele ya waarab,
 
Tusikariri tu mambo,
GDP kubwa tu bila kutazama GDP per Capita haina maana yoyote. Misri ina GDP kubwa kuliko Oman, Qatar na Kuwait ila raia wa hizi nchi wana maisha mazuri mara elfu moja kuliko raia wa Misri na nchi zao zinaikopesha na kuipa Misri misaada
Ahahahahaha! Thibitisha kama Wamisri wana maisha mabaya kumlinganisha na nchi zengine za Afrika.
 
Ahahahahaha! Thibitisha kama Wamisri wana maisha mabaya kumlinganisha na nchi zengine za Afrika.
Mfumoko wa bei ni 15% Kuna mwaka huwa unafika hadi 30%.
Msongomano wa watu wa kutisha na slums( ashwaiyat) kila kona kutokana na Overpopulation
Uchafu kama kwa Wahindi,
Ukosefu wa maji safi,
Huduma duni za afya,.
Unyanyasaji wa kingono uliopitiliza.
 
Back
Top Bottom