Nyalotsi
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 6,978
- 5,025
Hii tabia ya viongozi wa kiafrika kupenda kwenda kutibiwa nje ndo inadidimiza sekta ya afya ya nchi zetu. Wakienda nje ya nchi wanakuwa monitored na medical students na residents huku specialists wakiwaona kwa siku chache sana. Wakiwa kwenye hospitali zetu wanakopitia kama njia wanaonwa kwenye wodi zao special na specialists tu, medical students hamruhusiwi hata kwenda labda lecturer wenu akiwataka mumsaidia kushikilia vifaa. Hata bp wanapimwa na specialists huko wanakokimbilia wanawekwa kwenye general wards na kugeuzwa sehemu ya kujifunzia tropical diseases. Wengine wanaishia kupewa PLACEBO na kurudishwa huku wakijisifu kwamba wametibiwa vizuri sana!! Hata bp, glucose, cholesterol, urinalysis mnataka kwenda ulaya/india?Hii imesababisha hata bp machine,glocometer na vifaa vingine hakuna kwenye hospitali zetu, sababu watu wa kuzisemea wamegeuka maadui wa sekta ya afya ya nchi hii. Mfano kuna mbunge alitakiwa kufanyiwa upasuaji wa nyonga moi akagoma kwa reason ya kwamba kuna mapaparazi wengi mno maeneo haya. Sababu nyingine aliyotoa ni kwamba na yeye anataka KUCHUMA kama wengine wanavyochuma. Hivi karibuni nimesoma humu wanasema kafanyiwa india kwa dharura, nikajiuliza, dharura gani wakati alikuwa anabargain apelekwe nje? Kwa kauli kama hizi nani atazisemea hospitali zetu? Madaktari wakisema wanaambiwa ni cdm,ina maana cdm ndo wanahitaji huduma bora kwa wananchi peke yao? Poleni kwa washabiki wa mafisadi wa nchi za kiafrika, kuna fisadi mwenzenu kalazwa nje huko akiendelea kuwa sehemu ya medical students kujifunza. Haya ni malipo ya hapa hapa duniani baada ya kuua sana wapinzani wake na kuwaacha wananchi wake wafe kwa njaa ya ukame huku yeye akitanua na familia yake. Mungu bariki mapinduzi ya nchi nchi ili tunufaike na rasilimali zinazogunduliwa kila siku.