THE BOILER ROOM
JF-Expert Member
- Sep 17, 2018
- 1,054
- 3,210
Sawa Zanzibar tayari wanalo bunge lao linalojadili mustakabathi wa Zanzibar na watu wake we huoni kupeleka bunge kule kutalimeza hili na kuondoa maana kbs,kwa mtazamo wangu mimi naona waendelee kushughulikia kero za muungano,pia iangaliwe namna bora ni kwa namna gani Zanzibar itajitegemea yenyewe pasipo kuidekea dekea bara,kama kuna madeni ilipe na pia Zanzibar iachwe ifanye maamuzi yenyewe kwnye kusimamia na kunufaika na rasilimali zake yenyewe.Shida baadhi ya wa Zanzibar wanatamani mwarabu arudi tena awatawale wakafanye kazi za uyaya na kusoma juzuu upenuni.Sisi wenyewe tunaweza amini nchi hizi mbili ndani ya jamuhuri moja zitastawi sana ndani ya miaka kumi ijayo kukata mzizi wa fitna 2035 linatandikwa daraja kuunganisha nchi hizi mbili, InshAllah,Zanzibar itainjoi sana,huna haja ya kuweka bunge watu watakuwa wanaflow tu,bata Zanzibar muda wowote tena ndani ya muda mfupi,swala la ardhi Zanzibar haitakuwa inshu tena unaweza ukalala bara kazi zako visiwani,safi kbs.Wizara zenye kushugulika na Muungano ofisi zake zote zipo Tanganyika. Wizara za Mambo ya Ndani, Wizara ya Ulinzi, Wizara ya Mambo ya Nje ambazo ndiyo mhimili wa dola.
Katika Muungano wa nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar hakuna kuzungumzia ukubwa bali ni wadau wawili sawa wanaounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ( Tan + Zan + ia).
Usawa wa wadau hawa ktk Muungano bila kujali 'ukubwa' , ingependeza mhimili wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kuweka makao yake Zanzibar ili sehemu hii nyengine ya Muungano kufaidi uwepo wa Taasisi kubwa ya Muungano visiwani na kuchuma manufaa yake kiuchumi, kisiasa na kijamii na kuuimarisha muungano huu kivitendo.
Dodoma iwe ni Bunge la Tanganyika . Mfano Jamhuri ya Afrika ya Kusini inaundwa na muungano wa state 4 ambazo ni za Cape Province, Transvaal Province, Natal Province and Orange Free State Province.
Hizo state 4 zinazounda nchi ya Republic of South Africa ((RSA) kufaidi muungano huo na majimbo 9 ambayo ni Western Cape, Eastern Cape, Northern Cape, North West, Free State, Kwazulu Natal, Gauteng, Limpopo and Mpumalanga.
Mhimili wa dola makao yake makuu yapo Pretoria jimbo la Gauteng , huku mhimili wa Bunge la Jamhuri / Legislative lipo Cape Town ktk jimbo laWestern Cape na mhimili wa Mahakama Kuu makao yake yapo Bloemfontein jimbo la Free Orange. Mgawanyiko huu ni kusambaza faida za 'muungano' .