Ujenzi wa Taasisi za Serikali ya Zanzibar Jijini Dodoma kuanza ndani ya wiki moja

Rahma Salum

Member
Sep 7, 2020
30
59
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdallah ametoa Wiki moja kwa Taasisi za Ardhi, Mipango Miji pamoja na Wakala wa Ujenzi Zanzibar kukamilisha utaratibu utakaowezesha kuanza kwa ujenzi wa Majengo ya Taasisi za Serikali katika Mji Mpya wa Dodoma.

Amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo lililotolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Ofisi ya uratibu wa shughuli za Serikali iliyopo Jijini Dar es Salaam ihamie Dodoma ndani ya kipindi kifupi.

Hemed Suleiman ametoa agizo hilo wakati alipofanya ziara Maalum ya kutembelea eneo lililokabidhiwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Kujenga Ofisi hizo katika eneo la Mji mpya Jijini Dodoma likiwa na ukubwa wa hekta 33.

Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeamua kuhamishia Makao Makuu ya shughuli za Serikali Jijini Dodoma katikati ya ardhi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, uamuzi uliokwenda sambamba na kuzingatia wazo la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alilolitoa mwanzoni mwa miaka ya 60.
IMG-20201113-WA0107.jpg
 
Makao makuu ya nchi ya Tanganyika yapo wapi? Maana nchi ya Zanzibar mji mkuu wake ni Unguja /Zanzibar.

Hii ni mojawapo ya kero za Muungano kulazimisha nchi ya Zanzibar kuhamishia Ofisi zake katika mji ambao ni makao makuu ya Tanganyika iliyofichwa ktk joho la Muungano.

Dodoma ni makao makuu ya nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ningeshauri Bunge la Muungano wa Tanzania wapeleke makao yake makuu Unguja ili Zanzibar nayo ifaidike kiuchumi kwa shuguli za kimuungano za kufanya vikao vyake vyote Zanzibar na siyo Tanganyika ifaidi kila kitu huku Zanzibar ikisubiri 4% ya mgao wa fedha ambayo ni ndogo kama baadhi ya taasisi taasisi za Muungano zingepeleka makao yake Zanzibar.

Mifano ya faida za kiuchumi kwa Zanzibar ni Nyumba za wabunge wa Muungano zingejengwa Unguja, Ukumbi wa Bunge na sekretariati yake Unguja, boti na ndege kibao zingeenda Unguja, magari ya kukodisha na mafuta n.k yangetumika Zanzibar , wageni wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wangejazana Unguja na kuongeza idadi ya wageni badala ya kutegemea wageni watalii, kazi za udobi, starehe, burudani kuhudumia mamia ya watu wanaoenda Bunge la Muungano likiwa Zanzibar hii ni mifano kiduchu tu Wazanzibari wangefaudu matunda ya Muungano na kelele kupungua
 
Makao makuu ya nchi ya Tanganyika yapo wapi? Maana nchi ya Zanzibar mji mkuu wake ni Unguja /Zanzibar.

Hii ni mojawapo ya kero kwa za Muungano kulazimisha nchi ya Zanzibar kuhamishia Ofisi zake katika mji ambao ni makao makuu ya Tanganyika iliyofichwa ktk joho la Muungano.

Dodoma ni makao makuu ya nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ningeshauri Bunge la Muungano wa Tanzania wapeleke makao yake makuu Unguja ili Zanzibar nayo ifaidike kiuchumi kwa shuguli za kimuungano za kufanya vikao vyake vyote Zanzibar na siyo Tanganyika ifaidi kila kitu huku Zanzibar ikisubiri 4% ya mgao wa fedha ambayo ni ndogo kama baadhi ya taasisi taasisi za Muungano zingepeleka makao yake Zanzibar.
Unahangaika kweli.
 
Makao makuu ya nchi ya Tanganyika yapo wapi? Maana nchi ya Zanzibar mji mkuu wake ni Unguja /Zanzibar.

Hii ni mojawapo ya kero za Muungano kulazimisha nchi ya Zanzibar kuhamishia Ofisi zake katika mji ambao ni makao makuu ya Tanganyika iliyofichwa ktk joho la Muungano.

Dodoma ni makao makuu ya nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ningeshauri Bunge la Muungano wa Tanzania wapeleke makao yake makuu Unguja ili Zanzibar nayo ifaidike kiuchumi kwa shuguli za kimuungano za kufanya vikao vyake vyote Zanzibar na siyo Tanganyika ifaidi kila kitu huku Zanzibar ikisubiri 4% ya mgao wa fedha ambayo ni ndogo kama baadhi ya taasisi taasisi za Muungano zingepeleka makao yake Zanzibar.

Mifano ya faida za kiuchumi kwa Zanzibar ni Nyumba za wabunge wa Muungano zingejengwa Unguja, Ukumbi wa Bunge na sekretariati yake Unguja, boti na ndege kibao zingeenda Unguja, magari ya kukodisha na mafuta n.k yangetumika Zanzibar , wageni wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wangejazana Unguja na kuongeza idadi ya wageni badala ya kutegemea wageni watalii, kazi za udobi, starehe, burudani kuhudumia mamia ya watu wanaoenda Bunge la Muungano likiwa Zanzibar hii ni mifano kiduchu tu Wazanzibari wangefaudu matunda ya Muungano na kelele kupungua
Sio kweli tukianza tu kwny ukubwa wa nchi hizi mbili ndani ya jamuhuri moja,pili ulinzi na usalama kwa upana wake,huwezi kuweka viongozi wote wakubwa wa nchi hii kisiwani...hakunaga assumptions kwny swala na ulinzi na usalama!!hata kwa haraka haraka ukifanya S.W.O.T (Strength, Weakness, Opportunities, Threat) Analysis, nakwambia hata mtu mwenye upeo mdogo tu atakwambia hapana,ashakum si matusi kwa sisi watu wa mkojani sheikh wangu,ndg mjumbe hapa umeandika kama mtu aliyekuwa kwny njozi.
 
Sio kweli tukianza tu kwny ukubwa wa nchi hizi mbili ndani ya jamuhuri moja,pili ulinzi na usalama kwa upana wake,huwezi kuweka viongozi wote wakubwa wa nchi hii kisiwani...hakunaga assumptions kwny swala na ulinzi na usalama!!hata kwa haraka haraka ukifanya S.W.O.T (Strength, Weakness, Opportunities, Threat) Analysis, nakwambia hata mtu mwenye upeo mdogo tu atakwambia hapana,ashakum si matusi kwa sisi watu wa mkojani sheikh wangu,ndg mjumbe hapa umeandika kama mtu aliyekuwa kwny njozi.

Wizara zenye kushugulika na Muungano ofisi zake zote zipo Tanganyika. Wizara za Mambo ya Ndani, Wizara ya Ulinzi, Wizara ya Mambo ya Nje ambazo ndiyo mhimili wa dola.

Katika Muungano wa nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar hakuna kuzungumzia ukubwa bali ni wadau wawili sawa wanaounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ( Tan + Zan + ia).

Usawa wa wadau hawa ktk Muungano bila kujali 'ukubwa' , ingependeza mhimili wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kuweka makao yake Zanzibar ili sehemu hii nyengine ya Muungano kufaidi uwepo wa Taasisi kubwa ya Muungano visiwani na kuchuma manufaa yake kiuchumi, kisiasa na kijamii na kuuimarisha muungano huu kivitendo.

Dodoma iwe ni Bunge la Tanganyika . Mfano Jamhuri ya Afrika ya Kusini inaundwa na muungano wa state 4 ambazo ni za Cape Province, Transvaal Province, Natal Province and Orange Free State Province.

Hizo state 4 zinazounda nchi ya Republic of South Africa ((RSA) kufaidi muungano huo na majimbo 9 ambayo ni Western Cape, Eastern Cape, Northern Cape, North West, Free State, Kwazulu Natal, Gauteng, Limpopo and Mpumalanga.

Mhimili wa dola makao yake makuu yapo Pretoria jimbo la Gauteng , huku mhimili wa Bunge la Jamhuri / Legislative lipo Cape Town ktk jimbo laWestern Cape na mhimili wa Mahakama Kuu makao yake yapo Bloemfontein jimbo la Free Orange. Mgawanyiko huu ni kusambaza faida za 'muungano' .
 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdallah ametoa Wiki moja kwa Taasisi za Ardhi, Mipango Miji pamoja na Wakala wa Ujenzi Zanzibar kukamilisha utaratibu utakaowezesha kuanza kwa ujenzi wa Majengo ya Taasisi za Serikali katika Mji Mpya wa Dodoma.

Amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo lililotolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Ofisi ya uratibu wa shughuli za Serikali iliyopo Jijini Dar es Salaam ihamie Dodoma ndani ya kipindi kifupi.

Hemed Suleiman ametoa agizo hilo wakati alipofanya ziara Maalum ya kutembelea eneo lililokabidhiwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Kujenga Ofisi hizo katika eneo la Mji mpya Jijini Dodoma likiwa na ukubwa wa hekta 33.

Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeamua kuhamishia Makao Makuu ya shughuli za Serikali Jijini Dodoma katikati ya ardhi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, uamuzi uliokwenda sambamba na kuzingatia wazo la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alilolitoa mwanzoni mwa miaka ya 60.View attachment 1625922

Ni upumbavu ulio wa juu , yaani hizo taasisi badala ya kujenga kisiwa cha pemba na kuboresha wanajenja Dodoma, hivi Dodoma kuna wazanzibari wangapi?

Hata hizo taasisi za muungano huko pemba hakuna, yaani mfano wizara ya mambo ya ndani, yaani passport mpaka itoke unguja.

Badala ya kujenga Zanzibar wanajenga Tanganyika ni uzuzu wa hali ya juu, Tanganyika ndio ijenge Zanzibar zile wizara za muungano tu. Shame SMZ
 
Makao makuu ya nchi ya Tanganyika yapo wapi? Maana nchi ya Zanzibar mji mkuu wake ni Unguja /Zanzibar.

Hii ni mojawapo ya kero za Muungano kulazimisha nchi ya Zanzibar kuhamishia Ofisi zake katika mji ambao ni makao makuu ya Tanganyika iliyofichwa ktk joho la Muungano.

Dodoma ni makao makuu ya nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ningeshauri Bunge la Muungano wa Tanzania wapeleke makao yake makuu Unguja ili Zanzibar nayo ifaidike kiuchumi kwa shuguli za kimuungano za kufanya vikao vyake vyote Zanzibar na siyo Tanganyika ifaidi kila kitu huku Zanzibar ikisubiri 4% ya mgao wa fedha ambayo ni ndogo kama baadhi ya taasisi taasisi za Muungano zingepeleka makao yake Zanzibar.

Mifano ya faida za kiuchumi kwa Zanzibar ni Nyumba za wabunge wa Muungano zingejengwa Unguja, Ukumbi wa Bunge na sekretariati yake Unguja, boti na ndege kibao zingeenda Unguja, magari ya kukodisha na mafuta n.k yangetumika Zanzibar , wageni wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wangejazana Unguja na kuongeza idadi ya wageni badala ya kutegemea wageni watalii, kazi za udobi, starehe, burudani kuhudumia mamia ya watu wanaoenda Bunge la Muungano likiwa Zanzibar hii ni mifano kiduchu tu Wazanzibari wangefaudu matunda ya Muungano na kelele kupungua
Wakati unaulizia Makao Makuu ya Serikali ya Tanganyika yako wapi, nami nisaidie kunieleza Makao Makuu ya Serikali ya England yako wapi. Natanguliza shukrani.
 
Wakati unaulizia Makao Makuu ya Serikali ya Tanganyika yako wapi, nami nisaidie kunieleza Makao Makuu ya Serikali ya England yako wapi. Natanguliza shukrani.
Miji mingi ya nchi zilizoendelea ipo katika pembezoni ya mito mikubwa mfano Paris mto La Siene, Miji ya Moscow , Berlin, Budapest, Alexandria yote pembezoni ya mto na kuchochea biashara uchumi n.k na mito ya maji ndiyo ilikuwa njia kuu ya usafiri wa kibiashara karne hizo . Pia miji mingi ya nchi zilizoendelea inapatikana katika Pwani za bahari.

Tukirudi kwa faida ya kuwekeza katika miji kuifaidisha nchi , Dodoma haina vigezo vya kiuchumi wala biashara bora uwekezaji wa makao makuu ya dola au Bunge kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ungefanyika Zanzibar na Dar es Salaam .

Jiji la London limekuwa kutokana na kuwa pembezoni mwa mto Thames miaka hiyo mingi iliyopita na kuwezesha kuinufaisha Uingereza kutokana na kuchochea uchumi na biashara siyo tu kwa United Kingdom tu bali hata iliyokuwa Empire ya Uingereza. Au mfano Brasilia vs São Paulo huko Brazil.


Turudi sasa sababu za kiuchumi za Dodoma kuibeba Jamhuri ya Muungano ni hasara kwa nchi zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar.

Hivyo badala ya kurundika kila kitu Dodoma nchini hizi mbili zirudi mezani na kuangalia vipi iwekeze kupitia makao ya dola au Bunge ili kufanya Dar es Salaam na Zanzibar vitovu vya kibiashara Afrika Mashariki na Kati kama enzi za Tipu Tippu au zama hizi Zanzibar iwe kama Dubai kibishara na Dar es Salaam iwe Singapore kuliko kupoteza rasilimali kutengeneza matamanio ya 'makao makuu Dodoma' yanayorudisha nyuma Tanzania ki geopolitics upande wa biashara, uchumi na muungano .

Sweettablet yote kwa yote hoja kubwa ni uhamishaji na uwekezaji makao makuu Dodoma ni hasara kubwa kwa wadau wa muungano wa Tanzania yaani Tanganyika na Zanzibar.
 
Ulinzi!?
Sio kweli tukianza tu kwny ukubwa wa nchi hizi mbili ndani ya jamuhuri moja,pili ulinzi na usalama kwa upana wake,huwezi kuweka viongozi wote wakubwa wa nchi hii kisiwani...hakunaga assumptions kwny swala na ulinzi na usalama!!hata kwa haraka haraka ukifanya S.W.O.T (Strength, Weakness, Opportunities, Threat) Analysis, nakwambia hata mtu mwenye upeo mdogo tu atakwambia hapana,ashakum si matusi kwa sisi watu wa mkojani sheikh wangu,ndg mjumbe hapa umeandika kama mtu aliyekuwa kwny njozi.
Fikra za kizamani Sana hizi!
 
Makao makuu ya nchi ya Tanganyika yapo wapi? Maana nchi ya Zanzibar mji mkuu wake ni Unguja /Zanzibar.

Hii ni mojawapo ya kero za Muungano kulazimisha nchi ya Zanzibar kuhamishia Ofisi zake katika mji ambao ni makao makuu ya Tanganyika iliyofichwa ktk joho la Muungano.

Dodoma ni makao makuu ya nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ningeshauri Bunge la Muungano wa Tanzania wapeleke makao yake makuu Unguja ili Zanzibar nayo ifaidike kiuchumi kwa shuguli za kimuungano za kufanya vikao vyake vyote Zanzibar na siyo Tanganyika ifaidi kila kitu huku Zanzibar ikisubiri 4% ya mgao wa fedha ambayo ni ndogo kama baadhi ya taasisi taasisi za Muungano zingepeleka makao yake Zanzibar.

Mifano ya faida za kiuchumi kwa Zanzibar ni Nyumba za wabunge wa Muungano zingejengwa Unguja, Ukumbi wa Bunge na sekretariati yake Unguja, boti na ndege kibao zingeenda Unguja, magari ya kukodisha na mafuta n.k yangetumika Zanzibar , wageni wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wangejazana Unguja na kuongeza idadi ya wageni badala ya kutegemea wageni watalii, kazi za udobi, starehe, burudani kuhudumia mamia ya watu wanaoenda Bunge la Muungano likiwa Zanzibar hii ni mifano kiduchu tu Wazanzibari wangefaudu matunda ya Muungano na kelele kupungua
Nchi ni moja tuu nayo ni Tanzania

Zanzibar na Tanganyika 'now days Tanzania bara' sio nchi, bali ni sehemu za nchi ya Tanzania

Zanzibar na Tanganyika zilikoma kuwa nchi siku ya kuungana/muungano 'April 26 1964'
 
Ni upumbavu ulio wa juu , yaani hizo taasisi badala ya kujenga kisiwa cha pemba na kuboresha wanajenja Dodoma, hivi Dodoma kuna wazanzibari wangapi?

Hata hizo taasisi za muungano huko pemba hakuna, yaani mfano wizara ya mambo ya ndani, yaani passport mpaka itoke unguja.

Badala ya kujenga Zanzibar wanajenga Tanganyika ni uzuzu wa hali ya juu, Tanganyika ndio ijenge Zanzibar zile wizara za muungano tu. Shame SMZ
Na uhakika mzee Abeid Karume asingekubali maamuzi ya serikali awamu ya Mwinyi Junior ya SMZ kwenda kujenga Dodoma masuala ya muungano. Tayari Tanganyika imefaidi vya kutosha.

Na Mzee Abeid Karume baharia mstaafu aliyesafiri sehemu nyingi ugaibuni angepigania baadhi ya shughuli na majengo ya taasisi za Muungano kuwa na makao yake Zanzibar ili kuchochea uchumi na biashara upande wa Zanzibar badala ya kuwekeza Dodoma kusipo na faida yoyote zaidi ya asilimia 4% ya mgao wa fedha toka kwa waziri wa fedha wa Tanganyika chini ya mwamvuli wa muungano.
 
Nchi ni moja tuu nayo ni Tanzania

Zanzibar na Tanganyika 'now days Tanzania bara' sio nchi, bali ni sehemu za nchi ya Tanzania

Zanzibar na Tanganyika zilikoma kuwa nchi siku ya kuungana/muungano 'April 26 1964'
Nchi za Zanzibar na Tanganyika zitadumu na kuwepo kwani haziwezi kufa, kusema "zilikoma" hayo ni maneno ya kisiasa.

Ila kweli Tanzania inaweza kufa kwa sababu ya kutoona mbali na kufanya maamuzi kumfurahisha mtu mmoja kisiasa zaidi na siyo kwa kuwaridhisha kiuchumi, kibiashara na kijamii zaidi raia wa nchi za Tanganyika na Zanzibar.
 

Ningeshauri Bunge la Muungano wa Tanzania wapeleke makao yake makuu Unguja ili Zanzibar nayo ifaidike kiuchumi kwa shuguli za kimuungano za kufanya vikao vyake vyote Zanzibar na siyo Tanganyika ifaidi kila kitu huku Zanzibar ikisubiri 4% ya mgao wa fedha ambayo ni ndogo kama baadhi ya taasisi taasisi za Muungano zingepeleka makao yake Zanzibar.

Mifano ya faida za kiuchumi kwa Zanzibar ni Nyumba za wabunge wa Muungano zingejengwa Unguja, Ukumbi wa Bunge na sekretariati yake Unguja, boti na ndege kibao zingeenda Unguja, magari ya kukodisha na mafuta n.k yangetumika Zanzibar , wageni wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wangejazana Unguja na kuongeza idadi ya wageni badala ya kutegemea wageni watalii, kazi za udobi, starehe, burudani kuhudumia mamia ya watu wanaoenda Bunge la Muungano likiwa Zanzibar hii ni mifano kiduchu tu Wazanzibari wangefaudu matunda ya Muungano na kelele kupungua
Mawazo yako ni muendelezo wa akili za kipuuzi za Zanzibar kutaka kila kitu, mbili kutaka usawa ilihali kwenye kugharamia kuanzisha na uendeshaji haichangii sawa na mara nyingi haichangii chochote

Hata kwenye biashara kama mtaji hamkuchanga sawa na katika gharama za uendeshaji hamkutoa sawa, faida inapopatikana hamuwezi gawana sawa
 
Miji mingi ya nchi zilizoendelea ipo katika pembezoni ya mito mikubwa mfano Paris mto La Siene, Miji ya Moscow , Berlin, Budapest, Alexandria yote pembezoni ya mto na kuchochea biashara uchumi n.k na mito ya maji ndiyo ilikuwa njia kuu ya usafiri wa kibiashara karne hizo . Pia miji mingi ya nchi zilizoendelea inapatikana katika Pwani za bahari.

Tukirudi kwa faida ya kuwekeza katika miji kuifaidisha nchi , Dodoma haina vigezo vya kiuchumi wala biashara bora uwekezaji wa makao makuu ya dola au Bunge kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ungefanyika Zanzibar na Dar es Salaam .

Jiji la London limekuwa kutokana na kuwa pembezoni mwa mto Thames miaka hiyo mingi iliyopita na kuwezesha kuinufaisha Uingereza kutokana na kuchochea uchumi na biashara siyo tu kwa United Kingdom tu bali hata iliyokuwa Empire ya Uingereza. Au mfano Brasilia vs São Paulo huko Brazil.


Turudi sasa sababu za kiuchumi za Dodoma kuibeba Jamhuri ya Muungano ni hasara kwa nchi zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar.

Hivyo badala ya kurundika kila kitu Dodoma nchini hizi mbili zirudi mezani na kuangalia vipi iwekeze kupitia makao ya dola au Bunge ili kufanya Dar es Salaam na Zanzibar vitovu vya kibiashara Afrika Mashariki na Kati kama enzi za Tipu Tippu au zama hizi Zanzibar iwe kama Dubai kibishara na Dar es Salaam iwe Singapore kuliko kupoteza rasilimali kutengeneza matamanio ya 'makao makuu Dodoma' yanayorudisha nyuma Tanzania ki geopolitics upande wa biashara, uchumi na muungano .

Sweettablet yote kwa yote hoja kubwa ni uhamishaji na uwekezaji makao makuu Dodoma ni hasara kubwa kwa wadau wa muungano wa Tanzania yaani Tanganyika na Zanzibar.
Nakushuru lakini bado hujajibu swali langu. Makao makuu ya England yako wapi?
 
Back
Top Bottom