Ujenzi wa nyumba za kuficha paa/contemporary/ hidden roof

Ukisoma changamoto ambazo wengi wanasema hapa ni uwezekano wa kuvuja kwa paa! Binafsi ningependa kufahamishwa ni kwanini hii ni changamoto ya aina hii ya ujenzi, na Kwa namna gani inatatulika? Kwa wajuzi/wataalam wa ujenzi, naomba msaada.
 
Kwa utafiti wangu mdogo nimeufanya, wengi wanaosema hazifai wapo na maneno ya kuambiwa. Hawajawahi hata kujenga hizo nyumba. Ni kama wale wanaokwambia usinunue Nissan haifai kabisa, ukiuliza kama amewahi hata kumiliki utagundua ni maneno ya kijiweni.

Nakubaliana na wanaosema tatizo ni mafundi. Nyumba hizi zinahitaji fundi anayezijua. Tatizo lipo kwa wenye nyumba, unamuamini fundi aliyekufanyia kazi za tofali akuezekee na bati tu kwa sababu gharama amefanya ndogo.

Contemporary ni zaidi ya kuezeka na mafundi wazuri wapo.
 
Unamawazo kama yangu mkuu nilikuwa najiuliza hapa
Inawezekana pia lakini bado utahitaji kui treat juu ya hiyo slab, utahitaji membrane cloth na bitumen nyeupe ili kuzuia unyevu hasa kipindi cha mvua za muda mrefu
Na vipi ukiamua kupiga zege badala ya kuweka bati dizain kama zile nyumba za wagogo ambazo zinajengwa kwa tope mwanzo mwisho hadi kuezeka?
 
Bro umeongea yote;
Iko hivi: nyumba hii inahitaji myaalam ambaye anajua namna ya kuanza hadi kumaliza.
Wengi anampa fundi wa kujenga tofali then analeta mwingine wa kuezeka....

Hii nyumba inajengwa na mtaalam mmoja mwanzo hadi mwisho.

Chukua haya yafuatayo;
1. Msingi uinuke
2. Boma liwe na tofali laini 11
3. Baada ya lenta hakikisha unatengeneza sehemu ya kupokelea maji
4. Pawepo na ducts za kupitishia maji na sio bomba
5. Upake bitumen pamoja na mebrane cloth maeneo ya wazi ya kupokelea maji.

6. Epuka slop ndefu za paa bali livunje vunje vipande vipande ili maji yashukie sehemu tofauti

Ukizingatia haya nyumba hii hsivuji na utaifurahia na haina gharama kubwa
Kwa utafiti wangu mdogo nimeufanya, wengi wanaosema hazifai wapo na maneno ya kuambiwa. Hawajawahi hata kujenga hizo nyumba. Ni kama wale wanaokwambia usinunue Nissan haifai kabisa, ukiuliza kama amewahi hata kumiliki utagundua ni maneno ya kijiweni.

Nakubaliana na wanaosema tatizo ni mafundi. Nyumba hizi zinahitaji fundi anayezijua. Tatizo lipo kwa wenye nyumba, unamuamini fundi aliyekufanyia kazi za tofali akuezekee na bati tu kwa sababu gharama amefanya ndogo.

Contemporary ni zaidi ya kuezeka na mafundi wazuri wapo.
 
Mimi nimeanza msingi baada ya mwaka ama miaka miwili nikishajichanga changa napandisha boma. Kwa kuwa nimeipenda ya huko mbele sijui mvua na jua,joto,gharama za finishing potelea pote nitaienga hata kwa miaka 10 mana nimeipenda mwenyewe
Hakikisha kwenye mdingi unaanda matoleo ya maji mkuu
 
Nyumba hizi zinahitaji mtaalam hasa wa kujenga ,pia finisha n urembo inapendezesha sana ,nyumba hizi zinapendeza hasa ikiinuka yaani msingi uwe juu kwa nyumba ya chini ,ila kwa ghorofa zinapendeza sana.

Ila mademu wengi wanapenda nyumba za kuonekana PAA.
Uko sahihi, nimeandika hapo juu pia
 
Uwe unawaambia pia kwamba zinahitaji kemikali maalumu kuunga paa na kuta zisivuje.

Pia uwaeleze kwamba kwa kuwa hazina roof overhang zinahitaji kupakwa rangi maalumu ambazo zitahimili jua na mvua/unyevu kwa kuwa kutazake zina direct contact na jua na mvua tofauti na traditional houses

La mwisho uwaeleze wateja wako kwamba hizo nyumba mara nyingi zinakuwa na extra costs Ili zipendeze yaani makuta kuta,maurembo mengi na finishing ya nguvu.Kiufupi gharama za ufundi ni kubwa zaidi kuliko nyumba za kawaida.

Mwisho wa siku unakuta ule unafuu wa gharama ya paa ume offset kwenye finishing tena ya nje ambapo on average zina gharama kubwa kuliko nyumba za kawaida.

All in all ni nyumba nzuri kama una pesa ila kama pesa ya kuunga bora ujenge traditional houses
Asante kwa ufafanuzi... binafsi nazipenda sana ila sioni unafuu wake
 
Asante kwa ufafanuzi... binafsi nazipenda sana ila sioni unafuu wake
Nyumba hizi ni nafuu sana kwa upande wa paa...bati na mbao.
Kitu kinachoongeza gharama ni urembo tu.

Kimsingi mtu mwenye uelewa sahihi urembo mwingi huharibu mwonekano wa nyumba hizi.

Jambo muhimu ni;
1. Msingi mrefu...nyumba iinuke
2. Madirisha makubwa
3. Urembo kiasi/ plain design inapendeza zaidi
 
Ukisoma changamoto ambazo wengi wanasema hapa ni uwezekano wa kuvuja kwa paa! Binafsi ningependa kufahamishwa ni kwanini hii ni changamoto ya aina hii ya ujenzi, na Kwa namna gani inatatulika? Kwa wajuzi/wataalam wa ujenzi, naomba msaada.
Soma hapa mkuu
Bro umeongea yote;
Iko hivi: nyumba hii inahitaji myaalam ambaye anajua namna ya kuanza hadi kumaliza.
Wengi anampa fundi wa kujenga tofali then analeta mwingine wa kuezeka....

Hii nyumba inajengwa na mtaalam mmoja mwanzo hadi mwisho.

Chukua haya yafuatayo;
1. Msingi uinuke
2. Boma liwe na tofali laini 11
3. Baada ya lenta hakikisha unatengeneza sehemu ya kupokelea maji
4. Pawepo na ducts za kupitishia maji na sio bomba
5. Upake bitumen pamoja na mebrane cloth maeneo ya wazi ya kupokelea maji.

6. Epuka slop ndefu za paa bali livunje vunje vipande vipande ili maji yashukie sehemu tofauti

Ukizingatia haya nyumba hii hsivuji na utaifurahia na haina gharama kubwa
 
Nyumba hizi ni nafuu sana kwa upande wa paa...bati na mbao.
Kitu kinachoongeza gharama ni urembo tu.

Kimsingi mtu mwenye uelewa sahihi urembo mwingi huharibu mwonekano wa nyumba hizi.

Jambo muhimu ni;
1. Msingi mrefu...nyumba iinuke
2. Madirisha makubwa
3. Urembo kiasi/ plain design inapendeza zaidi
Umelenga mulemule mkuu.
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom