Ujenzi wa nyumba ya vyumba sita kwa lengo la kupangisha ni sawa na biashara ya reja reja

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
1645609367330.jpeg
Nyumba hizi hujengwa nyumba vikiangaliana, ni ujenzi maarufu katika nchi nyingi za Afrika. Choo, bafu na jiko la jumuia hukaa katika vyumba vya nyuma. Siku hizi wengi hupikia majiko ya gesi hivyo chumba cha jiko hutumiwa na wachache wale wa kupikia kuni au wanao kaanga samaki.

Biashara hii ni sawa na duka la reja reja, inategemea sehemu ulipo, chumba chenye gypsum umeme, maji, madirisha ya aluminium hufika 70,000 - 80,000 kama nyumba iko karibu na mjini, au usafiri wa kwenda mjini si shida. Kwa sehemu za uchochoroni chumba huwa 30,000- 40,000.

Uzuri wa biashara hii ni kwa mwisho wa mwezi ni lazima utakusanya kodi. Changamoto inakuja kwa wapangaji wa muda mrefu mnakua mmezoeana na anapokosa hela ya kodiwkumfuka unashindwa. Wengine wanakueleza wanauguliwa, ada za watoto au wamefukuzwa kazi.

Changamoto nyingine ni idadi ya watu wanaokaa na kutumia miundo mbinu. Wengi wanaopanga nyumba hizi ni wa kipato cha chini. Unakuta mpangaji anauguliwa na mjomba wake na ukoo wao wote wako pale kuuguza. Hawafikiri maji, choo hasa kama ni choo cha shimo. Nyumba ya jirani choo kikijaa, mwenye nyumba anaweza kuomba watumie chako mpaka atakaporekebisha mambo kwake. Uswahilini maisha ni kusaidiana.

Ujenzi wa chumba na sebule ni advance na unatishia soko la wenye vyumba sita. Wakijiongeza watakao jenga simple one bedroom self contained nao watatishia soko la chumba na sebule.
 
Ni idea nzuri.... cha muhimu kwenye biashara ya upangishaji ni simplicity. Nyumba ya kupangisha isizidi vyumba viwili vya kulala.... piga chumba sebule au maximum vyumba viwili na sebule. Wapangaji wengi wapo kwenye range ya 100,000 mpaka 250,000. Kuanzia 300,000 kwenda juu, ni wachache na muda si mrefu huwa wanajenga zao.
 
Ni idea nzuri.... cha muhimu kwenye biashara ya upangishaji ni simplicity. Nyumba ya kupangisha isizidi vyumba viwili vya kulala.... piga chumba sebule au maximum vyumba viwili na sebule. Wapangaji wengi wapo kwenye range ya 100,000 mpaka 250,000. Kuanzia 300,000 kwenda juu, ni wachache na muda si mrefu huwa wanajenga zao.
We piga 100,000 mpaka 150000 tu. Ikizidi hapo ni wakutafuta sana.

Bachelor life na wale wanaoanza maisha kipato bado kinakuwa kidogo
 
Back
Top Bottom