Ujenzi wa Miradi hii Bagamoyo ni wa Lazima Kiasi Hiki?

bandari ya mtwara ndio yenye kina kirefu tz nadhani hulijui hilo

Ndugu yangu usiligeuza suala hili muhimu la kiuchumi kuwa la kisiasa. Umuhimu wa bandari kwa uchumi wa Tanzania hauna ubishi. Yapo mambo ya msingi muhimu kufahamika:
Bandari ya Dar imeelemewa kwasababu ya wingi wa mizigo inayopitia katika bandari hiyo ndio maana kuna foleni za meli kuingia hapo Bandarini. Kuelemewa huko, kunasabasha jiji kuzidiwa na wingi wa magari ya mizigo na abiria (traffic congestion) yanayoingia na kutoka Bandarini. Zipo jitihada za kufanya upanuzi wa bandari hiyo kwa kujenga gati mpya no 13 na 14. Upanuzi huo ni suluhu ya muda mfupi katika handling ya mizigo, lakini hakutoa suluhu ya tatizo la congestion jijini....sana sana utaongeza congestion. Ni kwa msingi huo ujenzi wa bandari mpya ni jambo la muhimu.

Kwanini Bagamoyo?
Eneo la ujenzi wa bandari la Bagamoyo, lina kina kirefu na mlango mpana wa kuingizia meli zitakazohitaji kutia nanga. Hizo ni sifa kubwa zinazopelekea interest ya Wawekezaji wa sekta ya bandari kupendelea kuwekeza kule. Miaka 20 ijayo, meli zitakazojengwa zitakuwa ni 4th Generation zenye size kubwa kwa ajili ya kubeba mizigo mingi. Meli hizo hazitoweza kuingia kwenye lango la bandari ya Dar es salaam unless lifanyike zoezi la kupanua mlango wa bandari na kuchimba zaidi kuongeza kina....jambo ambalo itabidi kuchimba eneo kubwa mpaka ilipo Ikulu. Bandari ya Tanga na ile ya Mtwara vilevile zina disadvantage ya kutokuwa na Kina kikubwa kinachotakiwa kwa ajili ya hizo 4th generation ships. Sisemi kwamba haziwezi kutengenezwa zika accomodate meli za aina hiyo, la hasha. Inawezekana, lakini kwa gharama kubwa. Hivyo mtu anayetaka kuwekeza kwenye bandari ni rahisi zaidi kuwekeza Bagamoyo kule eneo lingine.

Lakini pia,duniani kote, bandari huwa zinafanya vizuri panapokuwa na eneo la Export Processing Zone na miundombinu mingine. Kule Bagamoyo next to eneo la BandAri, kuna eneo kubwa la mamlaka ya EPZA kwa ajili ya viwanda vya uzalishaji kwa ajili ya mauzo ya nje. Hivyo, muwekezaji yoyote mwenye kutaka kuwekeza kwenye bandari, atavutiwa kuwekeza kwenye bandari iliyo karibu na EPZ.

Tatu biashara ya bandari inahitaji kuwa karibu na eneo la biashAra (Business/commerical district) kwa ajili ya kuwezesha transactions mbalimbali. Kwa TZ commercial district ipo Dar es salaam. Hivyo muwekezaji wa bandari ata prefer kwenda bagamoyo iliyopo karibu na Dar kuliko mahala pengine. Lakini pia, Bagamoyo ina potential ya kutengeneza new business district.

Mtwara
Bandari ya Mtwara ipo sorted. Wale investors wa kuchimba gesi wameshaelezea nia yao ya kuitumia bandari ile kama sehemu ya usafirishaji wa gesi. Pia tayari eneo la uzalishaji wa viwanda karibu na bandari limechukuliwa na makampuni yatakayowekeza kwenye viwanda vya kuzalisha mbolea kwa kutumia gesi, na makampuni mengine ya uzalishaji wa cement kama lile la Dangote......hivyo, investor mpya anayekuja sasa, hawezi kuwa na interest na Mtwara kwani tayari kuna strategic investors wa bandari ile.

TANGA
Tanga itaendelezwa soon kwa hesabu za kuitumia ku serve eneo la kaskazini, na pia ni altenative ya Mombassa na pia inahitajika na waganda. Mipango yake ipo. Soon utaona nayo inashughulikiwa.
 
"Bandari ya Dsm imeelemewa na bado nchi nyingi za jirani zinahitaji kutumia bandari zetu hapa Tz,hivyo serikali ina mpango wa kujenga bandari ya kisasa huko Bagamoyo hili kukabiliana na changamoto hii".
Nimeshtushwa kuisikia hii kauli kuto kwenye kinywa cha waziri na viongozi mbalimbali ktk taarifa ya habari ITV huku waziri mkuu akiwepo,walikuwa wanaongea na wachina ambao wanategemea kuchukua hilo dili.Hii nchi sijui tunaipeleka wapi,hivi tuna haja kweli ya kuingia garama kubwa ya ujenzi wa Bandari ilhali tuna Bandari kubwa huku Mtwara ama pale Tanga?.Naanza kuingiwa na mashaka na hii plan B ya kuipeleka gas yetu Bagamoyo kwa kigezo cha kuwa inakwenda kutumiwa na viwanda vikubwa vinavyotarajiwa kujengwa huko,kwa nini isiwe Mkuranga?.

Kwa nn kila kitu siku hizi ni Bagamoyo?,hivi viongozi wetu hamlioni hili?.Msitulazimishe tuanze kuangaliana kibaguzi ktk nchi ambayo haikuwa na hivi vitu vinavyopandikizwa sasa.Kama waliopita wangekuwa na hurka za ubinafsi kama hizi basi Butiama,Lupaso na Dole yangekuwa majiji muda huu.
Wacha ushabiki siyo kila kitu kinachofanyika bagamoyo ni cha upendeleo.
Kwa taharifa yako Bagamoyo inakuwa Free Economic Zone, ambayo inahitaji miundombinu kuliko uko Kigamboni ambapo kuna daraja la mabillioni wanaopelekewa watu wasiozidi 300,000.
 
Yapo mengi kwenye andiko lile ila Nadhani kwa haya machache uamuzi ni wa kupigiwa saluti. Huwa siungi mkono serikali ila kwa hili MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI.

HEKO SERIKALI
Vyovyote itakavyokuwa si haba. Bandari itainufaisha nchi kwa ujumla wake

Ila siku nyingine tuwe makini sana na hawa viongozi wetu. Ninachoona kwa JK ni upwani(umwinyi) hapo akistaafu mbona atakuja kutamba kwa wakwere wenzake kwamba "Nkapa kaifanyia nini Masasi, Mchonga kaifanyia nini Butiama, Mwinyi kaifanyia nini?"...er...eer...wapi? Mkuranga?
Tena JK atakuja hata kusema Nkapa ni bure kabisa badala ya kujenga kwao kajenga Lushoto!
 
Kama great thinker ungehoji ni vipi bandali ioanuliwe mpaka ikulu? Kweli una amini hilo?
Mbili nimesoma tokea mtoto kuwa bandali ya kina kirefu ni Mtwara, iweje leo aja ukuongopee na wewe hukubali?


Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums

To be a great thinker you also need to be a great reader, otherwise you will be thinking on the abstract. Kibanga nina mashaka kama umesoma vizuri nilichoandika.....hakuna mahala nimetamka eneo la Bagamoyo lina kina kirefu kuliko Mtwara. Nilichofanya ni kuorodhesha factors zilizo influence investor kuna interested na bagamoyo. Urefu wa kina ni moja ya factors uki benchmark na eneo lingine ambalo lina other comparable advantages (namaanisha bandari ya dar es salaam). Kuna mahala nimefanya comparison ya vina vya dar na bagamoyo with data! N takwimu hizo ndio zinatumiwa na wenye interest ya kuwekeza......na sio Kibanga alisomeshwa toka mtoto kwamba Bandari ya Mtwara ndio yenye kina kirefu. Mambo haya yanaangaliwa holistically, sio kushika factor moja na kuibebea bango.
 
Kwanini Bagamoyo?
Eneo la ujenzi wa bandari la Bagamoyo, lina kina kirefu na mlango mpana wa kuingizia meli zitakazohitaji kutia nanga. Hizo ni sifa kubwa zinazopelekea interest ya Wawekezaji wa sekta ya bandari kupendelea kuwekeza kule. Miaka 20 ijayo, meli zitakazojengwa zitakuwa ni 4th Generation zenye size kubwa kwa ajili ya kubeba mizigo mingi. Meli hizo hazitoweza kuingia kwenye lango la bandari ya Dar es salaam unless lifanyike zoezi la kupanua mlango wa bandari na kuchimba zaidi kuongeza kina....jambo ambalo itabidi kuchimba eneo kubwa mpaka ilipo Ikulu. Bandari ya Tanga na ile ya Mtwara vilevile zina disadvantage ya kutokuwa na Kina kikubwa kinachotakiwa kwa ajili ya hizo 4th generation ships.

.

Kwenye red: Naomba nitofautiane na wewe. Bagamoyo ina kina kifupi sana compared na Dar es Salaam. Mwanzoni nilikuwa nadhani wanataka kujenga Bandari-kavu maana Bagamoyo wana kina cha sinia - shallow. Na kama kweli mpango ni kujenga bandari itakayoweza kumudu meli kubwa - 4th generation basi mradi utakuwa extremely expensive, and that questions the wisdom of having such an expensice project wakati kina kirefu tayari kiko 40 -50 km away (Dar)!

Naungana na wanaosema kuwa mpango hapa ni kugeuza Bagamoyo iwe kama Dubai - sina tatizo na hilo ila swali ninalojiuliza kipi bora, kupanua kwanza Bandari ya Dar na kuimarisha reli au ku-divert resources kwenye mradi mpya wa Bandari?

Bandari ya Bagamoyo ingefuata baada ya kupanua hii ya Dar.
 
Vyovyote itakavyokuwa si haba. Bandari itainufaisha nchi kwa ujumla wake

Ila siku nyingine tuwe makini sana na hawa viongozi wetu. Ninachoona kwa JK ni upwani(umwinyi) hapo akistaafu mbona atakuja kutamba kwa wakwere wenzake kwamba "Nkapa kaifanyia nini Masasi, Mchonga kaifanyia nini Butiama, Mwinyi kaifanyia nini?"...er...eer...wapi? Mkuranga?
Tena JK atakuja hata kusema Nkapa ni bure kabisa badala ya kujenga kwao kajenga Lushoto!

Labda wangeijengea karatu hiyo bandari,kwanza ni karibu na mlima kilimanjaro.
 
Ndugu yangu usiligeuza suala hili muhimu la kiuchumi kuwa la kisiasa. Umuhimu wa bandari kwa uchumi wa Tanzania hauna ubishi. Yapo mambo ya msingi muhimu kufahamika:
Bandari ya Dar imeelemewa kwasababu ya wingi wa mizigo inayopitia katika bandari hiyo ndio maana kuna foleni za meli kuingia hapo Bandarini. Kuelemewa huko, kunasabasha jiji kuzidiwa na wingi wa magari ya mizigo na abiria (traffic congestion) yanayoingia na kutoka Bandarini. Zipo jitihada za kufanya upanuzi wa bandari hiyo kwa kujenga gati mpya no 13 na 14. Upanuzi huo ni suluhu ya muda mfupi katika handling ya mizigo, lakini hakutoa suluhu ya tatizo la congestion jijini....sana sana utaongeza congestion. Ni kwa msingi huo ujenzi wa bandari mpya ni jambo la muhimu.

Kwanini Bagamoyo?
Eneo la ujenzi wa bandari la Bagamoyo, lina kina kirefu na mlango mpana wa kuingizia meli zitakazohitaji kutia nanga. Hizo ni sifa kubwa zinazopelekea interest ya Wawekezaji wa sekta ya bandari kupendelea kuwekeza kule. Miaka 20 ijayo, meli zitakazojengwa zitakuwa ni 4th Generation zenye size kubwa kwa ajili ya kubeba mizigo mingi. Meli hizo hazitoweza kuingia kwenye lango la bandari ya Dar es salaam unless lifanyike zoezi la kupanua mlango wa bandari na kuchimba zaidi kuongeza kina....jambo ambalo itabidi kuchimba eneo kubwa mpaka ilipo Ikulu. Bandari ya Tanga na ile ya Mtwara vilevile zina disadvantage ya kutokuwa na Kina kikubwa kinachotakiwa kwa ajili ya hizo 4th generation ships. Sisemi kwamba haziwezi kutengenezwa zika accomodate meli za aina hiyo, la hasha. Inawezekana, lakini kwa gharama kubwa. Hivyo mtu anayetaka kuwekeza kwenye bandari ni rahisi zaidi kuwekeza Bagamoyo kule eneo lingine.

Lakini pia,duniani kote, bandari huwa zinafanya vizuri panapokuwa na eneo la Export Processing Zone na miundombinu mingine. Kule Bagamoyo next to eneo la BandAri, kuna eneo kubwa la mamlaka ya EPZA kwa ajili ya viwanda vya uzalishaji kwa ajili ya mauzo ya nje. Hivyo, muwekezaji yoyote mwenye kutaka kuwekeza kwenye bandari, atavutiwa kuwekeza kwenye bandari iliyo karibu na EPZ.

Tatu biashara ya bandari inahitaji kuwa karibu na eneo la biashAra (Business/commerical district) kwa ajili ya kuwezesha transactions mbalimbali. Kwa TZ commercial district ipo Dar es salaam. Hivyo muwekezaji wa bandari ata prefer kwenda bagamoyo iliyopo karibu na Dar kuliko mahala pengine. Lakini pia, Bagamoyo ina potential ya kutengeneza new business district.

Mtwara
Bandari ya Mtwara ipo sorted. Wale investors wa kuchimba gesi wameshaelezea nia yao ya kuitumia bandari ile kama sehemu ya usafirishaji wa gesi. Pia tayari eneo la uzalishaji wa viwanda karibu na bandari limechukuliwa na makampuni yatakayowekeza kwenye viwanda vya kuzalisha mbolea kwa kutumia gesi, na makampuni mengine ya uzalishaji wa cement kama lile la Dangote......hivyo, investor mpya anayekuja sasa, hawezi kuwa na interest na Mtwara kwani tayari kuna strategic investors wa bandari ile.

TANGA
Tanga itaendelezwa soon kwa hesabu za kuitumia ku serve eneo la kaskazini, na pia ni altenative ya Mombassa na pia inahitajika na waganda. Mipango yake ipo. Soon utaona nayo inashughulikiwa.

Nimeacha kukusona na kukuona unapiga POROJO pale uliposema kwamba sababu mojawapo ya kujenga bandari Bagamoyo ni kina kirefu compared to Mtwara and Tanag. Please give me a break! Bagamoyo iwe na kina kirefu kuliko Mtwara hata mtu ambaye hakusoma oceanography lakini anajua geography atajua this is a damn lies.

Pili eti Bagamoyo kwasababu kuna EPZA ndiyo maana wanajenga bandari! Please kaandika hayo maneno FB. Hivi hujui Tanga kuna eneo la EPZA? hadi leo wanannchi wa Kange waliochukuliwa ardhi yao kwaajili ya EPZA hawajalipwa?!

Kama hivi ndiyo mmejipanga kujibu hoja za CDM, then you have a far way to go!

Mark my word Bandari ya Bagamoyo is another WHITE ELEPHAT PROJECT. Hakuna masuala ya kiuchumi wala nini ni kutaka kumfurahisha JK tu.
 
Kwenye red: Naomba nitofautiane na wewe. Bagamoyo ina kina kifupi sana compared na Dar es Salaam. Mwanzoni nilikuwa nadhani wanataka kujenga Bandari-kavu maana Bagamoyo wana kina cha sinia - shallow. Na kama kweli mpango ni kujenga bandari itakayoweza kumudu meli kubwa - 4th generation basi mradi utakuwa extremely expensive, and that questions the wisdom of having such an expensice project wakati kina kirefu tayari kiko 40 -50 km away (Dar)!

Naungana na wanaosema kuwa mpango hapa ni kugeuza Bagamoyo iwe kama Dubai - sina tatizo na hilo ila swali ninalojiuliza kipi bora, kupanua kwanza Bandari ya Dar na kuimarisha reli au ku-divert resources kwenye mradi mpya wa Bandari?

Bandari ya Bagamoyo ingefuata baada ya kupanua hii ya Dar.

Naomba usubstantiate argument yako with data. Mie nimetoa za kwangu, naomba na wewe utoe za kwako ili ukweli ufahamike. Otherwise tutakuwa tunapiga porojo
 
Nimeacha kukusona na kukuona unapiga POROJO pale uliposema kwamba sababu mojawapo ya kujenga bandari Bagamoyo ni kina kirefu compared to Mtwara and Tanag. Please give me a break! Bagamoyo iwe na kina kirefu kuliko Mtwara hata mtu ambaye hakusoma oceanography lakini anajua geography atajua this is a damn lies.

Pili eti Bagamoyo kwasababu kuna EPZA ndiyo maana wanajenga bandari! Please kaandika hayo maneno FB. Hivi hujui Tanga kuna eneo la EPZA? hadi leo wanannchi wa Kange waliochukuliwa ardhi yao kwaajili ya EPZA hawajalipwa?!

Kama hivi ndiyo mmejipanga kujibu hoja za CDM, then you have a far way to go!

Mark my word Bandari ya Bagamoyo is another WHITE ELEPHAT PROJECT. Hakuna masuala ya kiuchumi wala nini ni kutaka kumfurahisha JK tu.

Naona great thinkers wameacha kuangalia mambo holistically na ku switch kwenye argument za mtaani kama za Simba na Yanga. Suala la kina cha bagamoyo ni only one of the factors zilizo influence mwekezaji kuwa na interest ya bagamoyo na sio Dar es salaam. Zipo factors nyinginezo ambazo naona mnazi ignore kwenye majibu yenu. Na isitoshe, kama umesoma vizuri nilivyoandika, hakuna mahala nimesema Bagamoyo ina kina kirefu kuliko mtwara......

Na mwisho kabisa, let us not confuse things hapa.......hii bandari hata ikiwa ni white elephant....sisi kama nchi hatutakuwa na hasara hata ya senti moja......this is private capital invested on PPP basis.

Na ni matakwa ya anayewekeza pesa yake, aende wapI......sio matakwa yangu, au yako au ya serikali.......... Tukisema hatuna interrest ya kuwekeza Bagamoyo, basi ataamua kwenda zake pengine popote.....Kenya....na sisi tutabaki kuwasifia wakenya, na kujilaumu.....maana tumezoea kuona post za kusifia flyover za Kenya, mradi mkubwa wa bandari ya Lamu wa Kenya, etc etc
 
Shida yetu watanzania tupo very persimistic na hatupendi kufanya utafiti kabla ya kuaza kulaumu na kuwa na negative opinion. Kujibia swali lako, hizo details za kodi itaanza kutozwa lini ndio zitajulikana kwenye mazungumzo baina ya Serikali na Mwekezaji. Bahati nzuri sheria za PPP zimeweka bayana mwongozo wa nini cha kufanyika. Definately Serikali itapata mrahaba, kodi ya ardhi, hisa katika mradi(ikiamua kununua) na kubwa zaidi ajira kwa vijana wasiopungua 2000 katika bandari hiyo mpya.
Mikataba ya aina hii Tanzania haitokuwa ya kwanza kuingia. Singapore majuzi wamejenga bandari mpya na ya kisasa kwa utaratibu huu. sri-Lanka (Colombo South Container Terminal) na Uturuki vilevile (Mersin Container Port), Uingereza-Great Yarmouth Terminals.....hii ni mifano michache tu ya karibuni.....chukua muda ku google usome zaidi kuhusu miradi hiyo upate kuelewa.
Wakati najaribu kufikiria jinsi ya kukuuliza maslahi yako kiasi gani.Nianze na haya:
Vijana wanaweza pewa kazi ahta milioni moja ,ila jumla ya mishahara yao haifikii wafanyakazi 30 wa kigeni.Kati ya hao watu na CCM panaweza kuwa na tofauti sana ktk kuangalia rushwa.UK, ni wazi hela haiwezi toka kirahishi, hao akina malaysia na singapore kunaweza kuwa na mengi sana yatakayoibulia kadii siku zinpokwenda,Sijui mtaweza reverse mlichohubiri sana.Mramb nae alisema kwa comfidence sana rais lazima anunuliwe ndege hata kama tutakula nyasi.Yeye alijiamini kuwa itaokoa hela nyingi, sijui na usalama wa rais.Kumbe ni wahuni tuu waliiweka mashinikizo jamaa akapewa sababu za kufurahisaha akageuka kuwa useful idiot.Sri Lanka na Malaysia ni mojawapo ya jamii zilizogawanyika ktk makundi makubwa yenye kumilikiwa na wahindi, pamoja na Wachina na wanayofanya yapo very ugly.
Kuhusu suala la mkataba utakuwa ni wa miaka mingapi litakuwa determined na uwekezaji utakayofanyika na muda wa return of investment utakaokadiriwa kwa kuzingatia vigezo mbalimbali vya kiutaalam wa masuala ya fedha na biashara. Ofcourse the more money invested, the longer it may take kurejesha faida. Ipo mifano kadhaa inayoweza kutupa picha..mfano uwekezaji wa treni iendayo kasi kutoka Uingereza kwenda Ufaransa (The Channel Tunnel) iliyojengwa kwa utaratibu huu wa PPP..iligharimu kiasi cha USD 10billion...mkataba wa miaka 55 (google taarifa hizi zipo wazi); mradi wa Mersin Container Terminal huko Uturuki umegharimu USD 755 Million na wameingia mkataba wa miaka 36, kule Pakistan wamejenga Quasin Container International Terminal 2 kwa USD 211 na wameingia mkataba wa miaka 21. Nimekupa mifano hiyo ili upate picha kwamba miaka ya mkataba inategemea aina ya uwekezaji- returns, na mambo mengine. Tanzania haitokuwa ya kwanza, na tusiwadanganye watu na cheap arguments za kuwaonyesha kwamba tunaibiwa n.k

CCM hadi sasa haijaweza toka ktk kitanzi cha rushwa, si nje yake tuu hata ndania yake watu wanalizwa.CCM hawajawahi fanya mradi successfull hata mmoja.SI machinaga complex, uwanja wa Taifa wala rel ya kati, wawekezaji wote kutoa wa bia wamekuwa disappointment.

Hizo nchi unazotaka jilinganisha nao, niambatanisha nao kwao rushwa ni kitu hakilindwi na dola na kuwajibika ni kukubwa sana.Na nyingine zipo katk amargin mbaya, pakistani ni very crrupt country na imeshikiliwa na wahuni wa usalama na jeshi
Hoja unayotoa kwamba vijana watanzania watafaidi leftovers na kwamba project za namna hii ni za kuzipora nchi masikini pesa nyingi kwakweli ni ya kisiasa zaidi. Why are you so persimistic kwenye mambo makubwa na ya kuleta maendeleo nchini?
Labda nikuulize, wewe ulitaka nini kifanyike? Pasijengwe kitu? Tubakie tu na umasikini....miradi isifanyike,ajira zisitengenezwe watanzania wenzako wasipate fursa?
Shida ya baadhi yetu, tushajiset na "maisha bora" ya ughaibuni, hatupendi kuona nchi yetu inaendelezwa kwa miradi mikubwa ili ndugu zetu tuliowaacha Nyumbani nao maisha yao yanaboreka kama sisi....
Nenda migodini, nenda Vodacom, nenda international schools,nenda makamapuni ya utalii, nenda haya EAC,nenda hata ICTR uone kazi zenye hela nyingi kabisa wato watanzania wangapi?Internationala school wapo wanaolipa walimu hadi milion 10, watanzania wanaofuatia ni million 2 tena kwa kozi kama kiswahili, wengine hata wakiwa na masters wanapewa hela chini la laki 7 bila nyumba, wla elimu kwa watoto.Yule mtoto wa Remmy Ongala mama yake angekuwa mtanzania halafu akafanya kazi IST yule kijana angesoma shule nyingine.

Hao investors wanajua hamjui mambo mnayoyaingia ndio maana wanachofanya ni kuwapandisha ego, kuwafanya muwe naive and excited ahalafu wanwatungua, mkija amka mnajikuta mikataba kama ya Tanesco.JK hii itasound vizuri sana kwake, kwa mjini mfu wa bagamoyo, kwa Zitto naye itakuwa ni habari nzuri kwani ni mojawapo ya watu walio too naive.Na itakuwa ni story inayosync ni fikra zake na hivyo kumfanya ajione kuwa ni sahihi.

Bagamoyo wanaihitaji kwa vile itakuwa na control ndogo sana ya serikali na safety kwa raia linapokuja suala la kusafirisha madini hatari kama uraniaum, silaha, magogo etc.Hata hawa mafisadiw etu si smart ebough kupata share kubwa ktk huo uwekezaji kw ahela walizotuibia.

Kwa ujumla hamuwezi fanya kitu acheni blah blah.
Miradi ya aina hii tuii structure vizuri (win-win) itakuwa na impact kubwa.....pengine hata mliopo mtoni mnaweza kurejea nchini kupata ajira zenye ujira unaofana na huo mnaopata ughaibuni. Kitu ambacho tungetegemea kutoka kwenu, ni kufanya utafiti huko mlipo project za aina hii zimekuwa structured vipi, nchi mlizopo zinafaidika vipi? Wale ambao wameingia kwenye such arrangement wakapata matatizo, walikosea wapi ili sisi tusirudie makosa yao.....etc etc......hayo ndio mambo ya kizalendo ya kufanya sio kuponda tuuuuuu haisaidii. Sisi tupo hodari kusifia vya wenzetu na kuponda vyetu....we need to change that negative attitude ili tuendelee

Nani kakuambia CCM walishawahi sema chochote ni kibaya, kila siku huwa inajichekesha na kusema mikataba yenye maslahi kwa taifa.Watu hawana negotiation skills watafanya nini?Membe mwenyewe hata ktk diplomasia ya kisiasa hawezi negotiate, itakuweje diplomasia ya kibiashara, etc.JK kapewa suti kafanya asichokijua, je akipewa nyumba california, au dubai?Atakuwa excited kama Yule mze wa coming to America.

Utakuwa na fikra nyembamba sana ukidhani mimi nikipewa kazi ya kulipwa $300,000/PM halafu kuwe na watanzania wenzangu wanalipwa $1,000PM kushuka chini na Jumla yao naikata kwa kiasi kikubwa , na wengine wa kigeni wanalipwa zaidi kwa sana, huku visingizio vikiwa ni specials skills, exporsure na Sijui kuw ana share.

Project ni risk kwa rasilimali asili na watu wetu, haitakuwa best investment hasa ilinganishwa na upande wa nyuma ya Bagamoyo, na vitu vingine vitakavyopanua maeneo ya influence.
 
msilaumu kila kitu, bandari ya Mtwara ipo kwenye project na ujenzi wake unaanza soon. Nimefanya ESIA pale na lengo la ujenzi wa bandari ya Mtwara ni kwa ajili ya miradi ya gesi, mafuta, makaa ya mawe na migodi ya Nickel iliyo mbioni kuanzishwa katika wilaya ya Nachingwea kwenye milima ya Ntaka
 
Nicholous sio kweli kwamba Bagamoyo haina tofauti sana na Dar kwenye kina. Kina kinachotakiwa standard ni 13.9 M ili kukidhi meli zenye ukubwa wa kwenda chini mita 12. Kina cha Dar es salaam katika eneo lililopo la kupanua bandari hakifiki 13.9M, kwa sasa kipo kwenye 12M hivyo inabidi kufanya zoezi la kuchimba zaidi. Kina cha Bagamoyo ni 13.4M hivyo uchimbaji unaotakiwa ni kidogo ukilinganisha na Dar.

Umeongelea kwamba Oysterbay,mbezi, kunduchi kuna gate kubwa.....are you serious na hoja hii? Kweli unataka kutuaminisha kwamba sasa bandari ijengwe Oysterbay? mbezi? Kunduchi? Kwenye eneo lipi hilo ambalo lina space kubwa ya ku accomodate operations za bandari na mpaka kuwa na Export Processing Zone? Na hata kama space ingekuwepo...tunataka kuongeza congestion ya traffic zaidi ya iliyopo sasa? Maana shghuli za bandari lazima ziongeze idadi ya movement za magari kwenye eneo la bandari kwa ajili ya usafirishaji wa mizigo.

Unasema bagamoyo ni front ya kufanya unyonyaji- hebu tupatie mawazo bora zaidi! From where am standing Bagamoyo project ni front ya kutoa ajira kwa vijana wengi ambao hivi sasa wamenitimu masomo yao katika ngazi mbalimbali na hawana ajira. Ni front ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara cha kuaminika; ni front itakayotuwezesha tuimili ushindani katika sekta ya bandari kwenye region yetu....wakenya wanapanua Mombassa, wanajenga bandari mpya Lamu.....sisi tumo humu kupiga porojo kwamba Bagamoyo ni front ya unyonyaji.

ume raise valid argument ya umuhimu wa kuwa na miundombinu ya kuisupport bandari mpya ya bagamoyo. Kama wewe umetambua umuhimu huo, hata yule anayetaka kuwekeza pesa yake kujenga ile bandari keshatambua hilo pia. Ndio maana ya kufanyika feasibility study na busines plan.....katika mpango mzima wa uwekezaji ule kuna ujenzi wa reli kuumganisha Tazara na reli ya kati kwenda Bandari ya Bagamoyo. Pia kuna mpango wa ujenzi wa Expressway ya Chalinze-Ubungo (alisha announce Magufuli bungeni) na express way ya Bagamoyo-Dar es salaam....na zile barabara za kati kuunganisha Bagamoyo na Kibaha zipo.
Nashukuru umesema kote patachimbwa, na ndicho nilichokuambia kuwa kwa nature ya mawimbi ya upande wetu wa mashariki na hemisphere tuliyopo mawimbi yanakuja na mchanga pwani,na kila mra tutahitaji hilo.Hiyo export processing zote ipi unataka iwe baharini?Mkijaza kila kitu bandarini si yatarudi mambo ya dar?Kwani mkuranga na kwingine palipokuwa pameanza hiyo paln imeishia wapi?

Pakiwa na structure hiyo export processing zone inaweza jengwa hata mlandizi na traina zikapeleka mzigo Bandarini kwa designated rails an trains.

Tanzania inahitaji chagua wanataka wawe nani ktk global business, wanataka kuwa business hub, world factory kama china na kuchafua mazingira sana, kuwamezwa na wafanyakazi wa bei rahisi kutoka uchina, phillipine,Pakistani,Bangladesh, india ,vietnam etc.

Au outsourcing hub?

Huyo mwekezaji ataridhia pale uwekezaji unaleta business sense kwa upande wake na haiwezi kuwa sababu kwetu sisi, kwani Yeye mambo muhimu kama kuwaacha maiskini na mazingira machafu, kuajiri vijana kwa kazi duni,kuwaibia si kitu kizuri kwake kujihusisha nacho.

Bado mpo too naive my friend, ndio umeoka shule kama mafuru wa NBC na morgage finace yake nini?Kwako nadhani ni kitu kinachoweza synch na mind yako na class uliyopo na drems zako ila kila kitu kinaweza kuwa ni mbegu ya kuharibu nchi kama walipotua kunguru dara kwa mara ya kwanza.
 
Nashukuru umesema kote patachimbwa, na ndicho nilichokuambia kuwa kwa nature ya mawimbi ya upande wetu wa mashariki na hemisphere tuliyopo mawimbi yanakuja na mchanga pwani,na kila mra tutahitaji hilo.Hiyo export processing zote ipi unataka iwe baharini?Mkijaza kila kitu bandarini si yatarudi mambo ya dar?Kwani mkuranga na kwingine palipokuwa pameanza hiyo paln imeishia wapi?

Pakiwa na structure hiyo export processing zone inaweza jengwa hata mlandizi na traina zikapeleka mzigo Bandarini kwa designated rails an trains.

Tanzania inahitaji chagua wanataka wawe nani ktk global business, wanataka kuwa business hub, world factory kama china na kuchafua mazingira sana, kuwamezwa na wafanyakazi wa bei rahisi kutoka uchina, phillipine,Pakistani,Bangladesh, india ,vietnam etc.

Au outsourcing hub?

Huyo mwekezaji ataridhia pale uwekezaji unaleta business sense kwa upande wake na haiwezi kuwa sababu kwetu sisi, kwani Yeye mambo muhimu kama kuwaacha maiskini na mazingira machafu, kuajiri vijana kwa kazi duni,kuwaibia si kitu kizuri kwake kujihusisha nacho.

Bado mpo too naive my friend, ndio umeoka shule kama mafuru wa NBC na morgage finace yake nini?Kwako nadhani ni kitu kinachoweza synch na mind yako na class uliyopo na drems zako ila kila kitu kinaweza kuwa ni mbegu ya kuharibu nchi kama walipotua kunguru dara kwa mara ya kwanza.

Nadhani tumefika mahala pa ku agree to disgree. Let us wait and see. Time will Tell
 
Eneo la ujenzi wa bandari la Bagamoyo, lina kina kirefu na mlango mpana wa kuingizia meli zitakazohitaji kutia nanga. Hizo ni sifa kubwa zinazopelekea interest ya Wawekezaji wa sekta ya bandari kupendelea kuwekeza kule. Miaka 20 ijayo, meli zitakazojengwa zitakuwa ni 4th Generation zenye size kubwa kwa ajili ya kubeba mizigo mingi. Meli hizo hazitoweza kuingia kwenye lango la bandari ya Dar es salaam unless lifanyike zoezi la kupanua mlango wa bandari na kuchimba zaidi kuongeza kina....jambo ambalo itabidi kuchimba eneo kubwa mpaka ilipo Ikulu. Bandari ya Tanga na ile ya Mtwara vilevile zina disadvantage ya kutokuwa na Kina kikubwa kinachotakiwa kwa ajili ya hizo 4th generation ships. Sisemi kwamba haziwezi kutengenezwa zika accomodate meli za aina hiyo, la hasha. Inawezekana, lakini kwa gharama kubwa. Hivyo mtu anayetaka kuwekeza kwenye bandari ni rahisi zaidi kuwekeza Bagamoyo kule eneo lingine.

nimesoma bagamoyo nakufahamu kwa kiasi kikubwa nakumbuka moja ya sababu zilizo wasababisha wajerumani wahamishe makao yao wakuu kuyapeleka Dar ni kina kifupi cha bahari leo hii imekuwaje?
binafsi ni bora tuendeleze mji huu kwa utalii ili watu wapate mji ambao wanaweza kupunguza shida wanazopata kwa ukali wa maisha.haka kamji kanaitaji kijbandari cha kawaida sana
 
Ndugu yangu usiligeuza suala hili muhimu la kiuchumi kuwa la kisiasa. Umuhimu wa bandari kwa uchumi wa Tanzania hauna ubishi. Yapo mambo ya msingi muhimu kufahamika:
Bandari ya Dar imeelemewa kwasababu ya wingi wa mizigo inayopitia katika bandari hiyo ndio maana kuna foleni za meli kuingia hapo Bandarini. ............

Kwanini Bagamoyo?
Eneo la ujenzi wa bandari la Bagamoyo, lina kina kirefu na mlango mpana wa kuingizia meli zitakazohitaji kutia nanga. Hizo ni sifa kubwa zinazopelekea interest ya Wawekezaji wa sekta ya bandari kupendelea kuwekeza kule. Miaka 20 ijayo, meli zitakazojengwa zitakuwa ni 4th Generation zenye size kubwa kwa ajili ya kubeba mizigo mingi. Meli hizo hazitoweza kuingia kwenye lango la bandari ya Dar es salaam unless lifanyike zoezi la kupanua mlango wa bandari na kuchimba zaidi kuongeza kina....jambo ambalo itabidi kuchimba eneo kubwa mpaka ilipo Ikulu. Bandari ya Tanga na ile ya Mtwara vilevile zina disadvantage ya kutokuwa na Kina kikubwa kinachotakiwa kwa ajili ya hizo 4th generation ships. Sisemi kwamba haziwezi kutengenezwa zika accomodate meli za aina hiyo, la hasha. Inawezekana, lakini kwa gharama kubwa. Hivyo mtu anayetaka kuwekeza kwenye bandari ni rahisi zaidi kuwekeza Bagamoyo kule eneo lingine.

.................
Soon utaona nayo inashughulikiwa.

Bandari ya Bagamoyo haina kina kirefu kwani kina kirefu kinaanzia baada ya continental shelf kuisha ukitokea bara/nchi kavu. Isitoshe, proposed port ni Mbegani, a very shallow fishing village on the continental shelf able to handle ngalawa za wavuvi na some leisure/recreational crafts. Piga ua, Mbegani will need expensive dredging - watakaofaidika hapa ni foreigners ambao wana utaalamu wa dredging.

Mtwara is one of the deepest ports on the east African coast with only Durban being deeper. It is a natural port that needs no dredging, has a wide opening to the sea as opposed to Dar-es-Salaam, it only needs some development in terms of infrastructure and it is going to be a big player once the Mtwara corridor comes into fruition.

If we are talking about a convinient natural port with lots of land surrounding it and infrastructure (roads, rail, airport) not too far away then we should look no further than Kilwa some 240 kilometers from Dar. This is a naturally deep port requiring no dredging. Abundant lands surround this town for container terminals, gas from Songosongo and Mtwara haipiti mbali sana, and this will greatly reduce the congestion in Dar. Kutandika reli kutoka hapa kwenda Lindi, Mtwara, Dar na hinterland would definitely be cheaper than dredging Mbegani/Bagamoyo, don't you think???
 
Nadhani tumefika mahala pa ku agree to disgree. Let us wait and see. Time will Tell

So what if time tells us we are screwed and we cant recover what have been damaged?Hawa ****** wanaopiga kelele na wapo tayari tuua ili wafanikishe kufurahisha tamaa zao ambazo hazijawahai katwa na chochote walichowahi tuibia?
 
wale wavivu wa bagamoyo watafunguliwa umalaya wa kuwamaliza, chalinze pekee na umbali wake, na kukosekaa barabara ya moja kwa moja,imewaua sana mabint wa bagamoyo,itakuweje wakiletewa karibu.
 
"Bandari ya Dsm imeelemewa na bado nchi nyingi za jirani zinahitaji kutumia bandari zetu hapa Tz,hivyo serikali ina mpango wa kujenga bandari ya kisasa huko Bagamoyo hili kukabiliana na changamoto hii".
Nimeshtushwa kuisikia hii kauli kuto kwenye kinywa cha waziri na viongozi mbalimbali ktk taarifa ya habari ITV huku waziri mkuu akiwepo,walikuwa wanaongea na wachina ambao wanategemea kuchukua hilo dili.Hii nchi sijui tunaipeleka wapi,hivi tuna haja kweli ya kuingia garama kubwa ya ujenzi wa Bandari ilhali tuna Bandari kubwa huku Mtwara ama pale Tanga?.Naanza kuingiwa na mashaka na hii plan B ya kuipeleka gas yetu Bagamoyo kwa kigezo cha kuwa inakwenda kutumiwa na viwanda vikubwa vinavyotarajiwa kujengwa huko,kwa nini isiwe Mkuranga?.

Kwa nn kila kitu siku hizi ni Bagamoyo?,hivi viongozi wetu hamlioni hili?.Msitulazimishe tuanze kuangaliana kibaguzi ktk nchi ambayo haikuwa na hivi vitu vinavyopandikizwa sasa.Kama waliopita wangekuwa na hurka za ubinafsi kama hizi basi Butiama,Lupaso na Dole yangekuwa majiji muda huu.

Umesema kila kitu Bagamoyo naomba ututajie hivyo vitu vyote.

Kwa taarifa yako tu ni kwamba bandari ya Bagamoyo ilikuwepo miaka nenda rudi kinachofanyika kama kuifufua. Bandari ile ilikuwa pale kabla hata ya Bandari ya Dar Es Salaam.
 
Back
Top Bottom