Ujenzi wa Makanisa na Misikiti kwenye makazi ni kirusi kinacholelewa na Serikali

kindikwili

JF-Expert Member
Oct 5, 2016
1,862
2,871
Habari iwe kwenu!
Kwanza nianze kwa kusema mimi ni muumini wa dini (Mkristo) na naheshimu sana dini za watu wengine. Niseme wazi kabisa kwamba Mungu ana utaratibu na Mungu anapenda utaratibu. Mungu hapendi kelele, hapendi vurugu na hapendi mambo yasiyo na mpangilio.

Pamoja na kwamba Mungu anatutaka kumuabudu, hataki kabisa tumuabudu hovyo hovyo, kila mahali (kwenye gari,njiani, sokoni, chooni, porini etc). Ndiyo maana Yesu anasema mnapotaka kusali ingia ndani mwako (inaweza kuwa kwenye nyumba kama kanisa au msikiti au ndani ya chumba chako) na usali katika roho na kweli. Kwahiyo Mungu wala si lazima asikie sauti zetu yeye anataka tumuabudu katika roho na kweli , unaweza kukumbuka habari ya yule mtoza ushuru na farisayo waliopanda kwenda hekaluni, jinsi mtoza ushuru alivyosali kwa moyo bila hata kusikika anasema nini , na Yesu ANASEMA SALA YAKE ILIPOKELEWA NA MUNGU.

Baada ya utangulizi huo, napenda kuikumbusha serikali kuacha kulea hiki kirusi cha kufanya kila sehemu kuwa nyumba ya Ibada. Yaani katikati ya nyumba za watu kuna makanisa na misikiti kama utitiri. Unavuka nyumba ya kwanza yapili kuna kanisa au msikiti, halafu kuna miziki mikubwa na sauti kubwa zinazofanya wengine washindwe kujipumzisha baada ya kazi za kutwa au hata kulala vizuri usiku. Najua watu wana haki ya kuabudu lakini pia ni wajibu kufuata utaratibu katika kutimizi haki hiyo. Na kama wenye imani yao hawataki kufuata utaratibu basi serikali ina wajibu wa kuwalazimisha wafuata utaratibu huo. Leo maeneo ya mijini hadi barabara zinafungwa na watu wanaosali/ swali. Ukitaka kuuliza unaambiwa ni haki yao au tuvumiliane, tunavumilianaje na watu wanaovunja haki za wenzao ya kutumia barabara?. Unamvumiliaje mtu anayekuzuia kulala kwasababu anatimiza haki yake ya kusali? , kwanini tuvumilie huku haki zetu zinavunjwa?. Watu wa dini watafute maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kuabudia, hii ya nyumba ya mbele kuna kanisa halafu ndani kuna wapangaji ni uholela.

Najua watu watasema kwanini navumilia kuwa karibu na baa au kumbi za harusi ila naona shida kuwa karibu na kanisa au msikiti mtaani?. Jibu ni rahisi sana, baa ikijengwa karibu na makazi ya watu siku serikali wakitaka kuivunja hakuna atakayeongea. Watu watakuwa kimya tu kuona greda linakuja kulibomoa kama walivyokaa kimya kuona nyumba za kimara au TANESCO zikivunjwa, lakini siku serikali ikisema tunavunja misikiti yote au makanisa yote yaliyojengwa karibu na makazi, hapo ndipo tutashuhudia maneno na kauli za kila aina za waamini na viongozi wao. Kama kwa wakati huo Rais atakuwa mkristo utasikia lawama kutoka kwa waisamu na udini utaingizwa na kama atakuwa muislamu basi huenda wakristo nao wakaona wananyanyaswa na kuingiza udini. Sasa kuondoa hayo yote ni vizuri serikali ikapiga marufuku ujenzi wa misikiti na makanisa kiholela. Bora tukubali raia kujenga bila kibali maana siku hata zikivunjwa hakuna madhara makubwa kwa taifa kuliko kuacha makanisa na misikiti ikajengwa kwa holela kama tunavyoshuhudia sasa.

Ni heri kuziba ufa kuliko kujenga ukuta, narudia Mungu napenda utaratibu na kuheshimu haki za wengine unapotimiza wajibu wako.
 
Mmmmh asee wenye comment ngoja waje

Waje tu ila ukweli ni huo, siku serikali itakapoanza kuvunja nyumba hizi zikishakuwa nyingi itakuwa issue , bora zipigwe marufuku sasa. Maeneo yawekwe kama hayapo ila kama ni kujenga kanisa au misikiti wakajenge kwenye hayo maeneo. Bora RC wao wanahamisha watu kupisha kanisa kuwa karibu na nyumba za watu, wanatafuta hela wanawalipa watu wanaondoka. Ni makanisa machache sana ya RC, Lutheran na Anglican ziko kwenye makazi yatu. Shida kubwa iko kwenye misikiti na ministries
 
Acha tu nyumba za ibada zijengwe kila kona maovu yanaweza kupungua mkuu maana binadamu tumekuwa wakatili sana
 
Acha tu nyumba za ibada zijengwe kila kona maovu yanaweza kupungua mkuu maana binadamu tumekuwa wakatili sana
Cha ajabu na cha kweli ni kwamba kwenye majumba haya mengi na waumini wengi ndiko kwenye ufirauni mwingi na makubwa kupitiliza.
 
Ndugu yangu kwanza nngependaa kujua elimu yako na pia umebobea katika nini maana unachokiongea nadhan huna elimu nacho kidogo nkujuze ni hivi katika suala la mipango miji kuna huduma ambazo ni muhimu kua close na makazi ya watu au within settlement forexample light industry(viwanda ambavyo n non polutant ) maduka warehouse zahanat open space n religious means maeneo ya kuabudu maana hizi n huduma ambazo watu wanazitua mara kwa mara hivyo unaposema maeneo hayo yatolewe maeneo ya makazi sijajua unatumia akili gani au elimu gani kutoa hoja zako hzo hvyo ndugu jaribu kua unafuatilia jambo zeni ndo utoe uzi huuumuu....
 
Naunga mkono hoja, halafu kutopata usingizi wa kutosha hata kitabibu huzua majanga. Mungu gani angeruhusu upuuzi huo? Hoja ina mashiko sana, na haswa ndicho kiini cha sera ya mipango miji.
 
Ndugu yangu kwanza nngependaa kujua elimu yako na pia umebobea katika nini maana unachokiongea nadhan huna elimu nacho kidogo nkujuze ni hivi katika suala la mipango miji kuna huduma ambazo ni muhimu kua close na makazi ya watu au within settlement forexample light industry(viwanda ambavyo n non polutant ) maduka warehouse zahanat open space n religious means maeneo ya kuabudu maana hizi n huduma ambazo watu wanazitua mara kwa mara hivyo unaposema maeneo hayo yatolewe maeneo ya makazi sijajua unatumia akili gani au elimu gani kutoa hoja zako hzo hvyo ndugu jaribu kua unafuatilia jambo zeni ndo utoe uzi huuumuu....
Labda Hujamuelewa mdau, hajasema yasiwepo, wala yasiwe karibu. Ktk kusimamisha hoja yake amesema, kila baada ya nyumba moja hekalu msikiti,ndivyo ilivyo ktk upangaji wa miji ulivyo? Nijuavyo, sehemu za ibada hutengwa maalumu kwa shughuli hiyo, makazi pia, biashara nknk. Elimu gani mpya zaidi ya hiyo.
 
Habari iwe kwenu!
Kwanza nianze kwa kusema mimi ni muumini wa dini (Mkristo) na naheshimu sana dini za watu wengine. Niseme wazi kabisa kwamba Mungu ana utaratibu na Mungu anapenda utaratibu. Mungu hapendi kelele, hapendi vurugu na hapendi mambo yasiyo na mpangilio.

Pamoja na kwamba Mungu anatutaka kumuabudu, hataki kabisa tumuabudu hovyo hovyo, kila mahali (kwenye gari,njiani, sokoni, chooni, porini etc). Ndiyo maana Yesu anasema mnapotaka kusali ingia ndani mwako (inaweza kuwa kwenye nyumba kama kanisa au msikiti au ndani ya chumba chako) na usali katika roho na kweli. Kwahiyo Mungu wala si lazima asikie sauti zetu yeye anataka tumuabudu katika roho na kweli , unaweza kukumbuka habari ya yule mtoza ushuru na farisayo waliopanda kwenda hekaluni, jinsi mtoza ushuru alivyosali kwa moyo bila hata kusikika anasema nini , na Yesu ANASEMA SALA YAKE ILIPOKELEWA NA MUNGU.

Baada ya utangulizi huo, napenda kuikumbusha serikali kuacha kulea hiki kirusi cha kufanya kila sehemu kuwa nyumba ya Ibada. Yaani katikati ya nyumba za watu kuna makanisa na misikiti kama utitiri. Unavuka nyumba ya kwanza yapili kuna kanisa au msikiti, halafu kuna miziki mikubwa na sauti kubwa zinazofanya wengine washindwe kujipumzisha baada ya kazi za kutwa au hata kulala vizuri usiku. Najua watu wana haki ya kuabudu lakini pia ni wajibu kufuata utaratibu katika kutimizi haki hiyo. Na kama wenye imani yao hawataki kufuata utaratibu basi serikali ina wajibu wa kuwalazimisha wafuata utaratibu huo. Leo maeneo ya mijini hadi barabara zinafungwa na watu wanaosali/ swali. Ukitaka kuuliza unaambiwa ni haki yao au tuvumiliane, tunavumilianaje na watu wanaovunja haki za wenzao ya kutumia barabara?. Unamvumiliaje mtu anayekuzuia kulala kwasababu anatimiza haki yake ya kusali? , kwanini tuvumilie huku haki zetu zinavunjwa?. Watu wa dini watafute maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kuabudia, hii ya nyumba ya mbele kuna kanisa halafu ndani kuna wapangaji ni uholela.

Najua watu watasema kwanini navumilia kuwa karibu na baa au kumbi za harusi ila naona shida kuwa karibu na kanisa au msikiti mtaani?. Jibu ni rahisi sana, baa ikijengwa karibu na makazi ya watu siku serikali wakitaka kuivunja hakuna atakayeongea. Watu watakuwa kimya tu kuona greda linakuja kulibomoa kama walivyokaa kimya kuona nyumba za kimara au TANESCO zikivunjwa, lakini siku serikali ikisema tunavunja misikiti yote au makanisa yote yaliyojengwa karibu na makazi, hapo ndipo tutashuhudia maneno na kauli za kila aina za waamini na viongozi wao. Kama kwa wakati huo Rais atakuwa mkristo utasikia lawama kutoka kwa waisamu na udini utaingizwa na kama atakuwa muislamu basi huenda wakristo nao wakaona wananyanyaswa na kuingiza udini. Sasa kuondoa hayo yote ni vizuri serikali ikapiga marufuku ujenzi wa misikiti na makanisa kiholela. Bora tukubali raia kujenga bila kibali maana siku hata zikivunjwa hakuna madhara makubwa kwa taifa kuliko kuacha makanisa na misikiti ikajengwa kwa holela kama tunavyoshuhudia sasa.

Ni heri kuziba ufa kuliko kujenga ukuta, narudia Mungu napenda utaratibu na kuheshimu haki za wengine unapotimiza wajibu wako.

Wacha meneno mengi. Nyumba za Ibada Tangu enzi za watawala waliojua kupanga miji iliwekwa karibu na Makaazi ya watu.
nyumba za ibada haziwekwi mbali ni shemu ya maisha na makaazi.
na hasa misikiti ni mambo ya kiroho , harusi maziko inakua karibu na makaazi yetu.
jiji la la Dar lipo hivo tangu wabara hawajaingia hapa na hakuna tatizo lolote.
labda kama unazungumzia kina Tito
 
Unamvumiliaje mtu anayekuzuia kulala kwasababu anatimiza haki yake ya kusali? , kwanini tuvumilie huku haki zetu zinavunjwa?. Watu wa dini watafute maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kuabudia, hii ya nyumba ya mbele kuna kanisa halafu ndani kuna wapangaji ni uholela.

Usijali, siku si nyingi utalalaaaa hadi uchoke. Ukiamka unajikuta umelala tu na tani 7 za blanketi juu yako. Huna dini yeyote weye bali deni tu.
Wewe unajiona una haki kuwazuia wenzio wasi swali kisa wewe hutaki kuswali bali unangojea siku ya mauti ili uswaliwe? Mbona kazi kubwa hii. Ndo maana kuna kiongozi yu asema kila siku kuwa tumwombee. Kuongoza watu ka wewe ni shughuli. Unaona wewe tu ndo mwenye haki ila huyo anayetaka kuswali hana haki??
 
ila ni kwer kuwe na mpangilio wa hizi nyumba za ibada maana siku wakisema zipo sehemu sio kweny kuziondoa ni issue kubwa sana inakuwa
 
Usijali, siku si nyingi utalalaaaa hadi uchoke. Ukiamka unajikuta umelala tu na tani 7 za blanketi juu yako. Huna dini yeyote weye bali deni tu.
Wewe unajiona una haki kuwazuia wenzio wasi swali kisa wewe hutaki kuswali bali unangojea siku ya mauti ili uswaliwe? Mbona kazi kubwa hii. Ndo maana kuna kiongozi yu asema kila siku kuwa tumwombee. Kuongoza watu ka wewe ni shughuli. Unaona wewe tu ndo mwenye haki ila huyo anayetaka kuswali hana haki??
Akili zenu huwa nazishangaa sana, ktk kila kitu kiwapendezacho ninyi ndicho kiwe, mmekuwa watoto ninyi? Sasa nani kakuambia msiswali? Na nani aliyekudanganya kwamba kuswali ndiko kuiona Pepo? Halafu kwanini msumbuke na kutishia kifo, inaonesha mnakiogopa sana, sasa huko kwa Mola kuna shoti kati ya kwenda? Si mnasema ni kuzuri, maisha mazuri nk iweje mkihofi kifo? Hata ninyi hamuamini mnachoambiwa.

Ktk hili umeona si vyema, kundi fulani lisipate haki kwakuwa tu kundi fulani litateseka, nawe Umeona kufanya hivyo ni sahihi kabisa. Labda kwakuwa unahisi kundi lako ndilo teule kwa Mungu, lakini unajisahaulisha kwamba imani hiyo iko ktk kila kundi jingine.

Uumbaji uko ktk utaratibu, na kila kitu kiko ktk utaratibu pia. Ni vyema kila jambo lisimamiwe na utaratibu pia, kufata utaratibu pia nako ni Ibada na kinyume chake ni mahasi.
 
Mada nzuri kabisa na umeeleweka !
Subiri manungaembe yaje yasioelewa chochote kazi yao kupinga na kuona yanaonewa
acha matusi, utatukanwa halafu useme oh usinitukanie mama, baba etc. Take care!
 
Halafu inakera sana, saa kumi Na moja unajionea Mungu wako aitangulie siku yako ya Leo, Mara unasikia kelele za lugha usiyoijua Wala kuielewa inatoka kwenye vipaza sauti na kukuvurugia uwepo. Mungu jukwaa mahali pa utulivu
 
NI KWELI KABISA, SUALA LA MIPANGO MIJI LIZINGATIWE, LAKN SYO TU KTK NYUMBA ZA IBADA, BALI PIA KTK MAMBO MENGNE IKIWEMO MAKAZ NA HZO BAR ULIZOSEMA
 
Back
Top Bottom