Ujenzi wa barabara unaondelea (kimara - Kibaha) Mkandarasi anajenga kambi yake ya vifaa vya ujenzi na ofisi ndani ya eneo la barabara. Ikumbuke jengo linalojengwa ni sehemu ya fedha za ujenzi wa barabara hiyo. Na nakumbuka kulikua na mpango mkakati wakandarasi wote wapewe maeneo ambayo majengo yatakayojengwa yabakie kuwa majengo ya serikali badala ya kuyavunja kama ilivyokua hapo awali.
kutokana na mpango huo kuna majengo kama pale Msata, Lugoba zilipo ofisi za halmashauri ya Chalinze na maeneo mengine nchini, zote ni matunda ya mpango huo. Kulikoni kwenye mradi huu wa Kimara - Kibaha? maana lazima hayo majengo yatavunjwa baada ya mradi kukamilika, je sio upotevu wa fedha za umma?
Mh. Rais na Waziri wa Ujenzi okoeni fedha hizo kwa kumpatia mkandarasi eneo la kudumu ili mwisho wa mradi tupate majengo yanayoweza kutumiwa kama ofisi za umma, Zahanati, kituo cha polisi, nyumba za walimu au shule ya awali.
kutokana na mpango huo kuna majengo kama pale Msata, Lugoba zilipo ofisi za halmashauri ya Chalinze na maeneo mengine nchini, zote ni matunda ya mpango huo. Kulikoni kwenye mradi huu wa Kimara - Kibaha? maana lazima hayo majengo yatavunjwa baada ya mradi kukamilika, je sio upotevu wa fedha za umma?
Mh. Rais na Waziri wa Ujenzi okoeni fedha hizo kwa kumpatia mkandarasi eneo la kudumu ili mwisho wa mradi tupate majengo yanayoweza kutumiwa kama ofisi za umma, Zahanati, kituo cha polisi, nyumba za walimu au shule ya awali.